Tafadhali naomba kujua ni Maombi gani hapa Mwenyezi Mungu anayependa na Kuyabariki upesi?

Tafadhali naomba kujua ni Maombi gani hapa Mwenyezi Mungu anayependa na Kuyabariki upesi?

Tukisema tuombe tukiwa hatuna dhambi hapa tutajidanganya wenyewe kwa sababu Biblia inasema wote ni wadhambi.Hakuna anayeweza kusimama mbele za Mungu na kusema yeye hana dhambi.

Kitu tunachoweza kujivunia ni kuwa Yesu ametufanya tuhesabiwe kuwa ni wenye haki mbele za Mungu kupitia damu yake iliyomwagika msalabani.Kumwamini Kristo kunatupa uhalali wa kusogea karibu na Mungu tukiwa na ukaribu wa baba na mwana.Na hii ni hakika kuwa maombi yetu yanafika.

Tusiwatishe watu na mambo ya uwe hauna dhambi.Hakuna atakayesimama kuomba kama hicho kikiwa ndo kigezo cha maombi kumfikia Mungu.

1 Yoh 1:8 SUV
Tukisema kwamba hatuna dhambi, twajidanganya wenyewe, wala kweli haimo mwetu.
Ndo maana unaposimama kwenye Maombi unatakiwa kuomba msamaha kwa Mungu, dhambi zote tulizofanya.Mungu anasemee Dhambi
Isaya 1: 18
“Haya, njoni, tusemezane, asema BWANA. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu”

Mathayo 5: 23-24 - Kwa hiyo ikiwa unatoa dhabihu kwenye madhabahu ndani ya Hekalu na unakumbuka kwa ghafla kuwa mtu ana kitu dhidi yako, aacha dhabihu yako huko kwenye madhabahu. Nenda na ufanane na mtu huyo. Kisha kuja na kutoa sadaka yako kwa Mungu

Kwa nini Yesu anasema tuache sadaka kutoa kwa Mungu twenda tukapatana na mtu tuliyekosana naye?

Kwa nini huyu mtu asiendelee kutoa sadaka kwa Mungu wakati kuna dhambi kafanya. Je akiomba huyu mtu Mungu atajibu Maombi Yake?
 
we mwamba ni muongo kinoma, haya yote ni kusadikika


Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa nini unasema ni ya kusadikika.
Unadhani hii Dunia watu wote tupo sawa kuna watu wanatoka kwenye hii Dunia yetu bila hata kutumia ndege na vitu vingine wakaenda kwenye nje ya Dunia na Sayari yetu.

Unaposikia mtu kaenda kwenye bahari au ziwa chini kakuta mji watu huwa hawafanani .

Endelea kuona uongo na kusadikika.
Binadamu hatupo Sawa
 
Ndo maana unaposimama kwenye Maombi unatakiwa kuomba msamaha kwa Mungu, dhambi zote tulizofanya.Mungu anasemee Dhambi
Isaya 1: 18
“Haya, njoni, tusemezane, asema BWANA. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu”

Mathayo 5: 23-24 - Kwa hiyo ikiwa unatoa dhabihu kwenye madhabahu ndani ya Hekalu na unakumbuka kwa ghafla kuwa mtu ana kitu dhidi yako, aacha dhabihu yako huko kwenye madhabahu. Nenda na ufanane na mtu huyo. Kisha kuja na kutoa sadaka yako kwa Mungu

Kwa nini Yesu anasema tuache sadaka kutoa kwa Mungu twenda tukapatana na mtu tuliyekosana naye?

Kwa nini huyu mtu asiendelee kutoa sadaka kwa Mungu wakati kuna dhambi kafanya. Je akiomba huyu mtu Mungu atajibu Maombi Yake?
Dhambi kusamehewa kwake ni kulipwa.Unapoomba msamaha kinachofanya usamehewe ni kwa sababu umemtambua aliyekulipia deni(Yesu) na sio kama Mungu ameamua tu kulipotezea.

Kwa hiyo unapoomba msamaha wa dhambi ni katika kukiri udhaifu ulionao(confessing) na kumwomba Mungu akupe nguvu usianguke tena mule.Lakini kuhusu kusamehewa ulishasamehewa kwa kumkiri kristu kuwa mwokozi wako.

Kusali au kuomba kunahitaji uhusiano na Mungu kwa hiyo ni remainder kwetu pia kuwa tunapaswa kuweka mahusiano yetu na watu wengine sawa.Hii ndo sababu inayofanya tukumbushwe kupatana na wengine kabla hatujaomba.
 
Je,

1. Yule anayesali kwa muda mfupi tu lakini akimaanisha huku akifupisha ( summarize ) matakwa yake kwa Mungu?

2. Yule anayesali Siku nzima na kwa Makelele mengi na akirudia rudia matakwa yake kwa Mungu?

3. Yule anayesali pale akijisikia tu ila Matendo yake kwa Wanadamu ni mema siku zote.
Kwenye maombi muda sio kipaumbele sana lakini content ya maombi yako ndio kinachokubeba zaidi.

Nanyi mkiwa katika kusali, msipayuke-payuke, kama watu wa mataifa; maana wao hudhani ya kuwa watasikiwa kwa sababu ya maneno yao kuwa mengi. Mathayo 6:7 SUV
 
Je,

1. Yule anayesali kwa muda mfupi tu lakini akimaanisha huku akifupisha ( summarize ) matakwa yake kwa Mungu?

2. Yule anayesali Siku nzima na kwa Makelele mengi na akirudia rudia matakwa yake kwa Mungu?

3. Yule anayesali pale akijisikia tu ila Matendo yake kwa Wanadamu ni mema siku zote.
Maswali yako ni magumu mnoo 🤣 🤣 🤣 ,In short naweza kusema yafuatayo kwendana na uelewa wangu mfupi-
1- Sala bora hujibiwa kutokana namsingi mkuu wa IMANI.
2-IMANI ni matendo,na IMANI pasipo matendo ni mfu.
3-Ubora wa sala haujalishi muda ambao mhusika anautumia kusali,bali sala bora ni ile inayotokana na MOYO mnyoofu,MOYO mnyoofu humpendeza MUNGU kuliko dhabihu za kuteketezwa.
4-Kusali kwa kurudiarudia kwenye kumaanisha kuna nafasi kubwa sana katika sala hasa pale tunapotafuta muongozo wa ki-MUNGU,ndo maana tumeambiwa ombeni bila kuchoka.
5-Matendo mema kwa MUNGU na kwa Wengine ni hazina kubwa sana mbele za MUNGU,na huweza kumpendeza MUNGU kwenye kujibu haja zetu.
6-Mwanadamu anapaswa kuswali kila wakati akiomba na kumshukuru MUNGU, na siyo wakati fulani tu.

A COMPLICATED PART ni kwamba mwenye kuamua ubora wa sala ni MUNGU mwenyewe,hvyo basi sisi kama wanadamu ni ngumu sana kuelezea hayo ya ubora kwa namna bora zaidi.
 
Back
Top Bottom