Swali la Kimkakati: Kwanini Tanga Isiunganishwe na SGR?

Swali la Kimkakati: Kwanini Tanga Isiunganishwe na SGR?

Barabara ya Tanga kwenda Bagamoyo imechelewa sana! Huu ni mradi wa maana kiuchumi.

Hivi unajua kwamba kutoka Tanga hadi Bagamoyo ni KM 273. Kwa gari itakyokwenda 100 KM /hr ni takribani masaa 3.Njia hii itarahisha sana mawasiliano kati ya Tanga- Pangani hadi Mombasa

Kwasasa Wananchi na Serikali inapoteza pesa nyingi kuzunguka. Dar -Chalinze ni KM 110. Chalinze- Segera KM 173. Segera- Tanga KM 78. Jumla ni KM 358 na kutumia saa 7. Hakuna sababu!
Kurahisishwa kwa mawasiliano mahali popote nchini ni jambo jema sana, na hata hii ya Tanga Mombasa Bagamoyo katika hali ya kawaida ni jambo jema; lakini kweli hii ilistahili kupewa kiupaumbele?
Na hasa ukiweka maanani kwamba barabara toka Tanga hadi Bagamoyo tayari ipo! Hailazimu kuzungukia Chalinze kama ulivyo eleza hapa.

Mradi huo wa hii barabara (mpya) bado siuelewi kabisa.
Lakini labda nipanue mjadala zaidi, kwa kueleza wasiwasi wangu kuhusu hii miundo mbinu inayo tuunganisha zaidi na nchi moja tu tunayo pakana nayo, kati ya nchi nane majirani zetu. Kuna nini hasa kati ya Kenya na Tanzania, kwamba miundo mbinu zetu ziwe zinaelekea zaidi upande wa Kenya, kuliko, kwa mfano: Uganda, DRC, Burundi, Rwanda, Zambia, Malawi, Mozambique, n.k..

Ngoja nitoe mifano ninayo ijuwa:
Kuna barabara toka Tanga hadi Mombasa, kupitia mpakani (Holoholo?).
Kuna barabara, toka Mombasa, kupitia Taveta na kuingia Tanzania mpakani (Holili?) na kuingia Moshi na kuelekea Arusha. Hii barabara sasa majirani wanaidai itumike kupitishia mizigo ya kwenda Burundi, toka Mombasa)!
Kuna barabara, tokea Arusha na kupandisha kwenda Kajiado kupitia mpakani (Namanga)
Kuna barabara toka Mwanza, kupitia Musoma kwenda Sirari na kuingia Kenya

Katika fikra zangu, nadhani kuna aina ya nguvu inayo tusukuma zaidi kuelekea upande huo mmoja; huku tukisahau kwamba kuna pande nyingine ambazo zinahitaji pia kutazamwa kwa umakini mkubwa.
Mpaka wetu na nchi ya DRC ni mrefu sana kuliko mipaka yetu mingine yote na majirani zetu. Hilo ziwa kuwepo hapo isichukuliwe kuwa kikwanzo, bali fursa nzuri ya kulitumia kuwasiliana na kufanya shughuli zetu na majirani hao.

Dah! Ni kama nimeingiza mada nyingine kabisa na ile inayojadiliwa hapa!
 
Tanga shughuli za kiuchumi zilishakwisha miaka ya 80 mwishoni , watu wengi wamefuata fursa nje ya mji ...idadi ya watu haifiki hata laki 4 pale mjini .

Bandari unakuta mwezi mzima meli mbili au moja .
Sasa Tanga kuna vitu gan vinafanyika na umeme wote huu bwelele. Kkulikuwa na kiwanda cha Mbolea na Kiwanda cha Chuma..vilikufa?
 
Hili jambo najiuliza sijui kama kuna sababu ya msingi ya kwanini Tanga isiunganishwe kwenye SGR. Kuna mtu yeyote au imeonekana haina faida kiuchumi?
na pia mm najiuliza kwann hamna safari za boti kama vile dar zenji same iwe dar tanga
 
Mzee Mwanakijiji samahani naomba uturuhusu tuvuruge mada yako, tuna chepuka kidogo
Tanga Mombasa Bagamoyo katika hali ya kawaida kweli hii ilistahili kupewa kiupaumbele?
Barabara toka Tanga hadi Bagamoyo tayari ipo! Hailazimu kuzungukia Chalinze kama ulivyo eleza hapa.
Barabara ya Bagamoyo Tanga ipo lakini haipitiki, magari hayatumii.
Ushahidi ni Mabasi yanapofika Bagamoyo yanatumia njia ya Msata.

Bagamoyo-Tanga ikiwekwa Lami ni masaa 2 hakuna mfanyabiashara angepoteza muda wa kuzunguka
Mradi huo wa hii barabara (mpya) bado siuelewi kabisa.
Ni master plan ya EAC kuunganisha nchi kimawasiliano. Ina 'make sense' Kwanini mtu atumie masaa 12 Mombasa-Dar wakati angeweza kutumia masaa 6? Muda na gharama za usafiri za ziada ni za nini?
Lakini labda nipanue mjadala zaidi, kwa kueleza wasiwasi wangu kuhusu hii miundo mbinu inayo tuunganisha zaidi na nchi moja tu tunayo pakana nayo, kati ya nchi nane majirani zetu.
Tuna mpaka mpana na Kenya ambao ni 'land' tena ukiunganisha majiji na miji mkikubwa
Arusha, Moshi, Tanga, Musoma, Kisumu , Nairobi, Nakuru, Maombasa
Hivi unakumbuka zamani tlisafiri kutoka Dar kupitia Nairobi kwenda Mwanza na Musoma?

Mipaka ya nchi nyingine inatusaidia kuingia lakini haiunganishi na miji au majiji lakini si sababu muhimu zaidi ya zile za uchumi. Trade partner wetu ni Kenya na volume ya business kati ya Kenya na Tanzania hailinganishwi na nchi zingine tunazopakana nazo

Kuna nini hasa kati ya Kenya na Tanzania, kwamba miundo mbinu zetu ziwe zinaelekea zaidi upande wa Kenya, kuliko, kwa mfano: Uganda, DRC, Burundi, Rwanda, Zambia, Malawi, Mozambique, n.k..
Hapana ! kuna vitu viwili, biashara na huduma.
Tunafanya biashara na Kenya kwasababu ya mpaka wetu 'naturally'' unaruhusu hali hiyo ikiwemo huduma za kibiashara kama Utalii. Tembelea Namanga au Sirari au Horohoro uone ile trade volume kisha ulinganishe na Uganda pale Mtukula, Rwanda au Burundi.

Pamoja na hayo hivi SGR na Barabara kama ile ya Kigoma-Tabora si sehemu ya mikakati?
Tayari kuna mkakati wa kufufua TAZARA ambayo itahudumu DRC , Zambia
Barabara ya Kwenda Malawi ni nzuri sana na inasaidia sana biashara

Sijaelewa kwanini una concerns kuhusu ''kuelekeza nguvu sehemu moja'' kwa mujibu wako
Ngoja nitoe mifano ninayo ijuwa:
Kuna barabara toka Tanga hadi Mombasa, kupitia mpakani (Holoholo?).
Mombasa ni mji wa pili kwa ukubwa Kenya, ukiunganishwa na Tanga ambalo ni Jiji kubwa kibiashara
Kuna barabara, toka Mombasa, kupitia Taveta na kuingia Tanzania mpakani (Holili?) na kuingia Moshi na kuelekea Arusha. Hii
Kuna Biashara kubwa katia ya maeneo hayoUtalii. Kuna Mbuga za wanyama sehemu zote
barabara sasa majirani wanaidai itumike kupitishia mizigo ya kwenda Burundi, toka Mombasa)!
Hii ni kwa faida yetu bahati mbaya sana hatujui kutumia fursa.
Kenya waliruhusu ma-bus ya Tanzania yapitie kwao kuingia Musoma na Mwanza, walikuwa na mkakati mzuri sana! Hata Dar es Salaam Aiport tungeweza kuitumia kama ''HUB' lakini hatujui kutumia fursa
Kuna barabara, tokea Arusha na kupandisha kwenda Kajiado kupitia mpakani (Namanga)
Biashara na Utalii
Kuna barabara toka Mwanza, kupitia Musoma kwenda Sirari na kuingia Kenya
Inaiunganisha na Kisumu na sehemu nyingine za Kenya na Uganda
Katika fikra zangu, nadhani kuna aina ya nguvu inayo tusukuma zaidi kuelekea upande huo mmoja; huku tukisahau kwamba kuna pande nyingine ambazo zinahitaji pia kutazamwa kwa umakini mkubwa.
Upande upi ambao haujatazamwa? Nimekuonyesha hapo juu. Si matakwa ya watu ni ' demand''
Niammbie biashara ya Tanzania na Msumbiji ipoje ukilinganisha na Kenya-Tanzania
Mpaka wetu na nchi ya DRC ni mrefu sana kuliko mipaka yetu mingine yote na majirani zetu. Hilo ziwa kuwepo hapo isichukuliwe kuwa kikwanzo, bali fursa nzuri ya kulitumia kuwasiliana na kufanya shughuli zetu na majirani hao.
SGR hadi Msonganti, Bujumbura na Kigali.Kuna barabara nzuri ya Kigoma inayounganisha na nchi za DRC, Rwanda na Burundi. Nishawishi ni wapi au ni kipi kilichokosekana?
 
Mbali na SGR,Mwendazake aliahidi kujenga barabara ya lami Tanga-Dodoma ambayao ni ya mkato na akasema fedha zipo,lakini huyu wa sasa hivi sijui anawaza nini
 
Mzee Mwanakijiji samahani naomba uturuhusu tuvuruge mada yako, tuna chepuka kidogo

Barabara ya Bagamoyo Tanga ipo lakini haipitiki, magari hayatumii.
Ushahidi ni Mabasi yanapofika Bagamoyo yanatumia njia ya Msata.

Bagamoyo-Tanga ikiwekwa Lami ni masaa 2 hakuna mfanyabiashara angepoteza muda wa kuzunguka

Ni master plan ya EAC kuunganisha nchi kimawasiliano. Ina 'make sense' Kwanini mtu atumie masaa 12 Mombasa-Dar wakati angeweza kutumia masaa 6? Muda na gharama za usafiri za ziada ni za nini?

Tuna mpaka mpana na Kenya ambao ni 'land' tena ukiunganisha majiji na miji mkikubwa
Arusha, Moshi, Tanga, Musoma, Kisumu , Nairobi, Nakuru, Maombasa
Hivi unakumbuka zamani tlisafiri kutoka Dar kupitia Nairobi kwenda Mwanza na Musoma?

Mipaka ya nchi nyingine inatusaidia kuingia lakini haiunganishi na miji au majiji lakini si sababu muhimu zaidi ya zile za uchumi. Trade partner wetu ni Kenya na volume ya business kati ya Kenya na Tanzania hailinganishwi na nchi zingine tunazopakana nazo


Hapana ! kuna vitu viwili, biashara na huduma.
Tunafanya biashara na Kenya kwasababu ya mpaka wetu 'naturally'' unaruhusu hali hiyo ikiwemo huduma za kibiashara kama Utalii. Tembelea Namanga au Sirari au Horohoro uone ile trade volume kisha ulinganishe na Uganda pale Mtukula, Rwanda au Burundi.

Pamoja na hayo hivi SGR na Barabara kama ile ya Kigoma-Tabora si sehemu ya mikakati?
Tayari kuna mkakati wa kufufua TAZARA ambayo itahudumu DRC , Zambia
Barabara ya Kwenda Malawi ni nzuri sana na inasaidia sana biashara

Sijaelewa kwanini una concerns kuhusu ''kuelekeza nguvu sehemu moja'' kwa mujibu wako

Mombasa ni mji wa pili kwa ukubwa Kenya, ukiunganishwa na Tanga ambalo ni Jiji kubwa kibiashara

Kuna Biashara kubwa katia ya maeneo hayoUtalii. Kuna Mbuga za wanyama sehemu zote

Hii ni kwa faida yetu bahati mbaya sana hatujui kutumia fursa.
Kenya waliruhusu ma-bus ya Tanzania yapitie kwao kuingia Musoma na Mwanza, walikuwa na mkakati mzuri sana! Hata Dar es Salaam Aiport tungeweza kuitumia kama ''HUB' lakini hatujui kutumia fursa

Biashara na Utalii

Inaiunganisha na Kisumu na sehemu nyingine za Kenya na Uganda

Upande upi ambao haujatazamwa? Nimekuonyesha hapo juu. Si matakwa ya watu ni ' demand''
Niammbie biashara ya Tanzania na Msumbiji ipoje ukilinganisha na Kenya-Tanzania

SGR hadi Msonganti, Bujumbura na Kigali.Kuna barabara nzuri ya Kigoma inayounganisha na nchi za DRC, Rwanda na Burundi. Nishawishi ni wapi au ni kipi kilichokosekana?
Mkuu 'Nguruvi3', kwa ujumla wake, niseme sijaona hoja hata moja ya nguvu ya kunishawishi katika yote haya uliyojibu hoja zangu zote.

Nitaeleza chache ya hizo ambazo sikuridhika nazo kama mifano.
Barabara ya Bagamoyo Tanga ipo lakini haipitiki, magari hayatumii.
Ushahidi ni Mabasi yanapofika Bagamoyo yanatumia njia ya Msata.

Bagamoyo-Tanga ikiwekwa Lami ni masaa 2 hakuna mfanyabiashara angepoteza muda wa kuzunguka
Wakati maeneo mengine ya nchi hakuna miundo mbinu inayotuunganisha na nchi jirani; lakini iwe ni kitu muhimu sana kushughulikia hiyo barabara ya ziada toka Mombasa hadi Bagamoyo, wakati zipo barabara kadhaa nzuri, hata kama zinachukua muda kiasi kufika Dar? Hii ni "Anasa".

Hii 'Master plan' ya EAC ni nani hasa anaibuni, maana inaonyesha wazi kuwa hiyo barabara ni mpango ulio buniwa kufurahisha baadhi ya watu tu! Ushirika wetu huu wa Afrika Mashariki, ushindwe kujuwa ni wapi palipo na uhitaji zaidi wa miundo mbinu kufanikisha ushirika itazame tu mradi ambao ni 'redundant' kama huu? hata ukichukulia Kenya yenyewe na Uganda, ambao wana mpaka mrefu kati yao. Sehemu za kuingiliana kuu ni mbili.
Uhitaji wa miundo mbinu kati yao ni mkubwa sana, hasa ukichukulia kwamba biashara kati ya nchi hizo ni kubwa zaidi kati yao, kushinda ilivyo huku kwetu!
Mipaka ya nchi nyingine inatusaidia kuingia lakini haiunganishi na miji au majiji lakini si sababu muhimu zaidi ya zile za uchumi. Trade partner wetu ni Kenya na volume ya business kati ya Kenya na Tanzania hailinganishwi na nchi zingine tunazopakana nazo
"Trade partner" ambaye siku zote yeye anafaidika zaidi na soko kwetu kuliko tunavyo faidika na soko kwake? Tunauza mali zetu nyingi zaidi nchi zingine kuliko tunavyouza Kenya, miaka yote. Na partner huyu haishi ulalamishi na kuweka vikwazo juu ya bidhaa zetu, huku yeye akitaka kufaidika zaidi na soko letu! Yeye anapenda sana kuchukuwa malighafi hapa, kama ngozi, pamba, mahindi alizeti, n.k., ili sisi tukanunue biskuti kwake

Kwa nini tushikiliwe na 'trade partner' wa namna hii huku tukipoteza nguvu zetu za kuendeleza hawa 'partner' wengine wengi wanao tuzunguka?
Tuweke juhudi; tutumie hicho kidogo kilichopo kuendeleza u-'partner' wetu na hawa ambao tumewasahau siku nyingi.

Mombasa na Tanga tayari zimeunganishwa. Kuna barabara nzuri tu toka siku nyingi.
Hii ni kwa faida yetu bahati mbaya sana hatujui kutumia fursa.
Kenya waliruhusu ma-bus ya Tanzania yapitie kwao kuingia Musoma na Mwanza, walikuwa na mkakati mzuri sana! Hata Dar es Salaam Aiport tungeweza kuitumia kama ''HUB' lakini hatujui kutumia fursa
Hapa kusema kweli unanishangaza pakubwa.
Fursa ya Burundi kutumia bandari ya Mombasa kwa kupitia kwenye barabara zetu, lakini tusione fursa ya Burundi kutumia bandari zetu za Tanga na Dar es Salaam?

Hili swala la utalii, kwani watalii hawawezi kuja Tanzania bila kwenda Kenya? Ukiniuliza mimi nitakwambia kwamba Tanzania ndiyo inayo tumika kuinufaisha Kenya katika swala hilo, na ndiyo maana wanalilia sana hiyo 'visa' ya pamoja; na ndiyo maana Mlima Kilimanjaro ulikuwa Kenya zaidi ya Tanzania, hali kadhalika Serengeti ipo kuiinua Maasai Mara!

Hilo la nchi kushindwa kuwa na miundombinu na kulazimika kutumia ya nchi zingine ili uweze kuyafikia maeneo yaliyomo nchini mwako ni aibu isiyofaa kusimulia hata kidogo.
Na kumbuka, wakati hayo yanatokea, miundo mbinu kati ya nchi hizi jirani ilikuwa mizuri tayari. Nani aliyekuwa akifanya hujuma ya nchi kuwa katika hali mbovu kiasi hicho!!
Sasa mpango ni huo huo wa kuendelea kutushikilia tusitazame majirani zetu wengin na hata baadhi ya maeneo yetu wenyewe ndani ya nchi, lakini tuwe na barabara za ziada za kutufikisha nchi jirani?
Hayo majiji yaliyopo huko, huku kwingine hayapo? Biashara haiwezi kuwa sehemu moja tu, biashara ipo kila mahali, kazi iliyopo ni kuitafuta tu na kuistawisha kwa uwepo wa miundo mbinu mizuri. .

Kuna uhitaji mkubwa sana kwa Tanzania kustawisha uhusiano wa kibiashara na majirani zake, Uganda, DRC, Zambia na hata Msumbiji. Kuendelea kusisitiza biashara kati ya Kenya na Tanzania, biashara ambayo matokeo yake ni hafifu sana ni kupoteza muda na fursa. Sioni sababu hata moja ya Tanzania kutokuwa na biashara kubwa kati yake na DRC; lakini nguvu kubwa zinatumika Kenya, ambako biashra imedumaa miaka na miaka, na sababu kubwa ikiwa kwa nchi moja kutaka kunufaika zaidi dhidi ya nchi nyingine.

Bahati nzuri iliyo nayo Tanzania, tofauti kabisa na Uganda; haina utegemezi wowote wa maana kwa hiyo nchi jirani. Tanzania inao uwezo wa kuendesha mambo yake yote bila ya kuitegemea Kenya. Ingekuwa vinginevyo, tunge lizwa sana, kama Uganda wasivyoisha kunyanyaswa.
 
Nitaeleza chache ya hizo ambazo sikuridhika nazo kama mifano.
Wakati maeneo mengine ya nchi hakuna miundo mbinu inayotuunganisha na nchi jirani;
Nimekuuliza ni eneo gani tulitazame! tusiongelee jumla tuwe specific kama Mombasa-Tanga
Hii 'Master plan' ya EAC ni nani hasa anaibuni, maana inaonyesha wazi kuwa hiyo barabara ni mpango ulio buniwa kufurahisha baadhi ya watu tu! Ushirika wetu huu wa Afrika Mashariki, ushindwe kujuwa ni wapi palipo na uhitaji zaidi wa miundo mbinu kufanikisha ushirika itazame tu mradi ambao ni 'redundant' kama huu?
Mradi umeandikiwa ''proposal' kisha ukafanyiwa analysis na ndipo pesa zikatoka kwa wahisani
Si suala la EAC pekee. Sijui kama umefika na kuona faida za barabara kati ya Namanga-Holili
hata ukichukulia Kenya yenyewe na Uganda, ambao wana mpaka mrefu kati yao. Sehemu za kuingiliana kuu ni mbili.
Uhitaji wa miundo mbinu kati yao ni mkubwa sana, hasa ukichukulia kwamba biashara kati ya nchi hizo ni kubwa zaidi kati yao, kushinda ilivyo huku kwetu!
Biashara kati ya Uganda na Kenya ni ndogo kuliko Kenya-Tanzania. Ni ukweli nitakuletea takwimu
Uganda-Kenya wana mradi wa EAC unaojulikana kama North corridor, unaufahamu!
"Trade partner" ambaye siku zote yeye anafaidika zaidi na soko kwetu kuliko tunavyo faidika na soko kwake? Tunauza mali zetu nyingi zaidi nchi zingine kuliko tunavyouza Kenya, miaka yote. Na partner huyu haishi ulalamishi na kuweka vikwazo juu ya bidhaa zetu, huku yeye akitaka kufaidika zaidi na soko letu! Yeye anapenda sana kuchukuwa malighafi hapa, kama ngozi, pamba, mahindi alizeti, n.k., ili sisi tukanunue biskuti kwake
Biashara imegeuka, Tanzania ina export zaidi Kenya kuliko ilivyokuwa.
Kasome gazeti la EA, Kenya wame opt kuelekea DRC.

Soko la Kenya ni la kwetu lakini ujinga unatuanguasha.Sisi tulitakiwa tuwe '' food basket' ya Kenya kwasababu ya arable land. Tuna madini kama Kioo ambayo tulitakiwa tuwe na viwanda kuongeza thamani! hatuna! Tunanunua biskuti kwasababu sisi ni 'stupid'
Kwa nini tushikiliwe na 'trade partner' wa namna hii huku tukipoteza nguvu zetu za kuendeleza hawa 'partner' wengine wengi wanao tuzunguka?
Kwani ni partner gani tuliyemuacha? Ni lazima katika uchumi tuwe ''strategic' .
Burundi na Rwanda zina population ya 30 Milion. Kenya ina 50M na uchumi mkubwa kuliko Burundi au Malawi.
Msumbiji hawafanyi biashara kubwa na sisi wame 'base' zaidi SADC kama mkakati wao.
Malawi hakuna shida ya kufikika. DRC Kuna SGR tena inaingia Burundi na Rwanda.
Tatizo liko wapi?
Tuweke juhudi; tutumie hicho kidogo kilichopo kuendeleza u-'partner' wetu na hawa ambao tumewasahau siku nyingi.
Partner wapi hao? Mbona huwataji tuwajadili!
Mombasa na Tanga tayari zimeunganishwa. Kuna barabara nzuri tu toka siku nyingi.
Tunachosema hapa ni Tanga-Bagamoyo! ambako kuna 'interest' zetu si Tanga-Mombasa.

Na Tanga- Bagamoyo ndipo hoja yangu ilipo, kwamba, hatuna sababu ya kusafiri kwa ''square' yaani Tanga-Segera-Chalinze-Dar! ni upotevu wa rasilimali na muda. Masaa 2 yanatosha Tanga-Bagamoyo
Fursa ya Burundi kutumia bandari ya Mombasa kwa kupitia kwenye barabara zetu, lakini tusione fursa ya Burundi kutumia bandari zetu za Tanga na Dar es Salaam?
Well, Burundi wanatumia kwasababu sisi ni 'stupid''. Bandarizilipaswa kuwapa incentive, kila siku tunabadili mameneja. Tumeshindwa kuendesha shirika la Reli, usiwalaumu tujilaumu
Hili swala la utalii, kwani watalii hawawezi kuja Tanzania bila kwenda Kenya? Ukiniuliza mimi nitakwambia kwamba Tanzania ndiyo inayo tumika kuinufaisha Kenya katika swala hilo, na ndiyo maana wanalilia sana hiyo 'visa' ya pamoja; na ndiyo maana Mlima Kilimanjaro ulikuwa Kenya zaidi ya Tanzania, hali kadhalika Serengeti ipo kuiinua Maasai Mara!
Hapana! kuna kutegemeana. Nenda Kenyatta Inter Airport utaona jinsi ndege zinavyotoka mataifa duniani zikileta Watalii. Again, ni ujinga wetu tulikuwa na akina PIA, AEROFLOTA, SAS, Luftansa, France, BA , Ethipoia, Egypt, n.k. Jiulize kwanini ziliacha kuja kwa muda mrefu zikaendelea Nairobi.
Tunategemea sana soko la utalii la Kenya lakini ni kwa ujinga wetu
Hilo la nchi kushindwa kuwa na miundombinu na kulazimika kutumia ya nchi zingine ili uweze kuyafikia maeneo yaliyomo nchini mwako ni aibu isiyofaa kusimulia hata kidogo.
Yes ilikuwa ni aibu na Kenya walitumia fursa
Na kumbuka, wakati hayo yanatokea, miundo mbinu kati ya nchi hizi jirani ilikuwa mizuri tayari. Nani aliyekuwa akifanya hujuma ya nchi kuwa katika hali mbovu kiasi hicho!!
Hapana, Barabara ya Dar-Mwanza ilikuwa haipitiki.
Hata KAMATA ililazimika kupitia Kenya.Niliyaona kwa macho yangu
Sasa mpango ni huo huo wa kuendelea kutushikilia tusitazame majirani zetu wengin na hata baadhi ya maeneo yetu wenyewe ndani ya nchi, lakini tuwe na barabara za ziada za kutufikisha nchi jirani?
Hayo majiji yaliyopo huko, huku kwingine hayapo? Biashara haiwezi kuwa sehemu moja tu, biashara ipo kila mahali, kazi iliyopo ni kuitafuta tu na kuistawisha kwa uwepo wa miundo mbinu mizuri. .
Kuna hoja yako 'imejificha' lakini nitakueleza. Hapa JF kuna uzi ukionyesha takwimu za BoT.

Mikoa ya kaskazini iliongoza sikumbuki vizuri nadhani kwa miezi 3 ikichangia Trilions katika pato la Taifa.
Daraja lilipovunjika pale Chalinze-Goba JK alisema '' anapeleka jeshi' kwasababu ile barabara ni ''life line of the economy'. Nina maana kwamba shughuli za uchumi ni hesababu si ku-balance kipi kiende wapi.
Trilioni zilizoingia BoT zinatakiwa zijenga Barabara ya Mtwara-Songea yenye faida sana kiuchumi.

Pesa zinazopatikana kwa shughuli za uchumi 'mikoa na nchi jirani'' zitumike kujenga barabara ya Tanga-Dodoma. Ni wendawazimu kuzunguka Tanga-Sgera- Chalinze-Morogoro-Dodoma.

Ni wendawazimu kusafiri Arusha-Kilimanjaro-Segera-Chalinze- Morogoro. Tayari kuna barabara kuanzia Korogwe- Handeni-Kilosa-Morogoro. Iwekwe lami tukikusanya pesa za 'Mikoa na jirani''

Ni wendawazimu mtu kwenda Dar-Lindi-Mtwara akitoka bara.
Ijengwe Barabara ya kupitia JNHPP kuanzia Chalinze ili kupunguza muda wa kusafiri na gharama zitokanazo

Nakubaliana na PPP kujenga barabara ya kulipia. Pesa zitakwenda kujenga miundo mbinu kunakohitajika.

Ukinishawishi Reli ya Mtwara-Songea nakubaliana nawe 100% kwasababu ina manufaa kiuchumi si kwasababu tunataka mikoa hiyo nayo iwe na reli.
Kuna uhitaji mkubwa sana kwa Tanzania kustawisha uhusiano wa kibiashara na majirani zake, Uganda, DRC, Zambia na hata Msumbiji.
Kimekosekana nini kwa majirani hawa! kwa miundo mbinu?
Kuendelea kusisitiza biashara kati ya Kenya na Tanzania, biashara ambayo matokeo yake ni hafifu sana ni kupoteza muda na fursa.
Biashara ya Tanzania-Kenya ni kubwa kuliko biashara ya jirani mwingine! huu ni ukweli wa wazi.
Unaweza kuwa na 'reservations' zingine lakini haziondoi ukweli

Nipe data ni nchi gani kati ya 8 tunazopakana nazo yenye biashara kubwa na sisi kuliko Kenya.
Katika EAC Kenya ni super power, sasa unakwenda ku trade na Burundi ili iweje
Sioni sababu hata moja ya Tanzania kutokuwa na biashara kubwa kati yake na DRC; lakini nguvu kubwa zinatumika Kenya,
DRC si kuna SGR hadi Msongati! kuna TAZARA kuna usafiri wa Ziwa Tanganyika, kuna Barabara ya Kigoma.
Unataka kipi tusichokiona wenzako!
Bahati nzuri iliyo nayo Tanzania, tofauti kabisa na Uganda; haina utegemezi wowote wa maana kwa hiyo nchi jirani. Tanzania inao uwezo wa kuendesha mambo yake yote bila ya kuitegemea Kenya. Ingekuwa vinginevyo, tunge lizwa sana, kama Uganda wasivyoisha kunyanyaswa.
Hata US inaweza kuendesha mambo yake bila kutegemea Taifa lolote lakini ukweli unabaki pale pale uchumi ni kitu 'intertwining' kwamba huwezi kuwa na uchumi wako.

Tunategeana sana na Kenya na napenda sana kwasababu Kenya wanatoa challenge! Ndio maana tunalazimika kufikiriData za BoT zinathibitisha umuhimu wa biashara na Kenya

Unaweza ''kuwa na concerns'' na Kenya na Mikoa jirani, hilo haliwezi kufuta ukweli wa takwimu za uchumi.
 
Sasa Tanga kuna vitu gan vinafanyika na umeme wote huu bwelele. Kkulikuwa na kiwanda cha Mbolea na Kiwanda cha Chuma..vilikufa?
Vyote chali ni magofu watu wamekimbia kenya ...Hata yule wa Helatho alitaka kukimbilia Kenya .

Kiufupi mwaka 90's Tanga ilikufa rasmi , kwa sasa hamna shughuli za kiserikali wala bandari hamna kitu haina promo
 
Nimekuuliza ni eneo gani tulitazame! tusiongelee jumla tuwe specific kama Mombasa-Tanga

Mradi umeandikiwa ''proposal' kisha ukafanyiwa analysis na ndipo pesa zikatoka kwa wahisani
Si suala la EAC pekee. Sijui kama umefika na kuona faida za barabara kati ya Namanga-Holili

Biashara kati ya Uganda na Kenya ni ndogo kuliko Kenya-Tanzania. Ni ukweli nitakuletea takwimu
Uganda-Kenya wana mradi wa EAC unaojulikana kama North corridor, unaufahamu!

Biashara imegeuka, Tanzania ina export zaidi Kenya kuliko ilivyokuwa.
Kasome gazeti la EA, Kenya wame opt kuelekea DRC.

Soko la Kenya ni la kwetu lakini ujinga unatuanguasha.Sisi tulitakiwa tuwe '' food basket' ya Kenya kwasababu ya arable land. Tuna madini kama Kioo ambayo tulitakiwa tuwe na viwanda kuongeza thamani! hatuna! Tunanunua biskuti kwasababu sisi ni 'stupid'

Kwani ni partner gani tuliyemuacha? Ni lazima katika uchumi tuwe ''strategic' .
Burundi na Rwanda zina population ya 30 Milion. Kenya ina 50M na uchumi mkubwa kuliko Burundi au Malawi.
Msumbiji hawafanyi biashara kubwa na sisi wame 'base' zaidi SADC kama mkakati wao.
Malawi hakuna shida ya kufikika. DRC Kuna SGR tena inaingia Burundi na Rwanda.
Tatizo liko wapi?

Partner wapi hao? Mbona huwataji tuwajadili!

Tunachosema hapa ni Tanga-Bagamoyo! ambako kuna 'interest' zetu si Tanga-Mombasa.

Na Tanga- Bagamoyo ndipo hoja yangu ilipo, kwamba, hatuna sababu ya kusafiri kwa ''square' yaani Tanga-Segera-Chalinze-Dar! ni upotevu wa rasilimali na muda. Masaa 2 yanatosha Tanga-Bagamoyo

Well, Burundi wanatumia kwasababu sisi ni 'stupid''. Bandarizilipaswa kuwapa incentive, kila siku tunabadili mameneja. Tumeshindwa kuendesha shirika la Reli, usiwalaumu tujilaumu

Hapana! kuna kutegemeana. Nenda Kenyatta Inter Airport utaona jinsi ndege zinavyotoka mataifa duniani zikileta Watalii. Again, ni ujinga wetu tulikuwa na akina PIA, AEROFLOTA, SAS, Luftansa, France, BA , Ethipoia, Egypt, n.k. Jiulize kwanini ziliacha kuja kwa muda mrefu zikaendelea Nairobi.
Tunategemea sana soko la utalii la Kenya lakini ni kwa ujinga wetu

Yes ilikuwa ni aibu na Kenya walitumia fursa

Hapana, Barabara ya Dar-Mwanza ilikuwa haipitiki.
Hata KAMATA ililazimika kupitia Kenya.Niliyaona kwa macho yangu

Kuna hoja yako 'imejificha' lakini nitakueleza. Hapa JF kuna uzi ukionyesha takwimu za BoT.

Mikoa ya kaskazini iliongoza sikumbuki vizuri nadhani kwa miezi 3 ikichangia Trilions katika pato la Taifa.
Daraja lilipovunjika pale Chalinze-Goba JK alisema '' anapeleka jeshi' kwasababu ile barabara ni ''life line of the economy'. Nina maana kwamba shughuli za uchumi ni hesababu si ku-balance kipi kiende wapi.
Trilioni zilizoingia BoT zinatakiwa zijenga Barabara ya Mtwara-Songea yenye faida sana kiuchumi.

Pesa zinazopatikana kwa shughuli za uchumi 'mikoa na nchi jirani'' zitumike kujenga barabara ya Tanga-Dodoma. Ni wendawazimu kuzunguka Tanga-Sgera- Chalinze-Morogoro-Dodoma.

Ni wendawazimu kusafiri Arusha-Kilimanjaro-Segera-Chalinze- Morogoro. Tayari kuna barabara kuanzia Korogwe- Handeni-Kilosa-Morogoro. Iwekwe lami tukikusanya pesa za 'Mikoa na jirani''

Ni wendawazimu mtu kwenda Dar-Lindi-Mtwara akitoka bara.
Ijengwe Barabara ya kupitia JNHPP kuanzia Chalinze ili kupunguza muda wa kusafiri na gharama zitokanazo

Nakubaliana na PPP kujenga barabara ya kulipia. Pesa zitakwenda kujenga miundo mbinu kunakohitajika.

Ukinishawishi Reli ya Mtwara-Songea nakubaliana nawe 100% kwasababu ina manufaa kiuchumi si kwasababu tunataka mikoa hiyo nayo iwe na reli.

Kimekosekana nini kwa majirani hawa! kwa miundo mbinu?

Biashara ya Tanzania-Kenya ni kubwa kuliko biashara ya jirani mwingine! huu ni ukweli wa wazi.
Unaweza kuwa na 'reservations' zingine lakini haziondoi ukweli

Nipe data ni nchi gani kati ya 8 tunazopakana nazo yenye biashara kubwa na sisi kuliko Kenya.
Katika EAC Kenya ni super power, sasa unakwenda ku trade na Burundi ili iweje

DRC si kuna SGR hadi Msongati! kuna TAZARA kuna usafiri wa Ziwa Tanganyika, kuna Barabara ya Kigoma.
Unataka kipi tusichokiona wenzako!

Hata US inaweza kuendesha mambo yake bila kutegemea Taifa lolote lakini ukweli unabaki pale pale uchumi ni kitu 'intertwining' kwamba huwezi kuwa na uchumi wako.

Tunategeana sana na Kenya na napenda sana kwasababu Kenya wanatoa challenge! Ndio maana tunalazimika kufikiriData za BoT zinathibitisha umuhimu wa biashara na Kenya

Unaweza ''kuwa na concerns'' na Kenya na Mikoa jirani, hilo haliwezi kufuta ukweli wa takwimu za uchumi.
bandiko linapokuwa refu hivi linapoteza ari ya kusoma.
Hata hivyo nitakapopata nafasi nitalipitia lote vizuri na kukujibu itakapohitajika kujibu.

Huko mwanzo tu nimekwisha ona tayari makosa. Biashara kati ya Kenya na Uganda ni kubwa zaidi kila mwaka. Uganda ni soko namba moja kwa Kenya Afrika.
 
Tanga ni mmoja ya sehemu yenye potatial kubwa sana ya kimaendeleo hapa nchini, Lakini thanks to CCM imekuwa ni sehemu ya kutilisha huruma
 
Reli hujengwa hasa kwa kusafirisha bidhaa na mizigo mizito na kwa wingi. Abiria ni nyongeza tu
Kama umesoma makampuni yaliyo 'Bid' kuingia ubia na TRC asilimia kubwa ni mizigo.
Concept yako kwamba reli ni kwa ajili ya abiria haina mashiko! na si kweli

Pili, sijui una umri gani, nikufahimishe kuwa miaka ya 70/80/hadi 90 kulikuwa na Treni ya Dar-es-slaam- Tanga-Moshi KILA SIKU saa 10 jioni na kufika asubuhi. Usafiri ulirahisisha sana biashara lakini pia ulilinda Barabara.
Ni usafiri uliotoa nafuu kwa abiria na mizigo.

Reli hii ya MGR ukiwapa wawekezaji utashangaa na macho yako.
Jamani eeh acheni kujidanganya, SGR haitaenda Tanga, wala Kilimanjaro, wala Arusha wala Mbeya. Sababu Arusha, Moshi,Tanga hakuna mizigo wala abiria kutosheleza uwekezaji huo ata waeke miaka 10. Mbeya kuna Cape gauge TAZARA ambayo toka 1970 haijawai kuendeshwa kwa faida, abiria kutoka Zambia kuja Tanzania ni wachache, mizigo kutoka Zambia ni changamoto sababu Zambia pia inabezi sana kusafirisha mizigo kupitia Angola ambpo ni karibu na Lusaka. Plan ya Tanzania ni kuelekea Central Congo kwa SGR tu, kufuata ( Pre colonial Central Caravan Route) hadi KINDU, ili kuipata Congo na Central Africa Republic (Bangue) kwa mizigo na Abiria sababu hapo kuna migodi na idadi kubwa ya watu na biashara. Sasa wewe unataka ujenge SGR kwenda Tanga alafu inabeba mzigo upi na kuelekea wapi maana Kenya Kuna SGR bandari ya Mombasa,a wana plan kuipeleka Malaba, Uganda, Rwanda hadi Congo ambapo wote tunagombania Congo, sasa kama plan ya SGR ni kuunganisha uelekeo wa nchi wenye biashara kubwa, Tanga ni hasara kubwa. Kumbuka SGR ni gharama kubwa, ndio maana hakuna nchi katika Africa inajenga kwa haraka. Dar Moro Mkotopola ni Km 750 tumewazidi wote katika Africa kwa urefu, tukimalizia ya mwanza na Msongati Burundi 2005 Km tutakua wa 5 au 6 duniani badala ya China, Spain, France, Germany alafu inakuja Tanzania. Yani tutakuwa tumewapita USA, Japan, Italy, Urus na wengine. Sasa wewe unataka tukope alafu tukajenge SGR Tanga, hakuna serikali ya namna hiyo. Ridhikeni na hiyo iliopo tu. Usione Morogoro abiria elfu 40 ndani ya wiki 3 ukajua basi Mikoa mingine inaweza, Morogoro ni namba nyingine inapokuja biashara za usafiri iwe wa basi au treni maana mkoa una mishe nyingi sana.
 
Reli ya tazara ikifanyiwa adjust kidogo sana (upgrading) ni SGR halisi, hakika!, uanze kuwekwa mfumo wa umeme taratibu.
Unai just vipi?. SGR railway ni pana, mataruma yake ya zege ni marefu hii inasababisha train ya sgr kukimbia sana bila kuyumba, na kubeba mzigo mzito sababu inalala kwenye rail vizuri. Cape gauge ya TAZARA haipo katika kiwango cha SGR ingawa ni bora kuliko Meter gauge ya Mkoloni. TAZARA inakona za kutosha, na ina miinuko pia, lazima ung'oe moja ujenge nyingine.
 
Unai just vipi?. SGR railway ni pana, mataruma yake ya zege ni marefu hii inasababisha train ya sgr kukimbia sana bila kuyumba, na kubeba mzigo mzito sababu inalala kwenye rail vizuri. Cape gauge ya TAZARA haipo katika kiwango cha SGR ingawa ni bora kuliko Meter gauge ya Mkoloni. TAZARA inakona za kutosha, na ina miinuko pia, lazima ung'oe moja ujenge nyingine.
Wakiamua kuingoa na kujenga nyingine itatumika gharama kidogo mno!
 
Wakiamua kuingoa na kujenga nyingine itatumika gharama kidogo mno!
Unajua TAZARA inapopita?. Tofautisha Central corridor na Southern Highland Corridor. TAZARA inapita sehem ngumu haswa kuliko rail zote, Kipande chake cha Morogoro, Kisaki, Mang'ula, Ifakala, Mngeta, Mbingu, Mlimba ni mwendo wa mito, milima, handaki na maporomoko, Mlimba, Mgololo hadi Makambako Njombe ni Handaki, nyanda za Juu na Kona nyingi, bado kule Chimala Mbalizi na Songwe. Lakini SGR ya kati inapita sehem nyingi tambalale, Mahandaki na Mito yapo Kilosa Morogoro tu. Gharama ni kama zote.
 
451250552_122158456112218164_8869557197472389158_n.jpg
 
Back
Top Bottom