Tafuta hela uheshimishe familia yako

Tafuta hela uheshimishe familia yako

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
Anaandika, Robert Heriel

Moja ya mambo yaliyonifanya nisome wakati ni mdogo, na sasa nahangaika kutafuta pesa ni suala la matukio ya misiba. Kwa kweli Taikon niliapa na katika hilo Mungu anajua, na atalisimamia yakuwa mke na watoto wangu kamwe hawataosheshwa masufuria na kutumwa tumwa bila adabu. Mke na watoto wangu lazima waheshimiwe, na hilo nitalifanya mimi mwenyewe ningali hai.

Kama ilivyo ngumu mimi kufanyiwa ujingaujinga ndivyo iwe hivyohivyo kwa mke na familia yangu. Unajiuliza leo nazungumzia nini?

Iko hivi; hakuna kitu kinauma kama mmeenda kwenye msiba halafu unaona mkeo au watoto wako wanatumwa tumwa na kufanyishwa makazi huku wake na watoto wa wenzako wakipiga tuu stori na kuagizwa kazi kwa adabu. Inauma! Inauma! Hasa sisi Watibeli jambo hilo tunajua linauma na ndio maana hatutaruhusu litokee kamwe.

Ni bora mtu asiende kwenye huo msiba. Hiyo kwetu ni bora, lakini kamwe hatutakubali mke na watoto wangu wahenyeshwe.

Sitaki mke wangu atumwe tumwe, sitaki watoto wangu watumwe tumwe bila adabu. Kama vile ambavyo hamuwezi kunituma tuma mimi na hamkuweza kunituma tuma mimi ndivyo hivyohivyo mtafanya kwa familia yangu. Dharau hazivumiliki.

Unakuta mama wa watu ameolewa labda mumewe kwenye hiyo familia ni maskini au tuseme anakipato duni, basi kwenye msiba atatumikishwa kama punda.

Kwenye kuchambua mchele yupo, hajamaliza utakuta anakuja mtu mwingine anamtuma akajaze maji kwenye pipa kwani tayari yamenunuliwa, anaacha kupembua mchele anaenda kuchota maji, akiwa huko amebeba ndoo saba anaambiwa na mwingine amalizie kwani wali unatakiwa kupikwa ajili ya wageni ambao wapo njiani, hajakaa vizuri anaambiwa masufuria yanatakiwa yasiribwe mchanga ili yasipate moshi.

Hajakaa vizuri, anatakiwa kusafisha vyombo vya mchana, halafu unakuta muda huohuo kuna wanawake kwa makumi wamekaa sebuleni au ukumbi wa msiba wanapiga stori. Ati wamependeza, ati wametoka Daslama, ati wametoka ng'ambo huko ughaibuni kwenye nchi za barafu. Kudadadadeki, mke wangu na binti zangu hujawatuma, labda kama sio familia yangu. Nasema hivi; labda sio familia yangu.

Mkewangu awe amesoma au hajasoma, hamuwezi kumfanyia hivyo. Awe mzuri au mbaya kulingana na macho yenu, hamuwezi mfanya mtumwa wenu. Awe na kazi au hana, haiwezekani kufanyiwa hayo. Kitendo cha kuwa mke wa Mtibeli hiyo ni hadhi ya juu kabisa ambayo anastahili kuheshimiwa.

Iwe Taikon nimechanga mchango mkubwa au mdogo, nimesoma au sijasoma, ninakazi au sina, kamwe haitowezekana mke na watoto wangu kuwa watumwa kwenye matukio ya misiba au ya sherehe.

Hakuna yeyote chini ya hii Dunia ambaye kwenye matukio ya namna hiyo ambaye anatakiwa kumgeuza mkeo na watoto wako kuwa watumwa. Hakuna. Na kamwe sitakubali na haitotokea mke wangu na watoto wangu wakageuza watu wengine kuwa watumwa na kuwadharau katika matukio ya misiba na sherehe kwa sababu sisi Watibeli hatupo hivyo. Sisi ni watu wa Upendo, Haki, ukweli na Akili.

Mkifika kwenye msiba wekeni taratibu, kila mtu atoe na kujitoa kadiri ya alivyowiwa. Msitake kufosi mambo makubwa ili yawe mizigo kwa watu wengine.

Mwenye milioni kumi akatoa milioni moja na mwenye laki moja akatoa elfu kumi wote wametoa sawa. Yupo atakayetoa kwa kuwiwa na mapenzi na yupo atakayetoa kwa sifa na kwa vile anavyo.

Mke afanye kazi vile moyo wake unavyotaka. Sio ajilazimishe au alazimishwe, hiyo sio Haki. Huo ni unafiki ambao sisi Watibeli ni jambo baya na linalofanywa na watu wa hovyo.

Kama mke na watoto kwa hiyari yao watataka kusafisha masufuria na kuwa wapishi bila kuangalia wengine wakiwategea au kuona ndio kazi inayowahusu (labda kwa vile wametoa mchango mdogo) basi hilo sio kosa kwa sababu ni hiyari ya mke na watoto wangu.

Kutoka kwako Dar au Ulaya na kuchanga pesa nyingi hakukufanyi uwanyanyase na kuwatesa wake na waume wa ndugu zako. Ni bora usitoe tuu hakuna kitakachopungua. Ni bora nisitoe mchango mkubwa ikiwa nitautumia mchango huo kuwanyanyasa wengine.

Nazungumzia unyenyekevu ambao ni sehemu ya Upendo. Kutojiona bora kuliko wengine.

Kama mimi na familia yangu sijioni bora kuliko wengine basi vivyohivyo siwezi ruhusu mtu ajione bora kuliko mke na familia yangu.

Vijana, na wote msomao ujumbe huu, kamwe usiruhusu yeyote akudharau. Kumbuka dharau ipo kwenye uovu. Yaani kama utafanya uovu na maasi au uhalifu basi utadharauliwa lakini hakuna dharau kwenye kuwa na kipato kikubwa au kidogo, hayo ni majaliwa.

Kuwa mtupi au mrefu, kuwa mweupe au mweusi, kuwa mzuri au usiye na sura ya kuvutia, yote ni majaliwa. Mtu asikudharau wala kuidharau familia yako Kwa mambo hayo. Hivyo ndivyo kuishi kwa kuheshimiana na kupendana.

Wewe ukiwa na pesa ni wewe na familia yako huko. Ukija nyumbani kwenye msiba pesa zako hazina maana yoyote isipokuwa moyo wako. Kama utataka unyenyekewe ili utoe hizo pesa hilo futa akilini mwako.

Tutafanya msiba wa gharama inayoendana na mioyo ya watu. Hatutahitaji sifa zisizo na maana yoyote. Lengo ni mpendwa wetu apumzike kwa amani na sio kumnyenyekea yeyote.

Halikadhalika na kwenye harusi na mambo mengine.

Hivyo ndivyo Taikon Master ninavyomaliza ujumbe huu ukiwa na usia kwa wana na binti za Tibeli.

Acha nipumzike sasa.

Robert Heriel,
Taikon wa Fasihi,
Kwa sasa Dar es Salaam.
 
Nadhani lengo la huu Uzi Ni kuwahamasisha vijana kutafuta pesa kwa bidii ili waweze kuziheshimisha familia zao.

Vijana wafanye kazi.

Heshima ya Pesa ni bandia (ya muda)

Lakini Vijana wawekeze zaidi kwenye uadilifu, upendo, Haki na mambo yote Mema. Hapo watapata heshima ya kudumu.

Zingatia, kufanya kazi pia ni sehemu ya uadilifu na wema
 
Kama kuna kitu nakichukia ni kuonewa au kuonea mtu just because ya kukosa pesa,binafsi hata niwe sina hunitumi kizembe ntafanya nikiona inafaa period!

Unakuta Kimama cha watu kinaendeshwa huku na huku alafu Wakati huo wapo wengine wameketi palepale. ATI kisa Bwanaake Hana Pesa.
 
Hiyo hali haitokei tu lazima kunakuwepo na sababu, ni Lazima utengeneze na yatengenezwe mazingira ya mkeo na watoto kutofanyiwa hayoo kutotumikishwa na kudharauliwa namna hiyo. Heshima kwa mkeo na watoto wako itaanza na wewe mwenye jinsi uishivyo na mambo ufanyayo Mathalani misimamo yako nk.
 
Hiyo hali haitokei tuu lazima kunakuwepo na sababu, Ni Lazima utengeneze na yatengenezwe mazingira ya mkeo na watoto kutofanyiwa hayoo kutotumikishwa na kudharauliwa namna hiyo. Heshima kwa mkeo na watoto wako itaanza na wewe mwenye jinsi uishivyo na mambo ufanyayo Mathalani misimamo yako nk.

Ukishakuwa ombaomba Kwa Ndugu unajiingiza kwenye hatari ya familia na Mkeo kutokuheshimiwa.
Na pili, ukiwa haujitambui na kujiamini kisa mapungufu Fulani labda umaskini au haujasoma au wewe ni wakijijini wanaweza kuburuza wewe na familia yako.

Huwezi kukataa Mkeo akitumwa Kwa MTU unayemuomba Pesa
 
Sisi kwetu misibani hua wanaume ndio tunapika, tuna chanja kuni, tunasomba maji, tunachimba makaburi, tunazika na wanawake kazi yao ni kulia tu..😶
 
Mke wangu mtarajiwa popote ulipo sijui upo wapi na unafanya nn ila Mungu anajua ww ndo utakua mke wangu, nakuomba sana fanya mazoezi ya mambo yafuatayo;

Jitahidi ujue kingereza kidogo, ujue jinsi ya kusmile jukwaani na kupungia mkono kadamnasi
Jitahidi uwe na uwezo wa kuendesha expensive cars na uwe na idea za matoleo mapya ya magari
Jifunze kua na stara na jinsi ya kubehave mbele ya wakubwa wenzangu
Uwe na idea na namna kampuni ina-operate mke wangu sio kila kitu nifanye mimi
 
Ukiwa na hela hata nguvu ya kuandika hasira zote hizo hutakua nazo. Cha msingi heshimisha familia yako kwa kuwa na mkwanja hayo mengine ni kelele tu zisizo na msingi.
 
Nadhani lengo la huu Uzi Ni kuwahamasisha vijana kutafuta pesa kwa bidii ili waweze kuziheshimisha familia zao.
Kuna watu watakua maskini mpaka wanakufa.... tunaishi kwenye mfumo wa kibepari, lazima kuwe na maskini ili ufanye kazi.... LAZIMA

Inaweza kua mimi, inaweza kua wewe unae soma, najua Iko nje ya mada kidogo ila nimeona niseme tu,

Sio kwamba ukitafuta hela utazipata....
Ukiwa na hela hata nguvu ya kuandika hasira zote hizo hutakua nazo. Cha msingi heshimisha familia yako kwa kuwa na mkwanja hayo mengine ni kelele tu zisizo na msingi.
Sio kweli, pesa au utajiri sio sababu ni Heshima na uoga wa KINAFIKI TU.

Kuna mzee mmoja hana pesa hakuwahi kuwa na pesa za maana lakini aina ya maisha anayoishi, ilikuwa ni ngumu sana kumuendesha kumdharau wala familia yake na watoto wake. Ni mtu wa haki haki na mwenye misimamo kweli kweli bila kujali mahali alipo, cheo wala sura ya mtu, hana uwoga wowote wala uonevu wowote ule ni haki haki mpaka leo mtaani masikini kwa matajiri wanamuogopa na kumuheshimu sana na familia yake.

Nakubaliana na mtoa mada pesa sio sababu kabisa ni heshima na Uoga wa kinafiki tuu.
 
Back
Top Bottom