Swali la Kimkakati: Kwanini Tanga Isiunganishwe na SGR?

Swali la Kimkakati: Kwanini Tanga Isiunganishwe na SGR?

Hili jambo najiuliza sijui kama kuna sababu ya msingi ya kwanini Tanga isiunganishwe kwenye SGR. Kuna mtu yeyote au imeonekana haina faida kiuchumi?
Hapa inabidi tufanye utafiti wa idadi ya abiria Tanga-dar, ukilinganisha na dar-moro, ama dar-dodoma Kwa siku, wiki, hadi mwezi pamoja na nauli yake
 
Hili jambo najiuliza sijui kama kuna sababu ya msingi ya kwanini Tanga isiunganishwe kwenye SGR. Kuna mtu yeyote au imeonekana haina faida kiuchumi?
Malori ni biashara kubwa sana Tanzania, usitalajie hilo kutokea, watu wanasubotage sukari ndio sembuse uharibu biashara zao? Maroli yao wayapeleke wapi?
 
Hili jambo najiuliza sijui kama kuna sababu ya msingi ya kwanini Tanga isiunganishwe kwenye SGR. Kuna mtu yeyote au imeonekana haina faida kiuchumi?
LOOOoooh!
Mzee Mwanakijiji, hili swali mbona umeliacha linaelea lenyewe hivi?

Mimi nitaongeza kwamba, kila sehemu ya nchi yetu inafaa kuunganishwa kwenye SGR, lakini natambua uwezekano huo haupo kwa sasa.
Tanga (mkoa/mji) iunganishwe kutoka/kwenda wapi, kwa mfano?
Ungetaka nijibu swali hili, ninge kwambia Toka Bandari ya Tanga hadi Musoma

Nikiwa bado sijui madhumuni ya hoja yako, umenikumbusha jambo ambalo hadi leo sielewi lilianzia wapi.

Huu mradi wa barabara itokayo Malindi, Kilifi , Kenya, inaambaa ambaa kando kando ya bahari hadi Tanga na kushuka kwenda hadi Bagamoyo. Hii barabara tayari ilisha anza kujengwa na mkopo toka AfDB ulisha kubaliwa.

Hii barabara ni nani hasa aliitaka sana?
 
Hakuna nchi inayoendelea kwa haraka kwa kusubiri mradi mmoja mmoja mkubwa. Kati ya vitu nilivipenda vya JPM ni uthubutu wa kwenda mzima mzima. Huku SGR, huku Bandari, kule Daraja la Tanzanite huku Daraja la Busisi, ukifungua macho flyover sijui wapi..yaani Bongo kulichangamka.
Ingekuwa rahisi hivyo, hata mimi ningejenga nyumba ya ghorofa na kuongeza wake wawili kwa mpigo!
 
Hili jambo najiuliza sijui kama kuna sababu ya msingi ya kwanini Tanga isiunganishwe kwenye SGR. Kuna mtu yeyote au imeonekana haina faida kiuchumi?
Nani ni mfanya maamuzi.

Kwanini hakuna kabisa mpango wa kupeleka reli hata ile ya zamani kusini.

Najiuliza tena nani ni mfanya maamuzi hapa nchini kutoka tabaka gani kama si lilelile tokea uhuru.

Tuliwaamini watafanya maamuzi kwa niaba yetu lkn wakatugeuka
 
Hili jambo najiuliza sijui kama kuna sababu ya msingi ya kwanini Tanga isiunganishwe kwenye SGR. Kuna mtu yeyote au imeonekana haina faida kiuchumi?
Ata Ulaya France au Germany si kila eneo kuna SGR , kiufupi hakuna mpango wa kupeleka SGR Tanga wala Kilimanjaro maana hakuna faida kubwa utakayoipata(Kumbuka reli iliyopo ya MGR yenyewe inakosa abiria hadi inasubiri mwezi wa 12 watu wakienda Kilimanjaro ndio inafunguliwa maana yake Tanga na Kilimanjaro zina biashara za msimu fulani tu, tofauti Morogoro ambapo kila siku watu wanasafiri)miundombinu iliyopo (MGR) inatosheleza, SGR itakwenda Mwanza kwa jicho la kuipata Uganda kupitia ziwa Victoria, pia itafika Kigokma kwa ajili ya kuzipata Burundi, Rwanda na Congo DRC. Mikoa Mingine itakua na Reli ya MGR tu.
 
Hili jambo najiuliza sijui kama kuna sababu ya msingi ya kwanini Tanga isiunganishwe kwenye SGR. Kuna mtu yeyote au imeonekana haina faida kiuchumi?
Roma haikujengwa ndani ya siku moja. Wameanzia kwenda Mwanza. Baada ya hapo wataendelea Kigoma kwa dhamira ya kuendelea mpaka Burundi na Rwanda. Baada ya hapo wataamua kipaumbele kielekezwa wapi.
 
Hili jambo najiuliza sijui kama kuna sababu ya msingi ya kwanini Tanga isiunganishwe kwenye SGR. Kuna mtu yeyote au imeonekana haina faida kiuchumi?
Zamani Tanga ilikua moja ya producer wakubwa wa raw materials kama Sisal, walihitaji reli kusafirisha zile materials kwenda viwandani na bandarini for export, sasa hivi Tanga haina kitu inazalisha, sisal imekua replaced na nylon skwahiyo zaidi wanaproduce Mabinti warembo, SGR ya nini ? Labda ipite tu iunganishe mikoa yote yakanda ya huko kaskizini kwaajili ya usafiri wa abiria mostly.
 
ningekuwa Rais, hela wanazoiba mafisadi ningezibana wasiibe, ningejengea reli ya SGR toka DSM hadi Tanga na toka Tanga hadi Musoma kupitia kilimanjaro. aliyojenga mjerumani ipo kazi ni ndogo sana, kutandua ya zamani, kuongeza kokoto na mwinuko wa tuta na kutandika SGR basi. sasaivi watu wanaoenda moshi, arusha hadi musoma, wangepiga SGR express chap wameshafika. hapa ndipo mzungu anapotuzidi, hatunaga vipaumbele.
Reli ile ya zamani vipande vingi haifai kutumia train za mwendokasi ya umeme sababu ya kona nyingi kali.a
Wakiweka watatengeneza njia mpya kabisa Kama hii ya SGR ya kati haijtumika ya zamani.
 
Malori ni biashara kubwa sana Tanzania, usitalajie hilo kutokea, watu wanasubotage sukari ndio sembuse uharibu biashara zao? Maroli yao wayapeleke wapi?
Uliosema linaweza kuelezea mambo mengine kwelikweli. Umeme, shule, afya nk. Yawezekana kuna watu wanafaidika hali inapokuwa mbaya.
 
LOOOoooh!
Mzee Mwanakijiji, hili swali mbona umeliacha linaelea lenyewe hivi?

Mimi nitaongeza kwamba, kila sehemu ya nchi yetu inafaa kuunganishwa kwenye SGR, lakini natambua uwezekano huo haupo kwa sasa.
Tanga (mkoa/mji) iunganishwe kutoka/kwenda wapi, kwa mfano?
Ungetaka nijibu swali hili, ninge kwambia Toka Bandari ya Tanga hadi Musoma

Nikiwa bado sijui madhumuni ya hoja yako, umenikumbusha jambo ambalo hadi leo sielewi lilianzia wapi.

Huu mradi wa barabara itokayo Malindi, Kilifi , Kenya, inaambaa ambaa kando kando ya bahari hadi Tanga na kushuka kwenda hadi Bagamoyo. Hii barabara tayari ilisha anza kujengwa na mkopo toka AfDB ulisha kubaliwa.

Hii barabara ni nani hasa aliitaka sana?
Miye nafikiria zaidi kwanini watu wanataa kuishi Dar na kufanya kazi Dar? Kwanini wasiishi Tanga na kufanya kazi Dar?
 
Back
Top Bottom