Tahadhari kwa Iran: Usijibu Mtego wa Israel

Tahadhari kwa Iran: Usijibu Mtego wa Israel

Hiyo inchi kuna mtu anaitwa mfalme shah reza .......huyo ndio anatakiwa arudishe utawala wa kiraia ........watu wamechoka na takbiir watu wanataka vimini na mipasuo kama hapo mwanzo ........ayatollah akijichanganya safari hii sijui atakimbilia wapi maana mara ya kwanza alikimbilia ufaransa ........sasa kashayatimba sijui kama atarudi tena kule............watu wamechoka utawala wa dini moja watu wanataka mseto na muingiliano ........na ndio maana ayatolah anapambana sana kulipa prox ili wawaweke busy magharibi wasitimize azma yao ya kumrudisha king reza...............
Naona unalilia haki za ndg zako wa Rainbow.
 
Umemaliza kila kitu, mkuu. Mengine yote ni porojo tu. Suala zima la Israeli vs Palestina na Israeli vs Iran ni sawa kabisa na suala la Ukraine vs Urusi.

Umoja wa BRICS ni tishio mno kwa ustawi wa Marekani. Shirikisho la BRICS likifana, NATO inaangukia pua mchana kweupe.
Wamarekani na Nato wote hao ni wacheza movie tuu. Wao mi Mastermind wa psychology tuu kuwaogopesha watu na uwongo uwongo wao.
 
Naungana na mtoa mada, Iran isijibu chochote ukizingatia kiongozi wao pia ni mgonjwa sana, Iran inatafutwa kwa muda mrefu sana, ili kupunguzwa nguvu za kivita na kiteknolojia ya nyuklia, wazungu hawawamini kabisa waarabu kwa akili zao kama wanaweza ku secure hizi teknolojia kwa amani na usalama wa kidunia, hivyo akijibu tu, njia itakuwa imepatikana ya kuharibu mifumo yote ya kimkakati, just imagine kiwanda cha misile kilchopigwa itagharimu 2-3yrs kukirudisha katika hali yake! View attachment 3136230


Hata kiduku wa Korea walisema pia maneno hayo
 
Sina hakika kama kwa sasa Iran itaweza kujibu kama mifumo ya kurusha makombora ya masafa marefu imeharibiwa.
Kama itafanikiwa kurusha makombora hayo na haina ulinzi wa anga yake basi vituo vya kinuklea na viwanda vya mafuta vitakuwa kwenye risk ya kuharibiwa kabisa.
Kitu ambacho kitaua uchumi wa Iran kabisa.
Na uchumi ukifa basi huenda raia wakaingia barabara kuungasha Utawala wa Iran.
Russia haiwezi kuisaidia Iran kwa sababu ya vita vyake na Ukraine.
 
Kama kuna mtu yupo karibu na Rais wa Iran, Ayatollah, amfikishie ujumbe huu: Asithubutu kujibu mashambulizi ya Israel – huu ni mtego wa hatari!

1️⃣ Mpango wa Kimkakati wa Israel
imeanza na mkakati wa kuwadhoofisha washirika wake wa karibu, makundi ambayo yamekuwa tishio kubwa kwake. Baada ya kuyapunguza nguvu, sasa macho yake yameelekezwa kwa “baba” wa makundi haya – Iran.

2️⃣ Hali hii si ya bahati mbaya. Israel haipigi bila hesabu. Wanajua wanachofanya na wanasubiri tu kosa dogo kutoka Iran. Kosa hilo linaweza kuwa jaribio la Iran kulipiza kisasi.

3️⃣ USA Ipo Tayari Kuingilia
Israel haitapigana vita hii peke yake. Marekani ipo nyuma yake ikisubiri wakati muafaka wa kuingilia vita moja kwa moja. Mashambulizi yoyote ya Iran kwa Israel yatatoa sababu kamili kwa Marekani kushambulia kwa nguvu zote. Vita hiyo haitakuwa tena kati ya Israel na Iran, bali Iran dhidi ya Marekani na washirika wake.

4️⃣ Intelijensia Imara ya Israel
Israel inazo taarifa za kina kuhusu miundombinu ya kijeshi na operesheni za Iran. Wanatafuta tu sababu ya kuanzisha mashambulizi makubwa zaidi. Kujaribu kurudisha mashambulizi kunaweza kuwa sawa na kuwasha moto mkubwa zaidi kwa Iran.

USHAURI: Iran inapaswa kuwa na subira sana kuepuka mtego huu. Siasa na diplomasia kwa sasa ni silaha muhimu zaidi kuliko vita ya wazi. Kujibu kwa pupa kutawapa israel na USA nafasi waliyoisubiria.

"Katika vita ya akili, nguvu huangukia kwa yule anayejua kucheza kwa busara."
Hakuna cha mtego Wala mama yake na mtego ni uoga wenu tu maana mnajua majibu yatakuaje
 
Naona unalilia haki za ndg zako wa Rainbow.
Ufaransa ndio inchi inayoongoza kuwa na mashoga wengi kama sijakosea ........ndiko huyo ayatollah alikokwenda kukaa maana alijua akiwashwa wale komasava watasugua ndevu mpaka bunyelo.......harafu eti aliporudi Iran akajifanya takbiiir nyingi huku Linda hana ..........na ndiko kobaz mmejazana kuliko inchi yeyote ya ulaya mkiendeleza kupakuliwa na wazungu.........hamuwapendi wamagharibi kwanini msikimbilie Iraq,Libya, Iran,Morocco, sudan,somalia,Yemen nyie kira siku mnakimbilia London,USA, france ,Canada, Belgium, Germany, Austria, Australia,..........naq mkifika mnataka mje na tamaduni zenu wakati mmekuta tamaduni zao kule......bakini na uchoko wenu kwenye hiyo mitakbiiir yenu .....
 
Kwa uzoefu wangu hakuna nchi ya kuirabu iliwahi kushinda vita ya waisrael au wamarekani, ndio maana waarabu wote wanakaa pembeni na kuishia kulaani kisanii na sio kusaidia kwa kujua matokeo, China kwa upande wa Iran ni mjanja kutaka pesa kwa kuuza zana, ila hawezi kutoa teknology ya juu kwani mwarabu akili yake ni reverse, Urusi janga alilonalo kwa miezi 32 tayari ni mzigo mzito
Kushinda vita ni nn, marekani amekaa Afghanistan miaka mingapi siku anaondoka si unaona kilichotokea
 
Ilikuwa ni vigumu kwa Israel kuingia katika vita kubwa ya moja kwa moja na Iran kwa sababu kubwa 2
1. Iran kwa muda mrefu amekuwa akiwajengea uwezo wa kivita vikundi vya Hamas &Hezbuloir kwa kuwapa mafunzo na silaha kali akiamini watasimama kama first line of defense na kuendeleza mapigano madogo madogo na Israel ili kum-keep busy wakati wao wakipambana kutengeneza bomu la nuclear. Hivyo ilikuwa nguvu kwa Israel kuanzisha vita ya mbali wakati ana adui hapohapo nyumbani.
2. Kwa muda mrefu Iran amekuwa akiwekeza katika kuimarisha air defense systems zake na kutengeneza makombora ya masafa marefu ambayo yamekuwa changamoto kubwa kwa air defense systems za Israel.
So nini mkakati wa Israel:
1. Kumalizana na Hamas na Hezbola na kuhakikisha hawana uwezo tena wa kuleta madhara kwa Israel kwa muda mrefu ujao. Na wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa sana katika hilli.
2. Kuharibu air defense systems na viwanda vya kuchakata mafuta magumu yanayotumika katika makombora ya masafa marefu. Itawachukua Iran sio chini ya miaka 2 kujenga uwezo huu.
Nini kitakachofuata;
1. Haijalishi kama Iran itajibu mashambulizi or not,lazima Israel itaishambulia Iran ili kuteketeza mitambo yake ya nuclear. Israel inaamini kuwa iwapo Iran itapata uwezo wa kutengeneza bomu la nuclear basi wao ndio wahanga namba 1 na hawako tayari kuona hilo linatokea.
2. Israel itamchokoza Iran kwa namna yoyote ili areact na ndio (unfortunately)itakuwa mwisho wa utawala wa ayatolah. Hili litafanyika kabla raisi mpya wa marekani hajaapishwa mwakani.
 
Ahsante sana mchambuzi wa siasa za mashariki ya kati kutoka hapo Tel Aviv, kwanza kabisa poleni na vita huko.

Ipo hivi, USA hata mwaka 2003 aliivamia Iraq akiwa na washirika wake pamoja ushirikiano wa nchi nyingine zaidi ya 40, just imagine hadi Rwanda ilienda, hadi Angola.

Kwa kuanza tu, US aliingia akiwa na wenzake Poland, UK, Australia.

Nchi nyingi hivi sasa zina uelewa wa kutosha kuhusu ujanja wa USA, waliingia Iraq kwa kile walisema wana silaha za maangamizi, wakakuta hamna kitu.

Usifikiri huo ushawishi USA anao tena hii miaka.

USA pekee haitoshi kuivamia Iran kijeshi, Iran inaweza kushambulia nchi yeyote mashariki ya kati kwa missiles zao zenye shabaha ya hali ya juu.
Hakuna nchi Ulaya ipo tayari kuivamia Iran, uongo wa USA na ujanja wake wengi wameufahamu, ndio maana hivi sasa unaona nchi nyingi zinataka kujiunga BRICS kama mpinzani wa umoja na ushawishi wa nchi za kimagharibi zikiongozwa na USA.

Iran kwa kurusha zile missiles 200, ilikuwa ni kutangaza vita tayari, kama USA alikuwa anatamani kuivamia Iran ilikuwa ni kesho yake, Israel imeshabuliwa mara mbili tunashuhudia, lakini wachambuzi kutoka Kibondo mnavyokuza mambo hajambo.


Israel inaogopa kuingia kwenye vita ya moja kwa moja na Iran, ingekuwa inajiamini na inataka vita, ingepiga kwa nguvu kama inavyofanya Gaza na Syria.

Iran sio Libya mzee.
Iran anadogosha shambulio ila kapigwa vibaya,unamsifu irani ila huoni aibu, yaani adui anaingia kwenye ardhi yako anakupiga na anaondoka tena katumia marubani wa kike kwa dharau bado unakaa hapa unamsifu(ikumbukww sio mara ya kwanza Israel anaingia na kutoka Iran kama kwake juzi tu hapa ametoka kuua kiongozi wa magaidi kwenye ardhi ya irani),Netanyahu alisema hakuna mahali Israel hawawezi kufika huko Iran na kweli katimiza lengo lake bila upinzani ,hiyo rasharasha tu bado shughuli yenyewe.
 
Naungana na mtoa mada, Iran isijibu chochote ukizingatia kiongozi wao pia ni mgonjwa sana, Iran inatafutwa kwa muda mrefu sana, ili kupunguzwa nguvu za kivita na kiteknolojia ya nyuklia, wazungu hawawamini kabisa waarabu kwa akili zao kama wanaweza ku secure hizi teknolojia kwa amani na usalama wa kidunia, hivyo akijibu tu, njia itakuwa imepatikana ya kuharibu mifumo yote ya kimkakati, just imagine kiwanda cha misile kilchopigwa itagharimu 2-3yrs kukirudisha katika hali yake! View attachment 3136230
Wazayuni wa jf mnaandika kama mmekatwa vichwa
 
Iran anadogosha shambulio ila kapigwa vibaya,unamsifu irani ila huoni aibu, yaani adui anaingia kwenye ardhi yako anakupiga na anaondoka tena katumia marubani wa kike kwa dharau bado unakaa hapa unamsifu(ikumbukww sio mara ya kwanza Israel anaingia na kutoka Iran kama kwake juzi tu hapa ametoka kuua kiongozi wa magaidi kwenye ardhi ya irani),Netanyahu alisema hakuna mahali Israel hawawezi kufika huko Iran na kweli katimiza lengo lake bila upinzani ,hiyo rasharasha tu bado shughuli yenyewe.
Wewe mzayuni tokea wapi
 
anajibuje wakati air defence system zake zimesambaratishwa? sasaivi kalala mlango wazi. myahudi atakuja na ndege pale na kuondoka bila wao kujua kama kaja. usicheze na stealth.
Hizo stealth zilishageuzwa majivu zikiwa parking na muajemi
 
Back
Top Bottom