jamiiforums #JFKUMBUKIZI: Mwaka 2008 Waumini
51 wa Dhehebu la Wasabato Masalia, walianzisha kambi katika maeneo ya Tabata baada ya kuzuiwa na kufukuzwa zaidi ya mara 3 Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere wakita kusafiri kwenda Ulaya kuhubiri Injili bila hati yoyote ya kusafiria huku wakidai wameagizwa na Mungu
Wakiwa Tabata, Waumini hao waliokuwa 17 na kuongezeka hadi 51 walikumbana na hali ngumu ya Maisha, (hivyo kugeuka ombaomba), pia walikuwa wakiugua hawaendi Hospitali kwa kudai "Mungu atawaponya". Majirani walilalamikia uchafuzi wa Mazingira na kero ya kuombaomba
Imeelezwa, 24 kati yao walihukumiwa kwenda jela Mwaka 1 baada ya kuvamia eneo la Watu, lakini hata walipokuwa wakipelekwa gerezani, bado walisema, "Hii ni safari pia na Mungu ana mipango yake."
Mdau, kipindi tukio hili linatokea ulikuwa wapi?
Source: JamiiForums