Tabora: Profesa Lipumba anahutubia kwenye Ziara ya Rais Samia kama nani?

Anahutubia kama msaliti wa chama chake, kwa kifupi, huyu Professor sasa ni official kuwa kafirisika kisiasa kama nduguye Zitto maana wananunuliwa na CCM huku wakidanganya wananchi kuwa wao ni wapinzani kumbe hamna kitu, ni magarasa tu kama wanaume wa Dar.
 
Yeye ni mwana ccm mkongwe hivyo amekumbukwa.

Haiwezekani kiongozi wa upinzani akamtabiria kiongozi wa chama kingine kuwa ndiye atakuwa mshindi wa uchaguzi.

Huyo ni kati ya watu wasiyo na faida kwa upinzani na hatufai kuitwa ni mpinzani.
 
Kaona haitwi Ikulu, kaamua kwenda kumvizia Rais barabarani! Tayari kaanza kuimba mapambio, kweli wapinzani wa nchi yetu bado wana safari ndefu! Kiongozi wa chama chama cha upinzani unazungumzia chama tawala kushinda wakati wewe pia unategemea kusimamisha mgombea!
 
Kama Prof.Lipumba sasa shida yako iko wapi? Mbona unawewwseka?

Na lazima tumpe kazi ya kuwa mshauri wa Uchumi
 
Lipumba kaonyesha Siasa za Kiungwana na kistaarabu, Siasa sio Chuki wala vita.

Baadhi ya Viongozi wa Chama cha Chadema wanadhani siasa ni Uhasama na kutengana, wanadhani ukiwa karibu na Mhe. Rais kama alivyo fanya Lipumba au hata kama Mbowe alivyo kutana na Rais Ikulu eti sio sahihi........wenye mawazo kama hayo wana matatizo ya kisaikolojia.
 

Siasa sio Vita wala chuki.

Tanzania kwa sasa Chini ya Mama Samia inaendesha siasa za kistaarabu.
 
Wewe kwani hujamsikia Lissu Star TV akisema kuwa mama anapiga kazi nzuri?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…