Swali kwa Ayubu Rioba: Siku hizi sera ya Taifa inaruhusu taasisi za kidini kunufaika na fedha za walipa kodi kupitia TBC?

Hapa tunajadili sera bora ya kulisaidia Taifa kutenganisha dola na dini kama Katiba inavyotaka.

Ulichokiandika hapa hakina uhusiano wowote na bandiko hili.

Futa na uanzishe uze wake tofauti.
 
Soma bandiko halafu ujibu hoja ya mwandishi badala ya kujibu hoja ya mchangiaji.
 
Hoja sio Mashindano ya Taifa ya Kurani.
Vaa miwani, soma hoja.
Jibu hoja iliyo mezani.
 
Ningemshauri mwandishi afungue macho aangalie Dunia, mfano.
BBC, RT, FRANCE 24 hizi zote ni TV za taifa husika.

Nimeshaona sana wakitangaza hewani habari za Mahujaji, Ramadan, Harakati za waislam Europe, Documetary za kidini, n.k

Nakushauri kijana usiwe NARROW MINDED
 
Soma bandiko halafu ujibu hoja ya mwandishi badala ya kujibu hoja ya mchangiaji.
Mama Amoni, umepotea wewe

Nionyeshe
mlipa Kodi anayeifanya TBC iwepo ukiwaondoa Waislamu na wakristo,

Maana kusudi la Andiko lako, ni kuwa TBC inatumia vibaya Kodi za wananchi Kuendesha vipindi vya kidini,
 
Mawazo ya mpagani utayajua tu! Kwa taarifa yako nchi yetu inatambua uwepo wa MUNGU. Ndiyo maana wimbo wa Taifa unamwomba Mungu aibariki Tanzania. Ndiyo maana tulipopatwa na janga la corona mara moja Rais wetu wa wakati ule aliitisha maombi ya kitaifa kumwomba Mungu atuponye na corona na alituponya na rais wetu akaitisha tena maombi ya shukrani kwa Mungu kwa kutuponya na corona. Kwa taarifa yako usalama mkubwa wa nchi yetu na tunakaa bila hofu ya cofona ni kutokana na majibu ya Mungu kwa maombi yetu!! Kwà mtanzania mwenye nia njema atajisikia vizuri tv ya taifa kurusha matangazo yenye maudhui ya Mungu!!
 
Mama Amoni, umepotea wewe

Nionyeshe
mlipa Kodi anayeifanya TBC iwepo ukiwaondoa Waislamu na wakristo,

Maana kusudi la Andiko lako, ni kuwa TBC inatumia vibaya Kodi za wananchi Kuendesha vipindi vya kidini,



Source: Religion in Tanzania - Wikipedia

Kumbuka kuwa hizo 3% za TAR na watu bali ni sehemu ya watu 60,000,000, yaani watu 1,800,000.

Hawa ni walipa kodi pia.

Nadhani umeelewa somo.

Lkn pia usisahau kuwa hizo takwimu za Wakristo na Waislamu zimekuzwa.

Takwimu sahihi zinasema kuwa TAR ni wengi kuliko Wakristo na Waislamu kwa pamoja.
 
Kichwa cha habari ktk maandishi yako inaonesha unaroho ya unafiki na uchanganyishi.

TV ikionesha habari sio kwamba anaefaidika ni mwenye habari bali pia waangaliaji nao ufaidika kwa kupata elimu na habari ambazo pengine walikuwa hawazijuwi.

Mimi sijali tv ikitowa habari za dini yoyote kwasababu naamini always kuna mambo ya kujifunza.

Kichwa cha habari ya hii nyuzi yako imeonesha kiasi gani umejidumaza kiakili
 
Mawazo ya mpagani utayajua tu! Kwa taarifa yako nchi yetu inatambua uwepo wa MUNGU. Ndiyo maana wimbo wa Taifa unamwomba Mungu aibariki Tanzania.
Kuna tofauti kati ya wimbo wa Taifa na wimbo wa nchi?
Wimbo wa Nchi hauwezi kutaja Mungu.
Wimbo wa Taifa unaweza kutaja Mungu kwa kuwa Watanzania wana dini.
Jipange upya.
 
Tumieni akili kulisaidia taifa.Chokochoko hizi hazitafua dafu.Tumeshatoka huko zamani.Unajua sakata la kuchinja lilivyoisha?Unajua mjadala wa MoU kati ya Serikali na taasisi za dini Ulivyotulizwa.Kama Kuna aliekutuma mwambie Watanzania hatutaki hayo mambo.
 

Msingi wa hoja huu hapa:

 
Naona wewe ndo unafanya chokochoko. Sababu hii hapa:

 
Mama lzm uelewe UENDESHAJI NA UHABARISHAJI.

TBC hairuhusiwi kuendesha shughuli za dini i.e Hawawezi kusimamia au kuendesha mipango ya mashindano ya Quraan

Ila niwajibu wao kutowa habari zozote hususan za kitaifa.

Nakuomba uelewe tafauti ya maandishi Mama
 
Umetumia muda mwingi kuandika kurasa tatu za gazeti.

Kumbuka unayoyataka kwa namna nchi yetu ilivyopatikana hayawezi kuja kufanikiwa.

Nchi yetu haina dini lakini mimi na wewe tuna dini zetu.

Hutaki kusikia kiarabu kikizungumzwa TBC kama huwezi badilisha Chanel au zima TV.

Kama wewe wakisikilizwa hatutakuwa na nchi iitwayo Tanzania.
 
Wanapoweka habari za waislam huwa wanaweka habari za wahindu na za wakatoliki.
 
Mama Amon ameshindwa kuelewa katiba sijuwi labda anamatatizo ya lugha.

Kuendesha shughuli za dini ni tafauti na kuonesha au kureport
 
Naona wewe ndo unafanya chokochoko. Sababu hii hapa:
Kwahiyo vipindi vya miziki vikiwekwa pale TBC watu wananengua, hao wakristo na waislamu huoni nao wanaona Kodi zao hazitumiki vizuri?.Kistaarabu wanahama chanel kusubiri kipindi wanachopenda.Huo ndio Utanzania.Ndio maana naamini umetumwa kupima maji.Safari hii hamtoboi.
 
Analeta siasa za udini kwa kivuli cha katiba.
 
TBC ni civic space ambayo inapaswa kucheza programu zinazokubalika kwa umma wote, babu, baba, mama, mtoto, mjukuu. Ndio maana hujaona wanaweka mikanda ya X. Hayo uliyoyataja ni mifano isiyoimarisha mjadala unaoendelea hapa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…