Sukari madukani hamna, tatizo ni nini wakati tayari kuna bei elekezi toka Serikalini?

Sukari madukani hamna, tatizo ni nini wakati tayari kuna bei elekezi toka Serikalini?

Wakuu Salaam;

Nimezunguka madukani kutafuta sukari ili nipate chai angalau nichangamke kipindi hiki cha mvua maana baridi ipo kweli huku duniani niliko, sasa kila duka naloingia naambiwa sukari hamna!

Nimejaribu kwenda hadi maeneo ya stendi lakini bado sukari najibiwa hamna.

Nimeamua ninywe chai na malimao tu maana yenyewe yataifanya hiyo chai hata iwe na ladha. Malimao yenyewe saivi kuyapata ni shughuli haswa mana watu wananunua wakachanganye kwenye mvukizo ili wajifukize.

Nimejaribu kuwauliza watu baadhi wanadai sukari hakuna kila sehemu na watu wameficha stock ila hawana uhakika kama kweli wameficha. Sasa tatizo ni nini wakati juzi limetoka tamko lenye bei elekezi ya sukari?

Kuna mmoja kanidokeza kua, wale waliokua na sukari kabla tamko la bei elekezi halijatoka, waliendelea kuuza kwa bei ile ile ya juu yani 3500. Sasa wakikutwa wanauza bei hiyo au mteja akisema kauziwa kwa bei hiyo, muuzaji anakamatwa.

Kwanini ifikie hali hii sukari iadimike ghafla? Au kweli sukari hamna?
Au wafanya biashara wanaficha sukari?

Kama vipi serikali ije na tathmini mpya juu ya hili swala.

Huko ulipo vipi sukari inapatikana kama kawaida au nako hamna kama maeneo ya huku?

Na vipi kuhusu bei ya sukari huko ulipo? Au unatumia malimao kama mimi?
Malimao bora kuliko sukari. Tafuta asali, itakuwa tamu zaidi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wasalaam,

Nipo maeneo ya pwani muda huu, mlandizi, bado natafuta sukari kila duka napita wanasema hawana sukari.

Najiuliza tu kulikoni? Huko kwenu vipi inapatikana nije?

Tuendelee kuchapa kazi huku tukichukua tahadhali, tuepukane na covid-19.

Mungu ibariki Tanzania


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wenye maduka wamegoma kuiuza....wameona ni hasara....unauziwa bei kubwa hlf serikali inaleta bei elekezi.....hlf kinachokera zaidi wateja wako wanakuchoma

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii nchi kila kitu ni cha kubahatisha.

Kwa nini kila mwaka hua inafikia sukari hakuna? Yaani hua wahusika wako wapi hadi inatokea sukari inakosa kabisa?
 
Hii nchi kila kitu ni cha kubahatisha.

Kwa nini kila mwaka hua inafikia sukari hakuna? Yaani hua wahusika wako wapi hadi inatokea sukari inakosa kabisa?
Sukari ipo shida ni serikal kuigilia soko hulia. Wao walitakiwa kupunguza tax kwenye sukar ili bei ishuke. Yani yenyewe inachukua chake alafu bei ishuke?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
sukari ipo ila wenye maduka wanaona kwa bei elekezi watakula hasara, na wateja wanawachoma... Mimi nilienda dukani nunua sukari mwenye duka akaniambia siuzi ila kwakuwa nakufahamu nitakuuzia wewe tu kwa bei isiyo elekezi maana nikiuza chini nitakula hasara .
 
Kwa tusiojulikana imekula kwetu daah!
sukari ipo ila wenye maduka wanaona kwa bei elekezi watakula hasara, na wateja wanawachoma... Mimi nilienda dukani nunua sukari mwenye duka akaniambia siuzi ila kwakuwa nakufahamu nitakuuzia wewe tu kwa bei isiyo elekezi maana nikiuza chini nitakula hasara .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wauzaji wa rejareja wananunua mfuko wa sukari wa 50kg laki na nusu.. wakiuza kwa bei elekezi ya tsh. 2600 kwa dsm watapata sh. 130,000/= hivyo atakua na hasara ya elfu ishirini bado gharama alizozitumia kwenye usafiri. Hili limekaaje wadau coz wafanya biashara wengi wamegoma kuuza sukari kwa kuhofia faini ya laki tano endapo atakamatwa akiuza sukari tofauti na bei elekezi?
 
Bunju ipo ila bei ya chini kabisa ni 3300 kwa maduka machache ila mengine 3500
 
Wauzaji wa rejareja wananunua mfuko wa sukari wa 50kg laki na nusu.. wakiuza kwa bei elekezi ya tsh. 2600 kwa dsm watapata sh. 130,000/= hivyo atakua na hasara ya elfu ishirini bado gharama alizozitumia kwenye usafiri. Hili limekaaje wadau coz wafanya biashara wengi wamegoma kuuza sukari kwa kuhofia faini ya laki tano endapo atakamatwa akiuza sukari tofauti na bei elekezi?
Tunarudishwa kwenye zama za Mchonga meno za chai na uji bila sukari
 
Tatzo wabongo sio waelewa....yan wanmkandamiza muuzaji kwa maneno ya mwanasiasa wa kwenye tv....!!mimi sukari ninayo....zote....lkn inanibidi kutoziuza kwa ajili ya watu wanavyokamatwa...!!za pakti ndo angalau hua nauza kulingana na mtu...!!ila ya kupima nmeiweka pemben kwanza....mpaka tuelewane
Tufanyeje sasa? Na huu mwezi sasa ndugu zetu waislam wamefunga

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom