Dada mi ni mkristo lkn niseme ukweli kwamba kimtazamo wang naona kama hoja yako haijakaa kitaifa bali imekaa kidini. Na ndo maana hoja hii imekosa wachangiaji wengi, hii ni kwa sababu watu wengi humu wameshachoka na hoja zenye kuleta malumbano ya kidini baina yetu kama Taifa. Wengi humu tumeoleana na kuzaliana ktk imani tofauti. Unakuta baba muislam mama mkristo, au baba mkristo mama muisilam, watoto wanaozaliwa wanapokuwa wakubwa wanaamua wenyewe imani ya kufuata nk, hapo sijaongelea mtaani, mashuleni, maofisini na sehem mbali mbali za miji na nchi kwa ujumla. Umekiri mwenyewe kwamba unafahamu kitambo kuhusu vipindi vya dini vinavyorushwa kila siku asubuh na usiku wakati wa kulala, yan muda wa kufungua vipindi na muda wa kufunga vipindi, pia umekiri kuwa kuna vipindi vya kikristo huwa vinapitishwa kila jumapili kwa ajili yetu sisi wakristo lkn haukuwahi kuja kuhoji chochote kuhusu vipindi hivyo vya jumapili, lkn leo umeona na ndugu zetu na wao wameanza kupewa muda wa kuangalia au kufuatilia vipindi vyao TBC siku ya ijumaa umekuja haraka haraka kuzungumzia habari za kodi, ila wakati walipokuwa wanarusha vya kwetu kila ijumapili bila kupitisha hiki cha ijumaa swala la kodi haukulihoji. Tupendane jamani sisi wote ni taifa moja hao waliotuletea hizi imani kwa sasa wapo mbali baada ya kupuuza mawazo ya aina hii.