TAHADHARI: Kuna matapeli! Fuata taratibu hizi...

Dah! Huu uzi umenikumbusha machungu ya mwaka 2019.
Kuna member anaitwa Tripp

Ebhana huyu jamaa na mwenzie walinitapeli laptop na pesa kwa kuniuzia kifaa kibovu na ningekaa vibaya wangepiga 1M+ ya kununua camera.

Hawa niliwalea kama wanangu kwa weeek nzima niliyokua dar. Pesa na laptop hainiumi sana zaidi ya buku nilizotuma zaidi ya mara moja ya kununua umeme kwa ajili ya kupasi nguo kwa ajili ya kwenda kwenye kazi, imeniuma kwa sababu kile kidogo nilichokituma kilikua na thaman sana kwake coz alikua anakihitaji sana kwa wakati ule.

Pia kabla hatujakutana na hatujuani vizuri, ni kuongea tu kwenye simu week mbili za mwanzo alinijulisha kufungiwa ofisi yake na TRA
nikaingiwa na huruma nikamtumia elfu 30 angalia hatujuani vizuri, inaniuma sana na naamini hio pesa kwa wakati ule ilikua na thamani sana sababu alihiitaji sana, na bado walinitapeli.

Sikuona sababu ya kupoteza mda wangu kuwafatilia, coz pesa inatafutwa.
 
Mkuu,Natamani kusikia stori hii zaidi,Nakumbuka uzi wako.Ujanja ujana mwingi sana Tanzania.
 
Mitandaoni kuna utapeli mwingi sana.Are you Gulible?
 
Sio kila mtu ana fake maisha mzee najua nilivyohangaika mwenyewe elimu kitaa imenifunza mengi

WEWE ni tapeli full stop, progress ya story zako ni uongo mtu! Too good to be true, umesumbua vijana wa watu kujieleza, then Hakuna lolote!
 
Pengine wakati utatusuta. Watanzania wengi hatuaminiki. Yani kuna wakati tunaiba hata kama wizi haukusaidii. Ni kama hulka hivi.
 

Mkuu, ahsante kwa kunishtua.

I assure you mleta mada ni tapeli mchanga, hajafuzu bado. Mduwanzi tu.

-Kaveli-
 
Nilitaka nikuhifadhi, ila no way. Wewe unaelekea 'kufuzu kozi' afu uanze kutusumbua na shuzi zenu mbofu mbofu ka za akina Parabora wa Uswisi ama yule mduwanzi PerDiem wa Norweeeyi.

Ngoja nikukaange kidogo...

1. Umeshahama Kiwalani (pale mtaa wa kijiwe Samli)?

2. Yule mdada wa jf (username yake inaanzia Di.......) ulimfanyia tukio gani pale maeneo ya Ofisi za UDART Jangwani? nusura akupeleke polisi na hadi leo unamuomba sana asiianike hiyo inshu hapa jf.

3. Yule jamaa muuza furniture pale Keko (somebody J H), umeshafanikiwa kumuingiza king ule mchongo wako fekero wa 'fenicha mtumba' za ughaibuni?

4. Why una WhatsApp Numbers nne za nchi tofauti tofauti ambazo unawapa watu humu jf?

If you think that you are behind a concrete 'camoufrage', you are totally wrong with your thinking. I can assure you... you are just as bare as foot!

Tumechoka na matapeli uchwara wa jf. Picha linakuja... soonest mtafurahia show. Tapeliz wote wa Jf (na washirika wenu wote) jiandaeni kisaikolojia.

Mmeshupaza shingo kitambo hapa jf, sasa tunaanza 'kubetua stuli'. 😎

-Kaveli-
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…