Tabia ya kukoroma inanivunjia ndoa yangu

Tabia ya kukoroma inanivunjia ndoa yangu

Wakuu,

Kwa kuanza, mimi ni kijana wa makamu, umri 35+, mfupi, kibonge, mweusi tiiiiiiii!

Nimeajiriwa kwenye NGO moja ya wazungu, alhamdulilah familia inaenda chooni. Nimebahatika kuwa na watoto wa3 kila mmoja na mama yake na nashukuru wanangu wanaishi vizuri lakini sikubahatika kuoa wazazi wenza kwa sababu ya tabia zao za midomo midomo na uswahili mwingi.

Nilikuwa nikiishi single na muda mwingi niliutumia nikiwa na jamaa zangu Jeffu na Bakari ambao tulikuwa tukifanya kazi pamoja.

Basi siku moja rafiki zangu Jeffu na BeKa wakanishauri ninyoe upara kwa madai eti utanipendeza kutokana na kujaaliwa na udevu kama brush la kupakia chachandu kwenye mihogo.

Kweli bwana nikaamua kuwasikiliza swahiba zangu Beka na Jeffu nikafunga safari mpaka kwa kinyozi wangu kevii aliyezoea kuninyoa mnyoo wangu wa pank la kiaskari, siku hii alishangaa sana kusikia nataka kunyoa upara, hakuwa na budi kwakuwa mteja ni mfalme.

Nilipata tabu sana wakati wa mwanzo, sikuzoea kabisa kuwa na kipara. Basi ni kipindi hiki ndio nilikutana na wife wangu wa sasa, huyu alikuwa bestie yake na mke wa swahiba yangu bakari (beka) weekend moja nilimtembelea Beka kwake na nilimkuta peke yake huku akidai mkewe kaenda kicoba, basi baada ya muda shemeji alirudi akiwa na huyo rafiki yake (wife wangu wa sasa)

Baada ya siku kadhaa nilitafutwa na namba ngeni ambapo baada ya kujitambulisha niligundua ni yule rafiki wa shemeji basi tukaanza ukaribu na kuwa marafiki, huyu dada alipenda sana kunisifia upara wangu, na kunifanya nijute kwanini nilichelewa kunyoa dongo.

Muda ukapita, siku, wiki, miezi ukaribu ukazidi na akawa mtu wangu rasmi (beka na mkewe wote walijua) ukiacha upara wangu, huyu bibie alikuwa akiniheshimu na kunishukuru sana nilipokuwa namuokoa na pesa za marejesho na vicoba kwani alikuwa na michezo zaidi ya 15 sijui alikuwa anapeleka wapi hizi pesa.

Penzi likakolea na bibie wote tukakubaliana kufunga ndoa na tafrija fupi iliyokutanisha watu wachache tu, wazazi, marafiki zetu wakina beka na Jeffu pamoja na wana kikundi wenzake wa kikoba.

Hii siku ya ndoa hakika nilipendeza sanaa, nilimwambia kinyozi wangu kevii ahakikishe anakwangua haswaa upara wangu ili nimfurahishe mke wangu kwenye harusi yetu. Harusi ilifana sana, watu walikula na kunywa.

Maisha ya ndoa yakaanza...............:.!


Itaendelea.....

View attachment 3117210
Niliangalia vibaya hiko kipara nikajuaaa nanliu🤔 au basi tuendelee na mada 😂🤣🤣🤣😎🤗
 
Pole sana na hongera kwa kufanya mazoezi kupunguza kitambi na unene uliopitiliza, endelea usikate tamaa matokeo chanya yatakuja tu bila shaka!

Kukoroma wakati umelala ni tatizo ambalo huwapata hasa watu wanene sana au wenye shida ya kimuundo kwenye njia ya hewa. Pia hutokea kwa wengine kutokana na kulala vibaya ambapo njia hewa hubanwa sana pamoja mtindo wa maisha mfano unywaji pombe nk.

Kwa hiyo inabidi uende hospital ukaonane na daktari bingwa wa koo, pua na masikio (ENT surgeon) ili uchunguzwe na kutibiwa ipasavyo. Naamini ndoa yako itabaki salama.
Kila lakheri!
 
Wakuu,

Kwa kuanza, mimi ni kijana wa makamu, umri 35+, mfupi, kibonge, mweusi tiiiiiiii!

Nimeajiriwa kwenye NGO moja ya wazungu, alhamdulilah familia inaenda chooni. Nimebahatika kuwa na watoto wa3 kila mmoja na mama yake na nashukuru wanangu wanaishi vizuri lakini sikubahatika kuoa wazazi wenza kwa sababu ya tabia zao za midomo midomo na uswahili mwingi.

Nilikuwa nikiishi single na muda mwingi niliutumia nikiwa na jamaa zangu Jeffu na Bakari ambao tulikuwa tukifanya kazi pamoja.

Basi siku moja rafiki zangu Jeffu na BeKa wakanishauri ninyoe upara kwa madai eti utanipendeza kutokana na kujaaliwa na udevu kama brush la kupakia chachandu kwenye mihogo.

Kweli bwana nikaamua kuwasikiliza swahiba zangu Beka na Jeffu nikafunga safari mpaka kwa kinyozi wangu kevii aliyezoea kuninyoa mnyoo wangu wa pank la kiaskari, siku hii alishangaa sana kusikia nataka kunyoa upara, hakuwa na budi kwakuwa mteja ni mfalme.

Nilipata tabu sana wakati wa mwanzo, sikuzoea kabisa kuwa na kipara. Basi ni kipindi hiki ndio nilikutana na wife wangu wa sasa, huyu alikuwa bestie yake na mke wa swahiba yangu bakari (beka) weekend moja nilimtembelea Beka kwake na nilimkuta peke yake huku akidai mkewe kaenda kicoba, basi baada ya muda shemeji alirudi akiwa na huyo rafiki yake (wife wangu wa sasa)

Baada ya siku kadhaa nilitafutwa na namba ngeni ambapo baada ya kujitambulisha niligundua ni yule rafiki wa shemeji basi tukaanza ukaribu na kuwa marafiki, huyu dada alipenda sana kunisifia upara wangu, na kunifanya nijute kwanini nilichelewa kunyoa dongo.

Muda ukapita, siku, wiki, miezi ukaribu ukazidi na akawa mtu wangu rasmi (beka na mkewe wote walijua) ukiacha upara wangu, huyu bibie alikuwa akiniheshimu na kunishukuru sana nilipokuwa namuokoa na pesa za marejesho na vicoba kwani alikuwa na michezo zaidi ya 15 sijui alikuwa anapeleka wapi hizi pesa.

Penzi likakolea na bibie wote tukakubaliana kufunga ndoa na tafrija fupi iliyokutanisha watu wachache tu, wazazi, marafiki zetu wakina beka na Jeffu pamoja na wana kikundi wenzake wa kikoba.

Hii siku ya ndoa hakika nilipendeza sanaa, nilimwambia kinyozi wangu kevii ahakikishe anakwangua haswaa upara wangu ili nimfurahishe mke wangu kwenye harusi yetu. Harusi ilifana sana, watu walikula na kunywa.

Maisha ya ndoa yakaanza...............:.!


Itaendelea.....

View attachment 3117210
Hii chai 😂😂😂
 
Wakuu,

Kwa kuanza, mimi ni kijana wa makamu, umri 35+, mfupi, kibonge, mweusi tiiiiiiii!

Nimeajiriwa kwenye NGO moja ya wazungu, alhamdulilah familia inaenda chooni. Nimebahatika kuwa na watoto wa3 kila mmoja na mama yake na nashukuru wanangu wanaishi vizuri lakini sikubahatika kuoa wazazi wenza kwa sababu ya tabia zao za midomo midomo na uswahili mwingi.

Nilikuwa nikiishi single na muda mwingi niliutumia nikiwa na jamaa zangu Jeffu na Bakari ambao tulikuwa tukifanya kazi pamoja.

Basi siku moja rafiki zangu Jeffu na BeKa wakanishauri ninyoe upara kwa madai eti utanipendeza kutokana na kujaaliwa na udevu kama brush la kupakia chachandu kwenye mihogo.

Kweli bwana nikaamua kuwasikiliza swahiba zangu Beka na Jeffu nikafunga safari mpaka kwa kinyozi wangu kevii aliyezoea kuninyoa mnyoo wangu wa pank la kiaskari, siku hii alishangaa sana kusikia nataka kunyoa upara, hakuwa na budi kwakuwa mteja ni mfalme.

Nilipata tabu sana wakati wa mwanzo, sikuzoea kabisa kuwa na kipara. Basi ni kipindi hiki ndio nilikutana na wife wangu wa sasa, huyu alikuwa bestie yake na mke wa swahiba yangu bakari (beka) weekend moja nilimtembelea Beka kwake na nilimkuta peke yake huku akidai mkewe kaenda kicoba, basi baada ya muda shemeji alirudi akiwa na huyo rafiki yake (wife wangu wa sasa)

Baada ya siku kadhaa nilitafutwa na namba ngeni ambapo baada ya kujitambulisha niligundua ni yule rafiki wa shemeji basi tukaanza ukaribu na kuwa marafiki, huyu dada alipenda sana kunisifia upara wangu, na kunifanya nijute kwanini nilichelewa kunyoa dongo.

Muda ukapita, siku, wiki, miezi ukaribu ukazidi na akawa mtu wangu rasmi (beka na mkewe wote walijua) ukiacha upara wangu, huyu bibie alikuwa akiniheshimu na kunishukuru sana nilipokuwa namuokoa na pesa za marejesho na vicoba kwani alikuwa na michezo zaidi ya 15 sijui alikuwa anapeleka wapi hizi pesa.

Penzi likakolea na bibie wote tukakubaliana kufunga ndoa na tafrija fupi iliyokutanisha watu wachache tu, wazazi, marafiki zetu wakina beka na Jeffu pamoja na wana kikundi wenzake wa kikoba.

Hii siku ya ndoa hakika nilipendeza sanaa, nilimwambia kinyozi wangu kevii ahakikishe anakwangua haswaa upara wangu ili nimfurahishe mke wangu kwenye harusi yetu. Harusi ilifana sana, watu walikula na kunywa.

Maisha ya ndoa yakaanza...............:.!


Itaendelea.....

View attachment 3117210
Sasa,maelezo meeengiii ni kwa ajili ya upara na brashi ya chachandu au kukoroma?🤔
 
Inaendelea......

Baada ya harusi, miezi ilikatika, hatimae mwaka, ila ndoa ikaanza kugeuka ndoano, mke wangu alikuwa na visirani visivyoisha na kupenda kununa nuna, hasa zikijaribia siku za marejesho. Basi nikiona visirani vinazidi nampa pesa aongezee kwenye marejesho, hapo utaanza kumuona anacheka.

Sasa huyu mwenzangu amekuwa na tabia ya kupenda kunisimanga sanaaa, hasa kuhusu kitambi changu, amekuwa akiniita majina yenye kukera mpaka kuna mda nakosa hata hamu ya kula. Basi kutokana na maneno kuniuma ikabidi nianze mazoezi, asubuhi napiga push up 30 na kukimbia na jioni pia, katika hili wife amenipongeza mno kwani mwili umeanza kupungua kidogo.

Sasa kutokana na uchovu wa kazi na mazoezi nimejikuta nakuwa nachoka sanaa usiku nikilala nakoroma kama gari bovu. Yani nakoroma mpaka nikiamka nasikia maumivu ya kifua na mdomo umekauka kwaajili ya kuachama.

Hii hali imekuwa ikimkera sana wife wangu, mara nyingi ananishtuka usingizini kwa vibao na mateke, nikishtuka huwa mapigo ya moyo huwa yanaenda mbio sana mpaka nahisi kufa.

Jana jumamosi nilishinda nyumbani, wife akaomba kuzungumza na mimi, kikubwa ni hii tabia yangu ya kukoroma hovyoo, anadai amechoka na nisipobadilika hivi karibuni ndoa itamshinda.

Ndugu zangu, kama kuna mtu anaweza kunisaidia tatizo hili la kukoroma naombeni msaada maana ndoa yangu inaenda kufa.

Hapa naandika uzi huu nipo sebuleni nawaza jinsi ya kwenda kulala, wife yupo kitandani toka saa tatu ila najua nikiingia mimi lazima tu ataamka kwa kukoroma kwangu.
Kukoroma sio tabia, bali ni maradhi na ninavyojua maradhi haya hadi sasa hayana dawa. Huyo mwanamme mwambie kama hawezi vumilia aende zake akaolewe na mwanamume asiyekoroma!!, asikutie stress za masimango . Utakuja mpata mke atakaevumilia kukoroma kwako.
 
Inaendelea......

Baada ya harusi, miezi ilikatika, hatimae mwaka, ila ndoa ikaanza kugeuka ndoano, mke wangu alikuwa na visirani visivyoisha na kupenda kununa nuna, hasa zikijaribia siku za marejesho. Basi nikiona visirani vinazidi nampa pesa aongezee kwenye marejesho, hapo utaanza kumuona anacheka.

Sasa huyu mwenzangu amekuwa na tabia ya kupenda kunisimanga sanaaa, hasa kuhusu kitambi changu, amekuwa akiniita majina yenye kukera mpaka kuna mda nakosa hata hamu ya kula. Basi kutokana na maneno kuniuma ikabidi nianze mazoezi, asubuhi napiga push up 30 na kukimbia na jioni pia, katika hili wife amenipongeza mno kwani mwili umeanza kupungua kidogo.

Sasa kutokana na uchovu wa kazi na mazoezi nimejikuta nakuwa nachoka sanaa usiku nikilala nakoroma kama gari bovu. Yani nakoroma mpaka nikiamka nasikia maumivu ya kifua na mdomo umekauka kwaajili ya kuachama.

Hii hali imekuwa ikimkera sana wife wangu, mara nyingi ananishtuka usingizini kwa vibao na mateke, nikishtuka huwa mapigo ya moyo huwa yanaenda mbio sana mpaka nahisi kufa.

Jana jumamosi nilishinda nyumbani, wife akaomba kuzungumza na mimi, kikubwa ni hii tabia yangu ya kukoroma hovyoo, anadai amechoka na nisipobadilika hivi karibuni ndoa itamshinda.

Ndugu zangu, kama kuna mtu anaweza kunisaidia tatizo hili la kukoroma naombeni msaada maana ndoa yangu inaenda kufa.

Hapa naandika uzi huu nipo sebuleni nawaza jinsi ya kwenda kulala, wife yupo kitandani toka saa tatu ila najua nikiingia mimi lazima tu ataamka kwa kukoroma kwangu.
kuna vizuia kukoroma vinauzwa
 
Hili sio la kuvumulia jamani? Linaonekana dogo mbona.
🤣🤣🤣🤣🤣🤣 hujawahi kulala na mkoromaji wewe! Sio kitu kidogo kama unahitaji kupumzika halafu mtu amefungulia sabufa mpaka mwisho..kila siku! Watoto wachanga 10 wananafuu

Ndugu mdau apunguze uzito, na aangalie namna ya ulalaji utakaofanya asikorome
 
Inaendelea......

Baada ya harusi, miezi ilikatika, hatimae mwaka, ila ndoa ikaanza kugeuka ndoano, mke wangu alikuwa na visirani visivyoisha na kupenda kununa nuna, hasa zikijaribia siku za marejesho. Basi nikiona visirani vinazidi nampa pesa aongezee kwenye marejesho, hapo utaanza kumuona anacheka.

Sasa huyu mwenzangu amekuwa na tabia ya kupenda kunisimanga sanaaa, hasa kuhusu kitambi changu, amekuwa akiniita majina yenye kukera mpaka kuna mda nakosa hata hamu ya kula. Basi kutokana na maneno kuniuma ikabidi nianze mazoezi, asubuhi napiga push up 30 na kukimbia na jioni pia, katika hili wife amenipongeza mno kwani mwili umeanza kupungua kidogo.

Sasa kutokana na uchovu wa kazi na mazoezi nimejikuta nakuwa nachoka sanaa usiku nikilala nakoroma kama gari bovu. Yani nakoroma mpaka nikiamka nasikia maumivu ya kifua na mdomo umekauka kwaajili ya kuachama.

Hii hali imekuwa ikimkera sana wife wangu, mara nyingi ananishtuka usingizini kwa vibao na mateke, nikishtuka huwa mapigo ya moyo huwa yanaenda mbio sana mpaka nahisi kufa.

Jana jumamosi nilishinda nyumbani, wife akaomba kuzungumza na mimi, kikubwa ni hii tabia yangu ya kukoroma hovyoo, anadai amechoka na nisipobadilika hivi karibuni ndoa itamshinda.

Ndugu zangu, kama kuna mtu anaweza kunisaidia tatizo hili la kukoroma naombeni msaada maana ndoa yangu inaenda kufa.

Hapa naandika uzi huu nipo sebuleni nawaza jinsi ya kwenda kulala, wife yupo kitandani toka saa tatu ila najua nikiingia mimi lazima tu ataamka kwa kukoroma kwangu.
Kama siyo chai, huyo mwanamke amemaliza marejesho ya vikoba.
 
Hapa tujiandae mwanamke mwenzetu kusemwa kwanini anashindwa kumvumilia mumewe mkoromaji, tena wataenda mbali zaidi na kutolea mifano ya bibi zetu kwamba mbona walivumilia madhaifu mengi ya babu zetu, yani africa ukizaliwa mwanamke automatically unatakiwa kuwa mvumilivu katika mabaya yote unayotendewa hasa na mumeo haijalishi yanakukera kiasi gani
Mbona hujagusia suala la vikoba hapo na pesa za marejesho ambazo mwamba hata hajui zinaendaga wapi???
Mlivyo wabinafsi ntie watu!!!
 
Sidhanj kama unaachwa kwa ajili ya kukoroma,inaonyesha unaongea sana maana mada imeanzia mbali mpaka kufika kwenye kukoroma sio mchezo...wanawake hawapendi hizo
 
Kama jamaa aliweza kuvumilia kulipia vikoba 15 kabla hajamuoa, yeye mwanamke anashindwaje kuvumilia mikoromo?

Mwanamke achague, jamaa afanye mazoezi apunguze kitambi ila usiku akorome au jamaa aache mazoezi, kitambi kirudi ila usiku mikoromo isiwepo.

Hakuna binadamu atakupa ukamilifu wa 100%. Chagua pungufu moja, vumilia.
Wewe unajuaje kama mtoa mada hana mapungufu mengine ambayo mkewe hayavumilii, mbona umeassume kama jamaa ni mkamilifu hana mapungufu mengi zaidi ya kukoroma, ndio maana nikasema binadamu tunatofautiana katika mambo yanayotukera, kwangu jambo linaweza kuwa dogo ila kwa mwingine ni kubwa, usikute huyo mke anavumilia mengi tu ya mumewe ila hilo la kukoroma ndio ameshindwa
 
Mbona hujagusia suala la vikoba hapo na pesa za marejesho ambazo mwamba hata hajui zinaendaga wapi???
Mlivyo wabinafsi ntie watu!!!
Wewe unajuaje kama mtoa mada hana mapungufu mengine ambayo mkewe hayavumilii, mbona umeassume kama jamaa ni mkamilifu hana mapungufu mengi zaidi ya kukoroma, ndio maana nikasema binadamu tunatofautiana katika mambo yanayotukera, kwangu jambo linaweza kuwa dogo ila kwa mwingine ni kubwa, usikute huyo mke anavumilia mengi tu ya mumewe ila hilo la kukoroma ndio ameshindwa
 
Back
Top Bottom