Swali gumu kidogo: Kwanini Urusi iliyosambaratika na dhaifu kuliko USSR inawasumbua sana NATO?

Swali gumu kidogo: Kwanini Urusi iliyosambaratika na dhaifu kuliko USSR inawasumbua sana NATO?

Hichi ulichokizungumzia hapa kinaitwa The Heartland Theory au Nadharia ya moyo wa dunia.
Iliandikwa mara ya kwanza kabisa na mwanasayansi wa siasa kutoka Uingereza aitwaye Sir Halford MckKinder ambaye mwaka 1904 alisema kwamba kama taifa litafanikiwa kutawala eneo la Ulaya Mashariki na Asia (Eurasia) basi litatawala Ulaya yote na Asia. Aliyaandika haya kwenye chapisho lake liitwalo The Geographical Pivot of History na akasema kutokana na utajiri wa rasilimali wa eneo hilo taifa lolote litakalotawala Ufalme wa Urusi basi linaweza tawala dunia.


Ikumbukwe Urusi ndiyo nchi inayoongoza kwa wingi wa rasilimali zenye thamani ya dola za kimarekani trilioni 75. Marekani na ujanja wake wote ana rasilimali zenye thamani ya dola za kimarekani trilioni 4, hivyo Urusi kama ikisambaratika nchi nyingi za Ulaya zinaweza kunufaika sana na utajiri wake.

Wanahistoria wanaamini kwamba moja ya sababu kubwa za Adolf Hitler kuvamia Urusi mwaka 1941 kabla ya nchi nyingine zote ni kwasababu Wanazi waliamini kwenye The Heartland Theory kwamba kama watampiga Urusi mapema basi watatumia rasilimali zake zote kuipiga dunia yote na ndiyo maana mataifa ya Ulaya na Marekani ikabidi watume msaada wa kipesa kwa Urusi. Hata baada ya vita ya dunia kuisha, Vita Baridi ilichangiwa sana na hii nadharia ambayo Waingereza na Wamarekani iliwakaa sana kichwani.



Tatizo la Urusi la anguko la Urusi ya Kisovieti lilikuwa siyo kusaidia mataifa mengine lakini mfumo wake mbovu na kukataa kubadilika kwa viongozi wa Kisovieti hasahasa wale kama Leonid Brezhnev. Tukisema kwamba tatizo ni kusaidia mataifa mengine tutakuwa tunasahau kitu cha muhimu sana kwamba hata Marekani naye alisaidia sana mataifa mengi sana duniani tena kwa nguvu nyingi sana kuliko hata Urusi.
Wakati Urusi alikuwa ana washirika wa Kijeshi wa Ulaya tu kupitia The Warsaw Pact, Marekani alikuwa na washirika wa kijeshi dunia nzima Kuanzia NATO, ANZUS, SEATO hadi CENTO. Mpaka leo Marekani ana mikataba ya ulinzi kama 60 hivi.


Misaada ya kiuchumi wote walitoa huku Marekani akianza na The Marshal Plan huku wasovieti wakija na The COMECON. Wote walisomesha watu huko Harvard, Yale, Moscow State University na University of St.Petersburg lakini Urusi aliachwa mbali sana. Kwanini ?? Mfumo mbovu wa kiuchumi au kuruhusu serikali kutawala uchumi kwa kila kitu (Command or Centralization of Economy). Uchumi wa Urusi haukuruhusu ushindani wa ndani ya nchi, wakati Marekani makampuni binafsi yalikuwa yanazalisha bidhaa na kupunguzia serikali mzigo. Uchina chini ya Deng Xiapoing waligundua hili mapema ndiyo wakaryuhusu mfumo wa masoko utawala nchi. Hivyo hapa sikubaliani na wewe kidogo mkuu wangu kwasababu kama kusaidia wote walisaidia mataifa ya nje kwa sana tu.



Hapa nakubaliana na wewe kwamba Urusi alikuwa na nguvu sana hadi kutanua lile eneo lake lote. Alifanya hivyo kwenye Vita Baridi ya kwanza aliyopigana na Muingereza tokea mwaka 1813 hadi 1907 ambayo iliitwa kama The Great Game au The Tournament of Shadows. Lakini naomba nikukosea kidogo hapo uliposema Marekani alikuwa hana nguvu: Nifahamuvyo mimi mpaka kufika mwaka 1916 Ujerumani alikuwa ameshashinda vita ya kwanza ya dunia na Muingereza alikuwa anajiandaa kusalimu amri, lakini aliyebadilisha mwelekeo ule wote ni Marekani chini ya Prof. Woodrow Wilson.

Mbali na hapo ikumbukwe kwamba Ujerumani alipanga kumvamia Marekani mwaka 1897 na Mfalme Kaiser Wilhelm alimtuma Ebenhard Von Mantey kupanga uvamizi kwa kutuma vikosi 100,000 lakini mpango huu ulikufa baada ya Marekani kuonesha nguvu zake kwa kumtwanga vibaya Mhispania kwenye vita ya mwaka 1898 (The Spanish American War)na kumnyang'anya CUBA na makoloni yake muhimu. Hapa utasemaje Marekani alikuwa hana nguvu ???

Unahisi Uingereza angeshinda Vita ya kwanza ya dunia dhidi ya Ujerumani bila Marekani kuingilia kati ?
Pia tusisahau kwamba Urusi ilisalimu amri mapema sana kutoka kwa Ujerumani wakati wa vita ya kwanza ya dunia hadi wakina Lenini wakasaini Mkataba wa hovyo kabisa wa Brest-Litovsk ambao ulikubali kumruhusu Ujerumani achukue sehemu za Urusi kama Poland, Estonia, Finland, Latvia, Ukraine na Lithuania. Bila Marekani kuingia kwenye vita uandhani haya maeneo yangerudi kirahisi ?


CC: Wick , muyovozi , MASAMILA , neo1

Kwanini unazungumzia vita vya kwanza vya dunia baadala ya vita vya pili vya dunia?? Ukitaka kuielewa Russia na iliyokuwa Soviet Union zungumzia WWII...Soviet union ndiyo iliyoiokoa dunia kutoka kwa Hitler...Eastern Front ambako Hitler alipambana na Soviet ndiko kulikoamua hatima ya WW II.
 
Baada ya kusambaratika kwa Soviet Union siyo kweli kwamba kila kitu kilipotea...Mambo mengi yaliridhiwa na Russia federation ambayo ndiyo iliyokuwa kubwa kuliko karibu nchi au jamhuri zote 16 zilizounda USSR...silaha za nyuklia zilimilikiwa na Russia...n ikweli kiuchumi karibu asilimia 40 ilipotea, watu karibu asilimia 30 hivi na kadhalika lakini bado Russia ndiyo iliyokuwa mhimili wa USSR ilibaki..vijamhuri kama Georgia vilikuwa na watu karibu milioni 4 tu, Lithunia, Estonia na Lativia karibu milioni mbili tu...Lakini Russia ilikuwa na watu karibu milioni 140...Russia ndiyo nchi yote kubwa duniani, ina raslimali nyingi na hasa gas na mafuta na pia teknolojia...Russia sasa imepata kiongozi thabiti PUTIN ambaye alikuwa ni jasusi (KGB) na hivyo kuwa well informed na masuala mengi ya dunia na namna USSR ilivyosambaratika...PUTIN amewaweka marafiki zake wa iliyokuwa KGB kwenye madaraka ya nchi na wanajua mengi...PUTIN alichofanya ni kujenga ndani ya RUSSIA suala la nationalism au uzalendo....amevivunja vi- NGO vya nchi za magharibi ambavyo huanzishwa kwa kisingizio cha demokrasia kumbe ni wakala wa ubepari na maslahi ya nchi hizo...

Naomba nikubaliane na wewe kwamba hakupoteza kila kitu, lakini kitaalamu mifumo ya nchi ikiparanganyika na kufa basi nchi inayozaliwa huwa nyingine kabisa. USSR ilikufa na RF siyo USSR:
Urusi ilipoteza mengi makubwa ndiyo maana NATO ikaamini kwamba Urusi hiawezi inuka tena.
1. Ilipoteza asilimia 23.8% ya eneo lake.
2. Iliopoteza asilimia 48.5% ya watu wake (Hili likitokea Tanzania haponi mtu)
3. Iliopoteza asilimia 41% ya GDP hapa nchi lazima ife.
4. Iliopoteza asilimia 39.9% ya nguvu ya viwanda (Angalia vizuri ukubwa wa hii asilimia)
5. Ilipoteza asilimia 44.6% ya mifumo ya ulinzi na mejeshi.


Kiuchumi nchi yoyote ikikutwa na haya majanga lazima ipoteane kabisa, Uingereza aliyemilika Asilimia 23% ya ardhi ya dunia hadi kufika mwaka 1923, aliuponyang'anywa maeneo kama India na Pakistan mwaka 1947-1948 hajaweza kuamka mpaka leo. Japo unaweza kusema hajapoteza kila kitu lakini The British Empire is no more.
 
Naomba nikubaliane na wewe kwamba hakupoteza kila kitu, lakini kitaalamu mifumo ya nchi ikiparanganyika na kufa basi nchi inayozaliwa huwa nyingine kabisa. USSR ilikufa na RF siyo USSR:
Urusi ilipoteza mengi makubwa ndiyo maana NATO ikaamini kwamba Urusi hiawezi inuka tena.
1. Ilipoteza asilimia 23.8% ya eneo lake.
2. Iliopteza asilimia 48.5% ya watu wake (Hili likitokea Tanzania haponi mtu)
3. Iliopteza asilimia 41% ya GDP hapa nchi lazima ife.
4. Iliopteza asilimia 39.9% ya nguvu ya viwanda (Angalia vizuri ukubwa wa hii asilimia)
5. Ilipoteza asilimia 44.6% ya mifumo ya ulinzi na mejeshi.


Kiuchumi nchi yoyote ikikutwa na haya majanga lazima ipoteane kabisa, Uingereza aliyemilika Asilimia 23% ya ardhi ya dunia hadi kufika mwaka 1923 aliuponyang'anywa maeneo kama India na Pakistan hajaweza kuamka mpaka leo. Japo unaweza kusema hajapoteza kila kitu lakini The British Empire is no more.

Thanks comrade...Hivi ndivyo Jamii forums inavyopaswa kuwa...Asante sana ndugu yangu....hojaza aina hii huwafikirisha vijana wengi humu ambao hawajui kabisa masuala mengi ya dunia...wanachukulia 'uhasama' wa Russia na USA kama ushabiki wa Simba na Yanga...
 
Kwanini unazungumzia vita vya kwanza vya dunia baadala ya vita vya pili vya dunia?? Ukitaka kuielewa Russia na iliyokuwa Soviet Union zungumzia WWII...Soviet union ndiyo iliyoiokoa dunia kutoka kwa Hitler...Eastern Front ambako Hitler alipambana na Soviet ndiko kulikoamua hatima ya WW II.
Sawa kabisa Eastern Front ndiko kuliamua hatma ya vita ya pili ya dunia kwasababu Ujerumani alitumia asilimia 80% ya nguvu yake yote ya jeshi lakini akashindwa, hivyo The Great Patriotic War 1941 hadi 1945 ndiyo ilibadili mwelekeo wote wa vita ya pili ya dunia.

Japo sasa, kamwe huwezi kuzungumzia USSR bila kuzungumzia vita ya kwanza ya dunia (Haiwezekani)
Hadi Hitler anavamia USSR mwaka 1941 yote hii mzizi wake ulitokana na Mkataba wa Versailles wa mwaka 1919-1920 ambao ulivunja Mkataba wa Brest-Litovsk ambao ulimfanya Urusi aweke silaha chini na kukubali kumgawia Poland na nchi nyingine za Ulaya Mashariki.


Hivyo ndugu yangu, lazima ukumbuke kwamba matukio yote ya karne ya 20 hasa yale makubwa kama Vita ya Kwanza ya dunia, Vita ya Pili ya dunia, Vita Baridi, Mapinduzi ya Oktoba yamefungamana sana na huwezi kusema unadiriki kuyatenga hata siku moja.
 
Sawa kabisa Eastern Front ndiko kuliamua hatma ya vita ya pili ya dunia kwasababu Ujerumani alitumia asilimia 80% ya nguvu yake yote ya jeshi lakini akashindwa, hivyo The Great Patriotic War 1941 hadi 1945 ndiyo ilibadili mwelekeo wote wa vita ya pili ya dunia.

Japi sasa, kamwe huwezi kuzungumzia USSR bila kuzungumzia vita ya kwanza ya dunia (Haiwezekani)
Hadi Hitler anavamia USSR mwaka 1941 yote hii mzizi wake ulitokana na Mkataba wa Versailles wa mwaka 1919-1920 ambao ulivunja Mkataba wa Brest-Litovsk ambao ulimfanya Urusi aweke silaha chini na kukubali kumgawia Poland na nchi nyingine za Ulaya Mashariki.


Hivyo ndugu yangu, lazima ukumbuke kwamba matukio yote ya karne ya 20 hasa yale makubwa kama Vita ya Kwanza ya dunia, Vita ya Pili ya dunia, Vita Baridi, Mapinduzi ya Oktoba yamefungamana sana na huwezi kusema unadiriki kuyatenga hata siku moja.

Sawa comrade...nimekuelewa....you are well informed and knowlegeable...congratulations....
 
KISIASA
1. Amesababisha sintofahamu kubwa ndani ya siasa za Marekani hasa kwa Donald Trump.
2. Anavuruga mipango ya Marekani kwa kutumia VETO kule Umoja wa Mataifa.
3. Amefanikiwa kuugawanya Umoja wa Ulaya (Schoeder wa Ujerumani anafanya kazi Rosneft)
4. Anaisaidia Korea Kaskazini kukwepa vikwazo vya Umoja wa Mataifa.
5. Alimsaidia Raisi wa Uturuki asipinduliwe na kuuwawa ambapo inasemekana CIA walihusika sana.
6. Amemtunza Edward Snowden ambaye kavujisha siri nyeti za Marekani.


KIJESHI
1. Kavamia Ukraine kijeshi na kumega Crimea kwa nguvu mno ya wanajeshi 70,000.
2. Kavuruga mpango wa Marekani na Israel wa kuvamia Syria na kumtoa Assad.
3. Anauza silaha nzito kwa mataifa hasimu wa Marekani kama Iran.
4. Anasidia Korea Kaskazini kukwepa vikwazo vya Umoja wa Mataifa.
5. Amevuruga majimbo ya Lugansk na Donestky hadi leo majeshi ya Ukraine hayana amani.
7. Yeye ndiyo mwenye jeshi la pili kwa ubora hapa duniani mbali na shida zote kiuchumi.


KITEKNOLOJIA
1. Marekani mpaka leo anategemea injini kutoka Urusi kwa ajili ya kurusha roketi zake.
2. Ametengeneza makombora mazito ambayo yanasafiri mara 10 zaidi ya sauti.
3. Walimwekea vikwazo vya injini za ndege kutoka Ukraine lakini katengeneza zake kwa haraka sana.
4. Ana wasomi wa sayansi ambao ni World Class kama 1,000,000 hivi.
5. Teknolojia ya kimtandao (Cyber Technology) yuko mbele sana na amethibitishia dunia mara nyingi.



KIUCHUMI
1. Amefanikiwa kutumia makampuni yake ya nishati kuwaumiza Ulaya hasa NORD Stream 2.
2. Amefanikiwa kutumia ushawishi wa nishati kuyavuta karibu mataifa kama Uchina, India na Uturuki.
3. Uturuki ameagiza silaha kutoka Urusi kitu ambacho kitampa faida za kiuchumi Mrusi.
4. Saudi Arabia ametengeneza viwanda vya Kalashnikov Ak-47 nchini kwake na Urusi karuhusu.
5. Amesaidia kutengeneza vyombo kama BRICS, The Shanghai Cooperation na Eurasia Economic Union


NB: Haya ni machache tu, sasa nchi iliyosambaratika inalisumbuaje taifa kubwa duniani ??
Safi kabisa. VIVA PUTIN VIVAAAA
 
Duniani hapa kama una Technology na Leadership lazima tu utaendelea na hivyo ndivyo vitu ambavyo sisi kwa masikitiko makubwa hatuna.

Sisi kabla ya vita na Uganda tulikuwa na uchumi mzuri ktk ukanda wote huu lkn baada ya tu ya vita tuliambiwa tufunge mikanda kwa miezi 18 lkn hadi leo hiyo miezi 18 haijaisha...!!!

Kwa nchi za wenzetu wanasiasa wanawaheshimu sana wataalam na hawawaingilii ktk utendaji wao wa kazi na haya yanayoongelewa humu ni matokeo ya kuheshimu fikra za wataalam.

Sisi tunafanya mambo tukilenga kupata sifa za kisiasa ili iwe mtaji ktk uchaguzi na watalaam wetu wamekuwa heavily brainwashed politically na wenyewe kwa kuendekeza njaa wamekuwa hawawezi ku-practise kile wanachokiamini hasa hilo likiwa tofauti na anachoamini mwanasiasa.

Tumeona mengi kwa akina Mwakyembe, Kabudi na wengine wengi tu. Angalia miradi mingi inayoanzishwa ktk nchi hii ni ile inayochochewa kisiasa pasipo kuangalia Economic Benefits / Viability au hata Environmental Impact zake.

Nchi kama Russia ktk elimu yao wameangalia nini wanahitaji kama taifa na waka-design curriculum yao mahsusi kulenga hicho na ndio maana wana bajeti kubwa sana inayotengwa kwa ajili ya Research kwani pasipo Research hakuna Innovation.

Russia wana kila sababu ya kuendelea na watazidi tu kuendelea kwani wanawekeza ktk maendeleo na wana sera thabiti zinazolenga ktk dhana nzima ya maendeleo. Sisi ngoja tuendelee kuwawinda wale wapinzani wanaokataa sera yetu ya kuunga juhudi.
 
Sawa kabisa Eastern Front ndiko kuliamua hatma ya vita ya pili ya dunia kwasababu Ujerumani alitumia asilimia 80% ya nguvu yake yote ya jeshi lakini akashindwa, hivyo The Great Patriotic War 1941 hadi 1945 ndiyo ilibadili mwelekeo wote wa vita ya pili ya dunia.

Japi sasa, kamwe huwezi kuzungumzia USSR bila kuzungumzia vita ya kwanza ya dunia (Haiwezekani)
Hadi Hitler anavamia USSR mwaka 1941 yote hii mzizi wake ulitokana na Mkataba wa Versailles wa mwaka 1919-1920 ambao ulivunja Mkataba wa Brest-Litovsk ambao ulimfanya Urusi aweke silaha chini na kukubali kumgawia Poland na nchi nyingine za Ulaya Mashariki.


Hivyo ndugu yangu, lazima ukumbuke kwamba matukio yote ya karne ya 20 hasa yale makubwa kama Vita ya Kwanza ya dunia, Vita ya Pili ya dunia, Vita Baridi, Mapinduzi ya Oktoba yamefungamana sana na huwezi kusema unadiriki kuyatenga hata siku moja.
Big up Comred, naona umeyachimbua madini kwelikweli....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu Malcolm shida ni kwamba urusi ina wasomi wa tecnolojia kubwa ya kijeshi hakuna wanachoshindwa kutengeneza wakitaka
Na kumbuka NATO iko na inaongozwa na marekani kwa hiyo mrusi anapoona mmarekani yuko Karibu na NATO hasira zinazidi
Na NATO haiwezi kufanya jambo bila kuruhusiwa na Marekani


E&K
 
Mkuu Malcolm shida ni kwamba urusi ina wasomi wa tecnolojia kubwa ya kijeshi hakuna wanachoshindwa kutengeneza wakitaka
Na kumbuka NATO iko na inaongozwa na marekani kwa hiyo mrusi anapoona mmarekani yuko Karibu na NATO hasira zinazidi
Na NATO haiwezi kufanya jambo bila kuruhusiwa na Marekani


E&K
Wameshindwa kutengeneza stealth plane..
 
Ewaah, sawa kabisa na huu ndiyo msingi wa swali langu:
Sasa nchi ambayo imeshindwa kutengeneza Stealth Plane kama zile F-35 inawasumbuaje NATO ??
Uchumi uko chini, imewekewa vikwazo vizito na imetengwa, kwanini wasiimalize tu mara moja ???
Haiwezekani kuimaliza Russia bila kuweka usalama wa dunia nzima hatihati. Ukisha kuwa nuclear power to the level of Russia lazima uheshimiwe duniani bila ya kujali uchumi wako upo level gani.
 
Thanks comrade...Hivi ndivyo Jamii forums inavyopaswa kuwa...Asante sana ndugu yangu....hojaza aina hii huwafikirisha vijana wengi humu ambao hawajui kabisa masuala mengi ya dunia...wanachukulia 'uhasama' wa Russia na USA kama ushabiki wa Simba na Yanga...
Yes indeed! Hususani kijana kama Mimi mkuu.
 
Back
Top Bottom