mjingamimi
JF-Expert Member
- Aug 3, 2015
- 42,209
- 51,004
Kujitoa ufahamu hakujawahi kuwa solution ya Tatizo,mwambie Jamaa yako aache kujificha arudi mjini,mwanaume hakimbiagi matatizo
KWani wewe una tatizo la corona au unalisikia redioni na TV , sasa unataka dawa? Wafie mbali huko!Hii inaitwa 'rationalisation'. Labda kama TAHURI wangekuja na utafiti kuonyesha kuwa wamegundua dawa ambayo ni mbadala wa hiyo chanjo au bado wanaendelea nao. Lakini 'maneno matupu hayavunji mfupa'.
Malawi mpaka sasa wamepoteza mawaziri wanne,si nchi zote africa wanejitoa ufahamu
hapa ndio penye tatizo,mkuu sio siasa ila ujinga na upuuziEti wangeleta TIBA badala ya chanjo msipende kudiscus mambo ya kitaalam ki siasa zaidi VIRUS vinakufa kwa dawa gani.?
Mawaziri 4 = 4/18 mil = 2.2 e-5% Insignificant number!Malawi mpaka sasa wamepoteza mawaziri wanne,si nchi zote africa wanejitoa ufahamu
Ngetti njoo utueleze ukweli ukoje.Taasisi ya Haki za Binadamu, Tanzania Human Rights-Foundation (TAHURI) imetoa tamko la kuwataka Watanzania kuungana pamoja katika vita dhidi ya Shirika la Afya Duniani, WHO na Rais Magufuli huku likiwataka wananchi kumuunga mkono Rais wao.
Akiongea na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam, Katibu Mtendaji wa taasisi hiyo Bollen Ngetti amesema;
"Tunaweza kutofautiana katika mambo mengi ya kiitikadi, kimtazamo na maono lakini katika mambo ya msingi kwa nchi kama hili la chanjo ni sharti tuungane kuwa kitu kimoja".
Aidha, Ngetti ambaye ni mwandishi wa habari nchini amesema Watanzania wasikimbilie tu athari za kiafya kwa chanjo hiyo na badala yake waangalie athari za kiuchumi.
"Tutambue kuwa dunia iko katika vitu kubwa ya kiuchumi. Kama Tahuri hatutajikita sana katika athari za kiafya za chanjo hiyo lakini tufikirie ni fedha kiasi gani chanjo hiyo itaswaga?"
"Ikumbukwe kwamba, kwa mujibu wa WHO ili nchi za ki-Afrika kupata chanjo kutoka makampuni yaliyojiorodhesha kwenye mkataba wa COVAX ambayo ni BioNTech na Moderna itazigharimu kiasi cha Dola za Marekani kati ya 7-11 kwa chanjo moja".
Ngetti ameendelea kusema, "kwa Tanzania pekee kama Rais Magufuli ataruhusu chanjo itatugharimu Tsh104Trilioni kwa idadi ya watu wetu nchi nzima. Hii ni fedha nyingi sana kwa nchi changa kama sisi".
Ngetti amefafanua kuwa fedha hizo zitatakiwa kukopwa kutoka Benki ya Dunia kwa udhamini wa ADB na itachukua miaka zaidi ya kumi kuzirejesha kwa riba ya asilimia 7.2.
Aidha, Ngetti amehoji, "kama nia njema kwa nini wazungu wamekimbilia kutafuta chanjo badala ya tiba kamili? Walijua kwa tiba utahitaji dozi chache sawa na idadi ya walioambukizwa ambao kwa sasa ni milioni 100 lakini kinga utacheza namba ya watu duniani".
"Jambo la pekee kama Taifa tunalotakiwa kufanya ni kufuata masharti ya kujikinga huku tulifanya kazi kwa bidii, huu ni upepo unaovuma na kupita, tusiondoshwe kwenye reli".
Ngetti amemaliza kwa kusema, "Magufuli si kichaa, wala hana historia ya ukichaa, anatutakia mema tusimvunje moyo. Lakini pia wataalamu wetu nao wakeshe maabara kukuna vichwa aidha kuchunguza chanjo hizo au kugundua za kwetu kama Waganda wanavyofanya"
My Take: Kwa vita hii tutashuhudia na kusikia mengi. Vita hii ya Magu na wanasayansi itaibua makubwa. Subiri tuone!
Hapo sasa, kwani hizi chanjo kama vile wanalazimisha?? Kuna nini ndani yake??Wao walipiga hesabu zao waje kuuza Africa.sasa mungu NAE Ana mipango yake wanaokufa niwao.
Kufa TUFE sisi huruma waone wao.
Ngetti njoo utueleze ukweli ukoje.
Magufuli aliongelea ubaya wa chanjo na kwamba zina athari kwa kwa binadamu. Akasema Wazungu hawana nia njema na kama wangekuwa na nia njema wangeshaleta chanjo ya TB, Malaria, Kipindupindu na Kansa. Akasisitiza kwa kuna nchi wasichana wake wa miaka 14 walipewa chanjo ya kansa ya kizazi mpaka Leo ni Wagumba.
Hakuna mahali popote alipoongelea gharama za chanjo ya Covid19 kuwa kubwa. Wewe haya ya trillion 11 kuwa sababu ya nchi kukataa chanjo umeyatoa wapi? Mbona mpaka sasa mnalipisha wagonjwa wa Corona zaidi ya mil.10 kwenye hospitali binafsi na hamuwakemei wamiliki? Unajua gharama ya chanjo hizo mpaka kukamilika ni kiasi gani?
Unaposema tiba ni rahisi kuliko chanjo unatumia kigezo gani? Unapokinga watu uanazuia watu kuugua, hivyo hakutakuwa na gharama za tiba. Chanjo ya Ndui inatolewa mara moja kwa kila Mtanzania mara tu azaliwapo, Je ingekuwa gharama kiasi gani kumtibu Mtanzania mmoja anayeugua Ndui hata mara 10 tu maisha yake yote? Na tungekuwa na uhakika kiasi gani kama tiba inaokoa maisha kwa 100%? Malaria ina tiba na Watanzania wanakufa na tiba ipo, itakuwaje kwa Corona ambayo Leo mnaomba tiba badala ya Chanjo kwa kisingizio cha gharama?
Linapokuja suala la kununua ndege za Masifa mnasema tutanunua kwa gharama yoyote, lakini kwenye uhai wa Watanzania mnaona ni gharama kubwa?
Kwani chanjo ilikuwepo? Se waliumiza ndonga wakagundua?sasa CORONA ina tiba?
Mkuu wewe ni binadamu,hapo kwenye familia yenu unataka wafe watu wangapi ndo iwe significant number?Mawaziri 4 = 4/18 mil = 2.2 e-5% Insignificant number!
Kuna uzio Kati ya hizi nchi mbili wa kuzuia covid-19 isifike Tanzania,au mtukufu akisema basi kirusi kinatii na kukimbiaMalawi NI Malawi na Tanzania ni Tanzania.
Nakukumbisha tu hizo ni nchi mbili tofauti
Takwimu za magonjwa mbalimbali na vifo vinavyotokana na magonjwa hayo zinakusanywa na hospital zote nchi na kuchakatwa na wizara ya afya.kuniomba mimi nitoe takwimu ndo kujitoa ufahamu kwenyewe ninakozungumzia,maana najua ukweli unaujua ila umeamua kujitoa ufahamuWeka kwanza takwimu za Corona nchini Tanzania.
Wagonjwa wangapi vifo vingapi.
Basi tusilazimishane kununua.
Binafsi yangu hata wangetoa bure nisingetumia
Pole sana.kwa hiyo sasa shida yenu si ubora wa chanjo bali shida ni umasikini wenu. Poleni sanaBasi tusilazimishane kununua.
Binafsi yangu hata wangetoa bure nisingetumia
Usiwe na shaka. Huyo hasemi anayosema kwa bahati mbaya.Hii taasisi itanyimwa misaada si muda mrefu na huyu msemaji wazungu watakula kichwa chake soon.
Anadunisha biashara ya mzungu
Kama kinga inawezekana, basi hata tiba inawezekana.Eti wangeleta TIBA badala ya chanjo msipende kudiscus mambo ya kitaalam ki siasa zaidi VIRUS vinakufa kwa dawa gani.?