Swali Fyatu la Mwezi: Wakimpa Sifa Zake, Watapunguza za Kwao?

Swali Fyatu la Mwezi: Wakimpa Sifa Zake, Watapunguza za Kwao?

Mjadala sio faida na hasara za kuhamia Dodoma, bali watu kujivisha sifa wasizostahili kabisa. Bora wangesema ni white elephant za Magufuli tuelewe kuwa wanamalizia miradi kwavile hawana jinsi.
.....swali lipo Juu kabisa na tumetafuniwa hata majibu.
Lakini, baadhi wameamua kupuuza kwa makusudi au kwa msukumo huo huo waliokuwa na hao hao "Wanao pungukiwa"

.... Kuna maelezo tosha tu kujibu kifyatu tu ikibidi angalau kupata 65% bila ya kuumiza kichwa!

Watapungukiwa na nini?

Hatahivyo, kiufyatu tu, swali hili linawezekana lishajibiwa na aliyekuwa Spika aliyejiuzulu Bwana Job Ndugai.
 
Mwisho wa siku hizo hela zilizotumika/zinazotumika kujengea hiyo moundombinu, ni kodi za Watanzania! Ni mikopo ambayo italipwa na watanzania wote!

Na siyo hao wanasiasa unaotaka wapewe acknowlegment.
Amen
 
Una uhakika hawakufanya? Na kama wangekuwa hawajafanya chochote, hii nchi ingekuwepo hapa tulipo?

Unayafahamu mambo yote aliyoyafanya Nyerere tangu alipoichukua nchi kutoka kwa Wakoloni?

Tatizo mnalazimisha wote tuamini kama huyo JPM wenu alikuwa ni the best, kumbe wengine tunamuona alikuwa ni the worst.
Walifanya lakini ukilinganisha na awamu ya tano walifanya kidoogo sana.

Tatizo CCM ni laanifu ndo maana inaua hata wanachama wake wanaopinga ufisadi
 
View attachment 2642893
Na. M. M. Mwanakijiji

Kuna watu ambao tunawakumbuka kwa umahiri na weledi katika kazi, vipaji au matendo yao. Michael Jordan aliichezea timu ya mpira wa vikapu ya Chicago Bulls na kujionesha kuwa ni mchezaji bora Zaidi wa mchezo huo duniani. Wengi wanalijua jina la Michael Jordan lakini ni wachache wanaweza kukutajia majina ya wachezaji wenzake wanne waliokuwa wanaunda kikosi cha kwanza. Hili pia ni kweli kuhusu mchezaji bora Zaidi wa soka duniani Pele. Wengi wanalijua na kukumbuka jinsi Pele alivyoongoza Brazili kwenye makombe ya dunia. Ni wachache sana wanaweza kukutajia wachezaji kumi wengine walioshinda na Pele kombe la dunia mara ya mwisho.

Hata hapa Tanzania kuna watu wanakumbukwa kwa umahiri wao lakini ni wachache wanaweza kukutajia majina ya watu wengine kwenye vikosi vyao. Mbaraka Mwinshehe, Marijan Rajabu, au hata Remmy Ongara. Tunajua nyimbo zao, tumewahi kuzisikia lakini tukiuliza wana bendi wenzao ni kina nani ni wachache wanaweza kutaja hata majina mawili.

Ukweli ni kuwa kuna watu wanatokea katika fani mbalimbali na wanakuwa vinara na bora kuliko wengine. Tunapowataja hawa wengine na kuwasifia haina maana tunadharau mchango wa wengine. Ukimtaja Lionel Messi kwa mfano au Cristiano Ronaldo mara moja watu watajua unawazungumzia kina nani lakini ni wachache wanaweza kukutajia majina ya wachezaji wenzao kwenye zile timu zilizokuza majina yao. Unaposema sifa za vinara haina maana unafuta sifa au unadharau sifa za wengine!

Juzi wakati wa uzinduzi wa Ikulu mpya ya Dodoma ambayo sasa inaifanya Ikulu ya Dar-es-Salaam kuwa Ikulu Ndogo kuna watu walisimama na kumwaga sifa mbalimbali. Niliamka mapema (huku niliko) niweze kushuhudia kama watakuwa na ujasiri wa kumtaja mchezaji kinara aliyewafanya wawepo pale siku ile. Bahati mbaya karibu kila aliyesimama ama alinyemelea kulitaja jina la mchezaji huyo bora au alilitaja kama kulipita tu kuwa “alikuwa ni mmoja wa timu”.

Jina la Joseph Pombe Magufuli, kinara wa marais wote waliowahi kutokea Tanzania, shujaa wa uthubutu, na mbunifu wa maono ya maendeleo ya haraka lilitajwa kana kwamba na yeye alikuwa na mchango kama wengine tu. Yote hiyo ilifanywa kwa makusudi kabisa wakijaribu kufifisha jina hilo na hawakutaka kusikia makofi na shangwe ambazo wangelitendea haki zingesikaka. Waliogopa kuona kuwa yumkini huyu bwana akiwa amelala kaburini milele kuna watu wanamkumbuka na kummiss!

Wanatuambia kuwa mpango wa kuhamishia Ikulu ulianza toka miaka ya sitini na hatimaye maamuzi yakachukuliwa na taratibu hatua mbalimbali zilianza kuchukuliwa ili kuhamia taratibu Dodoma. Jakaya Kikwete akatupa stori kuwa aliagiza watu waende Malaysia waone mambo yanavyofanyika huko na sisi tuje kuiga. Sikumbuki kwa miaka kumi ya Kikwete kama kuna siku ulifanyika mjadala hata mmoja Bungeni wa jinsi ya kuhamia Dodoma na kujenga Ikulu Dodoma na kuwa aliwaambia Watanzania kuwa ametuma iende Malaysia! Sijui hiyo timu iliongozwa nan ani! Lakini tunakubali.

Tunaambiwa kuwa viongozi wote waliotangulia wamekuwa wakifanya kama kupokezana vijiti kuliongoza taifa. Wanasahau kuwa Magufuli hakumwachia Samia kijiti; kamwachia gogo! Ni wazi Rais Samia anajitahidi kwa uwezo wake wote kuonekana anaweza kukamilisha miradi hii yote; na kweli tunaona ikimalizwa. Lakini ndugu zetu hawa wanataka tuamine kuwa kama Magufuli asingefanya alivyofanya leo tungekuwa na Ikulu Dodoma au Mji wa Serikali, au miradi hii mingine mikubwa siyo tu ya kimkakati kama inavyoitwa bali ya uthubutu uliopitiliza.

Yaani, kwa miaka Zaidi ya arobaini hawa jamaa walishindwa kuhamia Dodoma walikuwa wanalipia vipindi vya CDA hata sijui tulikuwa tunaambiwa nini. Kwa miaka arobaini walikuwa wanajipanga, na kuandaa ramani, na kuandaa warsha na semina. Kwa miaka arobaini wanaenda Dodoma, usiku usiku wanawahi kurudi Dar, kwa miaka arobaini wanaimba “Dodoma Dodoma” lakini kila wakiama ni “Dar, Dar”.

Akaja Magufuli akasema maneno matupu hayaliwi na upepo haufungwi kanga! Akawakimbiza mchakamchaka watu wazima na majasho hadi kwenye kucha; mambo yakaanza Kwenda. Yaani, yaliyowashindwa kwa miaka arobaini mtu kayaweza kuyasukuma kwa miaka mitano! Halafu wanatuambia “na sisi tulicheza”. Wanasema kweli Pele alifunga goli lakini sisi tulitoa pasi; wanasema Lionel kachukua kombe la dunia lakini sisi tulimbeba! Hatutaki kuwakumbuka!

Sasa wameamua tu kuwa hawamtaja Magufuli kwa sifa zake; hawatamtaja kwa uthubutu wa barabara, meli, mashule, madaraja. Yaani, kuna watu walijenga daraja moja kubwa kwa miaka kumi halafu anakuja mtu anajenga Matano wanajilinganisha naye! “Na sisi tulijenga barabara na sisi tulijenga daraja” msimpe sifa sana yule; alikuwa ati wa kawaida tu. Ni wivu gani huu?

Hivi kweli wakisema sifa za Magufuli kwa haki kabisa, na kusema kuwa alikuwa ni mchezaji nyota wao watapunguziwa sifa zao? Hivi watakapoenda kuwasha umeme wa Bwawa la Nyerere si wataanza kutupigisha stori tena kama za Ikulu! “Oh hili wazo lilikuwa la Nyerere, na sisi wengine tukapokezana vijiti”! Hivi mkimpa sifa Magufuli anazostahili nyinyi mtapungukiwa? Mtaonekana mnamshusha Samia? Au Samia mwenyewe anaweza kuona wivu badala ya kuona Fahari kuwa alikuwa ni sehemu ya miaka mitano ya Magufuli.

Ndio maana ile sauti anayoisikia Rais Samia haikomi. Itaendelea kumlilia na kumkumbusha kutimiza miradi lakini aifanye kwa haki isiwe kana kwamba anaona ana kivuli cha Magufuli. Magufuli akishangiliwa haina maana nay eye hatoshangiliwa; sifa za Magufuli zikiimbwa haina maana za kwake na timu yake hazitaimbwa. Ikulu ya Dodoma wangeachiwa haya ingekuja 2050! Labda wajukuu zao ndio wangeweza kuthubutu! Kama kwa miaka arobaini walichofanikiwa ni kile kilichokuwepo kabla ya Magufuli basi hawa wangeendelea kutenga bajeti ya kula tu kwa kisingizio cha kupanga makao makuu.

Hili ni swali la kwani wakimpa sifa Magufuli wao watapungukiwa naamini bado linahitaji majibu muafaka kwa wakati huu. Ni swali ambalo kama halitajibiwa vyema basi tutajikuta tunaendelea kuliuliza hata kama ni kwa kung’ong’a. Lakini kama siyo wivu, kama siyo kisirani, kama siyo kukereka na kivuli cha Magufuli basi ndugu zetu hawa waanze kuwa wa kweli; mnyonge mnyongeni sifa zake mpeni; hata kama mnaona zinawapunguzia zenu. Siyo ndivyo haki yenyewe hiyo.

Kwa hiyo basi natangaza hadharani, Ikulu na uamuzi wa kuharakisha kuhamia Dodoma sasa hivi na maendeleo yote ya ujenzi tunayoyaona ni matokeo ya uthubutu, maono, na kujituma kwa Rais wa Awamu ya Tano John Joseph Pombe Magufuli. Mchango wake haulinganishwa na Rais mwingine yeyote kabla yake na baada yake. Anayebisha asimame. Wangekuwa na uwezo na uthubutu huo; wangekuwa wamehamia Dodoma miaka 40 nyuma!

Niandikie:klhnews@gmail.com
Andiko lako refu kutaka Magufuli akumbukwe ungeli "summarise" kwa mistari isiyozidi mitano.

Waswahili wanasema "kuchamba kwingi....".

Wanamichezo wote uliowataja sijaona mtu teyote akiandika kwa kulalamika hawatajwi, jiulize kwanini wanatajwa bila mtu kujilazimisha? au mwengine kulazimisha watajwe?


Jibu ni simpo, ukiona mtu au watu walio wengi au hata wachache wenye akili zao wanajitahidi wasimtaje basi elewa kuwa ana aibu zake nyingi hawataki kuzikumbusha kwa makusudi au kwa bahati nbaya.
Jema halilazimishwi.

Wazo la kuhamia dodoma siyo la Magufuli. Na siyo yeye aliyeanza kuhamishia jiji Dodoma na aliyoamuru yeye ijengwe, pia siyo Ikulu ya kwanza kujengwa Dodoma.

Waliokuwa kabla yake wamefanya yao na yeye kafanya yake na waliopo hivi sasa wanafanya yao.

Kwanini iwe mwao kama watu hawataki kumtaja? Au ni sukuma boy mwenzako?
 
Haikua rahisi watu kama hawa kumtaja Magufuli kwa namna hii.

Hakuna jinsi kila mtu atamtaja Magufuli kila mmoja kwa wakati wake, lakini atatajikana kwa wema tu.
View attachment 2642952
Hawa wapinzani kuna wakati huwa hawajielewi kabisa. Wao kila wakati ni kutafuta namna ya kushinda sasa, hawana mipango endelevu bali ni mipango kulungana na upepo. Wapo tayari kumsifu aliyetangulia kwa namna yoyote ili mradi sifa hizo kwa mtangulizi zinambomoa aliyepo.

Magu yupi ambaye angechomoa watu maofisini kwa report ya CAG?
Magu huyu ambaye alimchomoa CAG mwenyewe baada ya kutoa report?
 
View attachment 2642893
Na. M. M. Mwanakijiji

Kuna watu ambao tunawakumbuka kwa umahiri na weledi katika kazi, vipaji au matendo yao. Michael Jordan aliichezea timu ya mpira wa vikapu ya Chicago Bulls na kujionesha kuwa ni mchezaji bora Zaidi wa mchezo huo duniani. Wengi wanalijua jina la Michael Jordan lakini ni wachache wanaweza kukutajia majina ya wachezaji wenzake wanne waliokuwa wanaunda kikosi cha kwanza. Hili pia ni kweli kuhusu mchezaji bora Zaidi wa soka duniani Pele. Wengi wanalijua na kukumbuka jinsi Pele alivyoongoza Brazili kwenye makombe ya dunia. Ni wachache sana wanaweza kukutajia wachezaji kumi wengine walioshinda na Pele kombe la dunia mara ya mwisho.

Hata hapa Tanzania kuna watu wanakumbukwa kwa umahiri wao lakini ni wachache wanaweza kukutajia majina ya watu wengine kwenye vikosi vyao. Mbaraka Mwinshehe, Marijan Rajabu, au hata Remmy Ongara. Tunajua nyimbo zao, tumewahi kuzisikia lakini tukiuliza wana bendi wenzao ni kina nani ni wachache wanaweza kutaja hata majina mawili.

Ukweli ni kuwa kuna watu wanatokea katika fani mbalimbali na wanakuwa vinara na bora kuliko wengine. Tunapowataja hawa wengine na kuwasifia haina maana tunadharau mchango wa wengine. Ukimtaja Lionel Messi kwa mfano au Cristiano Ronaldo mara moja watu watajua unawazungumzia kina nani lakini ni wachache wanaweza kukutajia majina ya wachezaji wenzao kwenye zile timu zilizokuza majina yao. Unaposema sifa za vinara haina maana unafuta sifa au unadharau sifa za wengine!

Juzi wakati wa uzinduzi wa Ikulu mpya ya Dodoma ambayo sasa inaifanya Ikulu ya Dar-es-Salaam kuwa Ikulu Ndogo kuna watu walisimama na kumwaga sifa mbalimbali. Niliamka mapema (huku niliko) niweze kushuhudia kama watakuwa na ujasiri wa kumtaja mchezaji kinara aliyewafanya wawepo pale siku ile. Bahati mbaya karibu kila aliyesimama ama alinyemelea kulitaja jina la mchezaji huyo bora au alilitaja kama kulipita tu kuwa “alikuwa ni mmoja wa timu”.

Jina la Joseph Pombe Magufuli, kinara wa marais wote waliowahi kutokea Tanzania, shujaa wa uthubutu, na mbunifu wa maono ya maendeleo ya haraka lilitajwa kana kwamba na yeye alikuwa na mchango kama wengine tu. Yote hiyo ilifanywa kwa makusudi kabisa wakijaribu kufifisha jina hilo na hawakutaka kusikia makofi na shangwe ambazo wangelitendea haki zingesikaka. Waliogopa kuona kuwa yumkini huyu bwana akiwa amelala kaburini milele kuna watu wanamkumbuka na kummiss!

Wanatuambia kuwa mpango wa kuhamishia Ikulu ulianza toka miaka ya sitini na hatimaye maamuzi yakachukuliwa na taratibu hatua mbalimbali zilianza kuchukuliwa ili kuhamia taratibu Dodoma. Jakaya Kikwete akatupa stori kuwa aliagiza watu waende Malaysia waone mambo yanavyofanyika huko na sisi tuje kuiga. Sikumbuki kwa miaka kumi ya Kikwete kama kuna siku ulifanyika mjadala hata mmoja Bungeni wa jinsi ya kuhamia Dodoma na kujenga Ikulu Dodoma na kuwa aliwaambia Watanzania kuwa ametuma iende Malaysia! Sijui hiyo timu iliongozwa nan ani! Lakini tunakubali.

Tunaambiwa kuwa viongozi wote waliotangulia wamekuwa wakifanya kama kupokezana vijiti kuliongoza taifa. Wanasahau kuwa Magufuli hakumwachia Samia kijiti; kamwachia gogo! Ni wazi Rais Samia anajitahidi kwa uwezo wake wote kuonekana anaweza kukamilisha miradi hii yote; na kweli tunaona ikimalizwa. Lakini ndugu zetu hawa wanataka tuamine kuwa kama Magufuli asingefanya alivyofanya leo tungekuwa na Ikulu Dodoma au Mji wa Serikali, au miradi hii mingine mikubwa siyo tu ya kimkakati kama inavyoitwa bali ya uthubutu uliopitiliza.

Yaani, kwa miaka Zaidi ya arobaini hawa jamaa walishindwa kuhamia Dodoma walikuwa wanalipia vipindi vya CDA hata sijui tulikuwa tunaambiwa nini. Kwa miaka arobaini walikuwa wanajipanga, na kuandaa ramani, na kuandaa warsha na semina. Kwa miaka arobaini wanaenda Dodoma, usiku usiku wanawahi kurudi Dar, kwa miaka arobaini wanaimba “Dodoma Dodoma” lakini kila wakiama ni “Dar, Dar”.

Akaja Magufuli akasema maneno matupu hayaliwi na upepo haufungwi kanga! Akawakimbiza mchakamchaka watu wazima na majasho hadi kwenye kucha; mambo yakaanza Kwenda. Yaani, yaliyowashindwa kwa miaka arobaini mtu kayaweza kuyasukuma kwa miaka mitano! Halafu wanatuambia “na sisi tulicheza”. Wanasema kweli Pele alifunga goli lakini sisi tulitoa pasi; wanasema Lionel kachukua kombe la dunia lakini sisi tulimbeba! Hatutaki kuwakumbuka!

Sasa wameamua tu kuwa hawamtaja Magufuli kwa sifa zake; hawatamtaja kwa uthubutu wa barabara, meli, mashule, madaraja. Yaani, kuna watu walijenga daraja moja kubwa kwa miaka kumi halafu anakuja mtu anajenga Matano wanajilinganisha naye! “Na sisi tulijenga barabara na sisi tulijenga daraja” msimpe sifa sana yule; alikuwa ati wa kawaida tu. Ni wivu gani huu?

Hivi kweli wakisema sifa za Magufuli kwa haki kabisa, na kusema kuwa alikuwa ni mchezaji nyota wao watapunguziwa sifa zao? Hivi watakapoenda kuwasha umeme wa Bwawa la Nyerere si wataanza kutupigisha stori tena kama za Ikulu! “Oh hili wazo lilikuwa la Nyerere, na sisi wengine tukapokezana vijiti”! Hivi mkimpa sifa Magufuli anazostahili nyinyi mtapungukiwa? Mtaonekana mnamshusha Samia? Au Samia mwenyewe anaweza kuona wivu badala ya kuona Fahari kuwa alikuwa ni sehemu ya miaka mitano ya Magufuli.

Ndio maana ile sauti anayoisikia Rais Samia haikomi. Itaendelea kumlilia na kumkumbusha kutimiza miradi lakini aifanye kwa haki isiwe kana kwamba anaona ana kivuli cha Magufuli. Magufuli akishangiliwa haina maana nay eye hatoshangiliwa; sifa za Magufuli zikiimbwa haina maana za kwake na timu yake hazitaimbwa. Ikulu ya Dodoma wangeachiwa haya ingekuja 2050! Labda wajukuu zao ndio wangeweza kuthubutu! Kama kwa miaka arobaini walichofanikiwa ni kile kilichokuwepo kabla ya Magufuli basi hawa wangeendelea kutenga bajeti ya kula tu kwa kisingizio cha kupanga makao makuu.

Hili ni swali la kwani wakimpa sifa Magufuli wao watapungukiwa naamini bado linahitaji majibu muafaka kwa wakati huu. Ni swali ambalo kama halitajibiwa vyema basi tutajikuta tunaendelea kuliuliza hata kama ni kwa kung’ong’a. Lakini kama siyo wivu, kama siyo kisirani, kama siyo kukereka na kivuli cha Magufuli basi ndugu zetu hawa waanze kuwa wa kweli; mnyonge mnyongeni sifa zake mpeni; hata kama mnaona zinawapunguzia zenu. Siyo ndivyo haki yenyewe hiyo.

Kwa hiyo basi natangaza hadharani, Ikulu na uamuzi wa kuharakisha kuhamia Dodoma sasa hivi na maendeleo yote ya ujenzi tunayoyaona ni matokeo ya uthubutu, maono, na kujituma kwa Rais wa Awamu ya Tano John Joseph Pombe Magufuli. Mchango wake haulinganishwa na Rais mwingine yeyote kabla yake na baada yake. Anayebisha asimame. Wangekuwa na uwezo na uthubutu huo; wangekuwa wamehamia Dodoma miaka 40 nyuma!

Niandikie:klhnews@gmail.com
Huwezi kujenga miundombinu kwa damu za watu wasio na hatia halafu utegemee na kustahili sifa. Licha ya hayo yote ulioyataja bado Magufuli ni kiongozi wa hovyo kuwahi kutokea Tanzania.

Aliua watu wenye mawazo tofauti na yake, kateka na kutesa wapinzani, kaanzisha magenge ya "wasiojulikana" wanaojulikana, kaiba pesa za umma na kuzificha kunakojulikana....
Kwa waliokuwa awamu ya tano na kujua aliyoyafanya Magufuli kwa undani, anatakiwa awe mvuta bangi au sukumagang kuweza kujitokeza hadharani kumsifia mwehu yule.
 
🤣🤣🤣🤣ila kweli tunatofautiana yaan mi nshasahau kama kuna rais aliyeitwa magufuli, ila watu bado mnakumbu kumbu
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Jina la Joseph Pombe Magufuli, kinara wa marais wote waliowahi kutokea Tanzania, shujaa wa uthubutu, na mbunifu wa maono ya maendeleo ya haraka lilitajwa kana

Niandikie:klhnews@gmail.com
Nimeupenda huo mstari, nitakuandikia.
Miongoni mwa makala ninazo zimisi kwenye local media yetu ni gazeti la Cheche, na makala za MM Mwanakijiji na Lula wa Ndali Mwananzela.
P
 
Anayekunyanyua ndio anayeweza kukudondosha,Magufuli he was nobody kama sio Kikwete kuamua kumpa huo Urais.
So,Kikwete ndio aliyemnyanyua na yeye na gang lake ndio waliomdondosha.Magufuli alishindwa game so acha washindi waandike History.

Acha malalamiko,politics is the game na Magufuli aliishindwa.
 
Andiko lako refu kutaka Magufuli akumbukwe ungeli "summarise" kwa mistari isiyozidi mitano.

Waswahili wanasema "kuchamba kwingi....".

Wanamichezo wote uliowataja sijaona mtu teyote akiandika kwa kulalamika hawatajwi, jiulize kwanini wanatajwa bila mtu kujilazimisha? au mwengine kulazimisha watajwe?


Jibu ni simpo, ukiona mtu au watu walio wengi au hata wachache wenye akili zao wanajitahidi wasimtaje basi elewa kuwa ana aibu zake nyingi hawataki kuzikumbusha kwa makusudi au kwa bahati nbaya.
Jema halilazimishwi.

Wazo la kuhamia dodoma siyo la Magufuli. Na siyo yeye aliyeanza kuhamishia jiji Dodoma na aliyoamuru yeye ijengwe, pia siyo Ikulu ya kwanza kujengwa Dodoma.

Waliokuwa kabla yake wamefanya yao na yeye kafanya yake na waliopo hivi sasa wanafanya yao.

Kwanini iwe mwao kama watu hawataki kumtaja? Au ni sukuma boy mwenzako?
Kwanza nchi hii kama tunapenda sifa za kijinga basi hakuna anayestahili sifa zaidi ya Mzee Mwinyi.

Mzee Mwinyi alikabidhiwa nchi ikiwa imefilisiwa na Nyerere kwa kuingia vita binafsi na Idd Amin.

Tulikuwa tunakula unga wa njano na kuvaa midabwada, mafundi cherehani walikuwa bize sana kushona midabwada.

Wengine tumezaliwa Dar na kukulia Dar lakini wakati wa Nyerere nakumbuka tulikwenda shuleni pekupeku, imagine hiyo ni Dar sijui hali ilikuwaje vijijini.

Leo hii watu wanaingiza tu eacher Marco polo kufanya biashara ya usafiri lakini hawajui Mwinyi ndio aliruhusu mpaka gari za mizigo zibebe abiria.

Tukianza kumrundikia sifa Mzee Mwinyi hapa basi ukurasa huu hautatosha.

Mwinyi alivyokuwa anampamba Magufuli hizo ndio tabia za watu waliostaarabika kutambuwa mchango wa wenzao na ndio maana Mungu amembariki umri mrefu wa kuishi.

Magufuli alidiriki kujipa Umungu kwamba akiondoka yeye hakuna wa kufanya hayo, haya sasa amekufa, Ikulu imesimamiwa na mama na imezinduliwa na leo tunapokea ndege ya mizigo ambayo ni usimamizi wa mama.
 
Kwanza nchi hii kama tunapenda sofa za kijinga basi hakuna anayestahili sofa zaidi ya Mzee Mwinyi.

Mzee Mwinyi alikabidhiwa nchi ikiwa imefilisiwa na Nyerere kwa kuingia vita binafsi na Idd Am in I.

Tulikuwa tuna kula unga wa njano na kuvaa midabwada, mafundi cherehani walikuwa bize sana kushona midabwada.

Wengine tumezaliwa Dar na kukulia Dar lakini wakati wa Nyerere nakumbuka tulikwenda shuleni pekupeku, imagine hiyo ni Dar sijui hali ilikuwaje vijijini.

Leo hii watu wanaingiza tu Teacher Marco polo kufanya biashara ya usafiri lakini hawajui Mwinyi ndio aliruhusu mpaka gari za mizigo zibebe abiria.

Tukianza kumrundikia sofa Mzee Mwinyi hapa basi ukurasa huu hautatosha.

Mwinyi alivyokuwa anampamba Magufuli hizo ndio tabia za watu waliostaarabika kutambuwa mchango wa wenzao na ndio maana Mungu amembariki umri mrefu wa kuishi.

Magufuli alidiriki kujipa Umungu kwamba akiondoka yeye hakuna wa kufanya hayo, haya sasa amekufa, Ikulu imesimamiwa na mama na imezinduliwa na leo tunapokea ndege ya mizigo ambayo ni usimamizi wa mama.
Kweli kabisa, Mzee Mwinyi ndiye aliyeipa uhai hii nchi, ilikuwa chali.

Mzee Mwinyi anastahiki jina lake liandikwe kwa wino wa dhahabu.
 
Andiko lako refu kutaka Magufuli akumbukwe ungeli "summarise" kwa mistari isiyozidi mitano.

Waswahili wanasema "kuchamba kwingi....".

Wanamichezo wote uliowataja sijaona mtu teyote akiandika kwa kulalamika hawatajwi, jiulize kwanini wanatajwa bila mtu kujilazimisha? au mwengine kulazimisha watajwe?


Jibu ni simpo, ukiona mtu au watu walio wengi au hata wachache wenye akili zao wanajitahidi wasimtaje basi elewa kuwa ana aibu zake nyingi hawataki kuzikumbusha kwa makusudi au kwa bahati nbaya.
Jema halilazimishwi.

Wazo la kuhamia dodoma siyo la Magufuli. Na siyo yeye aliyeanza kuhamishia jiji Dodoma na aliyoamuru yeye ijengwe, pia siyo Ikulu ya kwanza kujengwa Dodoma.

Waliokuwa kabla yake wamefanya yao na yeye kafanya yake na waliopo hivi sasa wanafanya yao.

Kwanini iwe mwao kama watu hawataki kumtaja? Au ni sukuma boy mwenzako?
Kwani Magufuli amedai kutajwa? angekuwa hai tungeacha ajitetee! Rudi kwenye hoja, Ma Rais waliopita walistahili sifa zipi kwenye ujenzi wa ikulu ya Dodoma? Hata mzee Mwinyi toka awali alikiri Ma Rais wote walifeli jambo ambalo mwenzao alifanya kwa muda mfupi.
 
Kweli kabisa, Mzee Mwinyi ndiye aliyeipa uhai hii nchi, ilikuwa chali.

Mzee Mwinyi anastahiki jina lake liandikwe kwa wino wa dhahabu.
Ni kweli na ikibidi fungua uzi maalum tukampe maua yake. Ila hapa bakia kwenye hoja. Hatuwezi kumpa Mkapa sifa za Mwinyi! Pia vilevile mambo aliyofanya JPM jamaa zenu wasipende kujichomeka waonekane wamo. Mama Samia anastahili maana alikuwa makamu Rais na amekamilisha akiwa Rais.
 
Kweli kabisa, Mzee Mwinyi ndiye aliyeipa uhai hii nchi, ilikuwa chali.

Mzee Mwinyi anastahiki jina lake liandikwe kwa wino wa dhahabu.
Nakumbuka sukari ilikuwa ni kwa mgao mpaka gari la NMC lije uende na daftari ndio reja yako ya kuuziwa sukari mwisho kilo mbili.

Magufuli ameachiwa nchi na Kikwete hazina ikiwa na pesa za kigeni za kutosha halafu waabudu mizimu wanatufanya wote hatuna akili au tumesahau.
 
Back
Top Bottom