Swali la uchumi: Kwanini vikwazo vya mataifa yenye nguvu kubwa kiuchumi havifanyi kazi dhidi ya Urusi?

Swali la uchumi: Kwanini vikwazo vya mataifa yenye nguvu kubwa kiuchumi havifanyi kazi dhidi ya Urusi?

Tokea mwaka 1944, baada ya kutengeneza mfumo wa Bretton-Woods hakuna taifa ambalo limewahi kuwa na uchumi mkubwa kama Marekani. Kufika mwaka 1945, Marekani ilikuwa inamiliki nusu nzima ya uchumi wa dunia. Fedha ya Marekani ikishikiliwa na dhahabu (Gold-Backed) ilikuwa ndiyo inatumiwa kwa kiwango kikubwa kwenye biashara zote za kimataifa.

Mwaka 1957, baada ya Raisi Gamal Abdel Nasser wa Misri kutaifisha mfereji wa Suez, Uingereza, Ufaransa na Israel waliunda mkakati wa kuvamia Misri ili kumtoa Nasser. Mkakati huu ulikufa kibudu baada ya Raisi wa Marekani General Dwight Eisenhower kuwachimba mkwara mzito Waingereza kwamba wangeacha kununua hati-fungani (Sovereign Bonds) za Uingereza na nyingine wangeziuza, jambo ambalo lingeangusha uchumi wa Uingereza.

Kiufupi, baada ya hili kutokea Raisi wa Ufaransa General Charles De Gaulle alilalamika na kusema kwamba "The dollar gives America an exorbitant privilege in international financial system". Akimaanisha kwamba dola inampa Marekani nguvu iliyomithirika kwenye uchumi wa dunia dhidi ya mataifa mengine. Kiufupi Marekani akikutoa kwenye mfumo wake wa kifedha, lazima uumie.

Wataalamu wanatumia vipimo (Metrics) kama GDP na PPP kupima uchumi wa dunia. Ukitumia kipimo cha GDP, nadhani Marekani ndiyo taifa lenye uchumi mkubwa zaidi duniani likifuatiwa na Uchina. Uchumi wa Marekani peke yake ni asilimia 24% ya uchumi wa dunia (Global GDP). Kiufupi ni kwamba, all financial roads lead to America.

Marekani hayuko peke yake, anashirikiana na wenzake wa kule Ulaya (European Union) na wenzake wa chama cha mabwanyenye wa dunia almaarufu kama G7. Ukichanganya uchumi wa Marekani, Ufaransa, Uingereza, Ujerumani, Italia, Canada na Japan, ambao ndiyo nchi tajiri zaidi duniani unapata asilimia 30.7% ya uchumi wa dunia (Global GDP).

Kiuhalisia, haya mataifa saba ndiyo yanayoendesha uchumi wa dunia kupitia mifumo waliyoitengeneza baada ya mwaka 1945. Viwanda vikubwa duniani ni vyao, masoko makubwa ya hisa ni yao, mabenki makubwa duniani ni yao, wao ndiyo wanaongoza katika kuzikopesha fedha nchi nyingine na wao ndiyo wanaongoza kwa kuuza huduma zaidi hapa duniani.

Maswali yangu ya kiuchumi ni haya yafuatayo:
Mosi, kwanini Urusi ambayo ni asilimia 4% tu ya uchumi wa dunia (Share in Global GDP) bado haijaanguka baada ya mataifa makubwa yanayomilikia asilimia 30.7% ya uchumiwa dunia kuwawekea vikwazo vikali ?

Pili, kwanini makampuni ya Urusi ya nishati ndiyo yameongoza duniani kwa kuuza zaidi nishati, ilhali yamewekewa vikwazi baada vikali ? Takwimu zilizotolewa na Marekani yenyewe zinasema kiujumla mashirika ya nishati ya Urusi yameuza zaidi na kupata faida kipindi hiki cha vita na vikwazo kuliko kipindi kingine chochote. Tatizo liko wapi hapa ?

Tatu, Je, tutegemee kwamba kuna siku hivi vikwazo vitafanya kazi na vitauangusha uchumi wa Urusi kama ambavyo Raisi Biden alisema mwaka 2022 kabla ya uvamizi kuanza ? Alisema kwamba uchumi wa Urusi ungeanguka ndani ya wiki chache tu, sasa ni mwaka na zaidi. Mataifa ya Magharibi yamefanikiwa au tuendelee kusubiri ?
Kichuguu FRANC THE GREAT Drifter
 
Bwana Armata nimeuliza maswali rahisi sana ambaya hata mtoto anayesoma shahada ya uchumi, sheria au siasa angeweza kuyajibu. Nilihitaji uchambuzi wa kiuchumi uliojaa takwimu, mahesabu na kanuni za kiuchumi. Bahati mbaya mno nimeona maelezo na maoni yako binafsi. Haina shida twende taratibu hivyohivyo.

Nashangaa mno kuona kwamba msomi kama wewe kutofahamu kwamba The Oil Embargo ni moja ya sababu kubwa iliyosababisha kutengeneza mfumo mpya wa uchumi wa dunia Bretton Woods II na kusababisha American-Asia Corporate Inversion mambo makuu yanayoigharimu Marekani mpaka leo.

Kama vitu rahisi hivi vimekupita wewe mchambuzi wa mambo ya siasa basi kuna tatizo kubwa pahala. Ila tuendelee taratibu hivihivi naamini tutaelewana huko mbele.

Bwana Armata nimeuliza swali rahisi sana. Nini kimepelekea mataifa ya G7 kupandisha riba za mabenki juu (Hiking Interest Rates). Unaweza pia hata kunitajia sababu za kwanini Urusi naye alipandisha riba za mabenki juu. Ntakushukuru kama utanipa majibu.

Umejibu vyema kabisa, lakini hapa napata maswali mengine matatu;

Swali la kwanza, hao Ulaya wanavyotafuta mbadala wa nishati ya Urusi watapambanaje na tatizo la mdororo wa uchumi ambalo limewakumbuka au hili tatizo litaondoka ndani ya usiku mmoja ?

Ifahamike takwimu za International Energy Agency (IEA) zinasema itachukua miaka isiyopungua kumi kwa Ulaya kuweza kupata mbadala wa nishati ya bei rahisi kama ya Urusi.

Swali la pili, gharama za uzalishaji zikipanda juu kwasababu ya ghaarama za nishati mbadala unadhani viwanda vitaendelea kufanya uzalishaji katika kiwango ambacho kilikuwepo kabla ya mwaka 2022, ???

Kumbuka kanuni za uchumi wa kibepari zinasema hivi, ili uweze kupata faida kwenye uzalishaji ni lazima uwe na nishati ya bei ndogo na malighafi za bei ndogo. Wanavyotafuta mbadala wa nishati ya Urusi wataendelea kuwa na nguvu kubwa ya uzalishaji ???

Swali la tatu, wanavyotumia gharama kubwa kutafuta mbadala wa nishati ya Urusi, bara la Ulaya watakabilianaje na tatizo la mfumuko wa bei (Energy Inflation), ???

Mwisho kabisa, ndiyo Urusi imeingia kwenye mdororo wa uchumi kwasababu ya vikwazo vikubwa kutoka mataifa ya G7 ambayo ndiyo yenye uchumi mkubwa duniani. Ila ambacho kinanishangaza ni kwanini mataifa yanayomiliki asilimia 30.7% ya uchumi wa dunia nayo yawe kwenye kundi moja na Urusi taifa ambalo ni asilimia 4% ya uchumi wa dunia. Huoni hapa kuna walakini ???


Bwana Armata majawabu yako yanazidi kunishangaza mno. Urusi siyo taifa lenye uchumi wa mitaji (Capital Market Driven Economy) kama Marekani. Marekani ndiyo taifa tajiri duniani kwasababu asilimia 34% ya soko la mitaji (Capital Markets) duniani linashikiliwa kwa fedha za kimarekani (Denominated in US Dollars). Hivyo Marekani ndiyo makao makuu ya masoko ya mitaji duniani.

Mabenki ya Urusi yakiwa mufilisi haileti madhara kwa dunia hata kidogo, lakini mabenki ya Marekani yakiwa mufilisi dunia nzima itaona madhara kwasababu yeye peke yake ndiyo mwenye soko kubwa la mitaji duniani ambalo karibia benki kuu (Central Banks) zote zinanunua bidhaa na huduma.

Deni la Marekani linamilikiwa (US Treasury Bills are held by foreign states) na mataifa ya nje kama Uchina kama mbinu ya kuyawezesha mataifa hayo yapate fedha za kimarekani kwa wingi kama mbinu ya uwekezaji, lakini pia kupunguza thamani ya fedha zao , jambo ambalo kiuchumi ni muhimu mno kwenye kufanikisha biashara ya kimataifa (China uses this economic technique of devaluating her local currency against the dollar in-order to boost exports)

Nilitegemea haya unayafahamu hivyo usingeleta mfano wa mabenki ya Urusi. lakini kwasababu hukuyafahamu basi nimekupa takwimu na sababu za kiuchumi kwanini umufilisi wa mabenki ya Urusi na Marekani uko tofauti. Mtu yoyote aliyesoma uchumi na kufahamu vizuri siasa za dunia hawezi kufanya huu ulinganifu.

Turudi kwenye swali letu la msingi: Nini kimepelekea mabenki 1000 ya Marekani yanayouza mitaji duniani kote kuwa mufilisi (Insolvent), ???

Uko sawa kabisa, Urusi hauzi nishati ya bure, lakini ndiyo nchi inayoongoza kwa kuuza nishati ya bei nafuu kwa nchi za Ulaya, Uchina na India. Uchumi wa viwanda wa Ujerumani una thamani ya dola za Kimarekani Trilioni 1, lakini unaendeshwa na nishati kutoka Urusi yenye thamani ya dola za kimarekani Bilioni 60 tu. Huo mbadala watakoupata hapa ni upi ndugu yangu ?

Kuhusu mkataba baina ya Uchina na Saudi Arabia nilitegemea ufahamu kwamba nishati inayotoka ghuba ya Uajemi kwenda Uchina husafirishwa kupita bahari hivyo ni gharama kwasababu ya muda, bima (Maritime Insurance) na upakiaji (Packaging). Gesi inayokuja kutoka Saudi Arabia kwenda Uchina ni LNG, ambayo ni gharama mno kuitengeneza. Ila pia kumbuka kampuni la bima kama LLYODS OF LONDON la Uingereza linachaji dola za kimarekani milioni 50 kwa mzigo mmoja wa majini.

Unadhani kuliko kutumia Trans-Siberian Pipeline ambayo husafirisha gesi kwa haraka bila ukomo, Uchina atajikita kabisa kwenye kutegemea mkataba wake na Saudi-Arabia ???

Bwana Armata nakushauri kama kaka, usijibu hivi tena mbele za watu. Yaani unapima soko la nchi husika kwa kuangalia manunuzi ya magari kweli. Unataka kusema leo hii Tanzania ikununua magari mengi kuliko Kenya basi soko letu ndiyo kubwa ???

Halafu kuichumi huwezi kulinganisha nguvu ya manunuzi (Purchasing Power) ya nchi mbili moja kwa moja. Inabidi uzingatie mambo kadhaa wa kadhaa, ndani ya nchi unazozifanyia uwiano. Wachumi wengi hutumia kipimo kiitwacho THE BIG MAC INDEX, kupima nguvu ya manunuzi baina ya nchi mbili (Purchasing Power Parity). Hili linafanyika kwasababu bei za vitu kwenye nchi mbalimbali zinatofautiana.

Bwana Armata wewe mwenzangu ulisomea wapi uchumi, mbona mambo unauliza mambo ambayo yanatutia wenzako ukakasi ? Tunarudi kulekule kama nilivyosema.

Marekani ana mengi ya kupoteza kuliko Urusi kwasababu yeye nchi yake ndiyo makao makuu ya soko la mtaji hapa duniani (The Epicenter of World's Capital Market). Uchumi wa Marekani unaendeshwa na udhibiti wa masoko ya hisa, riba, hati-fungani na uchapishwaji wa fedha. Urusi ana sehemu ndogo mno kwenye uchumi wa mitaji.

Riba zinapopandishwa juu bila mpangilio, wawekezaji wengi zikiwemo benki kuu za (Central Banks) duniani kote, na mashirika mengine hupoteza imani kwenye mfumo jambo ambalo linaweza kusababisha mtafaruku kwenye masoko (Market Volatility), kuanguka kwa mabenki, hata mitaji kuondoka nchini (Capital Flight) au hata mtikisiko wa uchumi wa dunia kama ilivyokuwa mwaka 2008.

Ewaah, swali langu liko hapa. Kwanini matajiri wa G7 hawajawekea vikwazo makampuni ya nishati ya nchi masikini kama Urusi, na kuamua kutumia fedha zao kupata nishati mbadala ???

Kama uchumi wa Urusi unaendeshwa kupitia gesi na mafuta, kwanini uweke vikwazo kwingineko kwenye sekta ambazo hazina madhara makubwa, lakini uache kuweka vikwazo kwenye sekta ambazo zinaipa Urusi nguvu ya kuendesha vita yake ya kivamizi na uchumi wake, ???

Aidha unachanganya watu makusudi, unakwepa swali au hufahamu kitu. Binafsi nimeuliza kuhusu soko la hati-fungani (Bond Market) na siyo soko la hisa (Stock Market). Wewe umejibu kana kwamba hivi vitu viwili ni kitu kimoja, jambo ambalo limenishangaza sana.

Ungefahamu utofauti uliopo baina ya haya masoko mawili, na jinsi yanavyofanya kazi kwenye uchumi wa dunia sidhani kama ungetoa hata mfano wa Urusi. Nimekuuliza kwanini soko la hati-fungani, ambao ndiyo uwekezaji unaoaminika zaidi kule Ulaya limeanguka ???

Hujanijibu kitaalamu, umezunguka mbuyu na kuleta siasa.


Mkuu, unafahamu nini maana ya Quantitative Easing (QE), ???

Mkuu, unazidi kuchanganya mambo. Binafsi sijazungumzia fedha ya Marekani kutumika kama EXCHANGE peke yake. Hayo umeyasema wewe. Binafsi nimeuliza kuhusu asilimia 55%-59% ya matumizi ya fedha ya Marekani as COMMODITY, STOREHOLDE OF WEALTH and A BEBT-INSTRUMENT not only as a MEANS OF EXCHANGE.

Ikumbukwe kiuchumi, mbali na kabla ya kufanya manunuzi dola ya Marekani ni bidhaa kama bidhaa nyingine ambazo Marekani inauza kwa nchi mbalimbali. Hivyo nilivyozungumzia asilimia 55% nilizungumzia hili.

Nadhani hili tuliache, kwasababu ulilijibu bila kulielewa vizuri.

NB: Binafsi naendelea kusubiri majawabu yako nijifunze zaidi mkuu....
Hivi mkuu maswali yangu huyaoni? Au unaona sistahili kujibiwa. Maana naona unakazana kuuliza ila kujibu hutaki.
Kabla sijajibu maswali yako ya ziada kwanza jibu maswali yangu kisha tuendelee. Au kama huyaoni, nijulishe nitayapanga kwa namba kama unavyofanya
 
Mkuu data zipi zinaonyesha Russia kapoteza vifaa vingi na wanajeshi wengi kuliko Ukrein?.

Mkuu The Boy Wonder suali lake lamsingi ni je wakiinforce hivyo vikawazo bila huruma Kwa Moscow wao uchumi wao utabaki salama?.
cc Max II Jr kp kipanya44
Ukraine war, already with up to 354,000 casualties, likely to last past 2023 - U.S. documents

Data za Reuters na Al Jazeera zinathibitisha Hilo kwamba Russi imepoteza sio tu askari wengi zaidi Bali pia Tanks na drones zilizodunguliwa. If that wasn't the case wangeshateka kyiv zamani Sana.

2. Mkuu kwenye vita whether ushinde au ushindwe madhara ya kiuchumi hayaeupikiki. Tanzania hapa tulimpiga Idd Amina ila tulipoteza nguvu ya kiuchumi. So uchumi utayumba kwa kiasi chake kwa multiplier effects ila madhara ya kijeshi in case of Nuclear holocaust yanazidi faida za kuimaliza Russia!!
 
Mada ya uchumi na propaganda za kivita wapi na wapi.

Watu wengine bana yaani mtu na akili zako timamu Russia imepoteza kuliko Ukraine.

Wacha wajuvi watufundishe kuhusu uchumi, haya ya sijui kashindwa tutakuja kuyajua mwisho wa vita.
Ukraine war, already with up to 354,000 casualties, likely to last past 2023 - U.S. documents

Reuters and Al Jazeera have reported that

Kingine kama Russia hajapoteza askari wengi si angeshakua ameshinda vita?

Kama issue ni uchumi tumeshaeleza huko juu kwamba Russia Ina sustain vita sababu nchi zinakiuka masharti ya vikwazo ila kama zingeheshimu vikwazo Russia Hana ubavu wa kusurvive hata miezi 6 maana ana GDP mdogo mnoo
 
nchi gani ikipigwa vikwazo ita-survive?
US?
China?
EU?

kifupi, vikwazo alivyopigwa Russia ingepigwa EU leo tusingekua na eu,
Issue sio vikwazo issue ni ku enforce vikwazo Sasa Russia kawekewa vikwazo ila Bado anafanya Yale Yale aliyowekewa zuio. Ila mfano Venezuela ikiwekewa vikwazo unakuta nchi zinaufyata kufanya biashara naye ndio maana inaathirika.

Sanctions without enforcement are futile and obsolete.

So swali lako lingekuwa " nchi Gani ikiwekewa vikwazo na ikalazimishwa kutii ita survive"

EU inaweza survive
China inaweza survive
But Russia cannot survive if isolated completely due to weak economy
 
Russia kashindwa vita kabisa, hivi kuiteka Kiev imemshinda ndio sembuse apambane na USA? Russia kapoteza wanajeshi wengi na vifaa vingi kuliko Ukraine Sasa kivipi mnadai hajashindwa vita?

Russia is weak kilichombakiza ni huruma tu ya US kuepusha Shari kuwa kúbwa ila wakiamua ku enforce vikwazo Moscow haiwezi survive masaa 24
Hata NATO ikaamua kumpa full support ya zana za kijeshi Russia, sidhani kama itachukua wiki Russia kutapika maeneo aliyoteka.

NATO imeona mbali uwezekano wa matumizi ya Nuclear ktk hii vita, hii wanafanya waende step kwa step hapo Ukraine.

Tukumbuke walipotenga bajeti ya miaka mitano kuisaidia Ukraine, watu waliwaona NATO kama wehu, waliona ukubwa wa Jeshi la Russia dhidi ya Ukraine basi vita isingechukua hata miezi mitatu.
 
Matatizo ya kiuchumi yameikumba Dunia tokea COVID 19 na recession zilizofuata. So obvious whether Ukraine na Russia zingepigana or not Bado matatizo ya uchumi yangekuwepo G7.

Kingine Russia ana survive madhara ya kiuchumi sababu amekiuka vikwazo mfano Bado anauzia mataifa mengine mafuta, gesi na chuma n.k. Kuna nchi kama China Bado inafanya trade ya wazi na Russia so hiko ndio kina sustain ila kama angesusiwa na mataifa yote sidhani angeweza sustain hata mwezi tu.

Lakini it's worth noting nchi za ulaya zimepunguza dependence na gesi ya Urusi so obviously Mapato yanaanza shuka taratibu so vita ikiendelea miaka 5 mingine watafikia break-point. Huwezi sustain uchumi wakati nchi Yako ni closed economy so Kuna limits atafika mind you vita ya Ukraine pia inammaliza pesa na watu na nguvu za kidiplomasia.

Only time will determine the fate of Russia
Na endapo Russia kungekuwa na uhuru wa vyombo vya habari, tungesikia mengi juu ya uchumi wa Russia.
 
Anayeisaidia Russia kupata nfuu za kiuchumi ni Uchina tu,pamoja na vikwazo ulivyosema China imeendelea kuwa karibu na Russia kibiashara na kiuchumi I'll kuipa nafuu za vikwazo.
India pia inanunua mafuta mengi sana toka Russia.
 
Hivi mkuu maswali yangu huyaoni? Au unaona sistahili kujibiwa. Maana naona unakazana kuuliza ila kujibu hutaki.
Kabla sijajibu maswali yako ya ziada kwanza jibu maswali yangu kisha tuendelee. Au kama huyaoni, nijulishe nitayapanga kwa namba kama unavyofanya
Ungeanza kunijibu maswali yangu mwanzo kabisa na kitaalamu kama anavyofanya bwana zitto junior ningetoa majawabu ya kila swali ulilouliza. Ila bahati mbaya hujafanya hivyo zaidi ya kuzunguka mbuyu na kuchanganya mambo. Nadhani mimi na wewe tuishie hapa, niendelea kufanya mjadala na Zitto Jr ambaye ni mchumi aliyesomea.
 
Anayeisaidia Russia kupata nfuu za kiuchumi ni Uchina tu,pamoja na vikwazo ulivyosema China imeendelea kuwa karibu na Russia kibiashara na kiuchumi I'll kuipa nafuu za vikwazo.
India pia inanunua mafuta mengi sana toka Russia.
Mbona Ulaya na Marekani wananunua bado rasilimali muhimu kutoka Urusi na kuendelea kuwekeza nchini humo, kama ambavyo Uchina na India wanafanya. AU haya ninyi wataalamu wetu hamyaoni jamani, ???

Takwimu za UN zinasema kwamba, Urusi na Ukraine kwa pamoja ndiyo wauzaji wakubwa wa mazao ya chakula. Wanaendelea kusema kwamba asilimia 44% ya nafaka kutoka bahari nyeusi imeenda kwa wateja ambao ni mataifa makubwa ya Ulaya na Asia (High Income Countries).

Juzi Urusi katijoa kwenye The Black Sea Grain Deal, na angalia nini kimetokea. Takwimu za masoko ya dunia zinasema baada ya Urusi kujitoa tu kwenye huo makakati hapo majuzi, bei ya nafaka imepanda kwa asilimia 3% nzima ambayo ni sawa na senti 689.25 kwa kibaba kimoja (689.25 Per Bushel). Hii inamaanisha bei ya chakula itapanda sana na kuchochea mfumuko wa bei (Food Price Inflation) kule Ulaya na sehemu nyingine duniani.

Hapa hata upandishe riba juu (Hiking Interest Rates) kiasi gani ili kupambana na mfumuko wa bei, huwezi kufanikiwa. Njia rahisi ya kudhibiti mfumuko wa bei itakuwa ni kutafuta rasilimali, na siyo zenye uhaba na kuziingiza kwenye soko. Fedha zitapoteza thamani na nguvu ya manunuzi itaisha.

Hili nimemwambia ndugu yangu zitto junior , ila yeye anaamini kwamba huu utajiri wa vitu visivyoonekana (Imaginary/ Incorporeal wealth) ndiyo njia sahihi ya kupata taswira halisi ya uchumi wa nchi. Binafsi hili linanipa ukakasi, kwasababu tokea karne za 17 tulitumia vyote, (Utajiri unaoonekana na Utajiri usioonekana) kupima taswira ya utajiri na uchumi wa nchi.

Sasa narudia maswali yangu, tena;

Mosi, imekuwaje taifa ambalo ni asilimia 4% ya Uchumi wa dunia isababishe mfumuko mkubwa wa bei ya chakula kwenye soko la dunia hadi kuathiri nchi tajiri za G7 ambazo zinamiliki asilimia 37.7% ya uchumi wa dunia, ???

Pili, Je dunia na wachumi walikuwa sahihi kuacha kuangalia utajiri wa nchi kwa kurunzi ya Finance Economy peke yake bila kuzingatia Commodity Economy, ???
 
Mbona Ulaya na Marekani wananunua bado rasilimali muhimu kutoka Urusi na kuendelea kuwekeza nchini humo, kama ambavyo Uchina na India wanafanya. AU haya ninyi wataalamu wetu hamyaoni jamani, ???

Takwimu za UN zinasema kwamba, Urusi na Ukraine kwa pamoja ndiyo wauzaji wakubwa wa mazao ya chakula. Wanaendelea kusema kwamba asilimia 44% ya nafaka kutoka bahari nyeusi imeenda kwa wateja ambao ni mataifa makubwa ya Ulaya na Asia (High Income Countries).
Swali langu mimi ni rahisi tu ambalo mpaka sasa wengi hawajanijibu. Juzi Urusi katijoa kwenye The Black Sea Grain Deal, na angalia nini kimetokea. Takwimu za masoko ya dunia zinasema baada ya Urusi kujitoa tu kwenye huo makakati hapo majuzi, bei ya nafaka imepanda kwa asilimia 3% nzima ambayo ni sawa na senti 689.25 kwa kibaba kimoja (689.25 Per Bushel). Hii inamaanisha bei ya chakula itapanda sana na kuchochea mfumuko wa bei (Food Price Inflation) kule Ulaya na sehemu nyingine duniani.

Hapa hata upandishe riba juu (Hiking Interest Rates) kiasi gani ili kupambana na mfumuko wa bei, huwezi kufanikiwa. Njia rahisi ya kudhibiti mfumuko wa bei itakuwa ni kutafuta rasilimali, na siyo zenye uhaba na kuziingiza kwenye soko. Fedha zitapoteza thamani na nguvu ya manunuzi itaisha.

Hili nimemwambia ndugu yangu zitto junior , ila yeye anaamini kwamba huu utajiri wa vitu visivyoonekana (Imaginary/ Incorporeal wealth) ndiyo njia sahihi ya kupata taswira halisi ya uchumi wa nchi. Binafsi hili linanipa ukakasi, kwasababu tokea karne za 17 tulitumia vyote, (Utajiri unaoonekana na Utajiri usioonekana) kupima taswira ya utajiri na uchumi wa nchi.

Sasa narudia maswali yangu, tena;

Mosi, imekuwaje taifa ambalo ni asilimia 4% ya Uchumi wa dunia isababishe mfumuko mkubwa wa bei ya chakula kwenye soko la dunia hadi kuathiri nchi tajiri za G7 ambazo zinamiliki asilimia 37.7% ya uchumi wa dunia, ???

Pili, Je dunia na wachumi walikuwa sahihi kuacha kuangalia utajiri wa nchi kwa kurunzi ya Finance Economy peke yake bila kuzingatia Commodity Economy, ???
Itakua vp km maswal yako wakishindwa kuyajibu???
 
Hapa wengi naona tunashindwa kukubaliana kwamba wewe mwenye milioni(pesa) ndani ili uile(uitumie) lazima awepo mwenye mahindi ndani. So ni lazima kwanza yawepo mahindi ndo mwenye pesa anaweza kuishi na ndo kinachotokea kwa West vs Russia
 
Issue sio vikwazo issue ni ku enforce vikwazo Sasa Russia kawekewa vikwazo ila Bado anafanya Yale Yale aliyowekewa zuio. Ila mfano Venezuela ikiwekewa vikwazo unakuta nchi zinaufyata kufanya biashara naye ndio maana inaathirika.

Sanctions without enforcement are futile and obsolete.

So swali lako lingekuwa " nchi Gani ikiwekewa vikwazo na ikalazimishwa kutii ita survive"

EU inaweza survive
China inaweza survive
But Russia cannot survive if isolated completely due to weak economy
naona unaongea usichokijua, acha nikuache nitamaliza nguvu zangu!
 
Hapa wengi naona tunashindwa kukubaliana kwamba wewe mwenye milioni(pesa) ndani ili uile(uitumie) lazima awepo mwenye mahindi ndani. So ni lazima kwanza yawepo mahindi ndo mwenye pesa anaweza kuishi na ndo kinachotokea kwa West vs Russia
kwa lugha rahisi hapo, tajiri ni mwenye mahindi (maana akipandisha bei au akigoma kuuza wewe mwenye milioni utahangaika sana kupata mbadala, au pengine ukipata itakua bei juu mno,

ndipo ile nadharia kwamba ulaya magharibi ni maskini (pengine kuliko afrika) inapoingia,..... leo tukisema kila mtu aishi kwa kutegemea alichonacho, basi wale wenzetu wanaweza kufa sana,

na hii ndiyo inayombeba Urusi, ana bidhaa ambazo ulaya wanazihitaji ili waendelee kuishi na uchumi wao usitetereke pakubwa,......
 
Mosi, imekuwaje taifa ambalo ni asilimia 4% ya Uchumi wa dunia isababishe mfumuko mkubwa wa bei ya chakula kwenye soko la dunia hadi kuathiri nchi tajiri za G7 ambazo zinamiliki asilimia 37.7% ya uchumi wa dunia, ???
Narudia Tena mkuu, uchumi sio zero sum game ndio maana ukipunguza ajira uchumi haukui ila pia ukiongeza ajira ghafla uchumi unaporomoka. Uchumi is all about kung'ata na kupuliza ndio maana broad money supply (Demand deposits+ Forex + Currency in circulation) huwa inapdandishwa na baada ya muda Fulani inapunguzwa (kwa kuuza au kununua hati fungani) ila ukisema uongeze Hela tu uchumi unakufa ila pia ukipunguza pesa kwa mzunguko uchumi unakufa.

Having said that unakosea pale ambapo unaonyesha kwamba uwepo wa vita ya Ukraine na Russia ndio hiyo inayopelekea inflation kupanda USA Au EU? Ulifanya hivyo lazima uweke control variables (We ni msomi unanielewa hapa) mfano macroeconomic variables kama floating interest rates (Moving average), unemployment rate, COVID 19 repurcussions, kuanguka kwa benki za USA, housing crisis, scarcity ya dollar kwenye soko la kimataifa, Sasa ukifanya test yoyote iwe Panel data au hata Pooled OLS lazima tu utaona jinsi Gani hizo factor zingine zinachangia zaidi uchumi wa EU au US uanguke na sio necessarily Kwa Russia kuzuia mauzo ya grains or whatever resources wanauza kwa EU au USA.

TLDR: You can't conclusively say factor Moja ya Russo-Ukranian War ndio directly inasababisha matatizo ya kiuchumi huko western Bloc bila controlling for other macroeconomic variables ambazo zilishaleta athari za kiuchumi since 2020.

Correlation is not causation
 
Back
Top Bottom