Pre GE2025 Suala la maslahi ya Tanganyika tunataka liwe addressed kampeni 2025!

Pre GE2025 Suala la maslahi ya Tanganyika tunataka liwe addressed kampeni 2025!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
No reform no election ni kauli mbiu nyingine inayokuja na kupita, ni sawa na zile za Mbowe alizobuni kila kukicha na kupiga pesa kutoka kwa wazungu.
Kweli, unadhani hivyo?
Tusubiri tutayaona matokeo yake. Mambo yamebadilika sana. Pengine huko uliko wewe ndani ya CCM mmepofushwa na utamu mnao ufaidi.
 
Mkuu 'Steve' usidhani sikuelewi, na juwa tu ni kiasi gani tulivyo upenda muungano wetu huu pamoja na kasoro zake nyingi. Muungano toka mwanzo haukuwa 'perfect', lakini matarajio yalikuwa kwamba hapo tutakapo zoeana na kuona faida za kuungana, muungano wetu unge imarika zaidi. Lengo lilikuwa hilo tokea mwanzo, licha ya mapungufu yaliyo kuwepo toka mwanzo.
Badala ya matarajio hayo ya mwanzo kuwa kama ilivyo tegemewa, kero zikashika kasi mwaka hadi mwaka!

Umetumia mfano wa ndoa. Ni wazi unajuwa ni ndoa ngapi huishia njiani kwa sababu mbalimbali, au siyo?

Hii ndoa yetu ya muungano sasa hivi katika inashikiliwa na wachache sana wanao nufaika nayo moja kwa moja. Siyo ndoa inayo nufaisha taifa tena. Ni CCM pekee ndio wanao ona faida kwa kuendelea kuwaweka madarakani.
Sidhani kama mtu wa kawaida kule Munjebwe au Tandahimba ni mmoja wa wale wanaokerwa na uwepo wa muungano.

Watanzania wengi wa huko mikoani wanazo shida zao ambazo zikitatuliwa watakuwa hata hawahitaji kujua Kiembe samaki au mwanakwerekwe ni sehemu ya JMT.

Nyingi ni nadharia tu za humu mitandaoni katika maisha halisi ya kawaida ambayo Mtanzania anapata yale mahitaji muhimu ya kimaisha simuoni yoyote mwenye hata kuumiza kichwa kuzijadili hizo kero za muungano.

Hii ni mada ambayo msingi wake mkuu unamlenga Samia na awamu yake ya sita.
 
Lissu analo tatizo la ukosefu wa pesa kuelekea uchaguzi mkuu, huwezi kuwasikia chawa wake humu kina Erythrocyte wakiuongea huo ukweli watakuja na mada za kuwajaza ujinga vijana wa upinzani lakini ukweli ni kwamba Mbowe aliweza kuiendesha Chama kwa nguvu ya pesa, na Lissu kwa sasa yupo chali hana kitu. Hapo sijaongelea namna yeye mwenyewe alivyo tofauti na Mbowe.
Dah!
Mmenogewa hadi mnajitoa ufahamu kiasi hiki?
 
Kweli, unadhani hivyo?
Tusubiri tutayaona matokeo yake. Mambo yamebadilika sana. Pengine huko uliko wewe ndani ya CCM mmepofushwa na utamu mnao ufaidi.
Watanzania nawajua vizuri na nina uzoefu wa siasa zetu, Mbowe alipiga kelele kuhusu maandamano wakajitokeza watu wawili tu, yeye na binti yake tena wote wakakamatwa.

Watu wanazo shida zao na CCM inafahamu mbinu zote za kuwavutia ili siku ya uchaguzi waende wakapige kura.
 
Endel
Sidhani kama mtu wa kawaida kule Munjebwe au Tandahimba ni mmoja wa wale wanaokerwa na uwepo wa muungano.

Watanzania wengi wa huko mikoani wanazo shida zao ambazo zikitatuliwa watakuwa hata hawahitaji kujua Kiembe samaki au mwanakwerekwe ni sehemu ya JMT.
ea kudhani hivi, mkuu 'steve'. Sijui kama vitenge mnavyo wapa na kibaba cha unga vitaendelea kuwaziba akili hawa watu mnao wadharau kiasi hiki!
 
Watanzania nawajua vizuri na nina uzoefu wa siasa zetu, Mbowe alipiga kelele kuhusu maandamano wakajitokeza watu wawili tu, yeye na binti yake tena wote wakakamatwa.

Watu wanazo shida zao na CCM inafahamu mbinu zote za kuwavutia ili siku ya uchaguzi waende wakapige kura.
SAWA mkuu, nami ninao uzoefu wa kutosha kwa kukufahamu kupitia kwenye mijadala yetu hii.
 
Watanzania nawajua vizuri na nina uzoefu wa siasa zetu, Mbowe alipiga kelele kuhusu maandamano wakajitokeza watu wawili tu, yeye na binti yake tena wote wakakamatwa.

Watu wanazo shida zao na CCM inafahamu mbinu zote za kuwavutia ili siku ya uchaguzi waende wakapige kura.
EeeenHeeee Heeee!
Umetoa mfano sahihi kabisa wa huyo Mbowe na mwanae!
Hivi hukuwahi kudadisi kwa nini ilikuwa hivyo, na kama uliwahi kujiuliza; ulipata jibu kuwa hali itabaki kuwa hivyo milele?

Bila shaka nyinyi watu wa CCM mtakuwa mmewaroga hawa waTanzania daima warukwe na akili vichwani mwao!
 
Ndio maana machadomo mnapuuzwa,Tanganyika ndio Nchi gani tena? 😁😁
Pumbavu sana wewe, hatukuwa na zanzibar baada ya muungano tulikuwa na Tanzania visiwani. Kama ilionekana Zanzibar iriudi,unawezaje kusema Tanganyika ndo nini!
Tanganyika ni nchi kama ilivyo Zanzibar.
 
Alieanzisha wazo la ajira za bara 20% watoke Zanzibar alikosea sana na sijui alilenga nini hasa! Vijana wetu wanaandamana hawana ajira, kwenye halmashauri huku bara wamejaa wazanzibar tupu! Kweli inauma sana!
 
Naamini hapa ndipo mahali pa kuwa wazi na kueleza kilichopo mtaani ili viongozi wetu kama sio kujirekebisha basi watafute solution ya kudumu kwenye mambo mbalimbali.

1. Raia wengi, wanaamini mtu mwenye courage pekee kuongelea suala la muungano, ni TL.

2. eneo dogo kama zanzibar, lenye watu hada 2m hawafiki, kuwa sawa na eneo kubwa lenye watu zaidi ya 55m, watu hawaridhiki.

3. suala la ardhi, zanzibar wanamiliki bara wapendavyo, ila bara marufuku kumiliki zanzibar?

4. kazi, asilimia 20% kazi bara wanapata wazanzibar, ila marufuku mtanganyika kuajiriwa zenji.

5. raia wa zanzibar waliowengi hasa wasio na makazi bara, hawawapendi watanganyika wala muungano. hata wale waliofaidika na tanganyika na kuishi bara, chuki wanazo nyingi sana na ipo wazi.

6. viongozi wa kuteuliwa kama mawaziri, wakurugenzi n.k, hatuwezi kuwa sawa, not fair.

7. Rais anatoka zanzibar, anaweza kuwa Rais zanzibar na akawa rais bara, ruksa, nasemani rais bar akwa sababu hata akiitwa rais wa muungano akienda zanzibar anakuwa chini ya rais wa zanzibar.

8. wengi pamoja na kwamba wapo tayari hata uvunjike, lakini kwa sababu tumeshaishi pamoja miaka mingi, wanasema hata usipovunjika itakuwa safi, ila kipengele cha rais wa zanzibar kiondoke, issue ya umiliki wa ardhi iondoke, na issue za ajira ziwe fair mtu aajiriwe pande zote mbili.

9. haiji kichwani, wewe unasema unapenda muungano, ila hautaki tuungane. kama tungemiliki ardhi kwa pamoja, wabara wata assimilate zanzibar na wazanzibari wataassimilate bara, na hapatakuwa na Tanganyika wala Zanzibar, itakuwapo TANZANIA. sasa kama wewe haupendi tuassimilate to each other, muungano upo wapi sasa na ni wa nini? si utakuwa muungano wa upande mmoja? yaani leo hii zanziba anaamini anapenda muungano ila akiruhusu ardhi ya zanzibar imilikiwe watanganyika wataimiliki yote na wazanzibar watakosa au zanzibar haitakuwepo tena, sasa kama unataka iwepo, unataka muungano upi na kivipi?

TL akija na gia hii kwenye kampeni, ndipo ajajua nini hasa kilichopo kwenye mioyo ya watanganyika, hata kitendo cha kutawaliwa na mzanzibari ambaye hatujui maslahi yake yapo bara au zenji, na hatujui pesa zetu kama zinapelekwa kujenga zenji au la. ni hayo tu. TL nishakupa password ya kuteka mioyo ya wabara tayari, kuichukua au kuiacha ni juu yako.
Heko sana kiongozi kwa kuona mbali.
 
Kuungana kuna faida kuliko kutengana na mpaka leo heri wanaoungana kuliko wanaotafuta sababu za kutengana.
Kuungana kuna faida lakini lazima iwe ''win-win situation'' . Kwasasa Zanzibar si mshiriki wa Muungano

Nisaidie kuelewa hapa, ni faida gani inazopata Tanganyika au Zanzibar kwa muundo huu wa Mungano!
Nitajie chache tu! kama unazo
 
Sasa Mhuni Lissu atalielezeaje kwenye Kampeni za Uchaguzi Mkuu 2025 wakati yeye hautaki huo uchaguzi?
Kupitia 'no reform no election' ndipo hoja kama hizi zinaelezeka

Tundu Lissu (TAL) kaanza kulieleza suala hili kifundi sana.Ni wenye kutumia vichwa kwa usahihi na ukamilifu wanamwelewa. TAL akasema moja ya reform wanazotaka ni ugawaji wa majimbo ya uchaguzi

TAL akasema mfumo unaotumika sasa unazingatia miundo mbinu , na si population, akatoa mfano,Wapiga kura wote wa Zanzibar ni 500,000 wakiwa na majimbo 50 (yaani Wabunge 50).

Dar es Salaam peke yake in Wapiga kura Milioni 3 ikiwa na Wabunge 10. Usawa upo wapi?

TAL akatoa mfano, wastani wa jimbo la Zanzibar ni wapiga kura 11,000. Jimbo la Ubungo lina wapiga kura Laki 3. Kwa maneno mengine, Wabunge 30 wa Zanzibar wanawakilisha idadi sawa na Mbunge wa Ubungo.

TAL akauliza, imeandikwa wapi kwamba Zanzibar lazima iwe na Wabunge kadhaa! hivyo kufanya hata idadi yao kuwa na Wapiga kura 3,200 (Jimbo la Donge) Idadi ndogo kuliko Wanafunzi wa UDOM au UDSM

TAL anasema Mbunge wa Zanzibar anapata mshahara sawa na Mbunge wa Nyamagana, Ilala, au Arusha.
Kubwa Zaidi, Mbunge wa Zanzibar anapewa pesa za mfuko wa Jimbo kama yule wa Temeke au Tunduru!

Zaidi ya hapo, pesa za mfuko wa jimbo zinatoka JMT ambayo ni walipa kodi wa Tanganyika.
SMZ haina mfuko wa jimbo kwasababu Wabunge wake wanapata kutoka Dodoma.

Ndio maana TAL anasema lazima kuwe na reform za uchaguzi na muundo! hadi hapo hujamwelewa?
 
Naamini hapa ndipo mahali pa kuwa wazi na kueleza kilichopo mtaani ili viongozi wetu kama sio kujirekebisha basi watafute solution ya kudumu kwenye mambo mbalimbali.

1. Raia wengi, wanaamini mtu mwenye courage pekee kuongelea suala la muungano, ni TL.

2. eneo dogo kama zanzibar, lenye watu hada 2m hawafiki, kuwa sawa na eneo kubwa lenye watu zaidi ya 55m, watu hawaridhiki.

3. suala la ardhi, zanzibar wanamiliki bara wapendavyo, ila bara marufuku kumiliki zanzibar?

4. kazi, asilimia 20% kazi bara wanapata wazanzibar, ila marufuku mtanganyika kuajiriwa zenji.

5. raia wa zanzibar waliowengi hasa wasio na makazi bara, hawawapendi watanganyika wala muungano. hata wale waliofaidika na tanganyika na kuishi bara, chuki wanazo nyingi sana na ipo wazi.

6. viongozi wa kuteuliwa kama mawaziri, wakurugenzi n.k, hatuwezi kuwa sawa, not fair.

7. Rais anatoka zanzibar, anaweza kuwa Rais zanzibar na akawa rais bara, ruksa, nasemani rais bar akwa sababu hata akiitwa rais wa muungano akienda zanzibar anakuwa chini ya rais wa zanzibar.

8. wengi pamoja na kwamba wapo tayari hata uvunjike, lakini kwa sababu tumeshaishi pamoja miaka mingi, wanasema hata usipovunjika itakuwa safi, ila kipengele cha rais wa zanzibar kiondoke, issue ya umiliki wa ardhi iondoke, na issue za ajira ziwe fair mtu aajiriwe pande zote mbili.

9. haiji kichwani, wewe unasema unapenda muungano, ila hautaki tuungane. kama tungemiliki ardhi kwa pamoja, wabara wata assimilate zanzibar na wazanzibari wataassimilate bara, na hapatakuwa na Tanganyika wala Zanzibar, itakuwapo TANZANIA. sasa kama wewe haupendi tuassimilate to each other, muungano upo wapi sasa na ni wa nini? si utakuwa muungano wa upande mmoja? yaani leo hii zanziba anaamini anapenda muungano ila akiruhusu ardhi ya zanzibar imilikiwe watanganyika wataimiliki yote na wazanzibar watakosa au zanzibar haitakuwepo tena, sasa kama unataka iwepo, unataka muungano upi na kivipi?

TL akija na gia hii kwenye kampeni, ndipo ajajua nini hasa kilichopo kwenye mioyo ya watanganyika, hata kitendo cha kutawaliwa na mzanzibari ambaye hatujui maslahi yake yapo bara au zenji, na hatujui pesa zetu kama zinapelekwa kujenga zenji au la. ni hayo tu. TL nishakupa password ya kuteka mioyo ya wabara tayari, kuichukua au kuiacha ni juu yako.

Kwa sasa hakuna mtu wa kuitetea Tanganyika. Walioko CCM hawana ujasiri, na wengine wamelambishwa asali au waoga. Nje ya CCM wanatengenezewa zengwe kama Dr Slaa alivyofanyiwa.
 
Kuungana kuna faida lakini lazima iwe ''win-win situation'' . Kwasasa Zanzibar si mshiriki wa Muungano

Nisaidie kuelewa hapa, ni faida gani inazopata Tanganyika au Zanzibar kwa muundo huu wa Mungano!
Nitajie chache tu! kama unazo
Kule kuungana peke yake ni faida kubwa, unajua kitu gani kinachompa jeuri Donald Trump mpaka anafukuza wamexico wakiwa na pingu miguuni na mikononi?, ni muungano wa majimbo yanayounda kitu kinachoitwa USA.

Kumbuka kuwa kuna wapemba wameoa wandendeule wa kule Nyasa.

Kumbuka kuwa kuna watumbatu wameoa waha wa Kigoma,

Kumbuka kuwa kuna Wakerewe wameoa wakojani.

Hawa wote ndio nguvu kazi ya Taifa la JMT na ndio faida za kivitendo za uwepo wa muungano wetu.

Umeshawahi kuyafikiria madhara ya chuki inayoweza kuzaliwa baada ya muungano kuvunjika?. Busara za Mwalimu Nyerere bado zinaishi.
 
Kupitia 'no reform no election' ndipo hoja kama hizi zinaelezeka

Tundu Lissu (TAL) kaanza kulieleza suala hili kifundi sana.Ni wenye kutumia vichwa kwa usahihi na ukamilifu wanamwelewa. TAL akasema moja ya reform wanazotaka ni ugawaji wa majimbo ya uchaguzi

TAL akasema mfumo unaotumika sasa unazingatia miundo mbinu , na si population, akatoa mfano,Wapiga kura wote wa Zanzibar ni 500,000 wakiwa na majimbo 50 (yaani Wabunge 50).

Dar es Salaam peke yake in Wapiga kura Milioni 3 ikiwa na Wabunge 10. Usawa upo wapi?

TAL akatoa mfano, wastani wa jimbo la Zanzibar ni wapiga kura 11,000. Jimbo la Ubungo lina wapiga kura Laki 3. Kwa maneno mengine, Wabunge 30 wa Zanzibar wanawakilisha idadi sawa na Mbunge wa Ubungo.

TAL akauliza, imeandikwa wapi kwamba Zanzibar lazima iwe na Wabunge kadhaa! hivyo kufanya hata idadi yao kuwa na Wapiga kura 3,200 (Jimbo la Donge) Idadi ndogo kuliko Wanafunzi wa UDOM au UDSM

TAL anasema Mbunge wa Zanzibar anapata mshahara sawa na Mbunge wa Nyamagana, Ilala, au Arusha.
Kubwa Zaidi, Mbunge wa Zanzibar anapewa pesa za mfuko wa Jimbo kama yule wa Temeke au Tunduru!

Zaidi ya hapo, pesa za mfuko wa jimbo zinatoka JMT ambayo ni walipa kodi wa Tanganyika.
SMZ haina mfuko wa jimbo kwasababu Wabunge wake wanapata kutoka Dodoma.

Ndio maana TAL anasema lazima kuwe na reform za uchaguzi na muundo! hadi hapo hujamwelewa?
Huyo mhuni na Mropokaji atawapotosha hadi siku akili zinawaingia mtakuwa mnatoka Mirembe.
 
Kupitia 'no reform no election' ndipo hoja kama hizi zinaelezeka

Tundu Lissu (TAL) kaanza kulieleza suala hili kifundi sana.Ni wenye kutumia vichwa kwa usahihi na ukamilifu wanamwelewa. TAL akasema moja ya reform wanazotaka ni ugawaji wa majimbo ya uchaguzi

TAL akasema mfumo unaotumika sasa unazingatia miundo mbinu , na si population, akatoa mfano,Wapiga kura wote wa Zanzibar ni 500,000 wakiwa na majimbo 50 (yaani Wabunge 50).

Dar es Salaam peke yake in Wapiga kura Milioni 3 ikiwa na Wabunge 10. Usawa upo wapi?

TAL akatoa mfano, wastani wa jimbo la Zanzibar ni wapiga kura 11,000. Jimbo la Ubungo lina wapiga kura Laki 3. Kwa maneno mengine, Wabunge 30 wa Zanzibar wanawakilisha idadi sawa na Mbunge wa Ubungo.

TAL akauliza, imeandikwa wapi kwamba Zanzibar lazima iwe na Wabunge kadhaa! hivyo kufanya hata idadi yao kuwa na Wapiga kura 3,200 (Jimbo la Donge) Idadi ndogo kuliko Wanafunzi wa UDOM au UDSM

TAL anasema Mbunge wa Zanzibar anapata mshahara sawa na Mbunge wa Nyamagana, Ilala, au Arusha.
Kubwa Zaidi, Mbunge wa Zanzibar anapewa pesa za mfuko wa Jimbo kama yule wa Temeke au Tunduru!

Zaidi ya hapo, pesa za mfuko wa jimbo zinatoka JMT ambayo ni walipa kodi wa Tanganyika.
SMZ haina mfuko wa jimbo kwasababu Wabunge wake wanapata kutoka Dodoma.

Ndio maana TAL anasema lazima kuwe na reform za uchaguzi na muundo! hadi hapo hujamwelewa?
Inaonekana somo hili kwa Watanganyika hasa wale wa ccm ni gumu kwao.Mawazo fikirishi kwao yanayowatala ni masifu kwa viongozi.Hili jambo litatesa sana nchi yetu maana Watanganyika tumelala acha Wazanzibar wafaidi Muungano pamoja na viongozi wa ccm.
 
Kule kuungana peke yake ni faida kubwa, unajua kitu gani kinachompa jeuri Donald Trump mpaka anafukuza wamexico wakiwa na pingu miguuni na mikononi?, ni muungano wa majimbo yanayounda kitu kinachoitwa USA.
Nchi zinaungana kwasababu mahususi. Nchi zilizojaribu kuungana kwa maelezo yako hapo juu zimeishia pabaya. Tatizo si kuungana bali muundo wa Muungano unaofanya Zanzibar kuwa 'special''
Ni eneo linalowabebesha Watanganyika mzigo.

Mfano, Pesa za maendeleo kwa mkoa wa Dar es Salaam unaochangia 86% ya GDP ni ndogo kuliko zile zinazopelekwa Zanzibar! Kwanini Simiyu, Njombe au Geita ambayo ni mikoa michanga sana isipewe kipaumbele kama Zanzibar licha ya kuchangia Uchumi, Zanzibar ikichangia 0%.
Kumbuka kuwa kuna wapemba wameoa wandendeule wa kule Nyasa.
Kuna Waha wameoa Wamanyema wa DRC
Kumbuka kuwa kuna watumbatu wameoa waha wa Kigoma,
Kuna Watanzania wameoa Wakikuyu
Kumbuka kuwa kuna Wakerewe wameoa wakojani.
Kuna Wakurya wameoa Wamakonde
Hawa wote ndio nguvu kazi ya Taifa la JMT na ndio faida za kivitendo za uwepo wa muungano wetu.
Nguvu kazi haipatikani kwa kuoleana. Wazanzibar ni 1.5M , Watanganyika ni milioni 60. Ni upuuzi kudhani Muungano unasimamishwa na ndoa. Tumeoa Kenya, Musmbiji, na akina JUX wameoa Nigeria!
Umeshawahi kuyafikiria madhara ya chuki inayoweza kuzaliwa baada ya muungano kuvunjika?. Busara za Mwalimu Nyerere bado zinaishi.
Hakuna chuki! itoke wapi? Wazanzibar hawataki Muungano! waachwe warudi kuijenga Nchi yao kama ile ya Wakati wa Sultani. Wanataka iwe kama Dubai, wapewe fursa

Swali langu linabaki pale pale! Nje ya Muungano, Mtanganyika anapoteza nini! Ni swali tu
 
Kama haijabadilika sera ya CCM ni serikali mbili kuelekea moja. Hii iliwekwa hadharani lilipozuka kundi la G55. Sababu ya kuganda kwenye hatua ya serikali mbili hatuelezwi.

Labda ni mpango wa muda mrefu unaohusisha kubadilisha mchanganyiko wa wanaoishi Zanzibar.
 
Back
Top Bottom