DOKEZO Tabora Mjini hali tete, mafuta hakuna! Maji hakuna

DOKEZO Tabora Mjini hali tete, mafuta hakuna! Maji hakuna

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Niendee moja kwa moja kwenye mada husika!

Mkoa wa Tabora hivi sasa ninapoandika uzi huu, uko kwenye taharuki kubwa ya kukosa mafuta!

Hali ni mbaya hapa mjini, petro station moja tu mji mzima inatoa huduma ya mafuta!

Hakuna kiongozi yoyote wa chama (CCM) au serikali ambaye ametoa ufafanuzi wowote!

Mkoa huu wa kishu'shu'shu na KI'CCM hali ni tete..! Mkoa umebaki mtupu hakuna mtetezi!

Nikumbushe kuwa jumatano ijayo ya mwanzo wa mwezi kwa fununu zilizopo EWURA wanatangaza bei mpya za mafuta, kitu ambacho kinatarajiwa, ni mafuta kupaa zaidi bei.

Nikumbushe pia mwezi mmoja uliopita ilitokea taharuki kama hii ya sasa, na kuonekana baadhi ya wafanyabiashara wakificha mafuta na baada ya wiki moja na nusu mafuta yakapaa kwa bei ambayo haijawahi kushuhudiwa kwa kizazi hiki cha miaka 30 iliyopita!

SHIDA YA MAJI
Maji pia yamekuwa shida, zaidi ya wiki sasa maji hayapatikani...!
Hali ni mbaya tumefika pabaya!!
Yale maji ya kutoka ziwa Victoria yameyeyuka.
 
Wameficha wanasubiri bei chaajabu mkoa una viongozi wote mpaka maaafisa wa usalama wamekaa hapo na wanalipwa mishahara na serikali.
 
Jumanne ya kwanza ya kila mwezi ni tangazo la bei mpya za mafuta! Wameyaficha wakisubiri Jumanne ijayo yapande. Hizo ni indicators we are shitholes! Nchi ya kipumbavu kabisa.
Wanasubiri jumatano bei mpya
 
Kwasasa Tabora kuna shida ya maji, na yanatoka kwa mgao walau masaa matatu kila siku.
Hata umeme pia ni patashika kwasasa umekua wa mgao.
Nilikua tabora siku mbili zimepita hakuna shida ya maji, suala la umeme ni la kitaifa

Nilikua maeneo ya national
 
Hakuna maji ndio yametoka jana kwa masaa tu baada ya kukaa zaidi ya week nzima. Hata Leo hakuna maji.... Kote kidatu,Ipuli yoteee. Maji yanatoka maeneo ya ofisi za mkoani na pale brigedi
Nilikua national maji yapo ya uhakika
 
Ukiona hivyo ujiandae kusikia Ewura wametangaza bei mpya leo mafuta yanapanda kesho fuel station hizo hizo kesho utashangaa mafuta wanayo na utauziwa mafuta kwa bei ya juu ni mwendo wa super profit, kwa Dar wenye tabia hiyo sana ni Total.

Ningekuwa na mamlaka ningelitumia Jeshi kukomesha tabia hii nchi nzima, unaanzisha msako wa filling station zote ambazo wanasema hawana mafuta wanasachi visima vyote atakayekutwa amefungia mafuta anafutiwa Leseni hapohapo na mmiliki anawekwa ndani kwa uhujumu uchumi, ukiwafanyia demo watu kadhaa tu hii tabia ingekoma.
Hili la mafuta Dr. Biteko atoe maelekezo haraka sana hali ni mbaya.
 
Naweza nikaelewa ukosefu wa mafuta lakini maji kwanini yawe changamoto wakati yanatoka hapo hapo na watu wapo tayari kuyalipia bei yeyote wayapate? nimekaa sana nchi za nje na niliwahi kufanya kazi kwenye city utilities divison, maji yalikuwa safi hata kwa kunywa moja kwa moja kutoka bombani na sikuwahi kuona maji yakatike hata siku moja, na walikuwa hawana hata mto, maji yao yalikuwa ya underground (aquifer) na budget yao haikuwa kubwa sana na walikuwa wanapata faida na bill za maji ilikuwa ni karibu na bure, kuna kitu cha ovyo tunafanya ndio maana hatuna maji, hizi halmashauri inabidi zitafute solution za uhakika sio visingizio kila siku, watu wanalipa kodi na bill za maji pia, ujinga uishe
 
Kizimkazi Hana muda na haya kabisa. YY ni kuteua na kutengua tu.Anacho weza
 
Mbunge ana uwezo gani kwenye umeme na maji?
Mbunge kama ni mfuatiliaji mzuri na marafiki kule juu anaweza kufanya lobbying serikalini ili wilaya yake ipate pesa za mradi, kuna fund nyingi sana za maji zinaishia kwa wajanja
 
Back
Top Bottom