Swali gumu kidogo: Kwanini Urusi iliyosambaratika na dhaifu kuliko USSR inawasumbua sana NATO?

Swali gumu kidogo: Kwanini Urusi iliyosambaratika na dhaifu kuliko USSR inawasumbua sana NATO?

Ewaah, sawa kabisa na huu ndiyo msingi wa swali langu:
Sasa nchi ambayo imeshindwa kutengeneza Stealth Plane kama zile F-35 inawasumbuaje NATO ??
Uchumi uko chini, imewekewa vikwazo vizito na imetengwa, kwanini wasiimalize tu mara moja ???
Hahaha...mkuu, nakuelewa Sana! Dahlia...ningetumia lugha ya kusema unatu-enjoy!!! Naam, Mimi najifunza kwako/kwenu.
Naam, kuijua mienendo ya dunia.
 
Usumbufu unaoletwa na Urusi ni sawa na ule wa kunguni au chawa tu kwa binadamu. Sababu za usumbufu huo ni tatu:

1. Urusi tofauti na USSR imegeuka kuwa "rogue state" isiyo na lengo kuu la kimfumo (strategic objective) zaidi ya kuwepo tu (mere survival/existence). USSR ilikuwa na lengo la kuigeuza dunia nzima kuwa ya kikomunisti kwa misingi la Marx/Lenin. Hiyo ilishindikana, USSR ikasambaratika na kupoteza ushawishi huo duniani kote. Leo hii Urusi inaongozwa na kikundi maslahi kilichokumbatia madaraka na kugawana fursa za kibepari kwa kubebana (cronyism & patronage). Ukomunisti ulishatupiliwa mbali; sasa ni ma-oligarchs tu yanayojuana na Kremlin. Kikundi hiki kinajua kabisa kuwa maslahi yake yanategemea Marekani na Ulaya. Huko ndiko kwenye uhakika wa uchumi wake. Leo hii nenda Central London utakuta wamiliki wakubwa wa ardhi na mali ni kutoka Urusi/Ukraine. Wamewekeza kweli huko Marekani na Ulaya. Hivyo kila wakati wanahangaika kuhakikisha watu rafiki (sympathetic) (Trump & co.) wanakuwa madarakani.

2. Muhimu sana hawa wahuni (akina Putin) wamerithi rasilimali nzito za kiteknologia ikiwa ni pamoja na za nyuklia, ardhi, maliasili na mifumo ya elimu ya hali ya juu toka USSR. Na hapo wanajitahidi sana kutoa upendeleo kwa watu wao wenye kuweza kuziendeleza rasilimali hizo ili wazitumia kupambana na Marekani na Ulaya. Kule kuwepo kwa miundombinu ya uhakika ya nyuklia na sayansi za anga ni kinga/tishio (deterrence) tosha kwa yeyote atakayefikiria kupambana na Urusi. Tena wakiwa "rogue state" hawajali hata kutoa mhanga idadi kubwa ya watu wao kwa maslahi ya kikundi tawala kilichopo Kremlin. Tofauti na Marekani na Ulaya ambao watu wao wana thamani kubwa sana, wanaojali maisha bora kwa kila mtu na kuna mifumo thabiti ya kusimamia haki za binadamu. Marekani wakijua wanapambana na "wehu" si rahisi kuwavamia Warusi huko Crimea, Syria na kwingineko bila kujihakikishia kutozuka vita ya nyuklia!

3. Marekani na Ulaya ni jamii zilizo wazi (open societies). Mambo yao ni hadharani. Marais wao wakifanya faulo wanapashwa hadharani. Wanachunguzwa hadharani (Robert Mueller on Russian collusion). Wateule wa Rais wanapigwa interview hadharani. n.k. Kwa urusi, hiyo ni sawa na kuanika nguo zao za ndani hadharani. Rais wao (Putin) ni sawa na mungu! Athari zake ni kuwa watu hatari wanapata mianya kibao ya kuendesha uhalifu Marekani na Ulaya. Warusi wanatumia fursa hiyo kujaribu kuhujumu nchi za jumuia ya NATO. Marekani na Ulaya wanalijua hilo lakini hawako tayari kujifungia ndani kama Urusi. badala yake wanajiimarisha kitaaluma kukabiliana na chokochoko za Urusi na wahuni wengine. Na kwa kweli wamefanikiwa. Karibu harakati zote za Warusi wanazijua. Kuna wakati wanajifanya hawana uhakika ili kuwaingiza kwenye mitego.

Akina Putin wanajua vizuri sana kwamba hawaiwezi Marekani na washirika wake wa Ulaya. Kwanza, huko ndiko wanakohifadhia utajiri wao wa kifisadi. Ndiko wanakosomeshea watoto wao na ndiko ambapo kila Mrusi aliyefanikiwa anaotea kuwa na makazi na kumiliki mali kama ilivyo kwa watu wengine wa dunia ya tatu. Kitu nachoamini ni kuwa Urusi wangekuwa na viongozi wenye maono ya hali ya juu, kwa uwezo na rasilimali walizo nazo, wangekuwa tishio sana kwa washirika wa NATO. Bahati mbaya, wanaongozwa na watu wenye tamaa ya mali, madaraka na sifa (ujiko) bila falsafa kuu ya taifa. Watu ambao wanategemea kubebwa na miundombinu iliyowekwa na USSR ambayo sujui kama wataweza kuiimarisha ishindane na ya magharibi huko mbeleni.
 
Usumbufu unaoletwa na Urusi ni sawa na ule wa kunguni au chawa tu kwa binadamu. Sababu za usumbufu huo ni tatu:
Sawa kabisa mkuu na ahsante kwa hoja yako nzuri iliyokaa sana kisomi.
Hebu sasa tupitie huo mfano wako wa usumbufu wa kunguni au chawa kwa binadamu katika hoja zako tatu.


1. Urusi tofauti na USSR imegeuka kuwa "rogue state" isiyo na lengo kuu la kimfumo (strategic objective) zaidi ya kuwepo tu (mere survival/existence). USSR ilikuwa na lengo la kuigeuza dunia nzima kuwa ya kikomunisti kwa misingi la Marx/Lenin. Hiyo ilishindikana, USSR ikasambaratika na kupoteza ushawishi huo duniani kote.

Urusi kuwa Rogue State na kutokuwa na lengo kuu kimfumo hebu tuliangalie kiundani zaidi. Urusi anaitwa Rogue State kwasababu anavunja sheria za kimataifa (International Law) pamoja na tamaduni zake ambazo ziliwekwa na mataifa yaliyoshinda vita ya pili ya dunia kule San Fransisco mwaka 1945. Amevamia Ukraine na kumega Crimea kosa ambalo ni kinyume kabisa na sheria za dunia yetu. Lakini sasa kama Urusi anaitwa Rogue State kwa kuvamia Ukraine mwaka 2014, Marekani aliyevamia Yugoslavia mwaka 1999, Afghanistan mwaka 2001 na Iraq mwaka 2003 bila ruhusa ya Baraza la Ulinzi la Umoja wa mataifa tumwiteje sasa ??? Rogue State au Benign Hegemony ??? (Nijuavyo sheria inakata kote kote)

Pia nifahamuvyo mimi, kuachana na falsafa ya fulani hakukufanyi kuwa umekosa lengo kuu kimfumo. Maana ukiangalia kwa mapana hata Uchina aliachana na International Communist Enterprise na akajikitika katika masoko ya kujenga uchumi wake (Economic Pragmatism). Mwaka 2015 Urusi alitoa chapisho lake la mwelekeo na melengo makuu ya nchi (The National Security Strategy) ambapo aliainisha kila kitu wanachotarajia kukifanya kwa muongo ujao. Hapa utasemaje anatafuta kuwepo tu bila mkakati maalum ??? Au unaamini kwamba tokea mwaka 1999 baada ya Yeltsin kuachia madaraka Urusi imefika hapa kwa bahati nasibu au miujiza tu ??? (Kama umesoma Planning and Development naamini utakuwa umenielewa vizuri)

2. Munimu sana hawa wahuni (akina Putin) wamerithi rasilimali nzito za kiteknologia ikiwa ni pamoja na za nyuklia, ardhi, maliasili na mifumo ya elimu ya hali ya juu toka USSR. Na hapo wanajitahidi sana kutoa upendeleo kwa watu wao wenye kuweza kuziendeleza rasilimali hizo ili wazitumia kupambana na Marekani na Ulaya. Kule kuwepo kwa miundombinu ya uhakika ya nyuklia na sayansi za anga ni kinga/tishio (deterrence) tosha kwa yeyote atakayefikiria kupambana na Urusi.

Umezungumzia kwamba Urusi ni Rogue State na iko radhi kuuwa watu wake kwa ajili ya kikindi cha watu wachache. Hebu nikuulize swali la kihistoria ambalo naamini ni rahisi sana tu: Hivi kati ya Urusi ya Kisovieti (USSR) na Urusi hii ya Putin ipi imeua watu wake sana na kukanyaga haki za binadamu ??? Ipi ni sehemu bora zaidi ya kuishi ??

3. Marekani na Ulaya ni jamii zilizo wazi (open societies). Mambo yao ni hadharani. Marais wao wakifanya faulo wanapashwa hadharani. Wanachunguzwa hadharani (Robert Mueller on Russian collusion). Wateule wa Rais wanapigwa interview hadharani. n.k. Kwa urusi, hiyo ni sawa na kuanika nguo zao za ndani hadharani. Rais wao (Putin) ni sawa na mungu! Athari zake ni kuwa watu hatari wanapata mianya kibao ya kuendesha uhalifu Marekani na Ulaya. Warusi wanatumia fursa hiyo kujaribu kuhujumu nchi za jumuia ya NATO. Marekani na Ulaya wanalijua hilo lakini hawako tayari kujifungia ndani kama Urusi. badala yake wanajiimarisha kitaaluma kukabiliana na chokochoko za Urusi na wahuni wengine. Na kwa kweli wamefanikiwa. Karibu harakati zote za Warusi wanazijua. Kuna wakati wanajifanya hawana uhakika ili kuwaingiza kwenye mitego.

Katika hili nalo nakubaliana na wewe kidogo, lakini bado napata swali jingine gumu la kukuuliza. India ni jamii wazi na ndiyo nchi kubwa ya kidemokrasia hapa duniani (World Largest Democracy) lakini mbona bado kuna kiwango kikubwa sana cha rushwa na uhalifu ni mwingi kuliko hata Uchina ambako kumefungwa (Closed Society) ??? Kubwa zaidi Uchina imepiga hatua kwenye kila kitu kuliko India. Hapa tatizo liko wapi ??? Je, tukiruhusu demokrasia ndiyo tutakuwa tumeruhusu maendeleo ??? (Tafadhali angalia hii mifano vizuri kabla ya kujibu)
 
Mbona umoja wa Kisovieti (USSR) ulimalizwa bila kuleta madhara kwenye usalama wa dunia ???
Au hapa unamaanisha kumalizwa kivipi labda ???
Mie nilimaanisha kivita nhasa kutokana na swali lako "Sasa najiuliza kwanini taifa hili dhaifu ambalo lililoshindwa vita baridi linaendelea kumsumbua Marekani (The Only Super Power) pamoja na washirika wake kijeshi ambao ni zaidi ya 25 ??" . Labda maelezo ya ziada yanatakiwa tujue Marekani anasumbuliwa kivipi na situation gani iwepo ili aonekane hasumbuliwi.

Jinsi umoja wa kisoviet ilivyomalizwa ni mada ndefu na nafikiri haiwezi kuwa credited to NATO/US in its entirety. Matatizo ya ndani ya USSR kutokana na viongozi wa Communist Party kujilimbikizia mali kulileta manung'uniko kutoka kwa younde generation ambayo haikukubaliana na ideology ya wazazi wao. Vile vile reforms alizoleta Gorbachev kupitia sera zake za glasnost na perestroika hazikuleta mafanikio yaliyotarajiwa zaidi ya kusababisha uhaba wa bidhaa muhimu. Inaonyesha kuwa hata kuanguka kwa USSR hakukutegemewa na nchi za magharibi. Siutendei haki uzi huu kwa kutoa jibu hili kwani ni topic ndefu inayohitaji research kabla ya kuandika. Lakini kwa haya machache, inanyesha kuwa nchi za magharibi hazikusababisha umoja wa USSR kumalizwa, na kwa hiyo hakuna sababu ya kujiuliza kwa nini wasiimalize Russia ya sasa kama walivyoimaliza USSR. Na hata kama kweli waliimaliza USSR, haina maana ndio wana mkakati wa kuimaliza Russia sasa hivi.
 
Mie nilimaanisha kivita nhasa kutokana na swali lako "Sasa najiuliza kwanini taifa hili dhaifu ambalo lililoshindwa vita baridi linaendelea kumsumbua Marekani (The Only Super Power) pamoja na washirika wake kijeshi ambao ni zaidi ya 25 ??" . Labda maelezo ya ziada yanatakiwa tujue Marekani anasumbuliwa kivipi na situation gani iwepo ili aonekane hasumbuliwi.

Jinsi umoja wa kisoviet ilivyomalizwa ni mada ndefu na nafikiri haiwezi kuwa credited to NATO/US in its entirety. Matatizo ya ndani ya USSR kutokana na viongozi wa Communist Party kujilimbikizia mali kulileta manung'uniko kutoka kwa younde generation ambayo haikukubaliana na ideology ya wazazi wao. Vile vile reforms alizoleta Gorbachev kupitia sera zake za glasnost na perestroika hazikuta mafanikio yaliyotarajiwa zaidi ya kusababisha uhaba wa bidhaa muhimu. Inaonyesha kuwa hata kuanguka kwa USSR hakukutegemewa na nchi za magharibi. Siutendei haki uzi huu kwa kutoa jibu hili kwani ni topic ndefu inayohitaji research kabla ya kuandika. Lakini kwa haya machache, inanyesha kuwa nchi za magharibi hazikusababisha umoja wa USSR kumalizwa, na kwa hiyo hakuna sababu ya kujiuliza kwa nini wasiimalize Russia ya sasa kama walivyoimaliza USSR. Na hata kama kweli waliimaliza USSR, haina maana ndio wana mkakati wa kuimaliza Russia sasa hivi.

Anhaa kwahiyo Raisi Ronald Raegan alivyosema "And Ooh yes we won the cold war" alikuwa anafanya propaganda tu, wala hakuna ukweli wowote ule ???
 
China is cominng dear friend.

Sent using Jamii Forums mobile app
kweli kabisa na tena ana nafasi kubwa ya kufanya vizuri zaidi kuliko russia na marekani, anapiga hatua kwa kasi kwnye tech, uchumi na kijeshi, anachokikosa uchina ni ushawish mkubwa kisiasa but hicho kitakuja tu chenyew kadri uchumi wake unavyozidi kukua
 
Anhaa kwahiyo Raisi Ronald Raegan alivyosema "And Ooh yes we won the cold war" alikuwa anafanya propaganda tu, wala hakuna ukweli wowote ule ???
Labda. Sina facts zote za kilichotokea zaidi ya hizo sources nilizoweka hapo juu. Na kwa upande mwingine anaweza kuwa sahihi kusema hivyo kwani kama raisi anafahamu zaidi sana ya mimi kitu halisi kilichosababisha kwa USSR kuanguka. Lakini haimaanishi kuwa kwa sababu mwanzo walifanya hivyo, na sasa wafanye hivyo vile vile. Majibu yeyote yatakayopatikana hapa ni speculations tu. Ukweli wanajua US na washirika wake.

Ila ni vyema tujue Marekani anasumbuliwa kivipi na situation gani iwepo ili aonekane hasumbuliwi. Inawezekana tuna address swali tofauti na mletaji alivyotaka.
 
Sawa kabisa mkuu na ahsante kwa hoja yako nzuri iliyokaa sana kisomi.
Hebu sasa tupitie huo mfano wako wa usumbufu wa kunguni au chawa kwa binadamu katika hoja zako tatu.




Urusi kuwa Rogue State na kutokuwa na lengo kuu kimfumo hebu tuliangalie kiundani zaidi. Urusi anaitwa Rogue State kwasababu anavunja sheria kimataifa (International Law) pamoja na tamaduni zake ambazo ziliwekwa na mataifa yaliyoshinda vita ya pili ya dunia kule San Fransisco mwaka 1945. Amevamia Ukraine na kumega Crimea kosa ambalo ni kinyume kabisa na sheria za dunia yetu. Lakini sasa kama Urusi anaitwa Rogue State kwa kuvamia Ukraine mwaka 2014, Marekani aliyevamia Yugoslavia mwaka 1999, Afghanistan mwaka 2001 na Iraq mwaka 2003 bila ruhusa ya Baraza la Ulinzi la Umoja wa mataifa tumwiteje sasa ??? Rogue State au Benign Hegemony ??? (Nijuavyo sheria inakata kote kote)

Pia nifahamuvyo mimi, kuachana na falsafa ya fulani hakukufanyi kuwa umekosa lengo kuu kimfumo. Maana ukiangalia kwa mapana hata Uchina aliachana na International Communist Enterprise na akajikitika katika masoko ya kujenga uchumi wake (Economic Pragmatism). Mwaka 2015 Urusi alitoa chapisho lake la mwelekeo na melengo makuu ya nchi (The National Security Strategy) ambapo aliainisha kila kitu wanachotarajia kukifanya kwa muongo ujao. Hapa utasemaje anafuta kuwepo tu bila mkakati maalum ??? Au unaamini kwamba tokea mwaka 1999 baada ya Yeltsin kuachia madaraka Urusi imefika hapa kwa bahati nasibu au miujiza tu ??? (Kama umesoma Planning and Development naamini utakuwa umenielewa vizuri)



Umezungumzia kwamba Urusi ni Rogue State na iko radhi kuuwa watu wake kwa ajili ya kikindi cha watu wachache. Hebu nikuulize swali la kihostoria ambalo naamini ni rahisi sana tu: Hivi kati ya Urusi ya Kisovieti (USSR) na Urusi hii ya Putin ipi imeua watu wake sana na kukanyaga haki za binadamu ??? Ipi ni sehemu bora zaidi ya kuishi ??



Katika hili nalo nakubaliana na wewe kidogo, lakini bado napata swali jingine gumu la kukuuliza. India ni jamii wazi na ndiyo nchi kubwa ya kidemokrasia hapa duniani (World Largest Democracy) lakini mbona bado kuna kiwango kikubwa sana cha rushwa na uhalifu ni mwingi kuliko hata Uchina ambako kumefungwa (Closed Society) ??? Kubwa zaidi Uchina imepiga hatua kwenye kila kitu kuliko India. Hapa tatizo liko wapi ??? Je, tukiruhusu demokrasia ndiyo tutakuwa tumeruhusu maendeleo ??? (Tafadhali angalia hii mifano vizuri kabla ya kujibu)
Mkuu umeandika vizuri sana.Ila mimi nin swali dogo tu hapo kwenye paragraph yako ya mwisho kuhusu uchumi na Demokrasia,ulipozilinganisha India na China.Tunafahamu kuwa nchi hizo mbili zipo tofauti sana,nchi zimeundwa katika mifumo tofauti zikiwa na jamii tofauti. Kwa mfano wako huo wa demokrasia/rushwa na maendeleo kwa nini usilinganishe nchi ambazo zina historia sawa ? Kwa mfano linganisha South Korea na North Korea. Zote roughly the same size,jamii ni ile ile,geographic location almost identical,mtawala alikuwa mmoja na uhuru ulipatikana wakati mmoja na mtawala wao alikuwa mmoja.Tofauti ni kwamba South kuna democrasia na uwazi (ndo maana wamemfunga Park Geun-hye) kwa rushwa.
 
Sawa kabisa mkuu na ahsante kwa hoja yako nzuri iliyokaa sana kisomi.
(Nijuavyo sheria inakata kote kote)


Katika hili nalo nakubaliana na wewe kidogo, lakini bado napata swali jingine gumu la kukuuliza. India ni jamii wazi na ndiyo nchi kubwa ya kidemokrasia hapa duniani (World Largest Democracy) lakini mbona bado kuna kiwango kikubwa sana cha rushwa na uhalifu ni mwingi kuliko hata Uchina ambako kumefungwa (Closed Society) ??? Kubwa zaidi Uchina imepiga hatua kwenye kila kitu kuliko India. Hapa tatizo liko wapi ??? Je, tukiruhusu demokrasia ndiyo tutakuwa tumeruhusu maendeleo ??? (Tafadhali angalia hii mifano vizuri kabla ya kujibu)
Mkuu we sio mtu mzuri umempa jamaa moyo apo kwa apo una muuliza maswali magumu kuliko ya mahakamani !!?
Maswali magum sana kuyajibu labda uambiwe kushoto ni kulia!!
 
Mkuu umeandika vizuri sana.Ila mimi nin swali dogo tu hapo kwenye paragraph yako ya mwisho kuhusu uchumi na Demokrasia,ulipozilinganisha India na China.Tunafahamu kuwa nchi hizo mbili zipo tofauti sana,nchi zimeundwa katika mifumo tofauti zikiwa na jamii tofauti. Kwa mfano wako huo wa demokrasia/rushwa na maendeleo kwa nini usilinganishe nchi ambazo zina historia sawa ? Kwa mfano linganisha South Korea na North Korea. Zote roughly the same size,jamii ni ile ile,geographic location almost identical,mtawala alikuwa mmoja na uhuru ulipatikana wakati mmoja na mtawala wao alikuwa mmoja.Tofauti ni kwamba South kuna democrasia na uwazi (ndo maana wamemfunga Park Geun-hye) kwa rushwa.
Labda hukunielewa vizuri. Hoja ya mkuu Drifter ni kwamba Urusi iko nyuma ya Marekani kwasababu ni jamii iliyofungwa. Akasema kwamba jamii ya Urusi ikifungua mfumo wake na kupata viongozi wenye maono itafika mbali sana na kuwa tishio kwa NATO.

Mimi nikasema kuna jamii ambazo ziko wazi na bado siyo tishio na zina matatizo lukuki kuliko hata jamii zilizofungwa. Nikatoa mfano wa majirani na mahasimu wakubwa sana ambao ni India na Uchina. Nimezilinganisha hizi nchi kwasababu kuu zifuatazo:

Mosi,
Zote zimepata uhuru wa kisiasa kwa wakati mmoja. India Uhuru mwaka 1948 na huku mapinduzi ya Ukomunisti mwaka 1949. Hazikupishana sana kiuchumi lakini leo 2018 Uchina ni wa pili kiuchumi.


Pili
Zote ni nchi ambazo zimeendelea kwa ghafla na kufika kiwango kikubwa sana cha mafanikio ndani ya muda mfupi sana bila kutawala mataifa mengine kama ambavyo Ulaya na Marekani walifanya mnamo karne ya 18, 19 na 20. Lakini leo hii Uchina ni wa pili kiuchumi na India ni wa tano.


Tatu,
Zote ni nchi zenye idadi ya watu inayoringana. Uchina ana watu Bilioni 1.4 huku India akiwa na watu Bilioni 1.3. Hivyo faida anazopata Uchina kitokana na idadi ya watu ndiyo inategemewa apate pia India.


Nne,
Zote ni nchi zinazotegemea teknolojia, masoko na uwekezaji kutoka Ulaya, Marekani na Urusi kwa kiasi kikubwa sana ili kusukuma chumi zao. Maana hata kama wana teknolojia sehemu kubwa siyo yao


Hivyo nikatoa mfano kwa ndugu Drifter kwamba kama tatizo ni Demokrasia mbona India taifa ambalo ni la kidemokrasia na huru halijadiriki kulifikia taifa la kikomunisti na la kidikteta Uchina kwenye mambo mengi sana ??? Kuanzia nidhamu, kupambana na rushwa, uwajibikaji na uchapakazi

NB: Uchina na India zinalingana sana kuliko tunavyoweza kufikiri
 
KISIASA
1. Amesababisha sintofahamu kubwa ndani ya siasa za Marekani hasa kwa Donald Trump.
2. Anavuruga mipango ya Marekani kwa kutumia VETO kule Umoja wa Mataifa.
3. Amefanikiwa kuugawanya Umoja wa Ulaya (Schoeder wa Ujerumani anafanya kazi Rosneft)
4. Anaisaidia Korea Kaskazini kukwepa vikwazo vya Umoja wa Mataifa.
5. Alimsaidia Raisi wa Uturuki asipinduliwe na kuuwawa ambapo inasemekana CIA walihusika sana.
6. Amemtunza Edward Snowden ambaye kavujisha siri nyeti za Marekani.


KIJESHI
1. Kavamia Ukraine kijeshi na kumega Crimea kwa nguvu mno ya wanajeshi 70,000.
2. Kavuruga mpango wa Marekani na Israel wa kuvamia Syria na kumtoa Assad.
3. Anauza silaha nzito kwa mataifa hasimu wa Marekani kama Iran.
4. Anasidia Korea Kaskazini kukwepa vikwazo vya Umoja wa Mataifa.
5. Amevuruga majimbo ya Lugansk na Donestky hadi leo majeshi ya Ukraine hayana amani.
7. Yeye ndiyo mwenye jeshi la pili kwa ubora hapa duniani mbali na shida zote kiuchumi.


KITEKNOLOJIA
1. Marekani mpaka leo anategemea injini kutoka Urusi kwa ajili ya kurusha roketi zake.
2. Ametengeneza makombora mazito ambayo yanasafiri mara 10 zaidi ya sauti.
3. Walimwekea vikwazo vya injini za ndege kutoka Ukraine lakini katengeneza zake kwa haraka sana.
4. Ana wasomi wa sayansi ambao ni World Class kama 1,000,000 hivi.
5. Teknolojia ya kimtandao (Cyber Technology) yuko mbele sana na amethibitishia dunia mara nyingi.



KIUCHUMI
1. Amefanikiwa kutumia makampuni yake ya nishati kuwaumiza Ulaya hasa NORD Stream 2.
2. Amefanikiwa kutumia ushawishi wa nishati kuyavuta karibu mataifa kama Uchina, India na Uturuki.
3. Uturuki ameagiza silaha kutoka Urusi kitu ambacho kitampa faida za kiuchumi Mrusi.
4. Saudi Arabia ametengeneza viwanda vya Kalashnikov Ak-47 nchini kwake na Urusi karuhusu.
5. Amesaidia kutengeneza vyombo kama BRICS, The Shanghai Cooperation na Eurasia Economic Union


NB: Haya ni machache tu, sasa nchi iliyosambaratika inalisumbuaje taifa kubwa duniani ??
Hapo hakuna sababu hata moja inayoonyesha Russia anasumbua marekani, hivi kuiuzia nchi nyingine vitu ni kuisumbua marekani!!, haya sisi Tanzania tunapoiuzia China magogo tunaisumbua nchi gani?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Labda hukunielewa vizuri. Hoja ya mkuu Drifter ni kwamba Urusi iko nyuma ya Marekani kwasababu ni jamii iliyofungwa. Akasema kwamba jamii ya Urusi ikifungua mfumo wake na kupata viongozi wenya maono itafika mbali sana na kuwa tishia kwa NATO.

Mimi nikasema kuna jamii ambazo ziko wazi na bado siyo tishio na zina matatizo lukuki kuliko hata jamii zilizofungwa. Mikatoa mfano wa majirani na mahasimu wakubwa sana ambao ni India na Uchina. Nimeziringanisha hizi nchi kwasababu moja kuu zifuatazo:

Mosi,
Zote zimepata uhuru wa kisiasa kwa wakati mmoja. India Uhuru mwaka 1948 na huku mapinduzi ya Ukomunisti mwaka 1949. Hazikupishana sana kiuchumi lakini leo 2018 Uchina ni wa pili.


Pili
Zote ni nchi ambazo zimeendelea kwa ghafla na kufika kiwango kikubwa sana cha mafanikio ndani ya muda mfupi sana bila kutawala mataifa mengine kama ambavyo Ulaya na Marekani walifanya mnamo karne ya 18, 19 na 20. Leo hii Uchina ni wa pili kiuchumi na India ni wa tano.


Tatu,
Zote ni nchi zenye idadi ya watu inayoringana. Uchuna ana watu Bilioni 1.4 huku India akiwa na watu Bilioni 1.3. Hivyo faida anazopata Uchina kitokana na idadi ya watu ndiyo inategemewa apate pia India.


Nne,
Zote ni nchi zinazotegemea teknolojia, masoko na uwekezaji kutoka Ulaya, Marekani na Urusi kwa kiasi kikubwa sana ili kusukuma chumi zao. Maana hata kama wana teknolojia sehemu kubwa siyo yao


Hivyo nikatoa mfano kwa ndugu Drifter kwamba kama tatizo ni Demokrasia mbona India taifa ambalo ni la kidemokrasia na huru halijadiriki kulifikia taifa la kikomunisti na la kidikteta Uchina kwenye mambo mengi sana ??? Kuanzia nidhamu, kupambana na rushwa, uwajibikaji na uchapakazi

NB: Uchina na India zinaringana sana kuliko tunavyoweza kufikiri
Asante sana mkuu kwa jibu lililoenda shule. Nimekupata barabara.
 
Mkuu umeandika vizuri sana.Ila mimi nin swali dogo tu hapo kwenye paragraph yako ya mwisho kuhusu uchumi na Demokrasia,ulipozilinganisha India na China.Tunafahamu kuwa nchi hizo mbili zipo tofauti sana,nchi zimeundwa katika mifumo tofauti zikiwa na jamii tofauti. Kwa mfano wako huo wa demokrasia/rushwa na maendeleo kwa nini usilinganishe nchi ambazo zina historia sawa ? Kwa mfano linganisha South Korea na North Korea. Zote roughly the same size,jamii ni ile ile,geographic location almost identical,mtawala alikuwa mmoja na uhuru ulipatikana wakati mmoja na mtawala wao alikuwa mmoja.Tofauti ni kwamba South kuna democrasia na uwazi (ndo maana wamemfunga Park Geun-hye) kwa rushwa.
Ni kweli Korea kaskazini na Korea kusini ni nchi ambazo zipo eneo moja kijiografia lakini huwezi kuzifananisha kimaendeleo kwa muktadha wako,
Korea kaskazini na Korea kusini
ni kama mabondia wawili wanaopigna lakini mmoja kafungwa mikono ambaye ni Korea kaskazini na mwingine hajafungwa ambaye ni Korea kusini hawawezi kuwa na usawa katika kupigana

Ni kwamba huwezi kufananisha nchi iliyowekewa vikwazo na nchi yenye biashara huru

Halafu demokrasia ni mfumo tu sio nguzo au kisababishi cha kuleta maendeleo, japo demokrasia ni muhimu haswa kwa nchi kama yetu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom