Swali kwa Ayubu Rioba: Siku hizi sera ya Taifa inaruhusu taasisi za kidini kunufaika na fedha za walipa kodi kupitia TBC?

Swali kwa Ayubu Rioba: Siku hizi sera ya Taifa inaruhusu taasisi za kidini kunufaika na fedha za walipa kodi kupitia TBC?

Nawachukia wakristo kwa sababu wanajali dini yao kuliko watu, wamejaa unafiki. Akitawala mkristo hata akiua wanakaa kimya, watu wakipotea wanakaa kimya. Lakini mama ametufanya tutabasamu nyinyi mnanuna, alafu wanatulazimisha tusiyaone mema anayotutendea bali tumtazame kama muislamu na hivyo kumchukia yeye na mema yake.
Hapa tunajadili sera bora ya kulisaidia Taifa kutenganisha dola na dini kama Katiba inavyotaka.

Ulichokiandika hapa hakina uhusiano wowote na bandiko hili.

Futa na uanzishe uze wake tofauti.
 
Kwa ujumla mwandishi kaandika Andiko la kijinga lisilo pakegi ya yupi ndiye Mtanzania na yupi anastahili kuitumia TBC na nini maana ya Utaifa Kwa ujumla na Sura hiyo ya Utaifa inayo sehemu ipi ukitazama unauona huo utaifa. Anayelipa Kodi ili TBC ifanye kazi ni Nani, mwandishi na Andiko lake hajamtaja ni Nani mlipa Kodi anayesababisha TBC iwe hewani??
Soma bandiko halafu ujibu hoja ya mwandishi badala ya kujibu hoja ya mchangiaji.
 
Kumbe tatizo ni maandishi yaliyoandikwa chini ya TV screen eti

"MASHINDANO YA TAIFA YA QURAAN"
Mashindano ya taifa hiyo ndo nyuzi yenyewe, TV ya taifa ipo kwa ajili ya kutangaza habari za kitaifa whether ni mambo ya Dini, Siasa, Uchumi au Kabila. Chamsingi ni ukubwa wa habari.

Nahisi muandishi anasumbuliwa na chuki ya Udini. Natamani angetumia muda wake kuandika mambo muhimu yenye maslahi aachane na hizi chuki.
Hoja sio Mashindano ya Taifa ya Kurani.
Vaa miwani, soma hoja.
Jibu hoja iliyo mezani.
 
Ningemshauri mwandishi afungue macho aangalie Dunia, mfano.
BBC, RT, FRANCE 24 hizi zote ni TV za taifa husika.

Nimeshaona sana wakitangaza hewani habari za Mahujaji, Ramadan, Harakati za waislam Europe, Documetary za kidini, n.k

Nakushauri kijana usiwe NARROW MINDED
 
Soma bandiko halafu ujibu hoja ya mwandishi badala ya kujibu hoja ya mchangiaji.
Mama Amoni, umepotea wewe

Nionyeshe
mlipa Kodi anayeifanya TBC iwepo ukiwaondoa Waislamu na wakristo,

Maana kusudi la Andiko lako, ni kuwa TBC inatumia vibaya Kodi za wananchi Kuendesha vipindi vya kidini,
 
View attachment 1792731
Dk. Ayub Chacha Rioba, Mkrugenzi Mtendaji wa TBC

Swali hapo juu linatokana na ufa kati ya yale nilioyoyaona leo tarehe 21 Mei 2021, na matarajio yangu kwa kuzingatia misingi ya kikatiba hapa Tanzania na kwingineko.

Niliyoyaona TBC1

Leo nimeona matukio mawili yasiyo ya kawaida kwenye luninga ya Taifa TBC1, inayoongozwa chini ya Ukurugenzi wa Dk. Ayub Rioba.

  1. Asubuhi kabla ya kipindi cha Bunge cha mswali na majibu TBC1 walirusha kipindi cha "Madrasa" kilichokuwa na ujumbe unaotembea kwa upande wa chini ukisomeka "Mashindano ya Kuhifadhi Kurani Tukufu kwa Waislamu Wanawake Yameandaliwa na Taasisi ya Kiislam ya African Relief Foundation."
  2. Mchana, mara tu baada ya matangazo ya Maadhimisho ya miaka 40 ya kuanzishwa kwa SADC, ambako Ayub Rioba alikuwa mwongozaji, kilifuata kipindi ncha swala ya Kiislamu.
Nafahamu pia kwamba, TBC1 imekuwa na kawaida ifuatayo:
  1. Kila alfajiri madhehebu ya dini tofauti hupewa muda wa kusoma sala ya asububi.
  2. Kila usiku wa kati, kabla ya saa sita, madhehebu ya dini tofauti hupewa muda wa kusoma sala ya kufunga siku.
  3. Kila Jumapili pia, madhehebu ya dini tofauti hupewa muda wa kusoma ibada za Jumapili.
Matarajio kwa mujibu wa Katiba

Katiba ya Tanzania, ibara ya 19(2) inasema kuwa, "shughuli na uendeshaji wa jumuiya za dini zitakuwa nje ya shughuli za mamlaka ya nchi," ambapo mamlaka ya nchi ni mihimili mitatu ya Serikali, Bunge na Mahakama.

Hivyo, matarajio yangu ni kwamba, kwa kuwa TBC ni mali inayoendeshwa kwa kodi ya umma chini ya usimamizi wa serikali isiyofungamana na dini yoyote, kama tunavyosoma kwenye katiba ya nchi, basi yafuatayo yanapaswa kuonekana:

  1. Programu zenye sura ya kitaifa katika ngazi ya maudhui
  2. Programu zenye sura ya kitaifa katika ngazi ya lugha
Hii maana yake ni kwamba, yafuatayo hayapaswi kuonekana:
  1. Programu zenye sura ya kisekta katika ngazi ya maudhui
  2. Programu zenye sura ya kisekta katika ngazi ya lugha

Pia, dini nyingi tayari zinavyo vyombo vyake vya habari kwa ajili ya kuendesha shughuli zake za kidini. Kanisa Katoliki wana Tumaini TV, KKKT wana Upendo TV, Waislam wana Iman TV, Wapagani wa "Ramli TV," nk

Nakumbuka kuwa, kwa sehemu kubwa, sala nyingi za madhehebu ya KiIslamu zinatumia lugha ya Kiarabu, jambo ambalo linakiuka sera ya kujenga umoja wa kitaifa kwa kutumia lugha ya Taifa.

Hata ibada kadhaa na litania nyingi za Kikristo zinasomwa kwa lugha ya Kilatini ambayo sio lugha ya Taifa.

Nakumbuka kuna wakati Kardinali pengo alikuwa anaitwa na wazee wetu wa kule Mwenge Parokiani, Dar es Salaam, ili akawaendeshee ibada kwa lugha ya Kilatini, kama walivyokuwa wamezoea zamani, kabla Kanisa Katoliki halijatunga sera ya kuendesha ibada kwa Kiswahili na kimila.

Kwa hiyo, katika mazingira ya sasa, yafuatayo ni matarajio yangu:

  1. Kanisa Katoliki waendeshe programu zao za kisekta kupitia Tumaini TV,
  2. KKKT waendeshe programu zao za kisekta kupitia Upendo TV,
  3. Waislam waendeshe programu zao za kisekta kupitia Iman TV,
  4. Wapagani waendesha programu zao za kisekta kupitia "Ramli TV," nk
Uhalisia wa mambo

Pamoja na matarajio haya, uhalisia wa mambo ni kwamba, matakwa ya Katiba ya Tanzania kuhusu umuhimu na ulazima wa kutenganisha dini na dola hayajatimia kama ifyatavyo:

  1. Kanisa Katoliki wanaendesha programu zao za kisekta kupitia TBC1,
  2. KKKT wanaendesha programu zao za kisekta kupitia TBC1,
  3. Waislam wanaendesha programu zao za kisekta kupitia TBC1,
  4. Shughuli za Bunge zinaanza kwa kusoma dua kwa "Mola",
  5. Viapo vya watumishi wa umma vinamaliziwa kwa maneno "Ewe Mwenyezi Mungu Nisaidie," wakati Katiba ya nchi haitambui neno "Mungu."
Kama Katiba ya nchi inayakataza mambo haya, kwa nini tunayatenda, kama ambavyo mfano wa TBC1 leo umeonyesha?

Ni muhimu swali hili lijibiwe ili tujichunguze kama vyombo vya habari vya kitaifa vinakweza maslahi ya vikundi kama vile taasisi za dini au vinatweza maslahi ya pamoja kama vile umoja wa kitaifa.

Napendekeza kwamba ni kosa kutumia kodi ya raia asiye na dini kuhudumia taasisi za kidini. Ni kama ambavyo ni kosa kutumia kodi ya mtu asiye na chama cha siasa kutoa ruzuku kwa chama cha siasa. Kuna tatizo hapo.

Angalizo la kisera

Nakumbusha kwamba, kote duniani, sera za kutenganisha dini na dola hugawanyika katika sehemu mbili:

  1. Sera zinazofuata mtindo wa Kimarekani.
  2. Sera zinazofuata mtindo wa KIjerumani.
Sera zinazofuata mtindo wa Kimarekani. Hapa, serikali huyapiga kisogo masuala yote ya dini, kiasi kwamba hakuna senti ya mlipa kodi inatumika kufadhili taasisi za kidini. Habari ya sijuo airtime kwa programu za kidini, sijui kufungua bunge kwa dua, hakuna.

Sera zinazofuata mtindo wa KIjerumani. Hapa, serikali haiyapigi kisogo masuala yote ya dini, kwani kuna senti fulani ya mlipa kodi inatumika kufadhili taasisi za kidini. Kwa mfano, huko Ujerumani, mfumo wa "TRA" yao unatumika kukusanya sadaka kutoka kwa waumini ambao ni waajiriwa, halafu sadaka hiyo inakabidhiwa kwa makanisa yaliyosajili waumini wao. Lakini, mfumo huu unabagua baadhi ya madhehebu ya kidini.

Mapendekezo

Hivyo basi, kwa kuwa Sera zinazotenganisha dini na dola kwa kufuata mtindo wa Kijerumani zina ubaguzi; na kwa kuwa sera zinazotenganisha dini na dola kwa kufuata mtindo wa Kimarekani hazina ubaguzi, napendekeza yafuatayo:

  1. Kwamba, programu zote za kidini, ambazo kwa sababu hiyo ni programu za kisekta ziondolewe katika TBC;
  2. Kwamba, programu zote za kidini, ambazo kwa sababu hiyo ni programu za kisekta ziendeshwe kupitia vituo binafsi vya madhehebu ya kidini;
  3. Kwamba, TBC ijielekeze katika programu zenye kujenga umoja wa kitaifa kwa kueneza lugha ya Taifa, na sio lugha nyinginezo;
  4. Kwamba, utaratibu wa kusoma dua mwanzoni mwa shughuli za Bunge ufutwe.
  5. Kwamba, Bunge litunge sheria inayotoa mwongozo rasmi kuhusu sera ya kutenganisha dini na dola hapa nchini Tanzania. Yaweza kuitwa "The Wall of Separation Between Religion and State Act."
Naomba kuwasilisha.
Mawazo ya mpagani utayajua tu! Kwa taarifa yako nchi yetu inatambua uwepo wa MUNGU. Ndiyo maana wimbo wa Taifa unamwomba Mungu aibariki Tanzania. Ndiyo maana tulipopatwa na janga la corona mara moja Rais wetu wa wakati ule aliitisha maombi ya kitaifa kumwomba Mungu atuponye na corona na alituponya na rais wetu akaitisha tena maombi ya shukrani kwa Mungu kwa kutuponya na corona. Kwa taarifa yako usalama mkubwa wa nchi yetu na tunakaa bila hofu ya cofona ni kutokana na majibu ya Mungu kwa maombi yetu!! Kwà mtanzania mwenye nia njema atajisikia vizuri tv ya taifa kurusha matangazo yenye maudhui ya Mungu!!
 
Mama Amoni, umepotea wewe

Nionyeshe
mlipa Kodi anayeifanya TBC iwepo ukiwaondoa Waislamu na wakristo,

Maana kusudi la Andiko lako, ni kuwa TBC inatumia vibaya Kodi za wananchi Kuendesha vipindi vya kidini,

1621415777303.png


Source: Religion in Tanzania - Wikipedia

Kumbuka kuwa hizo 3% za TAR na watu bali ni sehemu ya watu 60,000,000, yaani watu 1,800,000.

Hawa ni walipa kodi pia.

Nadhani umeelewa somo.

Lkn pia usisahau kuwa hizo takwimu za Wakristo na Waislamu zimekuzwa.

Takwimu sahihi zinasema kuwa TAR ni wengi kuliko Wakristo na Waislamu kwa pamoja.
 
Kichwa cha habari ktk maandishi yako inaonesha unaroho ya unafiki na uchanganyishi.

TV ikionesha habari sio kwamba anaefaidika ni mwenye habari bali pia waangaliaji nao ufaidika kwa kupata elimu na habari ambazo pengine walikuwa hawazijuwi.

Mimi sijali tv ikitowa habari za dini yoyote kwasababu naamini always kuna mambo ya kujifunza.

Kichwa cha habari ya hii nyuzi yako imeonesha kiasi gani umejidumaza kiakili
 
Mawazo ya mpagani utayajua tu! Kwa taarifa yako nchi yetu inatambua uwepo wa MUNGU. Ndiyo maana wimbo wa Taifa unamwomba Mungu aibariki Tanzania.
Kuna tofauti kati ya wimbo wa Taifa na wimbo wa nchi?
Wimbo wa Nchi hauwezi kutaja Mungu.
Wimbo wa Taifa unaweza kutaja Mungu kwa kuwa Watanzania wana dini.
Jipange upya.
 
Tumieni akili kulisaidia taifa.Chokochoko hizi hazitafua dafu.Tumeshatoka huko zamani.Unajua sakata la kuchinja lilivyoisha?Unajua mjadala wa MoU kati ya Serikali na taasisi za dini Ulivyotulizwa.Kama Kuna aliekutuma mwambie Watanzania hatutaki hayo mambo.
 
Kichwa cha habari ktk maandishi yako inaonesha unaroho ya unafiki na uchanganyishi.

TV ikionesha habari sio kwamba anaefaidika ni mwenye habari bali pia waangaliaji nao ufaidika kwa kupata elimu na habari ambazo pengine walikuwa hawazijuwi.

Mimi sijali tv ikitowa habari za dini yoyote kwasababu naamini always kuna mambo ya kujifunza.

Kichwa cha habari ya hii nyuzi yako imeonesha kiasi gani umejidumaza kiakili

Msingi wa hoja huu hapa:

Katiba ya Tanzania, ibara ya 19(2) inasema kuwa, "shughuli na uendeshaji wa jumuiya za dini zitakuwa nje ya shughuli za mamlaka ya nchi."

Na ibara ya 4(1) inasema kuwa shughuli zote za Mamlaka ya Nchi katika Jamhuri ya Muungano zitatekelezwa na kudhibitiwa na vyombo vyenye mamlaka ya utendaji, mamlaka ya kutekeleza utoaji haki, na mamlaka ya kutunga sheria. Yaani, Serikali, Bunge, na Mahakama.
 
Tumieni akili kulisaidia taifa.Chokochoko hizi hazitafua dafu.Tumeshatoka huko zamani.Unajua sakata la kuchinja lilivyoisha?Unajua mjadala wa MoU kati ya Serikali na taasisi za dini Ulivyotulizwa.Kama Kuna aliekutuma mwambie Watanzania hatutaki hayo mambo.
Naona wewe ndo unafanya chokochoko. Sababu hii hapa:

Katiba ya Tanzania, ibara ya 19(2) inasema kuwa, "shughuli na uendeshaji wa jumuiya za dini zitakuwa nje ya shughuli za mamlaka ya nchi."

Na ibara ya 4(1) inasema kuwa shughuli zote za Mamlaka ya Nchi katika Jamhuri ya Muungano zitatekelezwa na kudhibitiwa na vyombo vyenye mamlaka ya utendaji, mamlaka ya kutekeleza utoaji haki, na mamlaka ya kutunga sheria. Yaani, Serikali, Bunge, na Mahakama.
 
Mama lzm uelewe UENDESHAJI NA UHABARISHAJI.

TBC hairuhusiwi kuendesha shughuli za dini i.e Hawawezi kusimamia au kuendesha mipango ya mashindano ya Quraan

Ila niwajibu wao kutowa habari zozote hususan za kitaifa.

Nakuomba uelewe tafauti ya maandishi Mama
 
Sioni kama unaelewa maana ya tunu ya uvumilivu. Nitakupa somo:

Fikiria kwamba, kuna mtu A anayemaini kuwa kitendo X ni haramu kidini, na hivyo kuamini kuwa kitendo hiki kinapaswa kupingwa.

Lakini, kwa mujibu wa tunu ya uvumilivu, mtu A anatakiwa kuamini kwamba ni sahihi kujizuia kupinga kitendo X, endapo kitafanywa na mtu baki B, kwa sababu kitendi hicho ni miongoni mwa matendo yanayopaswa kuvumiliwa na wanajamii.

Kwa hiyo, uamuzi wa mtu A kuvumilia kitendo cha B unaonekana kumaanisha kwamba, mtu A anakubali imani kwamba “X ni kitendo kinachopaswa kupingwa” na anakubali imani kwamba “X ni kitendo kisichopaswa kupingwa,” ambazo ni imani mbili zinazopingana kimantiki.

Hata hivyo, kama tunu ya uvumilivu ikitafsiriwa vizuri haitaonekana kuwa na mkanganyiko huu wa kimantiki. Kwa mujibu wa tafsiri sahihi ya tunu ya uvumilivu, kukubalika na kukataliwa kwa kitendo X kunategemea mazingira ya kitendo hicho.

Yaani, uvumilivu wa mtu A kuhusu imani X, katika mazingira M, haumaanishi kwamba mtu A anapaswa kuonyesha uvumilivu kuhusu imani X, katika kila mazingira mbali na mazingira M.

Ndio kusema kwamba, kitendo X sio haramu kila wakati, kila mahali na kwa kila mtendaji. Yaani, wema wa kitendo X, au ubaya wake, unategenea mazingira ambako kitendi hicho kitafanyika.

Kwa hiyo, tafsiri sahihi ya tunu ya uvumilivu iko hivi: fikiria kwamba kuna mtu A anayemaini kuwa kitendo X ni haramu kidini, na hivyo kuamini kuwa kitendo hiki kinapaswa kupingwa katika mazingira M.

Lakini, kwa mujibu wa tunu ya uvumilivu, mtu A anatakiwa kuamini kwamba ni sahihi kujizuia kupinga kitendo X, endapo kitafanywa na mtu baki B, kwa sababu kitendi hicho ni miongoni mwa matendo yanayopaswa kuvumiliwa katika mazingira N.

Kwa hiyo, uamuzi wa mtu A kuvumilia kitendo cha mtu B unamaanisha kwamba, mtu A anakubali imani kwamba “X ni kitendo kinachopaswa kupingwa” katika mazingira M na anakubali imani kwamba “X ni kitendo kisichopaswa kupingwa,” katika mazingira N.

Ukitumia somo hili katika mjadala wa sasa, maana yake ni hii: “X ni kitendo kinachopaswa kupingwa” katika mazingira M na anakubali imani kwamba “X ni kitendo kisichopaswa kupingwa,” katika mazingira N, ambapo:
  • X ni kitendo cha kuendesha programu za kisekta katika TV
  • M ni mazingira ya TV ta Taifa TBC
  • N ni mazingira ya TV ta taasisi ya kidini kama vile Tumaini TV, Iman TV, Upendo TV, nk.
  • Ambapo, mazingira M na mazingira N yote yanapatikana katika nchi moja ya Tanzania.
Huu ndio uvumilivu tuliofundishwa tangu shule ya chekechea, na sio vinginevyo.

Katika Taifa moja, lenye mseto wa kidini, lazima kuwepo na sehemu za umma wote ambako programu za kisekta hazikanyagi. Maeneo hayo ni pamoja na:
  • Vyombo vya habari vya Taifa (Hapa, lugha ya Taifa ni alama na nyenzio ya kujenga Utaifa)
  • Shule za Taifa (Hapa sare ni alama na nyenzio ya kujenga Utaifa)
  • Vyuo vya Taifa (Hapa mtaala mmoja ni alama na nyenzio ya kujenga Utaifa)
  • Vituo vya usafiri wa umma (Hapa vituo vya mabasi ni mfano wa uwepo wa maslahi ya pamoja Kitaifa)
  • Maktaba za Taifa Hapa vitabu mmoja ni mfano wa uwepo wa maslahi ya pamoja Kitaifa)
  • Barabara za Taifa (Hapa barabara ni mfano wa uwepo wa maslahi ya pamoja Kitaifa)
  • Nk
Katika maeneo haya ni marufu kuendesha mihadhara ya kidini.

Nadhani somo limeeleweka.
Umetumia muda mwingi kuandika kurasa tatu za gazeti.

Kumbuka unayoyataka kwa namna nchi yetu ilivyopatikana hayawezi kuja kufanikiwa.

Nchi yetu haina dini lakini mimi na wewe tuna dini zetu.

Hutaki kusikia kiarabu kikizungumzwa TBC kama huwezi badilisha Chanel au zima TV.

Kama wewe wakisikilizwa hatutakuwa na nchi iitwayo Tanzania.
 
Mama lzm uelewe UENDESHAJI NA UHABARISHAJI.

TBC hairuhusiwi kuendesha shughuli za dini i.e Hawawezi kusimamia au kuendesha mipango ya mashindano ya Quraan

Ila niwajibu wao kutowa habari zozote hususan za kitaifa.

Nakuomba uelewe tafauti ya maandishi Mama
Wanapoweka habari za waislam huwa wanaweka habari za wahindu na za wakatoliki.
 
Mama Amon ameshindwa kuelewa katiba sijuwi labda anamatatizo ya lugha.

Kuendesha shughuli za dini ni tafauti na kuonesha au kureport
 
Naona wewe ndo unafanya chokochoko. Sababu hii hapa:
Kwahiyo vipindi vya miziki vikiwekwa pale TBC watu wananengua, hao wakristo na waislamu huoni nao wanaona Kodi zao hazitumiki vizuri?.Kistaarabu wanahama chanel kusubiri kipindi wanachopenda.Huo ndio Utanzania.Ndio maana naamini umetumwa kupima maji.Safari hii hamtoboi.
 
Kwahiyo vipindi vya miziki vikiwekwa pale TBC watu wananengua, hao wakristo na waislamu huoni nao wanaona Kodi zao hazitumiki vizuri?.Kistaarabu wanahama chanel kusubiri kipindi wanachopenda.Huo ndio Utanzania.Ndio maana naamini umetumwa kupima maji.Safari hii hamtoboi.
Analeta siasa za udini kwa kivuli cha katiba.
 
Kwahiyo vipindi vya miziki vikiwekwa pale TBC watu wananengua, hao wakristo na waislamu huoni nao wanaona Kodi zao hazitumiki vizuri?.Kistaarabu wanahama chanel kusubiri kipindi wanachopenda.Huo ndio Utanzania.Ndio maana naamini umetumwa kupima maji.Safari hii hamtoboi.
TBC ni civic space ambayo inapaswa kucheza programu zinazokubalika kwa umma wote, babu, baba, mama, mtoto, mjukuu. Ndio maana hujaona wanaweka mikanda ya X. Hayo uliyoyataja ni mifano isiyoimarisha mjadala unaoendelea hapa.
 
Back
Top Bottom