Kwamba kila mkoa kuwe na Generation source ya umeme? Hilo linawezekana?Still zitabaki kuwa ni kubwa sana kwa uwezo wetu wa management.
Zikatwe kimikoa na huko kila idara kubwa zijitegemee.
Transmission iwe kila mkoa kivyake, distribution, kila mkoa kivyake, production kila mkoa kivyake, mikoa inayozalisha zaidi ya matumizi yake itawauzia mikoa ambayo uzalishaji wake ni mdogo.
National grid iwe na management yake kivyake
Hongera kwa uchambuzi mzuri!Umuofia kwenu....!
Kati ya mwaka 2018 na 2020 Tanzania ilipitia changamoto za uhaba mkubwa wa Cement na bei kuanza kupanda kiholela. Lakini baada ya kulifuatilia suala lile, nikaja kugundua kwamba, kuadimika na kupanda kiholela kulisababishwa Zaidi na utekelezaji wa miradi mikubwa ya ujenzi kipindi cha utawala wa Magufuli. Kwahiyo upungufu ulijitokeza kwa sababu ‘internal capacity’ ya kutengeneza cement ilikuwa ni ndogo na isingeweza kumudu ongezeko kubwa la demand ambayo ilitokana na mahitaji ya cement kwenye miradi mikubwa ya serikali. Kwa maana hiyo, Cement nyingi ikawa inauzwa kwa makampuni ya ujenzi na kidogo sana ikawa inaenda mtaani kwa wananchi, na ndio haswa ikaleta lile janga la cement kipindi kile cha Magufuli Serikali haiwezi kukwepa lawama ya kuadimika na kupanda kwa bei ya Saruji nchini. Waziri wa Viwanda ana kazi sana, kuna janga linatunyemelea
Baada ya kutafiti matukio yaliyotokea kwenye cement, nikaja kugundua ya kwamba, uchumi wa Tanzania unakosa kitu kwenye uchumi tunakiita ‘space capacity’. Yaani kwa tafsiri ya yake ni kwamba ‘space capacity’ ni ule uwezo au utayari wa sekta za kiuchumi kama viwanda, kuweza na kuendana na kasi ya mabadiliko ya haraka ambayo yanatokea kwenye uchumi bila kuwa na mtanziko kwenye soko mfano uhaba wa bidhaa au huduma.
View attachment 2758917
Ukiangalia kwa sasa, kwenye sekta ya cement, pamoja na ongezeko la haraka la uchumi kwa miaka miwili iliyopita, hali imekuwa ni ya usatahimilivu, na naweza kuvipa hongera viwanda vya cement na waagizaji wa cement kwa kuhakikisha hakuna mtanziko kwenye upatikanaji wa cement kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma.
Kwa upande mwingine imekuwa rahisi sana kwa sekta ya cement kustabilize kwasababu sekta yenyewe ni huria, kwa maana ya kwamba kuna players wengi kwenye sekta. Mtu kama Dangote ana capacity kubwa sana ya kuzalisha, na inawezekana kwa sasa Tanzania, space capacity kwenye cement industry ipo kubwa nay a kutosha, ndo maana husikii kelele za kuadimika kwa Cement. Hiyo ndio faida ya soko huria kwenye uchumi ambayo naona ndio inakosekana kwenye umeme.
Umeme
Kinachotokea kwenye umeme hakitofautiana sana na kilichotokea kwenye cement kipindi cha Magufuli kwenye miaka ya 2018 mpaka 2020. Na inatupeleka kule kule kwenye hoja ya kupishana speed kati ya mahitaji (demand) na uzalishaji (supply) kwenye uchumi.
Mwezi mmoja uliopita nilikuja na huu uzi Miezi 30 ya Rais Samia madarakani: Pamoja na kujikwaa kwenye Bandari, bado ni Rais mwenye record bora ya kukuza uchumi wa Tanzania kwa kipindi kifupi ambao nilijaribu kuchambua na kuonesha hali ya ukuaji wa uchumi kwa miaka hii miwili ya Rais Samia ambao mimi mpaka sasa, bado nashikilia msimamo kwamba kumekuwa na ongezeko maradufu kwenye shughuli za kiuchumi nchini, na hiyo inaweza uwa bayana kwa kuangalia baadhi ya viashiria vingi tu ambavyo nilivielezea kwa upana. Hata hichi cha ukuaji wa uzalishaji wa cement kikiwa pia kimojawapo.
Kwanza kabisa, kwa manufaa ya wengi, pamoja na nchi kuwa kwenye mgao mkali ambao binafsi sijawahi kuushuhudia, ukirejelea takwimu za hivi karibuni kwenye ‘supply ya umeme Tanzania’, utagundua ya kwamba, kati ya June 2021 mpaka June 2023, wastani wa supply ya umeme Tanzania kwa mwezi iliongezeka kwa asilimia 39.5% - kutoka kWh 617 millioni kwa mwezi June 2021 mpaka kWh 861 millioni kwa mwezi June 2023.
View attachment 2758919
Hivo, ni wazi kabisa kwamba tatizo la umeme linalojitokeza sasahivi lipo ‘driven’ Zaidi na demand side pressure, yaani, ongezeko la mahitaji limekuwa kubwa maradufu kushinda ongezeko la TANESCO ku supply umeme ili ku meet demand. Kwamba ni kweli TANESCO wanajitahidi, lakini mbio zao ni speed ya Km 60 kwa saa wakati mahitaji yanakimbia kwa speed ya Km 80 kwa saa, lazima TANESCO atashindwa vita. Na huu ni mwanzo tu wa mbio.
Utatuzi pekee hapa na wa maana ni endapo ‘space capacity’ itaweza kupatikana. Lakini ukifuatilia maneno ya serikali, ni kwamba bado wanaishi kwenye ulimwengu wa ahadi na matumaini kwamba ‘Bwawa la Nyerere likikamilika basi shida hii itatatuliwa’, au utasikia ‘Mvua zikinyesha shida hii ya umeme itatatuliwa’.
Miaka 10 iliyopita, Prof Sospeter Muhungo, alikuwa anasema maneno hayo hayo, kwamba sijui Tanzania itaanza kuuza umeme nje ya nchi. Kwahiyo, inakupa picha kwamba, serikali yenyewe kwa miaka kumi iliyopita na hata sasa bado hawana plan ya kuwa na ‘space capacity’ kwenye umeme wa uhakika, zaidi maneno matupu na mbambamba.
Lakini wanasiasa wa Tanzania wanazidi kutoa ahadi nyingi za kuboresha upatikanaji wa umeme na kusahau kwamba TANESCO yenyewe kama kampuni haipo tena kiushindani, na ni shirika ambalo tunaliita ni ‘deadhorse’ ama Farasi aliyekufa. Na itakuwa ni kuendelea kujidanganya kuwa na ndoto za kuinua uchumi wa hii nchi kwa kuendelea kuamini utendaji wa shirika dhaifu kama hili.
TSh. Million Jun-19 Jun-20 Jun-21Revenue 1,535,040 1,564,353 1,658,235Profit before Tax 45,094 43,891 54,845Current Assets 434,962 1,465,420 1,918,525Current Liabilities 1,972,800 2,884,503 3,250,450Free cash flow (2,229,212) (335,011) (1,452,405)
View attachment 2758923
Ukiangalia baadhi ya hizo number hapo juu, unaona kabisa kwamba kwa hali ilivo, TANESCO haina muscles za ku kuhimili ongezeko kubwa la ukuaji wa mahitaji ya umeme, kwa sababu shirika linajiendesha bila ufanisi hata faida ni kama vile haipo.
Ukiangalia current liabilities za kampuni bado ni kubwa maradufu kuzidi current assets na hizo current liabilities zinaongezeka mwaka hadi mwaka. Maana yake ni kwamba uwezo wa TANESCO kulipa suppliers wake kwasasa ni mdogo kitu ambacho kinaturudisha kule kule kwamba, TANESCO haina tena uwezo kugharamia shughuli yake ya muhimu ya kugenerate umeme kadri inavyotaka ili kukidhi mahitaji ya soko kwasababu haioneshi uwezo wa kuwalipa wazabuni wake kwa wakati.
Kingine, ukuangalia, hapo kwenye hicho kinachoitwa free cash flow, kwa miaka mitatu imekuwa ipo negative kwa wastani wa Zaidi ya Trilioni moja kila mwaka. Hiyo inakuambia ya kwamba, TANESCO ni shirika ambalo halina tena uwezo wa kugenerate cash lenyewe kama lenyewe. Kwa kigezo hiki, japo sijui huko serikalini kunaendelea kitu gani, ni wazi serikali kwa hii miaka miwili iliyopita wameipatia TANESCO fedha nyingi sana ili ku support kampuni kujiendesha.
Performance hiyo ya TANESCO mimi ndo huwa kila siku najiuliza, inakuwaje serikali wanazidi kuona kwamba TANESCO wana uwezo wa kufanya mapinduzi kwenye sekta ya umeme? Maana kwa wenye uzoefu wa biashara, ukiwa na kampuni la dizaini hii, maana yake ni mgonjwa ambaye yupo mahutihuti. Halafu eti, mgonjwa huyo huyo unamuweka awe mlinzi wa nyumbani. Yaani hii nchi kuna watu wanastahili kabisa kupimwa akili.
Maana mimi binafsi naiona TANESCO kama kitisho kwenye uchumi kwa sasa. Suluhisho la kudumu ambalo halikwepeki, ni kuifumua TANESCO na kuisuka upya.
The best structure ninayoiona mimi na ambayo nimekuwa nikiifikiria, ni kuwepo kwa soko huria kwenye sekta nzima ya umeme. Hii TANESCO inatakiwa kumegwa na kutengeneza makampuni kama matatu.
Lakini kama watawala wanazidi kuona hakuna haja, kuna siku yaja hili shirika litaangusha huu uchumi na kuturudisha nyuma miaka 5.
Tumechoka hizi ahadi za uwongo kila siku mawaziri kuendelea kutudanganya kwamba Tanzania itauza umeme nje ya nchi bila kutuambia itawezaje.
TANESCO ni kitisho namba moja kwa uchumi na usalama wa nchi, ifumuliwe harakaaaaa.
Wasalaaaam
N.Mushi
Pamoja mkuuGood insight
Inatakiwa bunge na serikali waangalie hili suala kwa jicho la tatu lasivo, kuna dhahama huko mbele... serilali ije na plan madhubutiViongozi wa nchi hii hawana tofauti na wamama wanaochukua chakula cha watoto wao na kuwapa majirani. Wako tayari watoto wao wafe njaa lakini wao wasifiwe kwa ukarimu!
Unafikiri Tanzania htuna akili! Basi tu huwa tunajitoa ufahamu...Si unaona hadi Chawa Mwandamizi FOX anaunga Sera ya CHADEMA ya ku menage nchi Kikanda!Huu uzi unachangiwa vema sana. Hakuna uchawa wa aina yeyote ile. Naamini kama kweli watawala wanapenda hii nchi na raia wake watapata kitu hapa cha kukifanyia upembuzi kwa haraka.
Rais Samia, auone huu uzi naamini anaweza pata nguvu ya kufanya kitu.
Hongera kwa wote mnaoweka hoja jadidi za kuinusuru nchi na janga la kukosa umeme.
Nje ya mada ...hivi mkuu wewe Ndio Nantoomba Mushi ,unehariri jina au ni Ndugu yake!?Inatakiwa bunge na serikali waangalie hili suala kwa jicho la tatu lasivo, kuna dhahama huko mbele... serilali ije na plan madhubuti
Hii ndo solution ambayo na mimi naiangalia... kwa namna ilivo hii monopoly ya Tanwsco kusambaza umeme inatakiwa kufa. Tanesco anaweza kuwa regulator tu wa kuangalia utendaji kazi wa makampuni ambayo yatakuwa yanaifanya hiyo kazi. Lakini kwenye kusema kwamba Tanwsco waendelee kushikilia monopoly ya kugenerate na kusambaz umeme, hiyo kazi wameshindwa tayarThe only way kuiendesha Tanesco kifaida, kwa capacity ya uelewa wa usimamizi wa Tanzania, ni kuikata mapande sawa na mikoa na kila kipande kiwe huru na kijiendeshe kama pande la kujitgemea kikamilifu.
Pamoja mkuuAkili kubwa
Tuishi humu 🙌!! Hapa huwez waona chawa wa mama wala wazee wa payroll ya buku tano!!Umuofia kwenu....!
Kati ya mwaka 2018 na 2020 Tanzania ilipitia changamoto za uhaba mkubwa wa Cement na bei kuanza kupanda kiholela. Lakini baada ya kulifuatilia suala lile, nikaja kugundua kwamba, kuadimika na kupanda kiholela kulisababishwa Zaidi na utekelezaji wa miradi mikubwa ya ujenzi kipindi cha utawala wa Magufuli. Kwahiyo upungufu ulijitokeza kwa sababu ‘internal capacity’ ya kutengeneza cement ilikuwa ni ndogo na isingeweza kumudu ongezeko kubwa la demand ambayo ilitokana na mahitaji ya cement kwenye miradi mikubwa ya serikali. Kwa maana hiyo, Cement nyingi ikawa inauzwa kwa makampuni ya ujenzi na kidogo sana ikawa inaenda mtaani kwa wananchi, na ndio haswa ikaleta lile janga la cement kipindi kile cha Magufuli Serikali haiwezi kukwepa lawama ya kuadimika na kupanda kwa bei ya Saruji nchini. Waziri wa Viwanda ana kazi sana, kuna janga linatunyemelea
Baada ya kutafiti matukio yaliyotokea kwenye cement, nikaja kugundua ya kwamba, uchumi wa Tanzania unakosa kitu kwenye uchumi tunakiita ‘space capacity’. Yaani kwa tafsiri ya yake ni kwamba ‘space capacity’ ni ule uwezo au utayari wa sekta za kiuchumi kama viwanda, kuweza na kuendana na kasi ya mabadiliko ya haraka ambayo yanatokea kwenye uchumi bila kuwa na mtanziko kwenye soko mfano uhaba wa bidhaa au huduma.
View attachment 2758917
Ukiangalia kwa sasa, kwenye sekta ya cement, pamoja na ongezeko la haraka la uchumi kwa miaka miwili iliyopita, hali imekuwa ni ya usatahimilivu, na naweza kuvipa hongera viwanda vya cement na waagizaji wa cement kwa kuhakikisha hakuna mtanziko kwenye upatikanaji wa cement kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma.
Kwa upande mwingine imekuwa rahisi sana kwa sekta ya cement kustabilize kwasababu sekta yenyewe ni huria, kwa maana ya kwamba kuna players wengi kwenye sekta. Mtu kama Dangote ana capacity kubwa sana ya kuzalisha, na inawezekana kwa sasa Tanzania, space capacity kwenye cement industry ipo kubwa nay a kutosha, ndo maana husikii kelele za kuadimika kwa Cement. Hiyo ndio faida ya soko huria kwenye uchumi ambayo naona ndio inakosekana kwenye umeme.
Umeme
Kinachotokea kwenye umeme hakitofautiana sana na kilichotokea kwenye cement kipindi cha Magufuli kwenye miaka ya 2018 mpaka 2020. Na inatupeleka kule kule kwenye hoja ya kupishana speed kati ya mahitaji (demand) na uzalishaji (supply) kwenye uchumi.
Mwezi mmoja uliopita nilikuja na huu uzi Miezi 30 ya Rais Samia madarakani: Pamoja na kujikwaa kwenye Bandari, bado ni Rais mwenye record bora ya kukuza uchumi wa Tanzania kwa kipindi kifupi ambao nilijaribu kuchambua na kuonesha hali ya ukuaji wa uchumi kwa miaka hii miwili ya Rais Samia ambao mimi mpaka sasa, bado nashikilia msimamo kwamba kumekuwa na ongezeko maradufu kwenye shughuli za kiuchumi nchini, na hiyo inaweza uwa bayana kwa kuangalia baadhi ya viashiria vingi tu ambavyo nilivielezea kwa upana. Hata hichi cha ukuaji wa uzalishaji wa cement kikiwa pia kimojawapo.
Kwanza kabisa, kwa manufaa ya wengi, pamoja na nchi kuwa kwenye mgao mkali ambao binafsi sijawahi kuushuhudia, ukirejelea takwimu za hivi karibuni kwenye ‘supply ya umeme Tanzania’, utagundua ya kwamba, kati ya June 2021 mpaka June 2023, wastani wa supply ya umeme Tanzania kwa mwezi iliongezeka kwa asilimia 39.5% - kutoka kWh 617 millioni kwa mwezi June 2021 mpaka kWh 861 millioni kwa mwezi June 2023.
View attachment 2758919
Hivo, ni wazi kabisa kwamba tatizo la umeme linalojitokeza sasahivi lipo ‘driven’ Zaidi na demand side pressure, yaani, ongezeko la mahitaji limekuwa kubwa maradufu kushinda ongezeko la TANESCO ku supply umeme ili ku meet demand. Kwamba ni kweli TANESCO wanajitahidi, lakini mbio zao ni speed ya Km 60 kwa saa wakati mahitaji yanakimbia kwa speed ya Km 80 kwa saa, lazima TANESCO atashindwa vita. Na huu ni mwanzo tu wa mbio.
Utatuzi pekee hapa na wa maana ni endapo ‘space capacity’ itaweza kupatikana. Lakini ukifuatilia maneno ya serikali, ni kwamba bado wanaishi kwenye ulimwengu wa ahadi na matumaini kwamba ‘Bwawa la Nyerere likikamilika basi shida hii itatatuliwa’, au utasikia ‘Mvua zikinyesha shida hii ya umeme itatatuliwa’.
Miaka 10 iliyopita, Prof Sospeter Muhungo, alikuwa anasema maneno hayo hayo, kwamba sijui Tanzania itaanza kuuza umeme nje ya nchi. Kwahiyo, inakupa picha kwamba, serikali yenyewe kwa miaka kumi iliyopita na hata sasa bado hawana plan ya kuwa na ‘space capacity’ kwenye umeme wa uhakika, zaidi maneno matupu na mbambamba.
Lakini wanasiasa wa Tanzania wanazidi kutoa ahadi nyingi za kuboresha upatikanaji wa umeme na kusahau kwamba TANESCO yenyewe kama kampuni haipo tena kiushindani, na ni shirika ambalo tunaliita ni ‘deadhorse’ ama Farasi aliyekufa. Na itakuwa ni kuendelea kujidanganya kuwa na ndoto za kuinua uchumi wa hii nchi kwa kuendelea kuamini utendaji wa shirika dhaifu kama hili.
TSh. Million Jun-19 Jun-20 Jun-21Revenue 1,535,040 1,564,353 1,658,235Profit before Tax 45,094 43,891 54,845Current Assets 434,962 1,465,420 1,918,525Current Liabilities 1,972,800 2,884,503 3,250,450Free cash flow (2,229,212) (335,011) (1,452,405)
View attachment 2758923
Ukiangalia baadhi ya hizo number hapo juu, unaona kabisa kwamba kwa hali ilivo, TANESCO haina muscles za ku kuhimili ongezeko kubwa la ukuaji wa mahitaji ya umeme, kwa sababu shirika linajiendesha bila ufanisi hata faida ni kama vile haipo.
Ukiangalia current liabilities za kampuni bado ni kubwa maradufu kuzidi current assets na hizo current liabilities zinaongezeka mwaka hadi mwaka. Maana yake ni kwamba uwezo wa TANESCO kulipa suppliers wake kwasasa ni mdogo kitu ambacho kinaturudisha kule kule kwamba, TANESCO haina tena uwezo kugharamia shughuli yake ya muhimu ya kugenerate umeme kadri inavyotaka ili kukidhi mahitaji ya soko kwasababu haioneshi uwezo wa kuwalipa wazabuni wake kwa wakati.
Kingine, ukuangalia, hapo kwenye hicho kinachoitwa free cash flow, kwa miaka mitatu imekuwa ipo negative kwa wastani wa Zaidi ya Trilioni moja kila mwaka. Hiyo inakuambia ya kwamba, TANESCO ni shirika ambalo halina tena uwezo wa kugenerate cash lenyewe kama lenyewe. Kwa kigezo hiki, japo sijui huko serikalini kunaendelea kitu gani, ni wazi serikali kwa hii miaka miwili iliyopita wameipatia TANESCO fedha nyingi sana ili ku support kampuni kujiendesha.
Performance hiyo ya TANESCO mimi ndo huwa kila siku najiuliza, inakuwaje serikali wanazidi kuona kwamba TANESCO wana uwezo wa kufanya mapinduzi kwenye sekta ya umeme? Maana kwa wenye uzoefu wa biashara, ukiwa na kampuni la dizaini hii, maana yake ni mgonjwa ambaye yupo mahutihuti. Halafu eti, mgonjwa huyo huyo unamuweka awe mlinzi wa nyumbani. Yaani hii nchi kuna watu wanastahili kabisa kupimwa akili.
Maana mimi binafsi naiona TANESCO kama kitisho kwenye uchumi kwa sasa. Suluhisho la kudumu ambalo halikwepeki, ni kuifumua TANESCO na kuisuka upya.
The best structure ninayoiona mimi na ambayo nimekuwa nikiifikiria, ni kuwepo kwa soko huria kwenye sekta nzima ya umeme. Hii TANESCO inatakiwa kumegwa na kutengeneza makampuni kama matatu.
Lakini kama watawala wanazidi kuona hakuna haja, kuna siku yaja hili shirika litaangusha huu uchumi na kuturudisha nyuma miaka 5.
Tumechoka hizi ahadi za uwongo kila siku mawaziri kuendelea kutudanganya kwamba Tanzania itauza umeme nje ya nchi bila kutuambia itawezaje.
TANESCO ni kitisho namba moja kwa uchumi na usalama wa nchi, ifumuliwe harakaaaaa.
Wasalaaaam
N.Mushi
Restructuring plan ya Tanesco ndo hoja inatakiwa kuwa mezani kwa sasa.. kama kuna nchi wamefaulu nadhani hapo ndo pakuanzia kujifunza... Case study zipo nyingi kwamba hicho kitu kinaweza kuwezekanaYeah...niliona kitu kama hiyo nchini Namibia, ya kuvunja shirika la umeme into generation na Distribution ambako kule unakuta Kuna kampuni zinazojiendesha as distribution, kulingana na eneo ..provincial company etc.ili kurahisisha kutoa huduma Kwa tija......labda Tanesco nayo waifanye hivyo kuifanya restructuring, kuisaidia sekta hiyo....
Umeona eee mpaka na grafu 😊😊Akili kubwa
Somehow ina make sense! But kwa ukiritimba wa CCM sidhan kama kutakua na solutions!!The only way kuiendesha Tanesco kifaida, kwa capacity ya uelewa wa usimamizi wa Tanzania, ni kuikata mapande sawa na mikoa na kila kipande kiwe huru na kijiendeshe kama pande la kujitgemea kikamilifu.
Pamoja mkuuUmeeleza pakubwa sana
Mawazo mazuri sana ila Sasa kwenye uongozi NDIO issue..... implementation yake Kwa Tz ni issue LABDA WATEULIWE MALAIKA KUJA KUSIMAMIAStill zitabaki kuwa ni kubwa sana kwa uwezo wetu wa management.
Zikatwe kimikoa na huko kila idara kubwa zijitegemee.
Transmission iwe kila mkoa kivyake, distribution, kila mkoa kivyake, production kila mkoa kivyake, mikoa inayozalisha zaidi ya matumizi yake itawauzia mikoa ambayo uzalishaji wake ni mdogo.
National grid iwe na management yake kivyake
wakiangalia kiwango cha matumizi kwa mkoa au kwa kanda itakuwa ni rahisi kupanga.. kikubwa hapo decentralization hata ikiwa kwa kanda au labda kampuni moja lishike mikoa miwiliKuna mikoa itakaa gizani milele
Nakuunga mkono, hoja ya kuwa na makampuni mengi ndio solution.. Tanesco ibaki kama mwangalizi tu au regulator...Kimantiki na mifano ipo nchi nyingi, shirika lolote la Kiserikali likiwa kubwa sana ni lazima litawanywe uendeshaji wake ili lisiwe kama serikali ndani ya serikali.
Tanesco kwa viwango na jiografia ya Tanzania ni shirika kubwa sana kuweza kuendeshwa kutokea makao makuu moja na DG mmoja. Ni vyepesi sana kutumika kufanya hujuma, japo iwe ya mkitengo kimoja tu, itaathiri shirika zima.
Suluhisho pekee ni kulikata viande vipande vitoke vikam[uni vingi vinavyojitegemea na uhusiano wao utakuwa wa kibiashara tu. Hakuna zaidi.
Niliwahi kupendekeza hili miaka mingi sana nyuma.
Tanesco ufanyike utaratibu wa kulivunja vunja. Nje ya hapo tutasewka na umeme maisha. Hata tuzalishe umeme zaidi ya tunaouhitaji, bado gtugtakuwa na kukosa umeme na hakuna wa kumwajibisha kwa haraka. Tutabadili mawaziri, tutabadili ma DG, tutafanya kila namna, ni mzigo mkubwa kuliko wabebaji.
Hahahaha pole sana mkuu kwa kukaa gizani... huwa inatia hasira unakuta umeme umekatika zaidi ya masaa 10, siku yote inakuwa imeshaishaWapeni DPW, TENESCO.
Hi ndio kampuni ya kuiuza jumla.
La mtaendelea kukaa gizani kila siku.
Karne ya 21 mji Mkuu unatawaliwa na Giza.
Tukisema habari za Unyani mnajifanya kukasirika.
Mipango ilianza enzi za mkapa: mipango si utekelezaji,jpm apewe maua yake.Acha siasa nyepesi mkuu ..haya matatizo ya Umeme yapo ndani ya CCM .JPM.alifanya Nini kikubwa iukabiliana nayo...zaidi ya kuanza ujenzi wa Bwawa la Mwalimu Nyerere ambao ni msiba ujao( subiri Mika kadhaa utasikia Maji yameisha) Huu si utabiri ni fact...kulingana na hali ya mazingira ya Bonde la Mto Ruaha ja Rufiji! Halafu huna hat Aibu Kuandika kuwa JPM alipeleka umeme Vijijini...ama hujui kuwa Mpango huu ulianza tangu enzi za Mkapa..Hawa Sasa wanamalizia ..!