Swali Gumu: Kwanini kila ninayemsaidia huwa hana shukrani?

Swali Gumu: Kwanini kila ninayemsaidia huwa hana shukrani?

Mkuu unawalipiaje ada watoto wawili wa mtu mmoja? Ni kwamba hana namna kabisa, yeye kuzaa kusomesha unasomesha wewe?. Wema usizidi ndio maana hawathamini unachowafanyia maana hawajui ugumu wake.
Huyo mtu ni ndugu yangu wa karibu, ila wakati mimi nanasoma shule yeye alikuwa akila maraha sana wala hakupata elimu ya kutosha; alitumia ujana wake vibaya. Sasa matokeo yake anaishi na familia yake maisha duni sana kiasi kuwa familia yake inapokuwa na matatizo yanayohitaji hela, wanaenda kuomba msaad kwa mama yangu mzazi ninayemlea mimi; hivyo mama analazimika kuwagawia sehemu ya allowance ambayo huwa ninampa. Nikaona kuwa kuondoa tatizo hili ngoja nisaidie watoto wake wapate elimu kusudi waje wachukue responsibility hiyo - yaani kuvunja vicious circle of poverty kwake. Sasa mpaka mtoto amemaliza digrii bado anaomba msaada! Naona ni kama vile tatizo liko kwenye damu.
 
Ndo walimwengu walivyo.

Hakuna ubaya mtu kukushukuru kwa chema ulichomfanyia.

Ndo ustaarabu huo.

Hata mimi watu wa hivyo ninao sana.

Mtu unamsaidia zaidi ya mara 10.

Hakuna ahsante hata moja.

Siku ambayo huwezi kumsaidia, anaanza kukutangaza kwa watu u mchoyo!

Kushukuru ni uungwana na kusambaza uzushi ni ushenzi.
 
Huyo mtu ni ndugu yangu wa karibu, ila wakati mimi nanasoma shule yeye alikuwa akila maraha sana wala hakupata elimu ya kutosha; alitumia ujana wake vibaya. Sasa matokeo yake anaishi na familia yake maisha duni sana kiasi kuwa familia yake inapokuwa na matatizo yanayohitaji hela, wanaenda kuomba msaad kwa mama yangu mzazi ninayemlea mimi; hivyo mama analazimika kuwagawia sehemu ya allowance ambayo huwa ninampa. Nikaona kuwa kuondoa tatizo hili ngoja nisaidie watoto wake wapate elimu kusudi waje wachukue responsibility hiyo - yaani kuvunja vicious circle of poverty kwake. Sasa mpaka mtoto amemaliza digrii bado anaomba msaada! Naona ni kama vile tatizo liko kwenye damu.
Kwahiyo huyo Ni ombaomba mtaalamu(a Professional Bagger)
 
Ukiwa unatenda wema na kutarajia urudishiwe chochote huo hukuwa unatenda wema bali unafanya biashara

Mm kuna jamaa yangu alikuwa anaumwa inatakiwa afanyiwe operations mbili moja ya kongosho na nyingine ya tezi dume na alikuwa na sh 60000 but gharama za pale kcmc hospital ni 2.3ml

Nkaampa bima yangu akafanyiwa operations zote hizo kwa bima yangu,nilijitoa tu kama rafiki wala sikuwa natarajia chochote kutoka kwake

Alivyopona akanitoa na konyagi ndogo ya 3500,
Ila mpaka Leo akiniona ananikimbia cjui ni kwa nn?
Du!!!!
 
Wewe ni mjinga , am sorry.
Una kipato kizuri na una roho nzuri ila umeshindwa kujua kuwa ndugu wa Kiafrika ni nusu mtu nusu shetani.
Huo ndio ujinga wako
[emoji1787][emoji1787][emoji16][emoji16]
 
Mkuu unawalipiaje ada watoto wawili wa mtu mmoja? Ni kwamba hana namna kabisa, yeye kuzaa kusomesha unasomesha wewe?. Wema usizidi ndio maana hawathamini unachowafanyia maana hawajui ugumu wake.
Vry true
 
Bora wewe! Narudia bora ndugu zako!
Dadangu ananifanyiaga figisu za ajabu ....yy figisu zake anachotaka anione nikiwa OMBA OMBA kama yeye !aliwah mwambia beki 3 atafute kwa hali na mali leseni yangu ya madini sijui alitaka aifanyie nn!!..[emoji119][emoji119]...majuzi changamoto ya upumuaji ikanipata naskia akawa anasema ehee . Naskia corona haitibiwi kwa bima[emoji1787]! Akihisi nitasanda chaaa!
Wanawake wana wivu sana...huwa nawakwepa hata ndugu zangu wa kike

Kuna mtoto wa mamaangu mdogo ile nimeenda kuoga tu akawa anachoma dawa huku ananena jina langu asee...
 
Mimi walinilani mpaka wakasahau kama Dua utakayo muombea mwebzio ndio itakayo kupata.. Nilimvuta Mzee pembeni nikampa ile wazungu wanasema fact.. Mungu amrehemu yule Mzee.. Akananiambia sikia Wafazilika wapundaka kaza buti nakutakia kilabla kheri.. TRA wali piga tukio nikawa hoi. Basi wale nilio wasaidia wakafurahi nikasikia na baadhi wakafanya sherehe ya kiko wapi...
Nikapigwa tafu na mtu nilie kwisha msahau kama kuna wema nilimfanyia..
Aysee maisha safari ndefu sana Ashukuriwe alietuleta hapa duniani..
Mimi niliwahi kula chakula kunacho semekana kina sumu,,bado kidogo niuwache huu ulimwengu dhaifu..
Ikawa haitoshi nilupo kuja Tanzania gari yangu ikalegezwa natt tairi za mbele..
Mkuu saidia lkn usisaidie nyoka..
Mkuu funguka vizuri nani aliweka sumu? Kulegeza nati tairi
 
Zamani sana bendi moja hapo Dar: ama Dar es salaama Jazz au Western Jazz iliimba kuwa "Tenda Wema, nenda zako, usingoje shukurani". Maudhui ya wimbo huu yamesharudiwa na waimbaji wengi sana siku za hivi karibuni.

Mimi ni mtu wa makamo sana wakati huu na katika maisha yangu nimeshasaidia watu wengi sana, jambo ninalojivunia mno. Kila msaada ninaotoa huwa ina maana ya mimi na familia yangu kujinyima ili tuwasaide wengine, siyo kwamba huwa nina dimbwi kubwa la pesa za kuchota bure bure bure.

Sasa kinachonishangaza ni kuwa ndugu na marafiki wengi niliowahi kusaidia huwa hawaonyeshi shukrani yoyote ukilinganisha na wale ambao huwa sina uhusiano nao. Ndugu na marafiki huwa wanataka zaidi wala hawawezi kutosheka na msaada, na ikitokea nikasema sasa msaada niliokwishatoa unatosha inabidi ajiendeleze mwenyewe, basi wananilaumu kama vile kile nilichokwishawafanyia siyo kitu kabisa. Yaani wanakuwa wananiongea vibaya tu bila shukrani yoyote.

Ni wapi ninapokosea katika kusaidia ndugu na marafiki ili watambue msaada wangu kwao?

Kuna mmoja nilimlipia mtoto wake kwa miaka minne mfulizo chuo kikuu cha dar es salaama wala hakuchukua mkopo wa serikali, akamaliza na 3rd class.

Sasa mtu huyo ananilaumu kwa nini simsaidii mtoto huyo kusoma masters! Kibaya anatumia lugha mbaya kuwa nina wivu sipendi watoto wake waendelee kama mimi wakati bado ninasaidia mtoto wake mwingine ambaye yuko sekondari ninayomlipia mimi!!
Tenda mema usingoje shukrani cheka na watu wote Muzamir Katunzi.

 
Wanawake wana wivu sana...huwa nawakwepa hata ndugu zangu wa kike

Kuna mtoto wa mamaangu mdogo ile nimeenda kuoga tu akawa anachoma dawa huku ananena jina langu asee...
Unaona sasa🤣🤣!yaani sijui kwanini inakua hvyo..mie hata sinaga mpango naye maanaaisha anayoishi ya kuomba omba ni adhabu tosha..kila anachofanya hakifanikiwi ..anapewaga mitaji mirefu balaa...mie kimyaa
 
Uwezo wa kuwasomesha ninao; ninachochukia ni hiyo tabia yao ya kutokutambua kuwa maisha siyo mtelemko tu. Halafu watoto wan huwa hawana makosa; hawakuchagua kuzaliwa na mzazi asiyekuwa na akili !!
 
Unaona sasa[emoji1787][emoji1787]!yaani sijui kwanini inakua hvyo..mie hata sinaga mpango naye maanaaisha anayoishi ya kuomba omba ni adhabu tosha..kila anachofanya hakifanikiwi ..anapewaga mitaji mirefu balaa...mie kimyaa
Atakuloga tu huyo kuwa nae mbali, ana wivu mpaka umekuwa sumu [emoji848][emoji848]

Be careful
 
Hongera kwa kujaliwa na roho ya kusaidia.Kumbuka neno wema hauozi.

N baraka utalipwa hata kwa wajukuu wako .Ikiwa unasaidia usiwe unategemea kupata chochote kutoka kwa hao uwasaidiao.Ipo siku hizi shukurani zitakuja kwako au hata kwa vizazi vyoko.
Mfano kuja kutokea katika familia yako Kama vile mtu kuwa tajili mkubwa Sana / kuwa kiongozi mkubwa Sana .

Kanuni ukitoa kwa kusaidia toa kwa Nia njema na sio kwa kujikweza au kutangaza kwa watu kwamba unasaidia haitafanyika baraka .

Kila la heri
 
Zamani sana bendi moja hapo Dar: ama Dar es salaama Jazz au Western Jazz iliimba kuwa "Tenda Wema, nenda zako, usingoje shukurani". Maudhui ya wimbo huu yamesharudiwa na waimbaji wengi sana siku za hivi karibuni.

Mimi ni mtu wa makamo sana wakati huu na katika maisha yangu nimeshasaidia watu wengi sana, jambo ninalojivunia mno. Kila msaada ninaotoa huwa ina maana ya mimi na familia yangu kujinyima ili tuwasaide wengine, siyo kwamba huwa nina dimbwi kubwa la pesa za kuchota bure bure bure.

Sasa kinachonishangaza ni kuwa ndugu na marafiki wengi niliowahi kusaidia huwa hawaonyeshi shukrani yoyote ukilinganisha na wale ambao huwa sina uhusiano nao. Ndugu na marafiki huwa wanataka zaidi wala hawawezi kutosheka na msaada, na ikitokea nikasema sasa msaada niliokwishatoa unatosha inabidi ajiendeleze mwenyewe, basi wananilaumu kama vile kile nilichokwishawafanyia siyo kitu kabisa. Yaani wanakuwa wananiongea vibaya tu bila shukrani yoyote.

Ni wapi ninapokosea katika kusaidia ndugu na marafiki ili watambue msaada wangu kwao?

Kuna mmoja nilimlipia mtoto wake kwa miaka minne mfulizo chuo kikuu cha dar es salaama wala hakuchukua mkopo wa serikali, akamaliza na 3rd class.

Sasa mtu huyo ananilaumu kwa nini simsaidii mtoto huyo kusoma masters! Kibaya anatumia lugha mbaya kuwa nina wivu sipendi watoto wake waendelee kama mimi wakati bado ninasaidia mtoto wake mwingine ambaye yuko sekondari ninayomlipia mimi!!
Loooh! Pole sana kaka, hali hii imetupelekea sisi wengine kuwa katili kwa watu, yaani sio kwamba hatusaidii, tunasaidia ila hatutaki mazoea tena, mara baada ya kutoa msaada. Hii inafanya wengi kutuita katili watu wa aina yangu. Ila ndiyo maisha niliyochagua, nimeshaumizwa sana kama wewe, nikakaa chini na kusema SASA BAAAASIII!
 
Bora wewe! Narudia bora ndugu zako!
Dadangu ananifanyiaga figisu za ajabu ....yy figisu zake anachotaka anione nikiwa OMBA OMBA kama yeye !aliwah mwambia beki 3 atafute kwa hali na mali leseni yangu ya madini sijui alitaka aifanyie nn!!..[emoji119][emoji119]...majuzi changamoto ya upumuaji ikanipata naskia akawa anasema ehee . Naskia corona haitibiwi kwa bima[emoji1787]! Akihisi nitasanda chaaa!
Upo timamu kweli wewe? Yaani unafurahi na kucheka kabisa? Mtu anakuombea kifo halafu unacheka?
 
Ni Qur-an tuu ndio kitabu pekee kilicho mueleza kwa undani mwanadamu na jinsi ya uumbwaji wake hadi matilio yake....
Binadamu ni kiumbe cha ajabu.. Ukimsaidi tabu, Usipo msaidia tabu..
Nilimuingiza kazini mtoto wa dada yangu baba mmoja na mimi..
Alivyoanza kupata pesa akawa jeuri kupindukia.. Nikamtimua kazini basi akanishushia fulushi la matusi na nikamtia adabu weka nyuma ya nondo miezi sita..
Alipotoka heshima na adabu japo Mama yake aongei na mimi.. Na mimi naona poa tuu..
Jamaa una roho mbaya hatari!
 
Back
Top Bottom