Tafadhali sana piga kura yako hapa: Swali: Je, unaamini kuwa Yesu yuaja upesi? Ndio au Hapana

Je, unaamini kuwa Yesu yuaja upesi kama alivyoahidi katika Ufunuo 22:12?


  • Total voters
    131
  • Poll closed .
Yesu Anarudi Upesi na sasa tupo Kwenye Kanisa la mwisho linaitwa Laodikia,Kabisa la viguvugu. Yesu Atusaidie sana Kuwa na Mwisho Mwema
Amen, Mtumishi wa Mungu 🙏
Ni kweli Kanisa limekuwa vuguvugu. Watu vuguvugu watatapikwa
Ufunuo 3:16 SRUV
Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu.
 
Alisharudi na hawakumpokea hasa manabii wakubwa maana walijua ila sasa hivi wanamsubiri ambaye alishakuja!

Wengi kutokana na mapokeo wana picha yao kichwani ya ujio wa Yesu ila haikuwa kama wengi walinavyodhani itakuwa.

Ni kama majira ile ameshukia Israel,walivyofundishwa ni tofauti na alivyokuja (Same situation na alivyorudi)ndo maana asilimia 90% ya waisrael hawakumpokea na Yesu akawaambia ufalme utahama Mathayo 21:43.
 
Usimcheke. Huyo ni wa kuombea sana maana ni vuguvugu. Hatari ya kuwa vuguvugu imeandikwa katika Ufunuo 3:16 SRUV
Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu.
Kwa hiyo anapaswa awe wa moto au awe wa baridi?
 
au unatuchora
Usiogope Mungu akikuchora kwenye vitanga vya mikono yake.
"Tazama, nimekuchora katika vitanga vya mikono yangu; kuta zako zi mbele zangu daima." (Isaya 49:16)
Lakini hiyo ni ahadi ya Mungu kwa watu wanaoishi katika utakatifu.
 
Usiogope Mungu akikuchora kwenye vitanga vya mikono yake.
"Tazama, nimekuchora katika vitanga vya mikono yangu; kuta zako zi mbele zangu daima." (Isaya 49:16)
Lakini hiyo ni ahadi ya Mungu kwa watu wanaoishi katika utakatifu.
Duuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuh
 
Hapana, siamini.

Yesu yupo hata sasa, hakuna Yesu atakuja zaidi ya aliyepo saa hii.
 
Kama biblia imefananisha maisha yetu na ukungu unaokuja tu chap na kupotena basi
Around the corner tu hapo yuaja
 
Mh, naona kama maelezo yako yamepotea njia, mkuu.
Hapa tunatafakari swali: "Je unaamini Yesu yuaja upesi kama alivyoahidi katika Ufu 22:12?"
Kama unaamini piga kura ya NDIYO. Kama huamini piga kura ya HAPANA.
 
Hakija siku parapanda itakapo lia tanzania wengi waliokuwa na jezi za chama cha ccm na mashabiki hawata paaa kwenda mbinguni.

Watakimbilia ofisi zao chama kuwauliza mbona tumeshindwa kupaa.
Sababu ni uwongo na hamna akili
Akiwepo Lucas Mwanshamba,Pascal Mayala na Wengineo
 
Hapana, siamini.

Yesu yupo hata sasa, hakuna Yesu atakuja zaidi ya aliyepo saa hii.
Yesu yupo nasi kiroho kama alivyoahidi: 'Na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.' (Mathayo 28:20). Lakini pia Yesu aliahidi kwamba atakuja tena. Na safari hii atakuja kwa utukufu. 'Huyu Yesu aliyepaa kutoka kwenu kwenda mbinguni, atarudi jinsi iyo hiyo mlivyomwona akienda mbinguni.' (Matendo 1:11).
 
Umeeleza scenario ileile. Baada ya Yesu katika mwili Arirudi katika roho, hiyo ndio kurudi kwa Yesu iliyoelezwa kila sehemu.

Sasa kama saa hii tunaye Yesu, kwahiyo akija tena huyo mwingine tunakuwa na Yesu wawili?
 
Nadhani tuanzie mstari wa juu ambao ni,
Ufunuo wa Yohana 22:11-12
11 Mwenye kudhulumu na azidi kudhulumu; na mwenye uchafu na azidi kuwa mchafu; na mwenye haki na azidi kufanya haki; na mtakatifu na azidi kutakaswa.

12 Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake iliv
yo.
Kila mtu na imani yake. Mwisho wa binadamu tunatofautiana, wengine watafariki lakini huko waendako me sijui na wengine atatukuka hapa hapa ni kitendo cha kufumba na kufumbua. Kwa hivyo unavyoishi lazima ujue una nafasi moja tu maishani, kutengeneza maisha yatakayokuja baada ya ujuo wake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…