Swali Fyatu: Kwani Tatizo Gani Wameweza Kulitatua Likaisha?

Swali Fyatu: Kwani Tatizo Gani Wameweza Kulitatua Likaisha?

Na. M. M. Mwanakijiji

Kuna mambo mengine yakijirudia unaweza ukafikiria bado uko ndotoni. Maana kuna baadhi ya ndoto zinajirudia rudia hata kama huzitaki. Wengine wanaita "jinamizi". Zinakuja zinatisha halafu unashtuka unasema "duh hii ndoto hii!". Unarudi kulala unafikiri itapita; kumbe ukisinzia tu jinamizi linaanzia pale lilipoishia!

Fikiria mambo ya Bodi ya Mikopo unaweza ukafikiria hili tatizo lingekuwa limeisha zaidi ya miaka ishirini toka tulipolivalia njuga suala la vijana wetu kule Ukraine enzi hizo. Suala la Sukari ni hivyo hivyo, toka miaka ya tisini bado tunazunguka nalo tu; kila baada ya muda linaibuka tena! Hapa naogopa hata kutaja suala la umeme. Yaani, unaweza kuamka asubuhi ukafikiria uko mwaka 1996! Sijagusa suala la uhaba wa fedha za kigeni, naogopa kuuliza kuchelewesha mishahara, nashindwa kuzungumzia mafao ya wazee/wastaafu, na hapa hatujataja suala la ajira kwa wahitimu.

Yaani, ukisoma sasa kuhusu "tuko mbioni", "serikali inajipanga", "tuko tayari kuanza kutekeleza", "tumetoa siku kadhaa hili liwe limeisha".. yaani, unaweza kukuta watu wanapiga makofi wakisahau kumbe baba zao na mama zao na wenyewe walipiga makofi miaka thelathini iliyopita kushangilia matamshi yale yale yaliyotolewa na watu wale wale kwenye matatizo yale yale!

Watanzania ni lazima waamue kama watu wale wale, wenye mipango ile ile, wakikabili matatizo yale yale kwa namna ile ile wanastahili kupewa nafasi zile zile za kuongoza tena! Nje ya hapo ni lazima tujiulize labda kuna vizazi vitaendelea kutushangaa sana kwanini tumeendelea kuwa vile vile! Kwani, matatizo gani wamewahi kuyatatua yakaisha kabisa? Yaani, watakuja tena kuomba miaka mitano mingine na tena wana ujasiri wa kuimba "CCM ni ile ile!"

Kwanini matokeo yasiwe vile vile?
Halafu ajabu ni kuwa watatatumia hizi kero kama ahadi ya kutaka kutushawishi tuwape kura.

Yaani utasikia tutashughulikia kero ya umeme. Ajira elimu n.k so mtupe kura.😂😂

Nadhani wapuuzi zaidi ni sisi wenyewe watanganyika.
 
Unakela sana na tabia za dini humu kwenye siasa.
Mumeanza kwa kisingizio cha demokrasia. Kama CCM ndio hiyo hiyo haijabadilika. Huyu MMM wakati wa Marehemu Magu alikua muungaji mkono mkubwa. Swali anasimamia wapi? Wakati wa Mkapa akitupa pongezi nyingi lkn alipokuja Jk kawa mkosoaji mkubwa.
CCM ndio hiyo
 
Ujinga mwingine tulio nao ni kuamini matamko ya majukwaani, tumbua tumbua ya barabarani ndio suluhisho na si kuweka mifumo inayohakikisha uwajibikaji.
 
Ccm ni ile ile na vioja vyao ni vile vile.
Baba alikuwa mwizi akamrithisha mtoto madaraka.
Mtoto anapambana kuwa zaidi ya baba. Yaani kuwa mwizi zaidi ya baba yake. Ndicho alichojifunza kwa baba yake.
Tatizo lililopo hapa Tanzania CCM wanacheza pande zote.
Wao wenyewe ndio watawala vilevile wao wenyewe ndio wapinzani.
Watanzania wapo tayari kwa mabadiliko ila hakuna kwa kubadilikia.
Mzee Mwanakijiji, na mzee@Dr slaa rudini kwenye siasa active mtuokoe, Nchi inazidi kupotea hii.
Kuna kizazi hiki cha 2000's kilichonyimwa elimu ni hatari zaidi.
 
Ccm ni ile ile na vioja vyao ni vile vile.
Baba alikuwa mwizi akamrithisha mtoto madaraka.
Mtoto anapambana kuwa zaidi ya baba. Yaani kuwa mwizi zaidi ya baba yake. Ndicho alichojifunza kwa baba yake.
Tatizo lililopo hapa Tanzania CCM wanacheza pande zote.
Wao wenyewe ndio watawala vilevile wao wenyewe ndio wapinzani.
Watanzania wapo tayari kwa mabadiliko ila hakuna kwa kubadilikia.
Mzee Mwanakijiji, @Dr Slaa rudini kwenye siasa active mtuokoe, Nchi inazidi kupotea hii.
Kuna kizazi hiki cha 2000's kilichonyimwa elimu ni hatari zaidi.

Yaani bado unaamini Dr Slaa aje atuokoe. Ndo haya haya anayosema mleta mada.

Muda mwingine ilikuwa ni heri kuunga mkono mabadiliko maana ilikuwa nafasi pekee ya kuanza kujenga uwajibikaji. Kukosea ukiwa umefanya mabadiliko ni nafuu kuliko kuogopa kufanya.
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Kuna mambo mengine yakijirudia unaweza ukafikiria bado uko ndotoni. Maana kuna baadhi ya ndoto zinajirudia rudia hata kama huzitaki. Wengine wanaita "jinamizi". Zinakuja zinatisha halafu unashtuka unasema "duh hii ndoto hii!". Unarudi kulala unafikiri itapita; kumbe ukisinzia tu jinamizi linaanzia pale lilipoishia!

Fikiria mambo ya Bodi ya Mikopo unaweza ukafikiria hili tatizo lingekuwa limeisha zaidi ya miaka ishirini toka tulipolivalia njuga suala la vijana wetu kule Ukraine enzi hizo. Suala la Sukari ni hivyo hivyo, toka miaka ya tisini bado tunazunguka nalo tu; kila baada ya muda linaibuka tena! Hapa naogopa hata kutaja suala la umeme. Yaani, unaweza kuamka asubuhi ukafikiria uko mwaka 1996! Sijagusa suala la uhaba wa fedha za kigeni, naogopa kuuliza kuchelewesha mishahara, nashindwa kuzungumzia mafao ya wazee/wastaafu, na hapa hatujataja suala la ajira kwa wahitimu.

Yaani, ukisoma sasa kuhusu "tuko mbioni", "serikali inajipanga", "tuko tayari kuanza kutekeleza", "tumetoa siku kadhaa hili liwe limeisha".. yaani, unaweza kukuta watu wanapiga makofi wakisahau kumbe baba zao na mama zao na wenyewe walipiga makofi miaka thelathini iliyopita kushangilia matamshi yale yale yaliyotolewa na watu wale wale kwenye matatizo yale yale!

Watanzania ni lazima waamue kama watu wale wale, wenye mipango ile ile, wakikabili matatizo yale yale kwa namna ile ile wanastahili kupewa nafasi zile zile za kuongoza tena! Nje ya hapo ni lazima tujiulize labda kuna vizazi vitaendelea kutushangaa sana kwanini tumeendelea kuwa vile vile! Kwani, matatizo gani wamewahi kuyatatua yakaisha kabisa? Yaani, watakuja tena kuomba miaka mitano mingine na tena wana ujasiri wa kuimba "CCM ni ile ile!"

Kwanini matokeo yasiwe vile vile?
Umeongea vizuri sana

Unadhani tatizo la Tanzania Au Africa ni vyama vya siasa au siasa?

Tatizo ni watu kama mimi na wewe ambao tunadhani siasa ndio solution ya umasikini wetu

The day we drop huu ubwege we western democracy through politicians ndio siku tutabadili bara letu

Wao walibadili mabara yao kabla ya kuja na hizi propaganda na Bendera za vyama

They started with sovereignty before parties

Btw, hata neno party tu may mean anything
 
Yaani bado unaamini Dr Slaa aje atuokoe. Ndo haya haya anayosema mleta mada.

Muda mwingine ilikuwa ni heri kuunga mkono mabadiliko maana ilikuwa nafasi pekee ya kuanza kujenga uwajibikaji. Kukosea ukiwa umefanya mabadiliko ni nafuu kuliko kuogopa kufanya.
Yale yale tu mkuu cha msingi tujisahihishe tulipokosea.
Ukinishangaa mimi kuendelea kumuamini Dr slaa, nami pia ntakushangaa wewe kuendelea kumuamini Mbowe.
 
Umeongea vizuri sana

Unadhani tatizo la Tanzania Au Africa ni vyama vya siasa au siasa?

Tatizo ni watu kama mimi na wewe ambao tunadhani siasa ndio solution ya umasikini wetu

The day we drop huu ubwege we western democracy through politicians ndio siku tutabadili bara letu

Wao walibadili mabara yao kabla ya kuja na hizi propaganda na Bendera za vyama

They started with sovereignty before parties

Btw, hata neno party tu may mean anything
Upo sahihi kabisa na hili ndio tatizo la kudeal nalo.
Na njia yakufika huko ni labda jeshi kuthubutu kuwa wazalendo zaidi.
Kufika huko ni ngumu, lazima uwe jiwe zaidi ya Magufuli.
 
Na alikua timu ileile… right?

When judging… balance

Mnajichanganya sana mjue
Timu Ile ile ila wachezaji tofauti. Wachezaji wengi wa sasa walikuwa benchi na tulianza kuona matokea chanya.
Huyu kocha mpya kabadilisha first eleven yote ya Magu.
Beki hakuna kipa hakuna ni mwendo wa kufungwa tu. Fowadi nazo hazishbulii kabisa.
 
Timu Ile ile ila wachezaji tofauti. Wachezaji wengi wa sasa walikuwa benchi na tulianza kuona matokea chanya.
Huyu kocha mpya kabadilisha first eleven yote ya Magu.
Beki hakuna kipa hakuna ni mwendo wa kufungwa tu. Fowadi nazo hazishbulii kabisa.
Wachezaji walewale

Usichanganye - kama focus ni siasa, basi focus kwenye siasa… wabunge, wenyeviti wa chama, makatibu, watendaji, na nafasi zote za siasa ni walewale

Tatizo mnajipiga chenga wenyewe… hamko clear mnataka nini

Change iliyopo haizidi hata 10%

We need to go deeper kama Kweli tuko serious

Or else kelele ni justification ya kushindwa kutoa solutions na kuanza kulaumu wenhkne

Mtikila alikua ahead of his generation
 
Back
Top Bottom