Swali kwa mliokulia vijijini: Mlivyokuwa mnasikia Dar mlidhani ikoje?

Swali kwa mliokulia vijijini: Mlivyokuwa mnasikia Dar mlidhani ikoje?

Dar mtaani unakuta mwandishi /mtangazaji anamhoji mtu wengine hawana time kuangalia, mshamba akionekana anageuzwa fursa
Watu wa mikoani hudhani Dar kuna shamrashamra sana..
Wanashangaa wakiona kila mtu Yuko bize na ishu zake..

Kingine watu dar wakiona mtu maarufu hujikausha Tu kama hawajaona kitu
Wa mikoani huwa wanazubaa hata wakimuona Pierre..
 
Nilidhani daresalama ni sehemu amazing siku nafika nilistaajabu kwanza kaubungo kalikuwa kituko mji haukuwa nilivyotegemea nilidhani kuwa bado sikufika daresalama
 
Mimi nilikuwa na fikilia kuwa dar hamna miti full majengo tu. Afu kuna mdada aliniambia kuwa alipofika dar alishanga kuwaona watu wengi wamesimama kuangalia video. Kwa kihaya wanaita (kushamaara) yaani wanashangalia video
 
Dar ya mwaka gani unauongelea? Dar ya leo siyo dar inayotamaniwa na watu mikoani hii ujue, dar iliyokuwa inatamaniwa na watu ni dar ya 1961 mpaka 2000, baada ya hapo hakuna jipya lilopo dar mkoani ukalikosa pengine bahari ya Hindi ila vyote mikoani vipo

Dar iliyotamaniwa ni ile mtu wa mkoani anasikia ukiwa dar radio unasikiliza Masaa 24, mtu wa mkoani anashangaa

Ukiwa dar wanawake wanajiuza uwanja wa fisi, Ohio, kinondoni makaburini mtu wa mkoani anashangaa

Ukiwa dar unapanda dala dala mtu wa mkoani anashangaa

Ukiwa dar kuna mikate mikubwa kweli mtu wa mkoani anashangaa

Ukiwa dar week end unaenda Beach mtu wa mkoani anashangaa na anapata hamu akaione dar na zone hivyo vitu

Dar ile mtu wa mkoani akisema naenda dar anaaga mtaa mzima, na siku akirudi mkoani washikaji wanajaa kijiweni kusikiliza story za dar, na anarudi kapendeza maana mitumba mikoani ilikuwa tatizo kwaiyo akirudi mkoani kavaa hata ronya ronya za manzese anaonekana kapendeza maana mkoni kupata nguo nzuri ilikuwa kazi na kama jamaa mjanja atarudi na kanda za radio karekodi miziki radio Tanzania haaa haaa basi anajiona mjanja

Dar ambayo TV na deki ndio zinauzwa mkoani ukuti duka la deki au TV mtu anatoka mkoani anakuja dar kwa lengo la kununua TV na deki 😀😀😀 hii nchi imetoka mbali basi tu

Dar ambao mikoa ya mbali watu wanatumia siku mbili mpaka tatu kufika kutokana na miundombinu ya Barbara

Dar ambayo haifiki uku mbezi mwisho ukifika kimara wewe upo porini ndio dar watu walitamani

Siyo dar ya leo mtu unaishi goba, mandale uko 😁😁😁 hii siyo dar inayotamaniwa maana ishakuwa vurugu mechi

leo hii hayo niliyoyasema mikoani yapo, dar ya leo vurugu mechi tupu manzese darajani si kivutio tena madaraja hayo kila kona dar yapo, mikoani yapo

So dar ipi unaisemea wewe?
 
Nilidhani daresalama ni sehemu amazing siku nafika nilistaajabu kwanza kaubungo kalikuwa kituko mji haukuwa nilivyotegemea nilidhani kuwa bado sikufika daresalama
Umetoka mkoa gani kwani? Na ni lini umekanyaga Dar? Isije ikawa umetinga mwaka huu au mwaka Jana? Maana hivi sasa ndio Ubungo imechoka. Before hakukuwa na kituo chochote cha basi mkoani cha kufananisha nacho!

Ingawa nimezaliwa Dar ila nilipata nafasi ya kuishi na kufika miji mingi hapa Tanzania na sikuwahi kuona bus stand kama ubungo ya kipindi kile. Nimekaa Tanga, Morogoro, Dodoma, Mtwara, Lindi, Arusha, Songea, Moshi, Tabora, Mbeya na Iringa. Kote huku hakukuwa na bus stand ya calibre ya Ubungo.
 
Watakuwa wanaangalia mpira
Mimi nilikuwa na fikilia kuwa dar hamna miti full majengo tu. Afu kuna mdada aliniambia kuwa alipofika dar alishanga kuwaona watu wengi wamesimama kuangalia video. Kwa kihaya wanaita (kushamaara) yaani wanashangalia video
 
Kuna watu huku mkoani wanataka kwenda dar,me niliye toka huko nawaambiaga tu Kama huna kaz ya kufanya usiende usije ukajilaumu

mchawi ni binadamu ,paka ni kijakazi
 
Nilizaliwa Dar, tukahamia mkoani nikiwa bado dogo, sijaielewa elewa mitaa vizuri.

Nilikuja kurudi Dar nikiwa mkubwa kimtindo. Kiukweli nilipaona pa kawaida sana tofauti na nilivyokuwa napafikiria.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kabla sijaja Dar miaka ya nyuma nilikuwa nikiambiwa Dar wanawake wote wanajiuza na ni Malaya, siku natoka kijijini babu alinionya sana kwamba Dar wanawake wote wana ukimwi. Dah jamaa mmoja aliyekuja kijijini akaniambia yaani wewe ukitaka mwanamke unamuita tu unamwambia ukamtie anakubali hakuna anaekataa! Doh nilimvamia Dada moja mitaa ya Sinza miaka hiyo ya nyuma sana nikamwambia we Dada twende nikakut.o.m.b.e kilichonikuta nakijua mwenyewe!

Sent using kidole gumba
 
Back
Top Bottom