Pre GE2025 Suala la maslahi ya Tanganyika tunataka liwe addressed kampeni 2025!

Pre GE2025 Suala la maslahi ya Tanganyika tunataka liwe addressed kampeni 2025!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
ila huu muungano daaah yani wanafunzi wa vyuo vikuu toka zanzibar wanaruhusiwa kuomba mkopo heslb na kwao pia zanzibar
 
ila huu muungano daaah yani wanafunzi wa vyuo vikuu toka zanzibar wanaruhusiwa kuomba mkopo heslb na kwao pia zanzibar
kwahiyo wamekuja kuziba nafasi ya watoto wa tanganyika masikini kupata mkopo.
 
na kuna issue nyingi tu za msingi, kipindi cha jiwe aliibua issue ya umeme wakawa wanadaiwa kama bilioni 200 kama nakumbuka, hawajawahi kulipa au wamelipa hatujui kwa sababu na rais naye ni wa kwao. na likija suala lolote la changamoto za muungano, huwa zinaangaliwa zaidi zile za wazanzibar, sasa ivi wametulia hata hatujui kama mama yao kawapendelea kimyakimya au vipi, inakuwaje miaka yote walikuwa wanaongea sasaivi wapo kimya? hivi wanasiasa huwa wanaakili kutafuta issue sensitive zinazoweza kuwadraw maccm waje kwenye meza ya mazungumzo na kutatua matatizo au?
Hilo deni la umeme walisamehewa kipindi hiki cha utawala wa Mama Abdul, yaani wao wanasamehewa sisi huku tunapandishiwa bei kuwalipia wao, huu muungano ni wa kishetani kabisa.
 
Hilo deni la umeme walisamehewa kipindi hiki cha utawala wa Mama Abdul, yaani wao wanasamehewa sisi huku tunapandishiwa bei kuwalipia wao, huu muungano ni wa kishetani kabisa.
ni muungano uliojaa hofu kwenye mioyo ya watanganyika, mzanzibari anaweza kuuongelea apendavyo ndio maana hata bungeni alitokea mmoja kuwa twende kwao kwa passport, yaani kawilaya kama kale kanatupelekesha hadi kanatuchagulia rais atutawale na bado kanasema twende kwao na passport. lakini uhakika, akitokea mtu akaadress hii hissue, 99% ya watanganyika hawataki hata kusikia na anaweza kupata hata kura kwa sababu hiyo tu. sasa opportunity ipo afu chadema wanazubaa kwa nini?
 
Upo sahihi ndgu mwandishi..
Point Namba 7. Hapo bora kungekua na rais wa tanganyika pia make zanzibar wanae. Na awepo rais wa tanzania
 
Upo sahihi ndgu mwandishi..
Point Namba 7. Hapo bora kungekua na rais wa tanganyika pia make zanzibar wanae. Na awepo rais wa tanzania
rais wa zanzibar anaweza kuja kugombea na bara akatawala. ila wa bara hawezi kugombea kule. ni kaeneo kadogo sana, likija suala la ajira wao wanataka wapate 20% ila wabara marufuku kuajiriwa kule, wanasema wasije kupora ajira za wazanzibari. ni nini hiki?
 
Na Zanzibar ni nchi Gani Tena?
ilitakiwa iwe wilaya kabisa hat amkoa haitoshi. halafu wanapata 20% ajira, wanapata mkopo wa elimu huku na kule, wakati watoto wa kitanganyika wanapata huku tu na kule kwao hawatakiwi kuonekana, wanamiliki ardhi wapendavyo wakati wewe huwezi kwenda kumiliki kule, nyerere angekuwepo leo alitakiwa kupigwa hata vibao viwili hakika.
 
Hoja muhimu sana hizi
nakuhakikishia, TL akisimama leo akasema muungano urekebishwe, kura zote zake kwa sababu hili jambo linawakera sana watanganyika, hata wanaojifanya wanapenda muungano wa aina hii wanasema tu kinafiki ila ukija kwenye kura wote wanataka muungano reasonable, sio kawilaya kanakuja kutuendesha nchi ya watu 50m+
 
Hii ni moja ya ajenda isiyo epukika kwenye kampeni zinazofuata.

Kumekuwa na uongo na hadaa nyingi toka kwenye uongozi wa CCM kwa sababu ya muungano huu ambao wameugeuza toka kweye malengo yake ya mwanzo; na kuufanya muungano ndio uwe sababu ya kufanya kila uchafu ili CCM iendelee kubaki kwenye madaraka.
Bila uwepo wa muungano kama ulivyo sasa, CCM hawana ujanja wa kubaki madarakani pande zote za muungano huo.
 
Naamini hapa ndipo mahali pa kuwa wazi na kueleza kilichopo mtaani ili viongozi wetu kama sio kujirekebisha basi watafute solution ya kudumu kwenye mambo mbalimbali.

1. Raia wengi, wanaamini mtu mwenye courage pekee kuongelea suala la muungano, ni TL.

2. eneo dogo kama zanzibar, lenye watu hada 2m hawafiki, kuwa sawa na eneo kubwa lenye watu zaidi ya 55m, watu hawaridhiki.

3. suala la ardhi, zanzibar wanamiliki bara wapendavyo, ila bara marufuku kumiliki zanzibar?

4. kazi, asilimia 20% kazi bara wanapata wazanzibar, ila marufuku mtanganyika kuajiriwa zenji.

5. raia wa zanzibar waliowengi hasa wasio na makazi bara, hawawapendi watanganyika wala muungano. hata wale waliofaidika na tanganyika na kuishi bara, chuki wanazo nyingi sana na ipo wazi.

6. viongozi wa kuteuliwa kama mawaziri, wakurugenzi n.k, hatuwezi kuwa sawa, not fair.

7. Rais anatoka zanzibar, anaweza kuwa Rais zanzibar na akawa rais bara, ruksa, nasemani rais bar akwa sababu hata akiitwa rais wa muungano akienda zanzibar anakuwa chini ya rais wa zanzibar.

8. wengi pamoja na kwamba wapo tayari hata uvunjike, lakini kwa sababu tumeshaishi pamoja miaka mingi, wanasema hata usipovunjika itakuwa safi, ila kipengele cha rais wa zanzibar kiondoke, issue ya umiliki wa ardhi iondoke, na issue za ajira ziwe fair mtu aajiriwe pande zote mbili.

9. haiji kichwani, wewe unasema unapenda muungano, ila hautaki tuungane. kama tungemiliki ardhi kwa pamoja, wabara wata assimilate zanzibar na wazanzibari wataassimilate bara, na hapatakuwa na Tanganyika wala Zanzibar, itakuwapo TANZANIA. sasa kama wewe haupendi tuassimilate to each other, muungano upo wapi sasa na ni wa nini? si utakuwa muungano wa upande mmoja? yaani leo hii zanziba anaamini anapenda muungano ila akiruhusu ardhi ya zanzibar imilikiwe watanganyika wataimiliki yote na wazanzibar watakosa au zanzibar haitakuwepo tena, sasa kama unataka iwepo, unataka muungano upi na kivipi?

TL akija na gia hii kwenye kampeni, ndipo ajajua nini hasa kilichopo kwenye mioyo ya watanganyika, hata kitendo cha kutawaliwa na mzanzibari ambaye hatujui maslahi yake yapo bara au zenji, na hatujui pesa zetu kama zinapelekwa kujenga zenji au la. ni hayo tu. TL nishakupa password ya kuteka mioyo ya wabara tayari, kuichukua au kuiacha ni juu yako.
Kwanza lawama zote angepewa hayati JPM kwa kumteua Samia kuwa makamu wake na akamteua tena 2020 akiwa makamu.

Huu upuuzi wa kuja kulalamikia humu jukwaani ni upotezaji wa muda, zipo mada za maana zaidi zenye kustahili mijadala kwani zinagusa maisha yetu ya kila siku.

Ni sawa na kipindi kile Magu akiwa hai tulivyopenda kujadili mada za kuiponda Chato kwa kigezo kuwa inapendelewa kupita maelezo.
 
tutajie hata moja tu. kama wewe mtu wa bara umepigwa marufuku kumiliki ardhi zanzibar, ila mnzanzibari ana ruhusa kumiliki hata eka milioni hapa bara,

kawilaya kama kale kanataka asilimia 20% ya ajira zinazotangazwa wapate wao, ila wewe marufuku kupata ajira kule kwao.

mawaziri na viongozi hadi marais toka zanzibar wanatawala bara, ila wewe marufuku kuteuliwa kwenda kutawala kule,

wao wana kitambulisho chao na kile cha NIDA wewe una NIDA peke yake.

ndio nauliza, kwani tunachojibembeleza sana ambacho hatuwezi kuishi bila wao ni nini? faida yao ipo wapi.
Ningekuwa na uwezo hivi visiwa vya Unguja na Pemba ningevisogezea mbali kabisa baharini - Julius Nyerere.

Aliyaona haya yote. Kijiografia visiwa hivi ni vidogo sana kuweza kuwa na uwiano ulio sawa na huku bara.

Vyakula vyao vingi vinatoka huku bara, mwaka 2008 May ulipotokea mgao mkubwa wa umeme wao pia waliteseka kwa miezi miwili.

Ni chuki za kisiasa kuanza kuongelea huo upendeleo kwenye ajira wakati huku Bara sisi ni wakubwa kuliko huko Zenji na sidhani kuwa yupo mtu wa bara anayeumizwa na huu mgawanyo wenye kuonekana hauleti haki kwetu.

Chuki hizi chanzo chake ni Rais Samia mwenyewe kuwa mwenyeji wa kizimkazi. Lakini anafanya mengi sana ya maana huku huku bara na yanagusa uhai wetu kwa mapana yake.
 
TL akija na gia hii kwenye kampeni, ndipo ajajua nini hasa kilichopo kwenye mioyo ya watanganyika, hata kitendo cha kutawaliwa na mzanzibari ambaye hatujui maslahi yake yapo bara au zenji, na hatujui pesa zetu kama zinapelekwa kujenga zenji au la. ni hayo tu. TL nishakupa password ya kuteka mioyo ya wabara tayari, kuichukua au kuiacha ni juu yako.
Ni ajenda muhimu, lakini hawezi kuibeba kama ulivyo iweka wewe hapa.
Hivi hukumsikia hivi karibuni akilizungumzia hili kwenye mahojiano yake, hadi udai ni 'Pasword" uliyo ubuni wewe?
Hata hivyo, haiwezi kuwa ajenda ta TL, hii ni ajenda ya waTanzania wote wenye kuutakia mema Muungano. Kilichopo sasa ni utawala wa kiinchi kidogo kuitawala nchi kubwa!
Sijui kamna unayo kumbukumbu ya haya mambo ya hovyo ndani ya Muungano yalianzia wapi; na kama unao ufahamu wa kutosha kwamba mkolezaji mkuu wa hali ilivyo sasa hivi ndani ya Muungano ni huyo huyo aliyeshika usukani mwenyewe; mtu asiye na chembe hata ndogo ya maslahi ya watu anaowatawala!

Hata sijui kama utaelewa ninacho kieleza hapa!
CHADEMA safari hii ni lazima waishikie bango hii ajenda muhimu, ili wananchi waelewe vizuri jinsi Muungano tulio anza nao haupo tena.
 
Back
Top Bottom