Swali kwa Malegendary, hivi unapotaka kuoa mke wa pili, mke mkubwa unamuweka sawa vipi?

Mdakuzi Tujaalie maoni yako tafadhali.
Kuna maombi naweza kuacha, lakini si maombi toka kwako. Kwenye hili labda niseme kama template na kila mtu aitumie kulingana na mazingira yake ili afanikishe.

Kwanza, ni lazima awe na sababu (sio moja) zenye faida za moja kwa moja kwake na kwa mke mkubwa. Kwa maana ya kuleta ahueni kwa wote wawili.

Katika sababu ni muhinu kuepuka sababu za kimapenzi au za tatizo la mpito. Pia, zisiwe sababu za kumfanya bora zaidi mke mdogo mtarajiwa, au mwokozi.

Pili, lazima kwenye maelezo aoneshe kuheshimu nafasi ya mke mkubwa na kumfanya ni mwamuzi wa mwisho, na bila maamuzi yake haliwezi kwenda. Yaani asionekani ana maamuzi tayari.

Tatu, kuhakikisha ana uwezo bila shaka wa kumhudumia mke mdogo mtarajiwa bila ya kumega kwa mke mkubwa, au kumpunja (uchumi na mapenzi).

Pia, kuepuka kuwa mwovu kwake, kwa siku za karibuni, hasa za utukutu wa 'kuchepuka'.

Ova
 
Mnunukie kuwanja. Ukiweza mjendew hata chumba. Utakuwa umemaliza
 
Mke wa pili kwenye rahaa tu! Kwenye shidaa Aaaah!

Wakina bmkubwa tukae kwa kutulia tumeambiwa shidaa Raha zinawenywewe
 
Waafrika pesa kidogo tu mawazo kuongeza mke
 
Maelezo mazuri sana b... Lakini kwako hayatokufaa, na usijaribu.
 
Naomba nkupe ID ya shemegi ako umwambie anifanyie haya kisha aoe wake wawili 😹
 
Mhhhhh! Mi mbona siwezi jamani? Nampenda sana.
Siku akinipiga tukio parapanda italia JF!
🤣🤣🤣🤣 Nifah unajitahidi kupenda.....
Tukupe tuzo ya mpendaji bora wa jf, mwanaume apewe Equation x
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…