Sura ya Mungu kupitia Wajapani

Ha haha...nacheka kama mazuri vile.

Yah, eti mtu anaenda kwa mwanasaikoloji,kwa black tunajijua wenyewe.
 
Sasa hayupo au kuna contradictions kwenye maelezo yenye kumuhusu huyo Mungu? Hivi mimi nikisema rais wa Tanzania Samia suluhu ni mnene na hapo hapo ni mwembamba je, ndio itakuwa na maana Tanzania hakuna rais kwa sababu ya hiyo contradiction au nitakuwa nimetoa maelezo yenye contradiction kumuhusu rais wa Tanzania Samia suluhu?
 
Blacks tena tulioko Afrika tunadunda. Kuna vitu mtu akikwambia vinamsumbua badala ya kumpa ushauri unaishia kumwambia acha ujinga wewe na hilo ni suala la kuwaza...😄
Tunashuhudia mengi sana,tukipewa roho za hao wajapani na wakorea hats kwa lisaa moja,nusu ya waafrika watakua wamejinyonga , maana it's hell here.
 
Itabidi u define mnene ni nini na mwembamba ni nini kwanza.

Inawezekana rais akawa mnene na mwembamba kama definitions zako za unene na wembamba zimeingiliana sehemu fulani.

Ila, ukisema kuna pembetatu ambayo pia ni duara katika Euclidean geometry, hapo tutajua kuna contradiction inayofanya pembetatu duara hiyo iwe ni kitu cha kufikirika tu na haiwezi kuwapo katika uhalisia.

Dhana ya kuwepo Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote, aliyeumba ulimwengu unaoweza kuwa na mabaya, licha ya kuweza kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani kuwepo, hayafikiriki, na hayapo, ina internal contradiction ile ile iliyopo kwenye dhana ya pembetatu duara kuweza kuwepo.

Uwepo wa Mungu huyu ni sawasawa na uwepo wa "pembetatu duara".

Ni wazo la kufikirika tu, ambalo halipo nje ya mawazo na hadithi.

Mungu huyu, ni kitu cha kufikirika tu, hayupo katika uhalisia.
 
Maji taka yao ya mifereji ni masafi saana kama ya kunywa hadi kuna samaki
 
Iroiro ossewani narimashita
 
What is the worst about that?
Wewe mwenye dini una tofauti gani na wao wasio na dini?
Umewahi kusikia Japan wanasiasa wanapigwa risasi, wanapotea au wanapewa kesi za michongo n.k?
We nae! hata Marekani wanasiasa hawapigwi risasi hawapotei na kupewa kesi za mchongo ila raia hasa weusi wanapigwa sana risasi huko, kwahiyo tutasema Marekani ni bora kwa sababu wanasiasa hawapigwi risasi?
 
Unene kwa maana ya kuwa na mwili mkubwa(bonge) na wembamba kwa maana ya kuwa na mwili mdogo(kimbaumbau).

Haya nikisema rais wa Tanzania Samia saluhu ni mnene na hapo hapo ni mwembamba hiyo contradiction itakuwa na maana Tanzania hakuna rais Samia suluhu?
 
Bado huja define unene ni nini na wembamba ni nini.

Kwa maana definition yako ni subjective si empirically logical.

Kwa mfano.

Definition empirical and logical itakuambia mtu mnene ana kiuno cha ukubwa gani, ratio ya body mass index inayolinganisha urefu na uzito gani, etc. Facts and figures. Unen3 na wembambq unakuwa na mutuql 3xclusivity. Mn3ne hawezi kuwa mwembamba na mwembambq hawezinkuwa mnene.

Hapo mtu kuwa mnene na mwembamba at the same time ni contradiction.

Ni sawa na mtu kuwa sehemu mbili physically kwa wakati mmoja.

Hiyo definition ya unene ni kuwa na mwili mkubwa haina mashiko, kwa sababu, mwili huohuo kwa mtu mmoja utaonekana mkubwa, kwa mtu mwingine utaonekana mdogo.

Rais Kagame wa Rwanda anaonekana mrefu kwa watu wengi. Lakini kuna picha alipiga kwenye harusi ya binti yake inaonesha katika familia yake yeye kaonekana ndiye mfupi kuliko wote. Sasa hapo tunahitaji empirical and unit standards kujua nani mrefu na nani mfupi. Kwa sababu wewe unaweza kusema Rais Kagame ni mrefu, kwa sababu wewe ni mfupi, lakini, binti yake na mkewe wakabisha wakasema huyu mfupi.

Your definition, up to now, is rather subjective.
 
Unaandika maelezo marefu uku ukijaribu kujisahaukisha swali langu.
Ninakukumbusha tena na tena. Nimekuuliza tena ikiwa unaamini kuwa Mungu yupo ama hayupo?. Nijibu tuendelee.
Sidhani kama swaliako ni swali la msingi. Yeye kaomba utoe ushahidi wa Mungu kuwepo, wewe unamuuliza kama anaamini Mungu yupo au hayupo, this is very irrelevant.
 
Chief, unakwama wapi hasa!!! Unapata nafasi ya kuandika maelezo marefu na mazuri ila unashindwa kujibu swali langu fupi na dogo, shida nini hasa?.

Jibu ikiwa Mungu YUPO AMA HAYUPO then tuendelee.
Wewe uliyemtaja Mungu umeambiwa uthibitishe uwepo wa Mungu. Yeye kasema hataki mambo ya kuamini bali anataka fact. Sasa unapomuuliza kama anaamini uwepo wa Mungu au haamini sijui umelenga nini kama ameshasema hataki mambo ya kuamini.
 
Yani kung'ang'ania kujibizana nami ung'ang'anie wewe, halafu lawama za kukupotezea muda unipe mimi?

Kwani nimekulazimisha kujadiliana nami hapa?
Kiranga my role model

Baada ya kumsoma Fyodor Dostoevsky katika vitabu vyake ya The Brothers Karamazov,hasa katika kitabu kidogo cha the Grand Inquistor katika kitabu hiko hiko cha the Brothers Karamazov aisee nilijifunza mambo mengi sana

Katika kitabu hiko kuna majibizano ya kuhusu Mungu kati ya Ivan na Father

Nilijifunza mengi sana

Nashukuru nilipokuja humu nikakutana na maongezi kama yale humu jf kupitia wewe

Siamini uwepo wa Mungu huyu wa dini hizi za Ukristo na Uislamu
 
Kwa hii comment yako hujathibitisha lolote zaidi kurudia yaleyale. Una ushahidi uli kuwa ulimwengu umeumbwa na Mungu?
 
Kumbe wako tofauti sana na majirani zao wachina...?
 
Nyie waamini mna matatizo makubwa mno, mara mwasema Hafananishwi na chochote ila hapa Afananishwa na Wajapan then Caucasians. Sasa mpaka hapo huoni kwamba huyo Mungu hana sifa ya kuwa wetu!?
 
Mkuu kwanini usithibitishe uwepo wa Mungu badala ya kupoteza muda wako kutafuta jina lake?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…