Uchaguzi 2020 Swali fikirishi: Je, kuna mtu timamu kiakili atamchagua John Magufuli licha ya ugumu wa maisha, uonevu kwa wafanyabiashara, wakulima na wafanyakazi?

Exactly yaani Mimi mwenyezi Mungu hajanipa akili za kuchezea kiasi cha kumchagua mtu aliyeshindwa kuajiri miaka mitano , kupandisha mishahara , madaraja , aliyesababisha watu kupotea ,kutekwa ,kuuwawa , aliyedhulumu hell za wastaafu , rambirambi za tetemeko la Kagera , aliyebomolea watu nyumba zao , aliyefunga watu kwa kuwaonea aliyefunga watumishi kisa vyeti feki huku mwenywe ana feki , yaani yapo mengi sana niishie happy kwa uchache .
 
Kiukweli ukiachana na wapiga mayowee wanaoganga njaa ili japo wateuliwe wapate ajira sioni kama kuna mpumbavu atamchagua huyu jamaa aliyezamisha nchi kwenye machafuko na umaskini mkubwa.
 
Hakuna mtu wa kuchagua ccm tz....... Tume ndo itamchagua
 
Lissu mzee wa MIGA huwezi kumfananisha na aliyetibiwa St Thomas.
Ukipata nafasi ya kukutana Magufuli muulize MIGA ni nini? Kisha muulize kwanini hatumii mkataba wa twiga kujipatia ujiko wa kumpatia kura
 
Ukipata nafasi ya kukutana Magufuli muulize MIGA ni nini? Kisha muulize kwanini hatumii mkataba wa twiga kujipatia ujiko wa kumpatia kura
Hahitaji kutumia mkataba wa Twiga kuombea kura. Ushujaa wake ni mkataba tosha wa kumpa kura.

Nenda katafute taarifa duniani ni wapi ambapo Makontena ya mchanga yamezuiwa yasipande melini kwa Amri ya rais.
 
Hahitaji kutumia mkataba wa Twiga kuombea kura. Ushujaa wake ni mkataba tosha wa kumpa kura.

Nenda katafute taarifa duniani ni wapi ambapo Makontena ya mchanga yamezuiwa yasipande melini kwa Amri ya rais.
Huo ndo ushujaa? Yaani mtu kufanya kazi na kutumia mamlaka aliyopewa ni ushujaa?mkuu upo serious au wewe ni miongoni mwa wale wasio na akili?
 
Kura atapata chache sana huenda hata zile za 2015 zikawa nyingi, ila shida ni mauzauza yanayofanyika nyuma ya pazia, hapa ndipo panatakiwa kupamulika kwa tochi ya mwanga mkali na kupambana wote na aina yoyote ya uovu huo! Tunamuomba Mungu akawanyong'onyeze kabisa walio kazini kuandaa mipango yoyote kinyume na maamuzi ya wananchi!
 
kazi ni moja kuhakikisha ushindi unakua wa kishindo maaaana kama ni kushinda ashashinda
 
Huo ndo ushujaa? Yaani mtu kufanya kazi na kutumia mamlaka aliyopewa ni ushujaa?mkuu upo serious au wewe ni miongoni mwa wale wasio na akili?
Wangapi wanapewa mamlaka makubwa na wanaishia kuwa vibaraka wa mipango ya mataifa makubwa ya Ulaya na marekani?.
 
Kwakweli ni wendawazimu kumpigia
Tena kura mtu huyu
 
SASA IKIWA NAWE LICHA YA KUWA VICTIM WA UKANDAMIZAJI WA KUJIELEZA NA KUHOJI UTAMCHAGUA JOHN MAGUFULI RAIS MWENYE KILA DALILI ZA UDIKTETA UNATUVUNJA MOYO.
Kwanza pole!, pili dalili za udikiteta ni jambo moja, na Udikteta halisi ni jambo jingine!.
Kwa Tanzania mahali tulipofikia, hadi kuwa shamba la bibi, tulihitaji mtu kama Magufuli, na matokeo tumeyaona, ndani ya miaka 5, tumeuaga umasikini na kuwa nchi ya uchumi wa kati!.

Tukumpa mitano mingine, tunakwenda kuwa nchi ya uchumi wa kati mkubwa, na tukibadili katiba aendelee tuu,Tanzania tunakwenda kuwa nchi ya uchumi mkubwa, nchi tajiri, a donor country.

Fuatilieni utawala wa Tiger Nations, bila udikiteta, zisinge toka!. Sio kila udikiteta ni udikiteta mbaya, au udikiteta katili, kuna udikiteta wa kizalendo unaitwa, benevolence dictatorship!, hivyo rais Magufuli ni dikiteta Mzalendo anayefanya udikiteta kwa nia njema kulikomboa taifa!.

Magufuli ni Dikiteta!, Tanzania Ilihitaji Dikiteta, Tumempata!. Atakayeleta Fyoko, Ataisoma Namba!

P
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…