Suala la wafiwa kuandaa chakula kwa ajili ya wanaokuja kuzika ni utaratibu wa kupigwa vita

Suala la wafiwa kuandaa chakula kwa ajili ya wanaokuja kuzika ni utaratibu wa kupigwa vita

Wewe endelea kujibana na hizo mali zako, siku ukifa tuko pale kupiga pilau na soda... dadadeeki!
Ahahhahaha daah haya bwana
Ila watu wa roho mbaya kwel.,chakula msibani it's is not a big deal...hizi ni chembechembe za roho mbaya...jaman...ebu mtoa mada fikiria vingine ila sio chakula msibani,...
Mkuu aliepatwa na tatizo ama msiba anatakiwa asaidiwe au yeye ndo asaidie watu ?

Je kwa nini kula msibani isiwe ni malipo ya kwenda kumzika ndugu yao ?
 
Ila niseme ukwel ,misaba ya saiv inaenda kisasa..zaid kuliko zaman ,nakumbuka kwenye kikundi cha mama yangu palitokea Mwana kikundi wao kufiwa na baba yake...,kilichofanyika kikundi chake kiligharamikia shuhuli za msiba kwa asilimia kubwa..ila asilimia..chache ndio anaachiwa mfiwa...,
 
Nilishatangaza nyumbani kuwa nikifiwa na mtu aliyeko ndani ya mamlaka yangu chakula ni kwa ajili ya familia tu kama kawaida na wale wageni wa mbali ambao hata bila msiba wangepikiwa na sio vinginevyo.

Mii nimependa huu ubeti... Kwa jinsi ulivyo jitoa, Ya kwamba nikifiwa! Na sio nikifa!
Nadhani ukija kuwa mkubwa na kujua majukumu ya wakubwa.... utagundua chakula wanachokula waombolezaji hakitolewi na mfiwa bali waombolezaji, ndugu, jamaa majirani na marafiki hujichangisha na wao ndio huhakikisha kinaandaliwa, kupikwa na kupakuliwa....
 
Nadhani haya majibu uliyotoa yalikuwa ni kwa ajili ya mtoa mada... Ata mimi nmechangia kama wewe! sasa sielewi huo ukubwa wa kuchangia na majukumu unaozungumzia ni upi...
Exactly... ulikuwa ujumbe wa mleta mada. Samahani kama nimekukwaza kwa kukunukuu kwa bahati mbaya
 
Uchoyo tabia mbaya, faraja inaendana na kula na majirani, ndugu na marafiki.

Mleta mada hujafiwa, ukifiwa hutatamani waondoke. Wakiondoka upweke unasumbua.

Chakula ni m*vi, ni kinyesi, siyo kitu ya kukosesha mtu usingizi.
Mwakaleli, wakija msibani, wanabeba, mahindi, maharage, viazi, mafuta n.k. mjini wanakuja na hela.

Basi hutaki kuwalisha, ukachimbe kaburi wewe, ukazike wewe, ukimaliza waje kukupa pole.

Everyday is Saturday............................... 😎
 
Mkuu chakula msibani ni mila ya kiafrika na ipo karne nyingi.

Kimsingi wafiwa wao hawapiki wao wenyewe kwa ajili ya msiba bali jamii inayo mzunguka mfiwa.

Nia ya mila hii ni kuwapunguzia wafiwa ukiwa na kuufanya msiba uwe wa jamii nzima.

Ukiitazama juujuu utafikiri msiba na kulisha waombolezaji ni jukumu la mfiwa, la hasha.

Tatizo linakuja pale mfiwa akiwa hana uhusiano mzuri na jamii inayomzunguka au hahudhurii misiba ya jamii yake.
Hapo mfiwa anaipata fresh.

Mila ya kuwapa waombolezaji chakula kabla ya mazishi ina ujumbe mzito zaidi. Kulisha watu ni kuwatakia heri ili maendeleo kimaisha yasikome, ni kama aliyefariki anawatakia heri wale waliobaki.

Huko Ulaya kuna jamaa yangu akiwa jirani na mzungu mmoja, apartment mlango huu unafuatana na mlango wake.

Kuna siku akapita jioni akitoka mishe zake akaona mlango wa jirani mzungu uko wazi na macho hayana pazia, kwenye kiti akamwona mke wa jirani yake kawasha mshumaa anaitazama picha ya mumewe huku machozi yakimtiririka.

Taratibu jamaa akaingia na kumuuliza mke wa jirani yake kulikoni?

Yule mama akamjibu kuwa mumewe amefariki mchana ule na hajui afanye nini maana amechanganyikiwa.

Huyu jamaa yangu akashituka, na akasikitika sana.

Lakini haraka akawaita waTanzania marafiki waliokuwa karibu.

Wakanunua vyakula na vinywaji na wakampa kampani yule mama hadi mazishi yalipofanyika.

Wazungu walioshiriki walikuwa wachache sana lakini waafrika walikuwa wengi.

Yule mama mfiwa kwa kweli alichangamka. Na baadaye alikiri kuwa waafrika wana moyo wa pekee duniani maana alikiri vile vile kuwa siku ile aliyomkuta akilia peke yake alikuwa akihisi kuchanganyikiwa na kutaka kujiua!

Alishukuru sana kwa kusaidia kubeba mzigo wa stress na kusema kuwepo kwao kulikuwa faraja kubwa.

Huu ni mfano ambao unaoonyesha jinsi sisi waafrika tumejaaliwa na Muumba namnaya kukabili misiba inayoleta matatizo makubwa kifikra kwa wafiwa.
Daaah, mkuu hakika wewe ni jembe. Umefafanua kwa umakini na hekima ya hali ya juu sana mzee baba. Asante sana mkuu. Hakika unautendea haki utu uzima wako.
 
Uchoyo tabia mbaya, faraja inaendana na kula na majirani, ndugu na marafiki.

Mleta mada hujafiwa, ukifiwa hutatamani waondoke. Wakiondoka upweke unasumbua.

Chakula ni m*vi, ni kinyesi, siyo kitu ya kukosesha mtu usingizi.
Mwakaleli, wakija msibani, wanabeba, mahindi, maharage, viazi, mafuta n.k. mjini wanakuja na hela.

Basi hutaki kuwalisha, ukachimbe kaburi wewe, ukazike wewe, ukimaliza waje kukupa pole.

Everyday is Saturday............................... 😎
Alaa kumbe kile chakula ni malipo ya wao kukuchimbia kaburi na kukubebea marwhemu wako sio ?
 
Jirani yetu kijana wao alifia Ughaibuni, mipango ya kusafirisha mwili ilichukua kama wiki mbili. Katika zile wikimbili masharobaro wote mtaani waliakua wanapata chai na maandazi pale msibani, wakishafungua kinywa wanakwenda kwenye mishe zao, mchana wana wahi msosi na jioni.
Daaah aisee hatari sana
 
Suala hili lipigwe vita vikali sana kwa sababu ni sherehe tu ndio inayo namna ya kupika ili waliokuja kwenye hiyo shughuli wapate kula.

Haiwezekani umefiwa na kipenzi chako halafu hapo hapo unawapikia wanaokuja kumzika wale washibe waende zao.

Wale wanaokuja kukupa pole na kuzika ndo wakupe chakula cha wewe kula kwa sababu umepatwa na msiba,umeshughulishwa na kuondoka kipenzi chako halafu inakuwaje uwaze kuwapikia wanaokuja kuzika, hiyo sio sherehe.

Mtu anatoka nyumba ya pili tu hapo halafu anataka kuja kula kwako uliyefiwa haoni haya kabisa.

Nilishatangaza nyumbani kuwa nikifiwa na mtu aliyeko ndani ya mamlaka yangu chakula ni kwa ajili ya familia tu kama kawaida na wale wageni wa mbali ambao hata bila msiba wangepikiwa na sio vinginevyo.

Ndugu wengi wakimaliza maziko wanabaki na madeni yasiyo ya lazima kwa sababu ya kutimiza utaratibu waliokuta katika jamii licha ya kuwa unawaumiza utaratibu huo lakini wamo tu.

Mfiwa kupika chakula ni sawa na mwenye sherehe kupika chakula

Kama kweli wameguswa na msiba wako wao ndio wakuletee chakula wewe uliyefiwa.

NB ; kwa zile ada ambazo wanaokuja kuzika ndo huwa wanakuja na chakula na pesa za michango pasi na kuwatia uzito wafiwa basi ada hii haihusiani na mada yangu na ndio inavyotakiwa.
Mkuu, mimi binafsi ninadhani ulipaswa kuhimiza zaidi watu kuchangia fedha na chakula katika changamoto hii ya dharura ya msiba na sio kuweka msimamo mkali wa kugoma kuwapa chakula waombolezaji au kuwapa chakula kwa kuwabagua kuwa huyu ni wa mbali na yula ni wa karibu.

Ninadhani una jambo zuri sana la kuzungumza ila umeliongelea kwa namna ambayo sio sahihi.
 
Hata sikuelewi unasema nini ndugu.
Umesema hujisikii vizuri kuona wafiwa wakigharamia chakula kwa waombolezaji, kwa hiyo nilikuwa naongea jinsi waombolezaji wanaweza kutoa michango ya fedha au vitu kama namna ya kufariji wafiwa
 
Amen mkuu.
Nafsi zote zinapita njia hiyo, kuagana vema ni ubinadamu.
Hakika njia yetu ni moja mkuu na chakula kwa mgeni ni sehemu ya utamaduni wetu sisi waafrika. Mgeni akija nyumbani kama sio kumpa chakula basi atakunywa soda au maji. Hivyo ndivyo tulivyokuzwa na hiyo ndio desturi yetu sisi waafrika.

Mimi ninaona huyu ndugu yetu safuher alipaswa kusisitiza watu kutoa michango katika misiba kadri ya vipato vyao na sio kubagua utoaji wa huduma ya chakula.

Michango ya msiba ndio ilipaswa kuwa dhima kuu ya mada hii.
 
Mchango tunachanga wenyewe. Mfiwa ww ni kuloloma tu, kikiiva unaletewa. Kupika tunapika wenyewe tatizo liko wapi?
Au huko pemba mfiwa ndio anawajibika kila idara?
 
Mchango umechangwa laki tatu

Gharama za chakula kwa wafiwa laki nne.

Ni sawa ndugu wa marehemu umewatia hasara ya laki moja nzima,bado ni gharama tu.

Ikiwa majirani watawachangia wafiwa haina shida.
Hiyo familia inaonekana ni ya Hali ya chini Sana au haina ndugu ambao wako tayari kubebana. Hiwezi ukawa mtu wa karibu na marehemu either rafiki au ndugu na kipato unacho ukaruhusu aibu ya aina hii. Mfiwa anatakiwa afarijiwe na sehemu ya kumfariji ni kuubeba msiba wake kwa mikono miwili.
 
Hakika njia yetu ni moja mkuu na chakula kwa mgeni ni sehemu ya utamaduni wetu sisi waafrika. Mgeni akija nyumbani kama sio kumpa chakula basi atakunywa soda au maji. Hivyo ndivyo tulivyokuzwa na hiyo ndio desturi yetu sisi waafrika.

Mimi ninaona huyu ndugu yetu safuher alipaswa kusisitiza watu kutoa michango katika misiba kadri ya vipato vyao na sio kubagua utoaji wa huduma ya chakula.

Michango ya msiba ndio ilipaswa kuwa dhima kuu ya mada hii.
Hujasoma mada yangu ukaielewa,umesoma coment ambazo nazo nyingi hazijaelewa nani kakusudiwa.

Rejeea uzi pengine ukaelewa makusudio.
 
Umesema hujisikii vizuri kuona wafiwa wakigharamia chakula kwa waombolezaji, kwa hiyo nilikuwa naongea jinsi waombolezaji wanaweza kutoa michango ya fedha au vitu kama namna ya kufariji wafiwa
Ni kweli hilo lipo,ila isiwe kuwa nakupa alfu kumi mfiwa alafu wewe unanipikia chakula cha alfu hamsini,hapo hujanifariji kwa alfu kumi yako,umeniongezea mzigo tu.

Zipo jamii hufanya hivyo.
 
Back
Top Bottom