Taarifa hizi za Mradi wa JNHPP zimefichwa kumlinda nani?

Taarifa hizi za Mradi wa JNHPP zimefichwa kumlinda nani?

Jibu tulivu sana hili ulilompa jamaa.

Tusitafute visababu hata mahala pasipostahili kuwepo visababu.

Kuna mambo makubwa zaidi na yaliyowazi wanayovuruga hawa viongozi, hakuna upungufu kabisa wa mambo ya kuwalaumu juu ya utendaji wao mbovu.
Shikia shoka hayo.
Kama hayo maelezo ni sahihi kwanini kila walipotakiwa na Spika kuyatoa bungeni wameshindwa
 
Sio kila ucheleweshwaji wa kukamilishwa kwa mradi unabidi mkandarasi alipe. Katika mikataba kuna vitu ambavyo vinaweza kuruhusu makubaliano ya mradi kuchelewa, ambavyo vinakuwa chini ya kitu kinaitwa Force Majeure. Hivi ni pamoja na vitu kama tetemeko la ardhi, mafuriko nk, ambavyo katika lugha ya sheria vinaitwa acts of god. Sasa hapa kumetajwa Covid kuchelewesha logistics za mradi, na within reason, ni kweli Covid iliathiri logistics za miradi mingi.

Kwa hiyo hata kwenye Nyerere HEP mradi kucheleweshwa kwa mwaka mzima kwa mazingira ya Covid ni suala linaloeleweka.

Mkandarasi analipishwa pale ambapo kunakuwa hakuna sababu za msingi za kucheweshwa tarehe ya kumaliza mradi, yaani contract inakuwa frustrated zaidi kwa negligence tu ya mkandarasi
Uchambuzi mzuri kabisa, anajitoa ufaham kwa mtikisiko wa dunia ulioikumba dunina 2020-2021
 
Kuna watu wajinga wajinga wanafikiri kujenga ni kama kuchomoa shati kutoka kwenye shelf ya duka.
Wanakera sanan.
Hapana. Hili si jibu sahihi hata kidogo.
Usifanye kazi ya ujenzi iwe ni jambo la kutisha kuliko lilivyo.
Mkuu, hata ile 'rocket science' iliyokuwa inatisha enzi zile, si kitu tena enzi hizi, itakuwa kazi ya ujenzi?

Kuna jambo hawa viongozi wanaoshindwa kulizungumzia waziwazi watu wajue. Hapo ndipo panapoanzia utata.

Wanachosema wao viongozi ni kwamba hadi sasa asili mia 78.8 ya mradi imekamilika, (katika muda wa miaka mingapi). Kuna kazi iliyobaki, ambayo ni asilimia 21.2, ambayo muda wa kukamilika kwake ni shida kuujua kwa nini?
Ujenzi wowote unakuwa umeshafanyiwa upembuzi yakinifu unaoonyesha kila hatua na kila kitu wewe unaongea kienyeji yaani tuache kuzungumzia mkataba tuzungumze mambo ambayo hatuyajui
Naona umeni'quote pale, sijui umeandika nini ngoja nikakusome.
Lakini hapa ninaungana na kuhoji kwako; na bado ninakubaliana na jibu alilotoa mkuu 'synthesiser' hapo juu.
 
Kama hayo maelezo ni sahihi kwanini kila walipotakiwa na Spika kuyatoa bungeni wameshindwa
Hili ndilo swali la msingi kabisa kuulizwa.
Kuna sababu na inaelekea ni sababu za kipumbavu wasizotaka watu wazijue, bila shaka ni kutafuta kupeana ulaji.

Kuna watu na vimiradi vyao pembeni vya gesi, jua, upepo. Wanataka hivi vipitishwe kabla ya mradi huo mkubwa haujakamilika, kwa sababu wataogopa maswali yatakayoulizwa.
 
Rais Samia na Waziri wa Umeme na MD wa TANESCO Maharage taarifa zao zote hazijaonyesha mradi utakamilika lini na utaanza lini uzalishaji hiyo ya Juni 2024 umeitoa kwenye kinywa cha nani kati ya hao viongozi watatu.
Kuwa mvumilivu basi usubiri hiyo June 2024.
Kama una kiwanda cha kutumia umeme mwingi anza kukijenga sasa.
 
Covid 19 ndiyo tatizo kubwa lililosababisha mradi kutokamilika Juni 2022. Na akaomba nyongeza ya mwaka mmoja zaidi hadi Juni 2023. Mpk hapa mm nakubaliana na mkandarasi.

Kitu ambacho kinanitia kinyaa ni huo mwaka mwingine wa ziada yaani kwamba mradi Sasa utakamilika Juni 2024. Why? Kwanini? Pourquoi?
Tuelewe kitu kimoja, kukamilika mradi siyo an end in itself.
Kuna transmission ya hiyo power kutoka Stiglaz hadi Chalinze.
 
Tuelewe kitu kimoja, kukamilika mradi siyo an end in itself.
Kuna transmission ya hiyo power kutoka Stiglaz hadi Chalinze.
Hii transmission line toka bwawani hadi Chalinze ukimsikiliza naibu waziri utakamilika mapema zaidi. Shida ipo kwenye unenzi na ukamilishaji wa bwawa lenyewe.
 
Uliongelea mkataba najua wewe mwanasuasa.
Jitahidi ufike site ujionee complexity.
Mradi huu ni Watanzania wote sio wa familia ya WAZURI HAWAFI... Maswali ya msingi yaliyopo hayaondoi kazi nzuri iliyofikiwa juzi...... Maswali ni machache sana 1. Mradi unakamilika lini?, 2. Madai ya Fedha Trilioni 1.3 kama faini ya ucheleweshaji wa mradi amelipwa nani? 3. CSR ya shilingi bilioni 240 iliyotakiwa kutolewa na Mkandarasi amepewa nani..... Maswali hayo ndio watanzania wanahitaji majibu.... Kazi nzuri ya kujaza maji imeanza vizuri na Bwawa litajaa mapema.
 
Tuelewe kitu kimoja, kukamilika mradi siyo an end in itself.
Kuna transmission ya hiyo power kutoka Stiglaz hadi Chalinze.
Hizo ngonjera wanawachezea nyie wanajua hamfuatilii mambo ya nchi....wamesahau kama hizo njia za kusafirisha umeme ni component iliyopo kwenye mradi tangu day 1 ya mkataba. TAFUTA HOTUBA YA WAZIRI WA NISHATI BAJETI YA MWAKA 2021............... Hii ni sehemu ya kipande cha hotuba hiyo.....

MIRADI YA KUZALISHA UMEME

Mradi wa Kuzalisha Umeme wa Julius Nyerere – MW 2,115

24. Mheshimiwa Spika,
Serikali imeendelea na utekelezaji wa mradi wa kimkakati na wa kielelezo wa kuzalisha umeme wa Julius Nyerere 19 Hydro Power Project (JNHPP) utakaozalisha MW 2,115 kwa kutumia maporomoko ya maji ya Mto Rufiji. Gharama za mradi huu ni Shilingi trilioni 6.55 zinazotolewa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa asilimia 100.

25. Mheshimiwa Spika,
katika mwaka 2020/21, kazi zilizofanyika ni pamoja na: kukamilisha uchimbaji na ujenzi wa handaki la kuchepusha maji ya Mto Rufiji (diversion tunnel), kuendelea na ujenzi wa bwawa (main dam and spillways), ujenzi wa njia kuu za kupitisha maji (tunnels), ujenzi wa kituo cha kuzalishia umeme (Power House) na ujenzi wa kituo cha kusafirisha umeme (Switch yard). Hadi kufikia mwezi Mei, 2021, jumla ya Shilingi trilioni 2.495 zimelipwa kwa mkandarasi sawa na asilimia 100 ya fedha iliyotakiwa kulipwa kulingana na hatua ya utekelezaji wa mradi iliyofikiwa.

26. Mheshimiwa Spika,
kwa ujumla utekelezaji wa mradi katika maeneo muhimu matano (critical path) hadi kufikia mwezi Mei, 2021 umefikia wastani wa asilimia 52. Hadi sasa jumla ya wafanyakazi 7,243 wameajiriwa. Kati ya wafanyakazi hao; 6,452 ni Watanzania sawa na asilimia 89.1 na kutoka nje ya nchi ni 791 sawa na asilimia 10.9.

27. Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha mwaka 2021/22, Serikali itaendelea na utekelezaji wa mradi ambapo kazi zitakazofanyika 20 ni pamoja na kuendelea na kukamilisha: ujenzi wa bwawa (main dam and spillways); ujenzi wa njia kuu za kupitisha maji (tunnels); ujenzi wa kituo cha kuzalishia umeme (Power House); na ujenzi wa kituo cha kusafirisha umeme (Switch yard). Jumla ya Shilingi trilioni 1.4 fedha za ndani zimetengwa katika mwaka 2021/22 kwa ajili ya kutekeleza kazi hizo. Ujenzi wa mradi huu ulianza mwezi Juni, 2019 na unatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2022.

28. Mheshimiwa Spika, kukamilika kwa mradi huu pamoja na miradi mingine kutafanya nchi yetu kuwa na jumla ya takriban MW 5,000 kufikia mwaka 2025. Katika kipindi hicho mahitaji yetu ya juu ya umeme yanatarajiwa kufikia MW 2,677 hivyo kuwa na ziada ya takriban MW 2,323 na kuweza kuuza umeme nje ya nchi na kuongeza mapato ya Shirika. Aidha, Serikali itaweza kutekeleza azma yake ya kupunguza bei za umeme kwa wananchi.
 
Taarifa muhimu kuhusu Mradi wa JNHPP zimeshindwa kuwekwa wazi licha ya kutambua kuwa Mradi huu ni wa watanzania na wala sio mali binafsi ya familia ya 'Watu wazuri hawafi"
Ni sababu zipi zilizosababisha watanzania washindwe kuambiwa Mradi utakamilika lini?
Ni sababu zipi zilisosababisha kutokuwekwa wazi uongo kuhusu Madai ya Trilioni 1.5 ambazo Mkandarasi alipaswa kuilipa Serikali kwa kukiuka mkataba na kuchelewesha mradi badala ya mradi kukamilika Juni 2022 hadi sasa mradi haijulikani utakamilika lini.
Spika wa Bunge, Tulia aliyeanzisha hoja hiyo ya mkanganyiko wa taarifa kuhusu kukamilika kwa mradi bungeni Novemba, 2022 amepewa nafasi ya kuongea ameshindwa kuuliza maswali hayo kwa lengo la kumfaidisha nani?
Mpaka sasa watanzania wote wako gizani hawajui mradi utakamilika lini na lini utaanza uzalishaji. Kwanini wanaomundalia Hotuba Mh Rais wameshindwa kuweka time frame ya mradi?
Kwanini Waziri mwenye dhamana ya nishati ameshindwa kuweka time frame ya mradi kukamilika.
Maswali haya yalipaswa kujibiwa siku ya jana
Nalo Hilo likangaliwe
 
Hizo ngonjera wanawachezea nyie wanajua hamfuatilii mambo ya nchi....wamesahau kama hizo njia za kusafirisha umeme ni component iliyopo kwenye mradi tangu day 1 ya mkataba. TAFUTA HOTUBA YA WAZIRI WA NISHATI BAJETI YA MWAKA 2021............... Hii ni sehemu ya kipande cha hotuba hiyo.....

MIRADI YA KUZALISHA UMEME

Mradi wa Kuzalisha Umeme wa Julius Nyerere – MW 2,115

24. Mheshimiwa Spika,
Serikali imeendelea na utekelezaji wa mradi wa kimkakati na wa kielelezo wa kuzalisha umeme wa Julius Nyerere 19 Hydro Power Project (JNHPP) utakaozalisha MW 2,115 kwa kutumia maporomoko ya maji ya Mto Rufiji. Gharama za mradi huu ni Shilingi trilioni 6.55 zinazotolewa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa asilimia 100.

25. Mheshimiwa Spika,
katika mwaka 2020/21, kazi zilizofanyika ni pamoja na: kukamilisha uchimbaji na ujenzi wa handaki la kuchepusha maji ya Mto Rufiji (diversion tunnel), kuendelea na ujenzi wa bwawa (main dam and spillways), ujenzi wa njia kuu za kupitisha maji (tunnels), ujenzi wa kituo cha kuzalishia umeme (Power House) na ujenzi wa kituo cha kusafirisha umeme (Switch yard). Hadi kufikia mwezi Mei, 2021, jumla ya Shilingi trilioni 2.495 zimelipwa kwa mkandarasi sawa na asilimia 100 ya fedha iliyotakiwa kulipwa kulingana na hatua ya utekelezaji wa mradi iliyofikiwa.

26. Mheshimiwa Spika,
kwa ujumla utekelezaji wa mradi katika maeneo muhimu matano (critical path) hadi kufikia mwezi Mei, 2021 umefikia wastani wa asilimia 52. Hadi sasa jumla ya wafanyakazi 7,243 wameajiriwa. Kati ya wafanyakazi hao; 6,452 ni Watanzania sawa na asilimia 89.1 na kutoka nje ya nchi ni 791 sawa na asilimia 10.9.

27. Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha mwaka 2021/22, Serikali itaendelea na utekelezaji wa mradi ambapo kazi zitakazofanyika 20 ni pamoja na kuendelea na kukamilisha: ujenzi wa bwawa (main dam and spillways); ujenzi wa njia kuu za kupitisha maji (tunnels); ujenzi wa kituo cha kuzalishia umeme (Power House); na ujenzi wa kituo cha kusafirisha umeme (Switch yard). Jumla ya Shilingi trilioni 1.4 fedha za ndani zimetengwa katika mwaka 2021/22 kwa ajili ya kutekeleza kazi hizo. Ujenzi wa mradi huu ulianza mwezi Juni, 2019 na unatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2022.

28. Mheshimiwa Spika, kukamilika kwa mradi huu pamoja na miradi mingine kutafanya nchi yetu kuwa na jumla ya takriban MW 5,000 kufikia mwaka 2025. Katika kipindi hicho mahitaji yetu ya juu ya umeme yanatarajiwa kufikia MW 2,677 hivyo kuwa na ziada ya takriban MW 2,323 na kuweza kuuza umeme nje ya nchi na kuongeza mapato ya Shirika. Aidha, Serikali itaweza kutekeleza azma yake ya kupunguza bei za umeme kwa wananchi.
Sasa ukivyo mweledi jibu swali.
Hiyo line imejengwa?
Stiglaz-Chalinze
 
Sasa ukivyo mweledi jibu swali.
Hiyo line imejengwa?
Stiglaz-Chalinze
ilikuwepo kwenye mpango wa mradi na bajeti ilishatengwa soma vizuri hiyo speech ya Waziri. Sio kitu kipya wao wamecheza na akili zenu wakidhani hamsomi taarifa zenu za Serikali kumbe mnazisoma
 
ilikuwepo kwenye mpango wa mradi na bajeti ilishatengwa soma vizuri hiyo speech ya Waziri. Sio kitu kipya wao wamecheza na akili zenu wakidhani hamsomi taarifa zenu za Serikali kumbe mnazisoma
Sijui watanzania mmelogwa na nini, hamjui kuwa hata SGR ipo toka 2017 na ilikuwa ikamilike ndani ya miaka mitatu.
Watu kodi hamlipi mnasubiri abracadabra!
 
Taarifa muhimu kuhusu Mradi wa JNHPP zimeshindwa kuwekwa wazi licha ya kutambua kuwa Mradi huu ni wa watanzania na wala sio mali binafsi ya familia ya 'Watu wazuri hawafi"
Ni sababu zipi zilizosababisha watanzania washindwe kuambiwa Mradi utakamilika lini?
Ni sababu zipi zilisosababisha kutokuwekwa wazi uongo kuhusu Madai ya Trilioni 1.5 ambazo Mkandarasi alipaswa kuilipa Serikali kwa kukiuka mkataba na kuchelewesha mradi badala ya mradi kukamilika Juni 2022 hadi sasa mradi haijulikani utakamilika lini.
Spika wa Bunge, Tulia aliyeanzisha hoja hiyo ya mkanganyiko wa taarifa kuhusu kukamilika kwa mradi bungeni Novemba, 2022 amepewa nafasi ya kuongea ameshindwa kuuliza maswali hayo kwa lengo la kumfaidisha nani?
Mpaka sasa watanzania wote wako gizani hawajui mradi utakamilika lini na lini utaanza uzalishaji. Kwanini wanaomundalia Hotuba Mh Rais wameshindwa kuweka time frame ya mradi?
Kwanini Waziri mwenye dhamana ya nishati ameshindwa kuweka time frame ya mradi kukamilika.
Maswali haya yalipaswa kujibiwa siku ya jana

ni sukuma gang tu hakuna lolote. mtu mmoja ukilala ukiamka ni taarifa za bwawa tuuuu.
si uandike na mengine basi?
January Makamba ndiyo waziri mengine ni siasa tu. kwamba kwa sababu alikataliwa na JPM basi hana jema siyo kweli hata kidogo
 
Hiyo time Frame umeisema wewe wahusika hawajaisema. au tuwekee ushahidi labda sikusikiliza vizuri
Habari leo hii wamesema
Screenshot_20221224-204303.jpg
 
Back
Top Bottom