Taarifa ya ufaulu wa wanafunzi wa kidato cha nne katika shule za kanisa katoliki Tanzania

Taarifa ya ufaulu wa wanafunzi wa kidato cha nne katika shule za kanisa katoliki Tanzania

Tumsifu Yesu Kristo. Taarifa hii inatolewa na Idara ya Elimu ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) kuhusu matokeo ya mtihani wa kidato cha nne wa mwaka 2024 kwa shule za Kanisa Katoliki.

Lengo la kutolewa kwa taarifa hii ni kutoa tathmini ya ufaulu wa shule hizo ili kubaini maendeleo ya kitaaluma, maeneo yanayohitaji maboresho, na mwelekeo wa jumla wa elimu katika taasisi hizo.

Kwa mujibu wa takwimu, jumla ya watahiniwa wote nchini Tanzania walikuwa 516,695. Kati yao, wanafunzi wa shule za Kanisa Katoliki walikuwa 19,182, sawa na asilimia 3.6 ya watahiniwa wote.

Kwa upande wa ufaulu, wanafunzi waliopata daraja la kwanza hadi la tatu walifikia 18,745, sawa na asilimia 97.72 ya watahiniwa wa shule za Kanisa. Wanafunzi waliopata daraja la nne walikuwa 128 (asilimia 2.23), huku waliopata daraja la sifuri wakiwa watu 9 tu, sawa na asilimia 0.04.

Ikilinganishwa na matokeo ya mwaka 2023, ufaulu wa shule za Kanisa umeendelea kuimarika. Mwaka huu, kiwango cha ufaulu kimeongezeka kwa asilimia 1.66, tofauti na ongezeko la asilimia 0.15 mwaka uliotangulia.

TAKWIMU ZA UFAULU KWA KILA DARAJA

Daraja la Kwanza
: Wanafunzi 12,308 (64.16%)

Daraja la Pili: Wanafunzi 4,991 (26.01%)

Daraja la Tatu: Wanafunzi 1,146 (7.53%)

Daraja la Nne: Wanafunzi 128 (2.23%)

Daraja la Sifuri: Wanafunzi 9 (0.04%)

TAKWIMU ZA UFAULU KWA SHULE
Katika shule za Kanisa, jumla ya shule 65 zilipata ufaulu wa A, shule 160 ufaulu wa B, shule 47 ufaulu wa C, huku shule 2 zikipata ufaulu wa D. Hakuna shule hata moja iliyopata ufaulu wa E.

SHULE KUMI ZILIZOONGOZA KWA UFAULU

1. St. Francis Girls, Mbeya

2. Cardosa Girls, Dar es Salaam

3. Tengeru Boys, Arusha

4. Precious Blood Girls, Arusha

5. Bethel Girls, Mafinga

6. Mawua Seminary, Moshi

7. Anuarite Girls, Moshi

8. St. Mary's Mazinde Juu, Tanga

9. Marian Boys, Morogoro

10. St. Aloysius Girls, Dar es Salaam

PONGEZI NA MAPENDEKEZO
Tunaipongeza jamii nzima ya shule za Kanisa, ikiwemo walimu, viongozi wa shule, wafanyakazi, na wanafunzi kwa kazi kubwa iliyofanikisha matokeo haya. Pia, shukrani kwa wazazi ambao wamewajibika katika malezi na elimu ya watoto wao.

Tunawashukuru maaskofu kwa kusimamia shule hizi, kuhakikisha zinazingatia maadili ya Kanisa, na kuimarisha huduma za kiroho kwa wanafunzi. Huduma hizo zimechangia mafanikio haya makubwa.

Hadi kufikia mwaka 2025, lengo ni kupunguza kabisa wanafunzi wanaopata daraja la sifuri na kuboresha zaidi kiwango cha ufaulu. Idara ya Elimu inahimiza waalimu na wakuu wa shule kuendelea kuweka juhudi kubwa zaidi ili kuhakikisha elimu inayotolewa inaleta mabadiliko chanya kwa jamii.

Tunaendelea kuwaombea baraka za Mungu katika kutekeleza jukumu la elimu na malezi ya wanafunzi wetu.


View: https://youtu.be/BDXmTW0SIZ8


Tumsifu Yesu Kristo. Taarifa hii inatolewa na Idara ya Elimu ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) kuhusu matokeo ya mtihani wa kidato cha nne wa mwaka 2024 kwa shule za Kanisa Katoliki.

Lengo la kutolewa kwa taarifa hii ni kutoa tathmini ya ufaulu wa shule hizo ili kubaini maendeleo ya kitaaluma, maeneo yanayohitaji maboresho, na mwelekeo wa jumla wa elimu katika taasisi hizo.

Kwa mujibu wa takwimu, jumla ya watahiniwa wote nchini Tanzania walikuwa 516,695. Kati yao, wanafunzi wa shule za Kanisa Katoliki walikuwa 19,182, sawa na asilimia 3.6 ya watahiniwa wote.

Kwa upande wa ufaulu, wanafunzi waliopata daraja la kwanza hadi la tatu walifikia 18,745, sawa na asilimia 97.72 ya watahiniwa wa shule za Kanisa. Wanafunzi waliopata daraja la nne walikuwa 128 (asilimia 2.23), huku waliopata daraja la sifuri wakiwa watu 9 tu, sawa na asilimia 0.04.

Ikilinganishwa na matokeo ya mwaka 2023, ufaulu wa shule za Kanisa umeendelea kuimarika. Mwaka huu, kiwango cha ufaulu kimeongezeka kwa asilimia 1.66, tofauti na ongezeko la asilimia 0.15 mwaka uliotangulia.

TAKWIMU ZA UFAULU KWA KILA DARAJA

Daraja la Kwanza
: Wanafunzi 12,308 (64.16%)

Daraja la Pili: Wanafunzi 4,991 (26.01%)

Daraja la Tatu: Wanafunzi 1,146 (7.53%)

Daraja la Nne: Wanafunzi 128 (2.23%)

Daraja la Sifuri: Wanafunzi 9 (0.04%)

TAKWIMU ZA UFAULU KWA SHULE
Katika shule za Kanisa, jumla ya shule 65 zilipata ufaulu wa A, shule 160 ufaulu wa B, shule 47 ufaulu wa C, huku shule 2 zikipata ufaulu wa D. Hakuna shule hata moja iliyopata ufaulu wa E.

SHULE KUMI ZILIZOONGOZA KWA UFAULU

1. St. Francis Girls, Mbeya

2. Cardosa Girls, Dar es Salaam

3. Tengeru Boys, Arusha

4. Precious Blood Girls, Arusha

5. Bethel Girls, Mafinga

6. Mawua Seminary, Moshi

7. Anuarite Girls, Moshi

8. St. Mary's Mazinde Juu, Tanga

9. Marian Boys, Morogoro

10. St. Aloysius Girls, Dar es Salaam

PONGEZI NA MAPENDEKEZO
Tunaipongeza jamii nzima ya shule za Kanisa, ikiwemo walimu, viongozi wa shule, wafanyakazi, na wanafunzi kwa kazi kubwa iliyofanikisha matokeo haya. Pia, shukrani kwa wazazi ambao wamewajibika katika malezi na elimu ya watoto wao.

Tunawashukuru maaskofu kwa kusimamia shule hizi, kuhakikisha zinazingatia maadili ya Kanisa, na kuimarisha huduma za kiroho kwa wanafunzi. Huduma hizo zimechangia mafanikio haya makubwa.

Hadi kufikia mwaka 2025, lengo ni kupunguza kabisa wanafunzi wanaopata daraja la sifuri na kuboresha zaidi kiwango cha ufaulu. Idara ya Elimu inahimiza waalimu na wakuu wa shule kuendelea kuweka juhudi kubwa zaidi ili kuhakikisha elimu inayotolewa inaleta mabadiliko chanya kwa jamii.

Tunaendelea kuwaombea baraka za Mungu katika kutekeleza jukumu la elimu na malezi ya wanafunzi wetu.


View: https://youtu.be/BDXmTW0SIZ8

Hizo shule ni biashara ya nani, waumini mnashirikishwa katika ujenzi. Shida ada zao wakatoliki wengi hawazimudu gharama za ada, kanisa lizingatie Hali za waumini wao. Ikiwezekana kuwe napunguzo Kwa waamini wakikatoliki
 
Hongera kanisa katoliki. Taasisi, serikali na wengine waige mfano huu

Waige nini sasa
hapo watoto wanachujwa sana; Shule zao zinataka wale ceam tu...
Sasa shule zote zikichuja, wale wa maksi za kawaida ambao ndio wengi watasoma wapi?
 
Ni wapi ulikabwa koo wakati wa ujenzi wa hizo shule? Nitajie na mfano hata wa shule moja tu uliyokabwa koo kwa michango wakati wa kujengwa kwake! Halafu unataka hizo shule zisitoze ada, halafu wale walimu mahiri watalipwa na nani mishahara mizuri ya kuwafanya wawe na ari ya kufundisha kwa bidii zaidi?

Kwenye dunia ya leo ya survival of the fittest, bado unawaza kupewa huduma za afya za bure kwenye hospitali za Kanisa! Na wale wahudumu nao watakuhudumia bure? Je, wewe hapo ulipo unafanya kazi bure pasipo na malipo?
Basi mkuu hizo shule zimejengwa kwa misaada ya watu wa Marekani.
 
Shule zimejengwa na waumini kwa kukabwa koo ya michango halafu ada inayowekwa waumini hawawezi kumudu kulipia watoto wao kwa shule waliyojenga wao wenyewe.

The same na hospitali, waumini wanachangishwa kujenga hospitali lakini wakiugua hawawezi kutibiwa bure kwenye hospitali walizojenga wenyewe. Huu ni wizi kama wizi mwingine kwa mgongo wa dini.

Dini ni utapeli kama utapeli mwingine Mungu hayupo.
Hospitali za umma zimejengwa kwa kodi za wananchi,SGR imejengwa kwa kodi za wananchi,ATCL ipo pale kwa fedha za walipakodi ambao ni sisi,vipi umewahipeleka hoja kama hiyo sehemu tajwa?
After all ada za shule za wakatoliki ni ndogo sana,ujilinganisha na akipatacho mtoto pale.Jenga hoja nyingine.
 
Hospitali za umma zimejengwa kwa kodi za wananchi,SGR imejengwa kwa kodi za wananchi,ATCL ipo pale kwa fedha za walipakodi ambao ni sisi,vipi umewahipeleka hoja kama hiyo sehemu tajwa?
After all ada za shule za wakatoliki ni ndogo sana,ujilinganisha na akipatacho mtoto pale.Jenga hoja nyingine.
Tofautisha vitu vya umma na vitu vya kikundi cha watu wenye malengo yao. Umma hauna quid pro quo. Dini ni sawa na kikundi kama saccos, ni muunganiko wa watu flani wenye malengo ama mtazamo ama imani flani inayofanana, hivyo chochote kinachofanywa na watu hao lazima kiwe kwa maslahi ha hao watu kwanza. Sasa inawezekanaje uchangishe hao watu ujenge miundombinu halafu hiyo miundombinu isiwafadishe hao wajenzi ama watoa fedha(investors) badala yake uweke vingezo vya vingumu ambavyo investors hawawezi kumudu kutumia hiyo miundombinu? Huo ni utapeli ama wizi, kujipatia pesa kwa njia ya udanganyifu.

Hao watoto wanapata nini ambacho watoto wengine hawapati kinachozidi thamani ya fedha zao walizolipa ada?

Hoja hapa sio watoto kupata faida kubwa, hao watoto ni wa wale original investors ama ni wa watu wengine?

Hii hoja sio rahisi wewe kuielewa ukija kwa mtazamo wa kidini. Dini hupumbaza sana, ni ulevi mkubwa kuliko cocaine.
 
Ni wapi ulikabwa koo wakati wa ujenzi wa hizo shule? Nitajie na mfano hata wa shule moja tu uliyokabwa koo kwa michango wakati wa kujengwa kwake! Halafu unataka hizo shule zisitoze ada, halafu wale walimu mahiri watalipwa na nani mishahara mizuri ya kuwafanya wawe na ari ya kufundisha kwa bidii zaidi?

Kwenye dunia ya leo ya survival of the fittest, bado unawaza kupewa huduma za afya za bure kwenye hospitali za Kanisa! Na wale wahudumu nao watakuhudumia bure? Je, wewe hapo ulipo unafanya kazi bure pasipo na malipo?
Hawajui hiyo survival for fittest, wako occupied na DELUSION za after life i.e Every muslim will be given a kingdom as their property and a palace as their house with angels as their servants🙁 , why suffer on planet earth😛
 
Kuna Marian Boys mbili, hii na ile ya Bagamoyo?
Ni hiyo hiyo. Msichofahamu wadau wengi ni kimoja tu! Bagamoyo kwenye mgawanyo wa Majimbo ya Katoliki, iko Jimbo la Morogoro! Na Katoliki hawana Jimbo la Pwani! Isipokuwa Jimbo kuu la Dar es salaam, Jimbo la Morogoro (na hiyo Bagamoyo ikiwemo), nk.
 
Waige nini sasa
hapo watoto wanachujwa sana; Shule zao zinataka wale ceam tu...
Sasa shule zote zikichuja, wale wa maksi za kawaida ambao ndio wengi watasoma wapi?
Wanatakiwa wakasomee elimu ya ufundi stadi, kucheza mpira, kuimba, nk.

Mbona jambo hili hata Mwanafalsafa mashuhuri kabisa wa Kigiriki (Plato) alishawahi kuwagawa hawa viumbe katika makundi matatu! (1. Golden Boys, 2. Silver Boys, 3. Iron Boys!!). Tena ni miaka hiyo ya BCE!!! Kwa hiyo hakuna namna nyingine Sheikh.
 
Semeni shule za kanisa Katoliki kwanini mnafichaficha, by the way lengo la ujumbe huu ni nini?
Taarifa kwa umma but pia lengo lingine, kanisa linajaribu kuwaonesha wateja wao kwamba hawakukosea kuchagua kupeleka watoto wao kwao. Ninacho wapendea Wakatoliki, wanaendesha mambo yao kitaasisi, kisomi kabisa. Yaani wana hadi idara ya elimu, na hi ndio imetoa taarifa yao kwa umma, kama serikali yaani. Hawa jamaa wamejipanga, kuanzia chekechea hadi chuo kikuu, daa
 
Nasemaje mi mwanasheria sinaaa.........lakini kwani hata raia namba moja naye si aliruka ruka tu mpaka kufika kwenye d.a.k.i.t.a.r.i.............miaa au nasema uwongo jamani
 
Semeni shule za kanisa Katoliki kwanini mnafichaficha, by the way lengo la ujumbe huu ni nini?
Ni taarifa tu kwa wadau wa eliminate,wazazi, walezi, wanafunzi wenyewe waliomaliza elimu hapo na hata ikawa ni tangazo la biashara kwa wanaotaka kujiunga na hizo shule.
 
Hospitali za umma zimejengwa kwa kodi za wananchi,SGR imejengwa kwa kodi za wananchi,ATCL ipo pale kwa fedha za walipakodi ambao ni sisi,vipi umewahipeleka hoja kama hiyo sehemu tajwa?
After all ada za shule za wakatoliki ni ndogo sana,ujilinganisha na akipatacho mtoto pale.Jenga hoja nyingine.

Hata hivyo mtoto kupata nafasi shule za Katoliki ni hadi awe na pass za juu sana, Kama mtoto anapass za kawaida asitegemee kupata nafasi huko. Hata sijui kwa nini wanajivunia kufaulisha wakati wamechukua wanafunzi magenius ambao wanauwezo wa kufaulu vizuri kwa msaada wa kawaida tu wa mwalimu....
 
Ni hiyo hiyo. Msichofahamu wadau wengi ni kimoja tu! Bagamoyo kwenye mgawanyo wa Majimbo ya Katoliki, iko Jimbo la Morogoro! Na Katoliki hawana Jimbo la Pwani! Isipokuwa Jimbo kuu la Dar es salaam, Jimbo la Morogoro (na hiyo Bagamoyo ikiwemo), nk.
Kuna jimbo la Mafinga?
 
Punguzeni ada maana hizo shule zimejengwa Kwa sadaka za waumini cha ajabu wao wanashindwa kuwasomesha watoto wao hizo shule
 
Semeni shule za kanisa Katoliki kwanini mnafichaficha, by the way lengo la ujumbe huu ni nini?
Lengo ni kuonyesha kuwa ''usione vinaelea, vimeundwa''. Kuna watu huwa wanapiga kelele sana kuwa nchi inaongozwa na mfumo kristo kwa sababu kila sehemu unakuta wakristo bila kujua kuwa taasisi zao zinafanya kazi nzuri ya kusomesha wanafunzi wake.
 
Back
Top Bottom