Swali Gumu: Kwanini kila ninayemsaidia huwa hana shukrani?

Swali Gumu: Kwanini kila ninayemsaidia huwa hana shukrani?

Siyo kuwa ninataka kukubalika, ila sipendi kuchafuliwa jina kwenye jamii yetu. Ni afadhali wawe wananyamaza tu kuliko kunijengea jeshi la uadui dhidi yangu huko nyumbani ambapo ni kwetu sote!

mkuu ni afadhali umeziona tabia zao mapema ili ujue unadeal na watu wa aina gani

Kiufupi ndugu zako hawana shukrani na kuna kila dalili kuwa wewe ndio tegemeo la ukoo na ndugu zako baadhi hawafurahii hali hiyo ndio maana wanatafuta kila sababu ya kukuonesha wewe ni mbaya ili kukudogosha na wao waonekane bora zaidi yako mbele za watu

Kitendo cha wao kutumia uwezo wako ili watoto wao wawe kama wako hakitoishia hapo. watataka wawe zaidi ya wa kwako someday ili wajione ni bora zaidi

hizo ni nafsi zao na unatakiwa kuwa makini nazo. Wasaidie tu ili watoto wao wasije kuwa mizigo kwa wanao ila usitarajie CHOCHOTE kutoka kwao
 
Saidia kwa kumuangalia MUNGU usiangalie malipo ya DUNIANI.Imeisha hiyo
 
Sipendi wanishukuru, ila sipendi wanilaumu vibaya na kunichafulia jina kwenye jamii.
Na wao hawapendi kukushukuru ila wanapenda kukulaumu na kukuchafulia jina.

Usichokipenda wewe ndicho sahihi kwao nafikiri ukabaliane tu na hali kwamba wema una gharama...
 
Saidia kwa kumuangalia MUNGU usiangalie malipo ya DUNIANI.Imeisha hiyo
Kama uwezo wa kuwasaidia unao wasaidie, washukuru wasishukuru wewe endelea na maisha yako. Ila tu wema usizidi uwezo.
Ninaumizwa sana na lawama za kifamilia zisizokuwa na msingi kiasi cha mimi kuogopa kukutana nao kama ndugu tena!
 
Unapenda sana Kutambulika kwa kila unachokifanya. Binafsi mimi nikimfanyia mtu jambo huwa sitaki hata anishukuru, yeye akwende zake tu akasaidie wengine huko mbele

Hukusoma vizuri post yangu; nimesema ikishafikia kuwa unamwacha ajiendeleze yeye bado anataka ku-cling on na kuanza lawama. Hata uliyemsaidia kumaliza chuo bado analalamika anataka msaada zaidi!

Swala la kutaka kutambulika ni gumu kulifafanua, kwani kama mtu akikusaidia halafu ukamlaumu, sijui jinsi ya kuzungumza scenario hiyo bila kutumia neno kutotambua msaada uliopata.
 
Pole sana mkuu, wewe endelea na maisha yako waache waendelee kulalama. Binadamu tuna kasumba ya kutokuridhika.
Best advice ever; ila sasa naogopa kwenda nyumbani na familia yangu tena kwani ninahisi kila mtu ananichukia.
 
Best advice ever; ila sasa naogopa kwenda nyumbani na familia yangu tena kwani ninahisi kila mtu ananichukia.

upo delicate mkuu na hili ndilo tatizo kubwa hapa kuliko yote. pole kwa hilo

unaonekana una upendo sana kwa ndugu zako na pengine unatamani mambo yangekuwa tofauti na yalivyo ili muishi kwa amani na furaha. Ila haiwezi kuwa hivyo, kubaliana na hali halisi tu.

Uliozaliwa nao ndivyo walivyo na Kamwe huwezi kuwabadilisha

wanasema
"don't wait for the storm to pass, learn how to dance in the rain".. hivyo tu
 
Binafsi sijawahi ona swala la kumsaidia au kutomsaidia mtu kuwa la lazima kiasi hiko. Nikitaka kukusaidia nitakusaidia, nisipotaka hata ulie unagalagala hapo, sikusaidii ng'oo!. Na mara zote hizo za kuogopa ndugu ndizo zinazopelekea kuwaogopa kwa maamuzi yako sahihi unaona bora uendelee kuumia kwa furaha zao. Kwangu ni Never.
 
Binafsi sijawahi ona swala la kumsaidia au kutomsaidia mtu kuwa la lazima kiasi hiko. Nikitaka kukusaidia nitakusaidia, nisipotaka hata ulie unagalagala hapo, sikusaidii ng'oo!. Na mara zote hizo za kuogopa ndugu ndizo zinazopelekea kuwaogopa kwa maamuzi yako sahihi unaona bora uendelee kuumia kwa furaha zao. Kwangu ni Never.
Nafikiri umeelewa vibaya. Silazimiki kuwasidia ndugu, ila sipendi wanilaumu na kunichafulia jina baada ya msaada niliokwisha wapa.
 
Mfadhili mbuzi binadamu atakuudhi!
Pia unataka kuonekana unasaidia, acha, unadhani watakupenda na kukubali, sahau. Hao ni narcissists.
Binafsi nilishaacha huo umaskini, ni kwamba kila mtu alee kwa nguvu zake.

Mema, mabaya, machungu yangu nakula mie na familia yangu. Kila anayeniambia ooh nina shida siku hizi jibu 1, SINA.

Zile lugha manipulative kubambikizana majukumu ooh mwanao kafaulu, ooh mwanao sijui nini, sizipokei.

Everyday is Saturday............................... 😎
 
Sawa kabisa boss, wazae wao kwa starehe zao, majukumu ubebe wewe, kivipi??

Binafsi natoa napojisikia mara 1,1 lakini sibebi jukumu. Tena najikita tu wenye pocket money sisomeshi.

Everyday is Saturday................................😎
Binafsi sijawahi ona swala la kumsaidia au kutomsaidia mtu kuwa la lazima kiasi hiko. Nikitaka kukusaidia nitakusaidia, nisipotaka hata ulie unagalagala hapo, sikusaidii ng'oo!. Na mara zote hizo za kuogopa ndugu ndizo zinazopelekea kuwaogopa kwa maamuzi yako sahihi unaona bora uendelee kuumia kwa furaha zao. Kwangu ni Never.
 
Mfadhili mbuzi binadamu atakuudhi!
Pia unataka kuonekana unasaidia, acha, unadhani watakupenda na kukubali, sahau. Hao ni narcissists.
Binafsi nilishaacha huo umaskini, ni kwamba kila mtu alee kwa nguvu zake.

Mema, mabaya, machungu yangu nakula mie na familia yangu. Kila anayeniambia ooh nina shida siku hizi jibu 1, SINA.

Zile lugha manipulative kubambikizana majukumu ooh mwanao kafaulu, ooh mwanao sijui nini, sizipokei.

Everyday is Saturday............................... 😎
Unachosema ni kweli ila sehemu kubwa ya ukoo wetu ni maskini sana na huenda ndiyo maana huwa naingilia kati, hivyo huwa najitahidi kufanya lolote litakalosadida kunyanua maisha yao.
 
Ukiwa unatenda wema na kutarajia urudishiwe chochote huo hukuwa unatenda wema bali unafanya biashara

Mm kuna jamaa yangu alikuwa anaumwa inatakiwa afanyiwe operations mbili moja ya kongosho na nyingine ya tezi dume na alikuwa na sh 60000 but gharama za pale kcmc hospital ni 2.3ml

Nkaampa bima yangu akafanyiwa operations zote hizo kwa bima yangu,nilijitoa tu kama rafiki wala sikuwa natarajia chochote kutoka kwake

Alivyopona akanitoa na konyagi ndogo ya 3500,
Ila mpaka Leo akiniona ananikimbia cjui ni kwa nn?
Matumizi mabaya ya bima!nyie ndio mnaotafutwa....
 
Mungu anaona na atakuzidishia kwa unachokitoa vile moyo wako anauona. Usingoje shukrani
 
Unachosema ni kweli ila sehemu kubwa ya ukoo wetu ni maskini sana na huenda ndiyo maana huwa naingilia kati, hivyo huwa najitahidi kufanya lolote litakalosadida kunyanua maisha yao.
Believe u me, from experience, huo umaskini unauona wewe, wenzako maisha yataendelea hata ukifa. Hawatakufa na umaskini.
Na watakulaumu watoto wao umewaharibu, umewasomesha wanajiona bora, hawataki kufanya kazi za kimaskini iwe kilimo Au kuchunga.

Maskini siku zote anawaza tajiri iko siku naye lazima awe maskini. Chukua hatua jitunze jilee wewe na familia.

Everyday is Saturday............................... 😎
 
Back
Top Bottom