Swali gumu kidogo: Kwanini Urusi iliyosambaratika na dhaifu kuliko USSR inawasumbua sana NATO?

Swali gumu kidogo: Kwanini Urusi iliyosambaratika na dhaifu kuliko USSR inawasumbua sana NATO?

Hapana sina tatizo na KGB kuwa nchi nyingine,hata hilo la rais wa zamani wa Ukraine sina wasiwasi nalo,kitu nisichoamini ni kuwa KGB waliratibu kuvunjwa kwa USSR,hebu funguka zaidi hapo mkuu.
Ni sawa na kusema uisambaratishe familia yako ili kesho uje kuitengeneza upya! Apa sijui utakuwa unatumia akili za wapi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
ushahidi mdogo unakumbuka rais wa ukraine aliyetoka kabla ya huyu? alikuwa ni KGB na alikimbilia Russia mpaka leo. sasa ina maana kuna mapandikizi Ukraine mpaka leo ndani ya serikali
Mpaka petro anahisiwa ni jasusi wa urusi pia usa wanajua kuwa Ukraine ni chimbo la
Majasusi wa urusi that why wanasita kumuingiza NATO

Pia kaimu wa ujasusi wa Ukraine mwaka jana alikimbilia urusi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna watu humu wanajua historia aiseee..hongereni sana....
Linapokuja suala la Russia na USA kuna mtu mmoja alikua anaitwa Dotworld kitu kama hicho..humu jamii forum....sijui alienda wapi huyu nae...maana alikua anatema cheche hatari....
 
Vita baridi ilikuwa ni vita kubwa sana, ilikuwa ni vita ya kueneza itikadi na kutafutwa kuungwa mkono ulimwenguni baina ya magharibi na mashariki, sasa basi pata picha dunia yote hii baba wa ujamaa na mwenezaji mkuu na mfadhili mkuu wa nchi zote za kijamaa alikuwa ni Urusi,wakati mfadhili na muenezaji mkuu wa ubepari zilikuwa nchi za magharibi pamoja na marekani, hapo utaona ni mzigo mkubwa ambao alikuwa nao urusi na ulihitaji zaidi fedha nyingi na uchumi mkubwa. Kutokana na kuangalia zaidi mataifa ya nje aliyokuwa anayafadhili akasahau kuimarisha ndani mwake, yaani hakuweka sana mkazo kuyaimarisha maeneo yake mwenyewe, mwishowe watu wakachoka maana waliona muungano wao hauna faidi,iliyonufaika ni moscow na mataifa ya nje, kutokana na hili kwahiyo akawa na maadui wa nje na akazalisha wasaliti wa ndani waliochoshwa na mzigo wa kuzifadhili nchi nyingine. Hapo ndipo kasi ya anguko lake ilipoongezeka.

Ni kweli kabisa, urusi iliwahi kuwa na nguvu nyingi kushinda marekani marekani ilianza kuonekana kwenye uso wa dunia kuwa ina nguvu baada ya vita vya pili vya dunia lakini kabla ya hapo hakuna aliyeiwaza na kuiogopa marekani, mataifa yenye nguvu yalitokea ulaya kama ufaransa,uingereza na ujerumani, ukiyatoa hayo kukawa kuna urusi na japani, ndio maana unaona urusi ina eneo kubwa kuliko nchi zote mpaka leo hii, hiyo inadhihirisha ni jinsi gani aliweza kutanua himaya yake na kuilinda....maana kutanua himaya ni suala la kumpiga mwenzio na kumnyang'anya ardhi na kuhakikisha kila kiapnde cha ardhi hakikuponyoki.

Kwa faida ya wote ni kwamba nchi za magharibi zinaamini mpaka kesho wakifanikiwa tu kumshusha urusi na kumtawala wamefanikiaa kuitawala dunia, hivyo mipango yao ya muda mrefu ni kuiangusha urusi ili wasiwe na kizingiti chochote duniani,maana watakuwa wamepata rasilimali kubwa sana
Mkuu umefungka knyamaaa Big Up
 
Huku hukupita aisee
Ndo hivyo yaani... lakini sikushangaa sana manake kuna wakati niliwahi kuhoji kwa mods hapa how come notifications zako huwa sizipati! Yaani in most cases, kuona ulichoandika ni lazima ni-view jina lako na kuangalia "current posts"!
 
Wala sio swali gumu mzee.The answer is simple and straightforward. Soviet Union iliyosambaratika under Gorbachev sio hii ya sasa mkuu.Soviet Union ya Putin ime-imarika sana,it is again a super power,kwa hiyo NATO hawawezi kuichezea.
 
USSR kweli ilimeguka na kudondoka, lakini tusisahau kuwa USSR ilibebwa na mambo yote yaliratibiwa huko Russia, hivyo hata baada ya kuvunjika Russia ilibaki na mambo yote,si kwamba ilisambaratika kabisa kama tunavyoona ila bali bado vyombo vyake viliwndelea kufanya kazi,warusi ni watu ambao sisi tunaona kama wazungu lakini wao wako tofauti kabisa na wazungu.wakati ulaya na marekani walikuwa wanaamini russia imekufa lakini rusia yenyewe ilikuwa inahangaika kuhakikisha inanyanyuka, ndo hapo alipokuja kutokea mtu kama Putin, putin kainyanyua russia muda mfupi sana,si kwasababu ana miujiza ila ni kwasababu walikuwa na kila kitu kasoro kiongozi tu wa kusimamia kukua kwa uchumi wa russia.

Kwanini NATO wanaihofia Russia?
Kwanza warusi ni watu wenye akili nyingi sana, hakuna kitu wanaweza panga wasishindwe kufanya, hivyo kwenye nyanja ya rasilimali watu ipo vizuri ina wasomi wa kutosha na wabunifu kwenye sekta zote kuanzia za ulinzi afya, na technolojia nyingine, kwahiyo NATO inawaogopa kwasababu wana uwezo wa kufanya chochote kwa akili na elimu zao walizonazo.
Wana technolojia, hapo nimekueleza kuwa wana akili na ni wasomi, sasa hivi vyote inawafanya wawe ni wavumbuzi wakubwa wa twchnolojia duniani,moja kati ya maeneno ambayo wamewekeza sana ni kwenye technolojia ya vita,huko hawa watu wana dhana za technolojia ya hali ya juu, wanaweza kupigana na yoyote aliyepopote pasipo hata wao kwenda, wanadhana za kinyuklia zenye uwezo mkubwa sana,wanamfumo mzuri wa mawasiliano pia ndio mabingwa wanaoendesha kituo cha anga cha kimataifa kwa sehemu kubwa, ikumbukwe kuwa maarifa ya anga za mbali urusi inashindana kwa karibu na marekani kuliko taifa lolote.

Urusi ina hadhina kubwa ya mariasili karibia zote duniani,nadhani ndiyo inaongoza kuwa na hiyo hadhina,kwa utajili walionao NATO wanajua kabisa wakimuacha atumie huo utajili kujiendeleza basi wameumia, nimekuambia awali hawa watu wana akili na ni wabunifu, hivyo wanachokosa wao ni uchumi tu wa kusaidia kufanya mambo yao, ana gesi ambayo ulaya nzima wanamtegemea yeye tu, ni miongoni mwa wazalishaji wakubwa wa mafuta na mengine mengi....kwa hizi rasilimali tu anatoa hofu tosha kwa NATO

Wana jwshi imara, jesho lao ni kubwa sana, ni la pili duniani baada ya lile la marekani,jeshi hili kama nilivyoeleza hapo juu lina dhana za kila aina na lina technolojia kubwa,warusi wanajua kuwa wako hatarini kwahiyo wanawekeza sana kwenye jeshi lao, japo bajeti yao ni ndogo kushinda ya marekani lakini wanafanya ma,bo makubwa sana, uimara wa jeshi hili ni tishio kubwa sana kwa NATO

Uongozi mathubuti, hawa watu kumpata Putin walikula bingo sana, huyu Putin ni mpelelezi mstaafu aliyepikwa na akaiva enzi za KGB, huyu kafanya sana kazi ujerumani hivyo anawajua wamagharibi nje ndani, ni kiongozi wenye misimamo isiyoyumba,ni kiongozi ambaye anatamani urusi iwe kama zamani, hivyo anaimarisha sana nguvu za urusi ili iwe na ushawishi kimataifa kwa kila jambo, uwepo wa huyu mtu ni tishio tosha kwa NATO.

Historia inawalinda, warusi historia pia inawalinda maana walishawahi kuwa wakubwa wa dunia,vita vya pili ni wao ndo waliompigs mjerumani, wana historia ndefu ya ubabe toka enzi hivyo historia hiyo inawalinda na kuwabeba kitambo na kufanya mataifa mengine waiogope.

Yako mengi ila naomba niishie hapo kwa leo
Waliokua na akili urusi na Jews hawapo Tena wameondoka, ndomaana Leo hii Russia kiuchumi gdp imezidiwa mpaka na Canada, anajua urusi ni kuwekeza kwenye Vita na silaha
 
Wala sio swali gumu mzee.The answer is simple and straightforward. Soviet Union iliyosambaratika under Gorbachev sio hii ya sasa mkuu.Soviet Union ya Putin ime-imarika sana,it is again a super power,kwa hiyo NATO hawawezi kuichezea.
Super power kivip nawakati kiuchumi gdp amepitwa mbali sana, kinachomfanya marekani awe kama alivyo na utemi kwa sababu ana gdp kubwa, anaweza sema mtu Fulani asifanye biashara na nchi fulan na nchi zote zikatii acha stori za vijiweni ndugu
 
Enzi hizo USSR ipo, USSR GDP ilikuwa theluthi mbili ya GDP ya USA ,USSR ilikuwa na GDP kubwa , per capita GDP kubwa kuliko India, China

Leo hii GDP ya Urusi haiachani ktk GDP na nchi kama Brazil, Australia, Mexico,Uturuki

Wanaosema hali chini ya Putin imeimarika hawajui wanaloliongea, Russia leo kapitwa per capita GDP na nchi nyingi sana duniani hadi Taiwan,nchi zilizo katika hali mbaya kama ugiriki, Ureno etc

Sent using Jamii Forums mobile app
 
KISIASA
1. Amesababisha sintofahamu kubwa ndani ya siasa za Marekani hasa kwa Donald Trump.
2. Anavuruga mipango ya Marekani kwa kutumia VETO kule Umoja wa Mataifa.
3. Amefanikiwa kuugawanya Umoja wa Ulaya (Schroeder wa Ujerumani anafanya kazi Rosneft)
4. Anaisaidia Korea Kaskazini kukwepa vikwazo vya Umoja wa Mataifa.
5. Alimsaidia Raisi wa Uturuki asipinduliwe na kuuwawa ambapo inasemekana CIA walihusika sana.
6. Amemtunza Edward Snowden ambaye kavujisha siri nyeti za Marekani.

KIJESHI
1. Kavamia Ukraine kijeshi na kumega Crimea kwa nguvu mno ya wanajeshi 70,000.
2. Kavuruga mpango wa Marekani na Israel wa kuvamia Syria na kumtoa Assad.
3. Anauza silaha nzito kwa mataifa hasimu wa Marekani kama Iran.
4. Anasidia Korea Kaskazini kukwepa vikwazo vya Umoja wa Mataifa.
5. Amevuruga majimbo ya Lugansk na Donestky hadi leo majeshi ya Ukraine hayana amani.
7. Yeye ndiyo mwenye jeshi la pili kwa ubora hapa duniani mbali na shida zote kiuchumi.

KITEKNOLOJIA
1. Marekani mpaka leo anategemea injini kutoka Urusi kwa ajili ya kurusha roketi zake.
2. Ametengeneza makombora mazito ambayo yanasafiri mara 10 zaidi ya sauti.
3. Walimwekea vikwazo vya injini za ndege kutoka Ukraine lakini katengeneza zake kwa haraka sana.
4. Ana wasomi wa sayansi ambao ni World Class kama 1,000,000 hivi.
5. Teknolojia ya kimtandao (Cyber Technology) yuko mbele sana na amethibitishia dunia mara nyingi.


KIUCHUMI
1. Amefanikiwa kutumia makampuni yake ya nishati kuwaumiza Ulaya hasa NORD Stream 2.
2. Amefanikiwa kutumia ushawishi wa nishati kuyavuta karibu mataifa kama Uchina, India na Uturuki.
3. Uturuki ameagiza silaha kutoka Urusi kitu ambacho kitampa faida za kiuchumi Mrusi.
4. Saudi Arabia ametengeneza viwanda vya Kalashnikov Ak-47 nchini kwake na Urusi karuhusu.
5. Amesaidia kutengeneza vyombo kama BRICS, The Shanghai Cooperation na Eurasia Economic Union

NB: Haya ni machache tu, sasa nchi iliyosambaratika inalisumbuaje taifa kubwa duniani ??

well said mkuu!
umeongea kweli tupu.
 
Back
Top Bottom