Tafakuri ya FaizaFoxy 9: Ushauri kwa Rais Samia, Dr. Hussein Mwinyi na Watanzania wote kuhusu Uchumi wa Bandari wenye tija

[emoji7]
 
Kwani Faiza Foxy ni "nabii" ?!!!

Hivi mlikwenda madawatini kusomea "kupakwa mafuta"?!!![emoji1787][emoji15][emoji15]
 
Huu ni utumbo mtupu kabisa maana haya yote uliyo yaongea hayatawezekana mpaka tuu makataba wa DP world na Tanganyika uvunjwe au baadhi ya vipengele vibadilishwe..,.

Hivi umeelewa kweli ule mkataba?
Hakuna ulichokitaja kinawezekana chini ya jua la Tanganyika kama mkataba ule wa DP world utaendelea kubaki kama ulivyo!
Hadi sasa hayo yote hatuna nguvu ya kuyafanya mpaka tumuombe au DP world ahamue mwenyewe kufanya…..! Hiyo ardhi yote ni mali ya DP world!

Hapa unajilisha upepo tuu na kujitekenya na kucheka mwenyewe……
 
Wazo lako lingewezekana kama Tanzania ingekuwa nchi moja yenye katiba moja lakini kwa muundo huu wa serikali mbili na hata zingekuwa tatu haiwezekani! Pale ambapo Wazanzibari watakoma kujiita nchi na Watanganyika wataacha kudai serikali yao bila shaka mpango wako ungepokelewa kwa mikono miwili!
 
Ukinisoma vizuri nimesema ijengwe bandari kubwa Zanzibar. Obviously ikisha kuwa ni gateway na hub ya Afrika, haina budi, ikitaka isitake inakuwa ni freeport.
Bandari, Wazanzibari walishaliondoa kwenye mambo ya Muungano. Hivyo hakuna uwezekano wa Serukali ya Tanzania kwenda kujenga bandari Zanzibar. Labda uwashauri SMZ wawaombe DP wakawajengee bandari Zanzibar.
 
Tanganyika ni nchi nyingine ambayo sio land locked. Inayo ardha ya kutosha kufanyia shughuli zake. Haihitaji Zanzibar - nchi ingine, yenye mamlaka yake!
 
Hiyo "win win situation" ndiyo inaleta maswali. Je, kuna mashindano kati ya bara na visiwani? Kama bara na visiwani ni nchi moja, kwann ujenge Bandari Unguja na uitapishe tena migo pwani nyingine ya nchi hiyohiyo moja? Ushauri wako ni wa kisiasa zaidi kuliko faida za kiuchumi.
 
Tuwajengee Zanzibar yenu kwa pesa zetu eeh? Umechemka.
 
Nani angeweza kuamini kubwa USSR ingesambaratika kirahisi vile, wewe ni myopic
 
Bandari si jambo la muungano.
Sidhani kama kuna mantiki
 
Hakuna haja ya kujenga tunnel ya treni, huo mradi ni white elephant project hauna manufaa.

Bandari ya Dar es Salaam na Zanzibar zote hazina sehemu ya kupaki (gati) meli kubwa za Abiria na Cruise ship. Hii ndio inatakiwa ijengwe hapo Posta sehemu ya abiria kupandia boti ni kama unaingia kariakoo shimoni. Inabidi ijengwe underground parking na tunnel road ya kuingia na kutoka hapo.

Volume ya mizigo ya kutoka Dar kwenda Zanzibar ni ndogo saizi PMM kaleta meli ya Judith Milembe inabeba empty container na magari au full containers za transhipment zinabebwa na meli za Dar Zanzibar.
 
Hakuna mkataba wowote na DPW.

Hapa mada ni badala ya kufikiria daraja serikali na wakuu wa nchi hizi mbili wafikirie tunnel.
 
Haina faida? Watu wanafikiri kujenga kinchi kidogo ambacho ukubwa wake ni kama wilaya moja tu ya Tanzania?


Tanzania kwa mradi huu, Zanzibar nzima igeuzwe Freeport, train kilometer 25 ni dakika 10 tu, na mizigo mingi haitakuwa hata na haja ya kudondoshwa Bagamoyyo. Bagamoyo ni shunting tu, haina haja ya kuwa na bandari kubwa ya kwenye maji.

Hizi ni fikra chanya za maendeleo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…