Tabia gani hupendi au unapenda ukiwa safarini?

Tabia gani hupendi au unapenda ukiwa safarini?

Napenda kukaa siti ya mwisho kwenye kona kabisa(benchi la ufundi),. Af dereva atembeze kiatu kwelkwel.
Sipendi kukaa na mtu mjuaji wa mambo.

Be like "oya unapaona hapa, yale ndo majabali ambapo wajerumani waliyatumia kama maficho ya dhahabu walizotuibia mwaka 1927. Wakati huo ..........." Wanakera sana.
 
Abiria jirani kutaka kunijua saaana na kuomba namba,, keroo mnatakiwa kujua si mara zote mtu Yuko safari kwa matembezi manake hizi ndo zenye raha, wengine safari ni za majonzi, mahangaiko nk kuuliza uliza habari za mtu Ni kumuongezea mahangaiko na makasiriko

Mpe namba ya kamanda fulani kikosi maalumu, zile namba zao huwa public...

Tafuta ya mmama mmoja hivi mpe...
 
Tupande ndege muache umaskini huo

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app

Kwenye ndege utakaa mwenyewe kama ni business class...lakini kule siti zetu za kajamba nani ni kama basi tu...

Tena bora kwenye basi unakaa na mzigua au mmasaai unaweza kummudu, imagine umekaa na vichina vile vinajamba jamba hovyo we utajulia wapi jina la ushuzi kwa kichina...

Imagine unanyanyuka toka Dar/Nairobi/Addis, Dubai kwenda Peking, NYC etc non stop flight, lazima utakaa na mtu au watu muda mrefu tu...
 
[emoji23]
Hasa sisi wembamba ndio unakuta tunabanwa hadi basi.
Dawa ni kuinuka na kukaa upya..nikiinuka nikikaa nakaa seat yangu yote
Kwahiyo kama niliyekaa naye amekaa na sehemu yangu yaani namkalia Sehemu iliyozidi.

Hahaha
 
Nani mwenye experience na Yale mabus yenye seat za kukaa watu wawili kushoto na watatu kulia na amepata Seat ya katikati kwenye upande wa Seat tatu na iwe safari ya zaidi ya masaa nane...
 
Napenda kukaa siti ya mwisho kwenye kona kabisa(benchi la ufundi),. Af dereva atembeze kiatu kwelkwel.
Sipendi kukaa na mtu mjuaji wa mambo.

Be like "oya unapaona hapa, yale ndo majabali ambapo wajerumani waliyatumia kama maficho ya dhahabu walizotuibia mwaka 1927. Wakati huo ..........." Wanakera sana.
Hahaah wanakuonyesha machimbo ya mjerumani
 
Nani mwenye experience na Yale mabus yenye seat za kukaa watu wawili kushoto na watatu kulia na amepata Seat ya katikati kwenye upande wa Seat tatu na iwe safari ya zaidi ya masaa nane...
Hapo bila shaka ni tabu sana.
 
Kuna wale wanaongelea kwa sauti mambo ya nyumbani kwao kwenye bus, wanakera sana

Unakuta mama anamwambia binti wa kazi tunakuja tupo njiani, hakikisha umepika hiki na hiki, halafu mjaze maji kwenye jaba eeh

Jana usiku mlikula nini? Hamjanimiss na wanacheka cheka sana

Mara Baba yenu yupo hapo mumpe simu nimsalimie Mume wangu???

Yaani mambo ya nyumbani kwao wanaongea kwa sauti kama vile yanatuhusu na sisi.

K E R O K U B W A
Hapo anataka kuwaonyeshea wasafiri wengine kua na yeye ana family na wanainjoi
 
Napenda kuchimba dawa kichakani, aisee huwa namiss kweli hako ka moment….

Sipendi kukaa na abiria mchafu mchafu, aisee safari inakuwa ngumu hasa safari za masafa marefu…
 
Back
Top Bottom