DOKEZO TAHADHARI: Afisa TRA ahatarisha maisha ya wakazi Mbezi Juu Kwa Sanya kwa kujenga ghorofa 4 bila kibali, kwenye msingi dhaifu wa nyumba ya chini

DOKEZO TAHADHARI: Afisa TRA ahatarisha maisha ya wakazi Mbezi Juu Kwa Sanya kwa kujenga ghorofa 4 bila kibali, kwenye msingi dhaifu wa nyumba ya chini

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Kwanza TAKUKURU/Sekretariati ya Maadili waanze na huyu wamfanyie Lifestyle audit. Kulinganisha kipato chake na uwekezaji anaoufanya.

Huyu atakuwa kwenye kutengo ambacho anakamua rushwa sana kutoka kwa wafanyabiashara
Sheria ya kuzuia na kupambana na Rushwa, imesema Kuwa kumiliki Mali zisizo na maelezo ni kosa mpaka utakapoweza kutoa maelezo ya Mali,
-huyo Ofisa wa Tra sheria ya maadili ya viongozi wa Umma haimuhusu inahusu Wale wakubwa wakubwa serikalini.
 
Huyo jamaa sijui anabwabwaja nini, udaktari haukimbiliwi hakuna kilaza anapeleka pua kule hata awe mtoto wa tajiri namna gani.
Udaktari unakimbiliwa na vilaza mbona wengi tu,
Kuna watu kibao wamesoma PCB wakapiga division one Chuo wakaenda Kusoma B.Com, Tax Nk na ndio hao Wengi wao wako TRA
 
Ulishawahi kuona mtoto wa bilionea anaajiriwa hovyo hovyo ?.

Ukiuliza huyo Bon anafanya biashara gani na analipa kodi iasi gani utabaki kushangaa na kusikitika.
Leo hii hakuna trafic asiyekuwa na usafiri wa uhakika,nyumba nzuri kwasababu ya rushwa za barabarani,jiulize kwanini askari anyelinda bank hana hata baskeli !.

Nchi yetu inahitaji viongozi watakao kuwa tayari kupambana na mifumo ya rushwa.
Kulinda bank hakukuzuii kufanyaa ujasiliamali mwingine nje ya ajira.
Mbona Pana walimu wapo njema
 
Afisa wa TRA mwenye uwezo wa kujenga ghorofa 4 mshahara wake ni tsh ngapi ?.Au ndio wale wa kubambika kodi kubwa kubwa halafu baada ya kushindwa kulipa mnakaa kitako mnazungumza.

Kodi zinatakiwa kueleweka vizuri mfano kodi za magari ukinunua gari aina fulani ya mwaa fulani kodi yake ipo wazi.Ukileta kontena 40ft kodi yake mazungumzo.

Hawa akina Bon tutawazalisha kweli kweli kama tunavyowazalisha matrafic wala rushwa kwa kushindwa kuweka mifumo mizuri barabarani.
Amekwambia kajenga kwa mshahara,vipi Kama ana vyanzo vingine vya pesa kutokana na yeye au familia yake.
Wapo watumishi kibao hata Hela ya ofisi hawakutani nayo zaidi ya mshahara, lakin wanamiundombinu yenye pesa ndefu.
Kupitia kilimo,madini, biasharaa,udalali nk.
 
Sheria ya kuzuia na kupambana na Rushwa, imesema Kuwa kumiliki Mali zisizo na maelezo ni kosa mpaka utakapoweza kutoa maelezo ya Mali,
-huyo Ofisa wa Tra sheria ya maadili ya viongozi wa Umma haimuhusu inahusu Wale wakubwa wakubwa serikalini.
Sawa basi TAKUKURU watusaidie hapa
 
Wivu tu unakusumbua.
Ukiona ghorofa imesimama hadi hapo jua ana kibali tayari vinginevyo ungeshakuta Alama nyekundu.
Upo seriazi kweli? Mwenzako anaongea kitu sensitive unaleta mipasho ya Kwa Mtogole na Manzese? Likitokea la kutokea utarudi tena humu au utasepa?

Huyu ni whisle blower, mamlaka ifuatilie ili ukweli upatikane.

Uswahili uswahili kila jambo haipendezi kama wewe ni "matured enough"
 
Moderator uliwekwa humu uzi wa kijana anaitwa Yona kwa tuhuma za utapeli, na receipts ziliwekwa, uzi ukaondolewa kwa muda mfupi sana.

Uzi wa huyu kijana wa TRA zisizo na receipts upo hadi sasa hivi, mbaya zaidi na picha yake imeanikwa humu? Why? Acheni double standars.
 
Back
Top Bottom