DOKEZO Tabora Mjini hali tete, mafuta hakuna! Maji hakuna

DOKEZO Tabora Mjini hali tete, mafuta hakuna! Maji hakuna

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Niendee moja kwa moja kwenye mada husika!

Mkoa wa Tabora hivi sasa ninapoandika uzi huu, uko kwenye taharuki kubwa ya kukosa mafuta!

Hali ni mbaya hapa mjini, petro station moja tu mji mzima inatoa huduma ya mafuta!

Hakuna kiongozi yoyote wa chama (CCM) au serikali ambaye ametoa ufafanuzi wowote!

Mkoa huu wa kishu'shu'shu na KI'CCM hali ni tete..! Mkoa umebaki mtupu hakuna mtetezi!

Nikumbushe kuwa jumatano ijayo ya mwanzo wa mwezi kwa fununu zilizopo EWURA wanatangaza bei mpya za mafuta, kitu ambacho kinatarajiwa, ni mafuta kupaa zaidi bei.

Nikumbushe pia mwezi mmoja uliopita ilitokea taharuki kama hii ya sasa, na kuonekana baadhi ya wafanyabiashara wakificha mafuta na baada ya wiki moja na nusu mafuta yakapaa kwa bei ambayo haijawahi kushuhudiwa kwa kizazi hiki cha miaka 30 iliyopita!

SHIDA YA MAJI
Maji pia yamekuwa shida, zaidi ya wiki sasa maji hayapatikani...!
Hali ni mbaya tumefika pabaya!!
Ngoja uzi huu tum tag Lucas mwashambwa
Maana yuko karibu na mfumo,ataufanyia kazi matatizo yenu huko

Ova
 
Ngoja uzi huu tum tag Lucas mwashambwa
Maana yuko karibu na mfumo,ataufanyia kazi matatizo yenu huko

Ova
Wawe na subiri maana serikali yao ipo kazini muda wote ,hailali wala kusinzia hata sekunde moja katika kuhakikisha inawapatia watanzania huduma bora zitakazo kidhi mahitaji yao. Serikali ya mama inafanya kazi ya kuhakikisha kuwa inamfikia kila mtanzania popote pale alipo.Ni serikali ya kazi,ni serikali ya kuwafuta watu machozi,ni serikali ya kuwapa watu matumaini hai,ni serikali ya kuwapatia watu Tabasamu,furaha na vicheko na ni serikali ya kuwatua watu mizigo ya kero na changamoto mbalimbali.

Waendelee kuiamini serekali yao na kumwamini Mh Rais wetu mpendwa kipenzi cha watanzania mama samia suluhu Hasssan.
 
Wakuu, binafsi sijui nchi inapo elekea. Tangu jana nimezunguka vituo vyote vya mafuta "fuel stations" wanasema mafuta yameisha, lakini kimtazamo inaonekana wazi kuna shida mahali ambayo imepelekea wafanya biashara hao kuamua kugoma kuuza mafuta.

Kwakweli sijui tunaelekea wapi hii nchi, maana hadi naandika uzi huu nimetoka kuzunguka mji mzima wa Tabora manispaa kila kituo wanasema mafuta yamekwisha. Ikiwa mimi binafsi nimejikuta natumia garama ya karibu shilingi 12,000 kuzunguka kutafuta maguta na bodaboda mji mzima.

Leo nimeshindwa kuwapeleka wanangu shuleni.
Nimeshindwa kumpelekea mgonjwa chakula hospitali.
Nimeshindwa kumpeleka wife kazini.
Nimeshindwa kufuata maziwa ya kiziwanda.
Nimeshindwa kwenda kwenye michongo yangu down town.

Na sijui jioni nitarudije home nikisha piga mtungi, maana kwenda nitaenda polepole kwa miguu.

Jamani wenye mamlaka ebu mtusaidie kwa hili maana kama mimi nimepata shida hizo, je, vipi wananchi wenzangu kwao imekuaje?
 
Ukiona hivyo ujiandae kusikia Ewura wametangaza bei mpya leo mafuta yanapanda kesho fuel station hizo hizo kesho utashangaa mafuta wanayo na utauziwa mafuta kwa bei ya juu ni mwendo wa super profit, kwa Dar wenye tabia hiyo sana ni Total.

Ningekuwa na mamlaka ningelitumia Jeshi kukomesha tabia hii nchi nzima, unaanzisha msako wa filling station zote ambazo wanasema hawana mafuta wanasachi visima vyote atakayekutwa amefungia mafuta anafutiwa Leseni hapohapo na mmiliki anawekwa ndani kwa uhujumu uchumi, ukiwafanyia demo watu kadhaa tu hii tabia ingekoma.
 
Tabora ni pa hovyo sana. Nilipata kufanya project moja kwa miezi miwili, ila niliona kama nimekaa mwaka.

Turudi kwenye mada;
Poleni sana. Hii janja janja ya Wafanyabiashara ikomeshwe.

Vumilieni, mpaka kesho jioni mafuta bwerere.
Hadi muda huu hakuna mafuta mji mzima
 
Niendee moja kwa moja kwenye mada husika!

Mkoa wa Tabora hivi sasa ninapoandika uzi huu, uko kwenye taharuki kubwa ya kukosa mafuta!

Hali ni mbaya hapa mjini, petro station moja tu mji mzima inatoa huduma ya mafuta!

Hakuna kiongozi yoyote wa chama (CCM) au serikali ambaye ametoa ufafanuzi wowote!

Mkoa huu wa kishu'shu'shu na KI'CCM hali ni tete..! Mkoa umebaki mtupu hakuna mtetezi!

Nikumbushe kuwa jumatano ijayo ya mwanzo wa mwezi kwa fununu zilizopo EWURA wanatangaza bei mpya za mafuta, kitu ambacho kinatarajiwa, ni mafuta kupaa zaidi bei.

Nikumbushe pia mwezi mmoja uliopita ilitokea taharuki kama hii ya sasa, na kuonekana baadhi ya wafanyabiashara wakificha mafuta na baada ya wiki moja na nusu mafuta yakapaa kwa bei ambayo haijawahi kushuhudiwa kwa kizazi hiki cha miaka 30 iliyopita!

SHIDA YA MAJI
Maji pia yamekuwa shida, zaidi ya wiki sasa maji hayapatikani...!
Hali ni mbaya tumefika pabaya!!
Mkurugenzi EWURA anamhujumu rais Dkt Samia. Afukuzwe haraka sana. Kinachotokea kuna watu ndani ya EWURA wanatoa taarifa. Ninashauri ili abaki na cheo chake safari hii ashushe bei ili kuwakomoa wanaofungia mafuta.
 
Ukiona hivyo ujiandae kusikia Ewura wametangaza bei mpya leo mafuta yanapanda kesho fuel station hizo hizo kesho utashangaa mafuta wanayo na utauziwa mafuta kwa bei ya juu ni mwendo wa super profit, kwa Dar wenye tabia hiyo sana ni Total.

Ningekuwa na mamlaka ningelitumia Jeshi kukomesha tabia hii nchi nzima, unaanzisha msako wa filling station zote ambazo wanasema hawana mafuta wanasachi visima vyote atakayekutwa amefungia mafuta anafutiwa Leseni hapohapo na mmiliki anawekwa ndani kwa uhujumu uchumi, ukiwafanyia demo watu kadhaa tu hii tabia ingekoma.

Hizi harakati aliziweza jpm,huyu wa sasa na genge lake la wahuni huwezi sikia hilo.
 
Kwamba wahuni wameficha [emoji849][emoji848]
100% wameficha mkuu.
Maana haiwezekani vituo vyote viseme vimeishiwa kwa siku moja na utofauti ni kidogo sana.
Wafanya biashara wamefucha mafuta mkuu.
 
Acha ngonjera wewe , unakaa tabora ipi ambayo hakuna maji
Hakuna maji ndio yametoka jana kwa masaa tu baada ya kukaa zaidi ya week nzima. Hata Leo hakuna maji.... Kote kidatu,Ipuli yoteee. Maji yanatoka maeneo ya ofisi za mkoani na pale brigedi
 
Wamegoma kuuza mafuta kisa mtetezi wao Makamba kaondolewa kwenye wizara nyeti ya nishati.
 
Nye CCM, wanyamwezi wamewakosea nini? mbona ni watiifu kuwapa ushindi wa kishindo japo hamuwajali baada ya matokeo.
 
Back
Top Bottom