Swali gumu kidogo: Kwanini Urusi iliyosambaratika na dhaifu kuliko USSR inawasumbua sana NATO?

Swali gumu kidogo: Kwanini Urusi iliyosambaratika na dhaifu kuliko USSR inawasumbua sana NATO?

Ni kweli Korea kaskazini na Korea kusini ni nchi ambazo zipo eneo moja kijiografia lakini huwezi kuzifananisha kimaendeleo kwa muktadha wako,
Korea kaskazini na Korea kusini
ni kama mabondia wawili wanaopigna lakini mmoja kafungwa mikono ambaye ni Korea kaskazini na mwingine hajafungwa ambaye ni Korea kusini hawawezi kuwa na usawa katika kupigana

Ni kwamba huwezi kufananisha nchi iliyowekewa vikwazo na nchi yenye biashara huru

Halafu demokrasia ni mfumo tu sio nguzo au kisababishi cha kuleta maendeleo, japo demokrasia ni muhimu haswa kwa nchi kama yetu

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu asante sana kwa hiyi reply yako na huwa napenda sana kujadiliana na watu ambao kichwani wapo sawa,na wewe upo sawa haswa.Ukwe;i ni kwamba nchi za magharibi zinachagua nani wa kumuwekea vikwazo na nani wa kumuachia huru kulingana na matakwa yao wenyewe.Kwa mfano China hakuna demokrasia na ukiinua kichwa wanakutwanga(Tianmanen square masacre 1989,sijui wewe ulikuwa wapi). Na hawakuwekewa vikwazo ambavyo ni nail biting. Western countries ndo sababu kubwa sana ya china kuendelea. Ingawa China ipo number 2 lakini living standard average chinese ipo way below Japanese. Kwa kiasi fulani nakubaliana na wewe kuwa demokrasia(kama inavyokuwa defined na western countries) sio kichocheo cha maendeleo.Kuna mifano mingi ya nchi ambazo hazina demokrasia( As defined by western countries) lakini zimeendelea,kwa mfano China,Saudi Arabia,Qatar etc etc.Lakini ukichukua data na kuangalia nchi tajiri na wananchi wana maisha mazuri zaidi unaona nchi gani zinakuwa nyingi ? Zenye Democrasia au zisizo na Demokrasia ?Nawasilisha
 
Sawa kabisa mkuu na ahsante kwa hoja yako nzuri iliyokaa sana kisomi.
Hebu sasa tupitie huo mfano wako wa usumbufu wa kunguni au chawa kwa binadamu katika hoja zako tatu.




Urusi kuwa Rogue State na kutokuwa na lengo kuu kimfumo hebu tuliangalie kiundani zaidi. Urusi anaitwa Rogue State kwasababu anavunja sheria kimataifa (International Law) pamoja na tamaduni zake ambazo ziliwekwa na mataifa yaliyoshinda vita ya pili ya dunia kule San Fransisco mwaka 1945. Amevamia Ukraine na kumega Crimea kosa ambalo ni kinyume kabisa na sheria za dunia yetu. Lakini sasa kama Urusi anaitwa Rogue State kwa kuvamia Ukraine mwaka 2014, Marekani aliyevamia Yugoslavia mwaka 1999, Afghanistan mwaka 2001 na Iraq mwaka 2003 bila ruhusa ya Baraza la Ulinzi la Umoja wa mataifa tumwiteje sasa ??? Rogue State au Benign Hegemony ??? (Nijuavyo sheria inakata kote kote)

Sijaitoa Marekani kwa vitendo vya kuwa rogue state. Lakini Marekani ina mfumo unaowezesha wananchi wake kujadili na "kuhukumu" watawala wao kwa maamuzi ya kihuni. Kwa mfano, rejea upinzani mkubwa wa ndani uliojitokeza kwenye vita za Vietnam na Iraq. Urusi iwe enzi za USSR au Russia Federation, hakuna mtu mwenye ubavu wa kuiuliza serikali kitu. It's always been a totalitarian state.

Pia nifahamuvyo mimi, kuachana na falsafa ya fulani hakukufanyi kuwa umekosa lengo kuu kimfumo. Maana ukiangalia kwa mapana hata Uchina aliachana na International Communist Enterprise na akajikitika katika masoko ya kujenga uchumi wake (Economic Pragmatism). Mwaka 2015 Urusi alitoa chapisho lake la mwelekeo na melengo makuu ya nchi (The National Security Strategy) ambapo aliainisha kila kitu wanachotarajia kukifanya kwa muongo ujao. Hapa utasemaje anatafuta kuwepo tu bila mkakati maalum ??? Au unaamini kwamba tokea mwaka 1999 baada ya Yeltsin kuachia madaraka Urusi imefika hapa kwa bahati nasibu au miujiza tu ??? (Kama umesoma Planning and Development naamini utakuwa umenielewa vizuri)

China wana mkakati kamili wa kuwa world economi and strategic power na wamejijengea nidhamu ya kimfumo kuelekea huko japo binafsi sipatani kabisa na totalitarian states. Urusi kiasi kikubwa inafanana na mafia state.

Umezungumzia kwamba Urusi ni Rogue State na iko radhi kuuwa watu wake kwa ajili ya kikindi cha watu wachache. Hebu nikuulize swali la kihostoria ambalo naamini ni rahisi sana tu: Hivi kati ya Urusi ya Kisovieti (USSR) na Urusi hii ya Putin ipi imeua watu wake sana na kukanyaga haki za binadamu ??? Ipi ni sehemu bora zaidi ya kuishi ??

Totalitarian states zote ziwe za kikomunisti au kibepari hazijali kabisa uhai na haki za binadamu. Zote zinaongozwa na vikundi iwe ni "party vanguards", juntas, oligarchs na "ruling cliques" za aina zote, vyenye tabia ya kutumia binadamu wenzao kama poni (pawns) katika kutimiza maslahi yao. Inapokuja suala la uhai na haki za binadamu huwa sipimi kwa idadi ya waliouwawa. It's all tragic! Kwa hapo, USSR na Russian Federation kwangu mimi ni walewale.

Katika hili nalo nakubaliana na wewe kidogo, lakini bado napata swali jingine gumu la kukuuliza. India ni jamii wazi na ndiyo nchi kubwa ya kidemokrasia hapa duniani (World Largest Democracy) lakini mbona bado kuna kiwango kikubwa sana cha rushwa na uhalifu ni mwingi kuliko hata Uchina ambako kumefungwa (Closed Society) ??? Kubwa zaidi Uchina imepiga hatua kwenye kila kitu kuliko India. Hapa tatizo liko wapi ??? Je, tukiruhusu demokrasia ndiyo tutakuwa tumeruhusu maendeleo ??? (Tafadhali angalia hii mifano vizuri kabla ya kujibu)

Careful, kuhusu kuiona China imepiga hatua kubwa. Jua kuna idadi kubwa ya Wachina wanaishi kwa dhiki sana nchini mwao. Inategemeana unavyopima maendeleo. Matajiri wakubwa China wanasomesha watoto wao Marekani na Ulaya; wamewekeza utajiri mkubwa huko na wanamiliki makazi huko. Wana akaunti nzito za dollars, Euro, Pounds, n.k.

Tukija kwenye suala la India, ni open society kweli lakini isiyo na mifumo imara ya utawala. Hivyo, rushwa lazima iwe kubwa na "ionekane". Marekani na ulaya ni open lakini wana mifumo advanced ya kudhibiti graft. China ni "closed" na kama kawaida ya jamii "closed" rushwa yao ni ya kimfumo na inadhibitiwa kati ya wateule tu. Hao wanajichotea mabilioni na hayasikiki nje ya wigo wao. Ukisikia China watu wanahukumiwa kwa rushwa ni wale walio nje ya wigo wa ruling class na walioanguka toka kwenye ufalme (fall from grace) - kwa sababu za kisiasa zaidi. Tena kesi zao zina maajabu. Utakuta mtu aliyekuwa mzito anasimamishwa mahakamani anakiri "kuhujumu uchumi" na kuomba radhi kisha anapigwa risasi. I have no iota of admiration for such a state!

Hakuna namna tunaweza kupata na kujivunia maendeleo ya kweli nje ya mfumo wa demokrasia. Na hakuna kitu kinachoniudhi kama unafiki mkubwa wa wale wanaopendelewa na mifumo ya kidikteta kudai kwamba eti demokrasia haitufai kama tunataka maendeleo. Eti ni urithi mbaya toka kwa wakoloni! Tunaishi mara moja tu hapa duniani. Ili maendeleo yetu yawe na maana katika maisha yetu, tujitahidi kufikia hatua kama zilizofikiwa na Marekani na Ulaya (unaweza kuongeza japan, S. Korea, n.k). Japan walikuwa na maendeleo makubwa chini ya mfalme lakini walipaa zaidi kitaifa na kibinafsi baada ya kuachana na udikteta wa kifalme na kujiunga na ulimwengu wa demokrasia.
 
Bw. Lumumba, samahani, sijui namna ya kutumia "multiquotes" na muda wangu JF ni limited sana.
 
NATO kwa pamoja wana idadi ya watu milioni 603.73.
URUSI peka yake ana idadi ya watu milioni 144.3.
NB: NATO ina watu mara sita zaidi ya Urusi lakini kwanini iwasumbue ??
MALCOM LUMUMBA

NAONA NDUGU UNAYATUMIA VIBAYA MAJINA YA WANAZUONI WAKUBWA DUNIA HII

TAYARI HAPO AWALI UMESHATAJA NGUVU ALIZONAZO MRUSI,HALAFU BADO UNAJIULIZA KWA NN ANAMSUMBUA MMAREKANI

JE HUONI KUWA HIZO NGUVU MRUSI ALIZONAZO KUWA NDIZO ANAZOZITUMIA KUMCHACHAFYA MUAMERIKA?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umoja wa Kisovieti (USSR au CCCP) taifa lililozaliwa mwaka 1914-1991,
Lilikuwa ni moja ya taifa lenye nguvu sana duniani lakini lenye mwisho mbaya sana ambao ni aibu kwa watu wake mpaka leo. Kiuchumi walikuwa wana nguvu sana, kiteknolojia walikuwa mbele, nguvu kubwa ya viwanda, kijeshi walikuwa mbele na mifumo yao ya kitamaduni iliyotokana na ukomunisti ilishawishi dunia kuanzia barani Marekani, Asia hadi Afrika na kubwa ziadi walikuwa na idadi kubwa sana ya watu ambapo takwimu zinasema kwamba walikuwa ni milioni 293.


Lakini baada ya kusambaratika nchi hii ilipoteza kila kitu ambacho ilikuwa nacho kuanzia Idadi ya watu, jeshi, viwanda na teknolojia maana kila nchi iliondoka na watu wake, majeshi yake na sehemu kama Ukraine ikapata viwanda vya bure kabisa, Poland na Georgia nao hawakuwa nyuma kabisa. Ikawa nchi dhaifu na masikini kweli....

Sasa najiuliza kwanini taifa hili dhaifu ambalo lililoshindwa vita baridi linaendelea kumsumbua Marekani (The Only Super Power) pamoja na washirika wake kijeshi ambao ni zaidi ya 25 ???

CC: chige , FisadiKuu
Mzeee huyo sio dhaifu bado wapo vizur sana kijeshi na technology japo ni kweli uchumi waliyumba lakin bado wanamiliki eneo kubwa zaid kwenye nchi yao ile ya awali

Sent using Jamii Forums mobile app
 
KISIASA
1. Amesababisha sintofahamu kubwa ndani ya siasa za Marekani hasa kwa Donald Trump.
2. Anavuruga mipango ya Marekani kwa kutumia VETO kule Umoja wa Mataifa.
3. Amefanikiwa kuugawanya Umoja wa Ulaya (Schoeder wa Ujerumani anafanya kazi Rosneft)
4. Anaisaidia Korea Kaskazini kukwepa vikwazo vya Umoja wa Mataifa.
5. Alimsaidia Raisi wa Uturuki asipinduliwe na kuuwawa ambapo inasemekana CIA walihusika sana.
6. Amemtunza Edward Snowden ambaye kavujisha siri nyeti za Marekani.


KIJESHI
1. Kavamia Ukraine kijeshi na kumega Crimea kwa nguvu mno ya wanajeshi 70,000.
2. Kavuruga mpango wa Marekani na Israel wa kuvamia Syria na kumtoa Assad.
3. Anauza silaha nzito kwa mataifa hasimu wa Marekani kama Iran.
4. Anasidia Korea Kaskazini kukwepa vikwazo vya Umoja wa Mataifa.
5. Amevuruga majimbo ya Lugansk na Donestky hadi leo majeshi ya Ukraine hayana amani.
7. Yeye ndiyo mwenye jeshi la pili kwa ubora hapa duniani mbali na shida zote kiuchumi.


KITEKNOLOJIA
1. Marekani mpaka leo anategemea injini kutoka Urusi kwa ajili ya kurusha roketi zake.
2. Ametengeneza makombora mazito ambayo yanasafiri mara 10 zaidi ya sauti.
3. Walimwekea vikwazo vya injini za ndege kutoka Ukraine lakini katengeneza zake kwa haraka sana.
4. Ana wasomi wa sayansi ambao ni World Class kama 1,000,000 hivi.
5. Teknolojia ya kimtandao (Cyber Technology) yuko mbele sana na amethibitishia dunia mara nyingi.



KIUCHUMI
1. Amefanikiwa kutumia makampuni yake ya nishati kuwaumiza Ulaya hasa NORD Stream 2.
2. Amefanikiwa kutumia ushawishi wa nishati kuyavuta karibu mataifa kama Uchina, India na Uturuki.
3. Uturuki ameagiza silaha kutoka Urusi kitu ambacho kitampa faida za kiuchumi Mrusi.
4. Saudi Arabia ametengeneza viwanda vya Kalashnikov Ak-47 nchini kwake na Urusi karuhusu.
5. Amesaidia kutengeneza vyombo kama BRICS, The Shanghai Cooperation na Eurasia Economic Union


NB: Haya ni machache tu, sasa nchi iliyosambaratika inalisumbuaje taifa kubwa duniani ??
Wewe umetumwa nn?
Nikisikia Russia uwa nachukia Sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
MALCOM LUMUMBA

NAONA NDUGU UNAYATUMIA VIBAYA MAJINA YA WANAZUONI WAKUBWA DUNIA HII

TAYARI HAPO AWALI UMESHATAJA NGUVU ALIZONAZO MRUSI,HALAFU BADO UNAJIULIZA KWA NN ANAMSUMBUA MMAREKANI

JE HUONI KUWA HIZO NGUVU MRUSI ALIZONAZO KUWA NDIZO ANAZOZITUMIA KUMCHACHAFYA MUAMERIKA?

Sent using Jamii Forums mobile app
Naondoa hoja baada ya kuufatilia uzi

Nilichogundua hapo awali bwana Malcom ulikuwa unachokoza mada huku ukweli ukiufahamu

KWELI LEO KATIKA SIKU AMBAZO GREAT THINKERS IMETENDEWA HAKI BASI LEO NI SIKU YENYEWE

KEEP UP GUYS

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kila nchi ni mfungwa wa jiograph..NATO kwa wingi wao wanategema udhaifu wa masoko hafidhina kiitikadi..uimara wa soko hafidhina ni msiba kwa NATO..ili uwe imara sokoni lazima uwe na maliasili hasa gas,mafuta na chuma pia mlango bahari wa maji moto bila kusahau rasilimali watu[IQ kubwa]..jeuri ya russia ni maliasili,innovation na ufundi[IQ].....globalization iliasisiwa NATO waki assume hakuna ng'ombe kama China ataja ibuka...China na NATO wanakiu ya maliasili ambayo Russia anayo tele ila mbabe....kumwangusha China lazima uanze na russia ....kiitikadi ni walewale..kimsingi USSR haikufa ila imevaa ngozi ya kondoo..inasubiri mlango bahari wa arctic uwe moto ndiyo kitu pekee hawana....tukumbuke tu kwamba wapo syria kuweka bendera ya kiu ya energy duniani.
 
daaaahh ahasanteni wakuu" nimeelimika vyakutosha ".
 
Umoja wa Kisovieti (USSR au CCCP) taifa lililozaliwa mwaka 1914-1991,
Lilikuwa ni moja ya taifa lenye nguvu sana duniani lakini lenye mwisho mbaya sana ambao ni aibu kwa watu wake mpaka leo. Kiuchumi walikuwa wana nguvu sana, kiteknolojia walikuwa mbele, nguvu kubwa ya viwanda, kijeshi walikuwa mbele na mifumo yao ya kitamaduni iliyotokana na ukomunisti ilishawishi dunia kuanzia barani Marekani, Asia hadi Afrika na kubwa ziadi walikuwa na idadi kubwa sana ya watu ambapo takwimu zinasema kwamba walikuwa ni milioni 293.


Lakini baada ya kusambaratika nchi hii ilipoteza kila kitu ambacho ilikuwa nacho kuanzia Idadi ya watu, jeshi, viwanda na teknolojia maana kila nchi iliondoka na watu wake, majeshi yake na sehemu kama Ukraine ikapata viwanda vya bure kabisa, Poland na Georgia nao hawakuwa nyuma kabisa. Ikawa nchi dhaifu na masikini kweli....

Sasa najiuliza kwanini taifa hili dhaifu ambalo lililoshindwa vita baridi linaendelea kumsumbua Marekani (The Only Super Power) pamoja na washirika wake kijeshi ambao ni zaidi ya 25 ???

CC: chige , FisadiKuu
Hoja nzuri sana hii,Mkuu ML
kwanza kabisa Urusi sio taifa dhaifu kabisa na wala halikuwahi kuwa dhaifu maishani,bali hizo ni propaganda za Mahasimu wake,bali Urusi iliwahi kupata ajali na kuugua,(ajali ni kuvunjika kwa umoja wa kisoviet,na kuugua ni madahra ya kupata ajali )yaani majeraha ya kuvunjiika Usovieti.
Ukuu wa Urusi ni uwezo wake wa kurudi haraka kutoka kwenye kuuguza majeraha(,kuvunjiaka usoviet).
Ni kweli haja ya Marekani ni kuitawala dunia bila upinzani wowote.
Sio tu furaha ya Marekani ilikua ni kuvunjika kwa Usoviet,bali kumaliza kabisa ushawishi, na allies wa Urusi,ndipo juhudi za kizigawa nchi zilizokua Warsaw pact ,na nchi za kisovieti zilipopamba moto.mfano mshirika mkubwa na ndugu wa damu wa Urusi nchi ya Yugoslavia ilipofanyiwa hujuma nzito na kubaki vipande vipande.
Urusi haikushindwa vita baridi kwa juhudi za west peke yake,bali kwa msaada wa taasisi nyingine kubwa duniani hasa kanisa KATOLIKI chini ya Baba Mt (PAPA) John Paul II,na hata Uislam.Hii haikua vita ndogo ya kuliangusha dubwana kuwa USSR.
UWEZO WA URUSI.
Elimu,maarifa,sayansi,teknolojia,mikakati na ulinzi na ufedhuri.
Marekani peke yake hamwezi Mrusi,hawezi kumdhibiti kwa sababu Urusi anavyo vitu vyote ambavyo marekani anavyo lakini wengine hawana navyo nimevitaja hapo juu,Urusi wana elimu,hapa ndio chimbuko la kila kitu duniani,ana maarifa kama vile marekani,ana sayansi na teknolojia kama vile marekani,ana mikakati thabiti ya kubaki kwenye game kama vile marekani ana uwezo wa ulinzi na usalama kama vile marekani,ili kumdhibiti labda uue wananchi wake wote ibaki ardhi tu.Ufedguri namaanisha ujasusi.
Ni kweli ML kuwa Urusi itawasumbua sana Marekani na washirika wake kwa sababu kiuchumi Urusi ana kila kitu ardhini hivyo hahitaji kununua kwa wengine, ambapo wangemfungia asinunue au asiuziwe.lakini kwa alivyonavyo watawazui wengine wasinunue kwake,hilo wanawewza.
kijeshi kumdhibiti Urusi ni kukusudia kuiangamiza dunia,kama sio kujaribu kujipiga risasi mwenyewe.vita ya Urusi na wao haitakua vita ya Kalashinikov na bunduki nyingine bali ita kua ni vita ya ICBM's
sasa fikiria marekani akirusha na urusi akirusha kuna kitu kitabaki?
 
NATO kwa pamoja wana idadi ya watu milioni 603.73.
URUSI peka yake ana idadi ya watu milioni 144.3.
NB: NATO ina watu mara sita zaidi ya Urusi lakini kwanini iwasumbue ??
USA,ndio nchi inayopokea misaada ya kijeshi kiulinzi na kijasusi Duniani kuliko nchi yeyote ili kuikabili Russiah Federation (RF)
.Baada ya vita kuu ya pili ya dunia,kukatokea vita nyingine mbili lakini sio za moto
1.vita baridi
2.mashindano ya kutengeneza silaha kali duniani.
Vita baridi USSR ilishindwa na USA
Vita ya kutengeneza silaha bado inaendelea, kama vile ilivyokua mwanzo kati ya USSR na USA.lakini USA bado anaendelea kusaidiwa na washirika wake ,wakati RF( Urusi) akiwa peke yake.
Hata baada ya kuvunjika umoja wa Kisovieti,bado USA anasaidiwa kutengeneza silaha na masuala ya Intelijensia ili kikabili Russian Federation( RF) yaani Urusi ya Vladimir Putin.
ONA.
Baada ya WWII, kukaibuka vita baridi kati ya USSR akieneza ukomunist na USA ikieneza ukapitalist.
USSR akaunda Warswa Pact kujihami,USA akaunda NATO kujihami.
USSR ikavunjika na Warsawa Pact ikavunjika ikabaki Russian Federation ( RF)peke yake,Wakati USA ikabaki na NATO ikabaki,lakini Bado hawajaweza kumcontain RF,Urusi.
Baadhi ya nchi zilizokua USSR,zikajiunga na NATO,bado Russia iko peke yake,lkn hawajamweka mkononi RF.
Baadhi ya nchi zilizokua Warswa Pact zikajiunga na NATO,bado Russia iko peke yake lakini hawajaweza kumdhibiti,RF.
Kwa kupitia NATO,USA anapata misaada mikubwa sana ya kiteknolojia,kijeshi na kiintelijensia ili kuikabili Urusi. Nchi kama UK,France,German,etc zimeisaidia sana USA kijeshi kudili na Russia.
MISAADA YA KIJESHI KWA MAREKANI NJE YA NATO
Israel,huisaidia sana USA kijasusi na tech dhidi ya Urusi,
Pakistan iliwahi kuisaidia USA kudili na USSR huko Afghanistan,
Ugiriki,hawa walinunua S300 toka Russia,wakawaalika Waisrael,wakaenda kuichunguza na kuifanyia mazoezi jinsi ya kuishinda,
Uingereza kama nchi pekee nje ya NATO ina bifu la asili na Urusi hapa mashirika ya kijasusi kama MI6,MI5 na CIA huishughulikia kwa pamoja Urusi,anaefaidika sana ni USA,
USA wameshiriki mara nyingi kuiba silaha za URUSI na kwenda kuzisoma na kisha kujua siri zilizowanufaisaha .Rubani mmoja wa jeshi la Iraki aliwahi kuiba MIG ya kirusi kwa faida ya Israel na aliyefaidika ni USA.
Hiyo mifano michache,na mara zote Urusi huwa haiteteleki wala kulalamika.
Ukraine,Georgia,Poland,Chek ni mfano wan chi zinazoinufaisha USA.
Hivyo mbinu zote za kijeshi,kijasusi na baadhi ya vifaa vilivyokua vya baadhi ya wanachama wa Warsaw Pact na nchi zilizokua za Kisoviet zilizohamia upande wa NATO na USA, ZIMEIFAIDISHA sana USA lakini bado wameshindwa kuimudu Russia Peke yake na kuitiisha.
VIKWAZO VYA KIUCHUMI.
Kwa kuwatumia EU na yeye mwenyewe USA,dhidi ya Russia ,bado wameshindwa kumtiisha na kumpinda.RUSSIA limebaki kuwa ni taifa imara.
Saud Arabia
Hawa hutumika kushusha mafuta ili bei ya mafuta ishuke ili kudhoofisha uchumi wa Russia,hii nayo ilifeli.
Haya ni machache tunayoyajua ,ni mangapi tusiyoyajua ,Je mpaka hapa USA haisaidiwi kuliangusha Dubu LILILOKATAA KUFA?
Haya ni maoni yangu tu,na hii ni makala ya kujifurahisha tu ili kuchangamsha ubongo,je si kweli kuwa USA inapewaga MISAADA kidili na URUSI?
Mjadala uko wazi.
 
Ahsante sana mkuu,
Sasa kama Urusi alikuwa na nguvu nyingi zaidi ya hizi za leo kwanini alishindwa Vita Baridi ??
Katika mantiki hii unataka kuniambia kwamba Urusi ya zamani ilikuwa na nguvu kuliko Marekani ??
UNAJUA MAANA YA VITA BARIDI???
 
KISIASA
1. Amesababisha sintofahamu kubwa ndani ya siasa za Marekani hasa kwa Donald Trump.
2. Anavuruga mipango ya Marekani kwa kutumia VETO kule Umoja wa Mataifa.
3. Amefanikiwa kuugawanya Umoja wa Ulaya (Schoeder wa Ujerumani anafanya kazi Rosneft)
4. Anaisaidia Korea Kaskazini kukwepa vikwazo vya Umoja wa Mataifa.
5. Alimsaidia Raisi wa Uturuki asipinduliwe na kuuwawa ambapo inasemekana CIA walihusika sana.
6. Amemtunza Edward Snowden ambaye kavujisha siri nyeti za Marekani.


KIJESHI
1. Kavamia Ukraine kijeshi na kumega Crimea kwa nguvu mno ya wanajeshi 70,000.
2. Kavuruga mpango wa Marekani na Israel wa kuvamia Syria na kumtoa Assad.
3. Anauza silaha nzito kwa mataifa hasimu wa Marekani kama Iran.
4. Anasidia Korea Kaskazini kukwepa vikwazo vya Umoja wa Mataifa.
5. Amevuruga majimbo ya Lugansk na Donestky hadi leo majeshi ya Ukraine hayana amani.
7. Yeye ndiyo mwenye jeshi la pili kwa ubora hapa duniani mbali na shida zote kiuchumi.


KITEKNOLOJIA
1. Marekani mpaka leo anategemea injini kutoka Urusi kwa ajili ya kurusha roketi zake.
2. Ametengeneza makombora mazito ambayo yanasafiri mara 10 zaidi ya sauti.
3. Walimwekea vikwazo vya injini za ndege kutoka Ukraine lakini katengeneza zake kwa haraka sana.
4. Ana wasomi wa sayansi ambao ni World Class kama 1,000,000 hivi.
5. Teknolojia ya kimtandao (Cyber Technology) yuko mbele sana na amethibitishia dunia mara nyingi.



KIUCHUMI
1. Amefanikiwa kutumia makampuni yake ya nishati kuwaumiza Ulaya hasa NORD Stream 2.
2. Amefanikiwa kutumia ushawishi wa nishati kuyavuta karibu mataifa kama Uchina, India na Uturuki.
3. Uturuki ameagiza silaha kutoka Urusi kitu ambacho kitampa faida za kiuchumi Mrusi.
4. Saudi Arabia ametengeneza viwanda vya Kalashnikov Ak-47 nchini kwake na Urusi karuhusu.
5. Amesaidia kutengeneza vyombo kama BRICS, The Shanghai Cooperation na Eurasia Economic Union


NB: Haya ni machache tu, sasa nchi iliyosambaratika inalisumbuaje taifa kubwa duniani ??
Kumbe majibu unayo alafu unauliza maswali jamani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ahsante sana mkuu,
Sasa kama Urusi alikuwa na nguvu nyingi zaidi ya hizi za leo kwanini alishindwa Vita Baridi ??
Katika mantiki hii unataka kuniambia kwamba Urusi ya zamani ilikuwa na nguvu kuliko Marekani ??
Eneo ambalo urusi litamsumbua sana kuweza kumfikia Marekani ni Propaganda, Intelligency na Millitari/War strategies.
Maeneo yote hayo matatu ndiyo yanampa nguvu sana Marekani na yamekua nguzo sababu ya financial Power aliyonayo.
Russia inabidi afanye ku customise hayo maeneo ili yaweze kumsaidia.
 
Back
Top Bottom