Nadhani hii inasidia kuimarisha suala la usafi mkuu.Desturi ya nyumbani kwetu ukisonga ugali ukimaliza mwiko lazima uuoshe. Marufuku kuacha mwiko mchafu. Hata sijui ina maana gani ila nimekua nayo mpaka leo nikimaliza kusonga ugali lazima nioshe mwiko kabla hata chakula hakijafika mezani.
Hapa tupo tofauti si mila zetu ila ni utaratibu wa familia yetu ,hatulali na chombo kichafu hata 7 usiku vitaoshwa ..Kutoosha vyombo usiku ni nuksi, mkipika chakula wakati wa kula jioni msimalize chote mbakize Kwa ajili ya mizimu yenu yaani wafu ndugu zenu wa familia, pia mwiko kupita ukimuona mtu wa jinsia tofauti au mtu mzima akiwa anakojoa kwenye njia, usimvuke mtu miguu yake
Jirani zanguMakabila yote hapa Afrika au nchi nyingine za Ulaya, Asia na Marekani, wanayo miiko, mila au desturi zilizozoeleka kiasi cha kurithiwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine.
Hapa Tanzania, kwa mfano, kuna mambo fulani ambayo ni mwiko kufanyika katika jamii na ikitokea mmoja wa wanajamii akaenda kinyume na mwiko huo anaweza kupata balaa au kuwasababishia wanajamii wengine balaa.
Baadhi ya mambo/matendo hayo ni kama ifuatavyo:
1. Jogoo akiwika usiku kabla ya mapambazuko huchukuliwa kuwa ni laana ama uchuro. Adhabu yake ni kuchinjwa na kufanywa kitoweo.
2. Bundi akilia usiku karibu na maskani ni balaa. Ili kuepukana na hiyo balaa, unatakiwa kuamka ukoke moto na kuchoma punje za mtama kwenye moto huo hadi punje hizo zilipuke.
3. Kwa kabila letu, hairuhusiwi mtu kutupa tula (Sodom apple) kumvuka msichana au mvulana ambaye bado yupo jandoni. Kufanya hivyo kunaweza kusababisha kifo au kuleta balaa kwa mhusika.
4. Ukiwa unapita porini na kukuta uyoga (edible mushroom) usiuache hapo ulipo. Hata kama huutaki au hujisikii kuula, ungoβe na kuuweka sehemu iliyoinuka ili mtu mwingine anayeuhitaji akipita auchukue akale. Kuuacha bila kuungβoa inaweza kukusababishia matatizo au mikosi.
5. Maisha ya kijijini ni ya kijamaa na watu huishi kwa kusaidiana. Kuna wakati unaweza kukosa unga ukaenda kuomba kwa jirani. Hata kama huyo jirani uliyemuendea naye hana unga wa kukugawiwa, chombo ulichoenda nacho hakirudi bure. Angalau akuwekee unga kisoda kimoja kwenye chombo hicho ili kisirudi tupu. Ni mwiko chombo hicho kurudi tupu.
6. Ukitembelewa na mgeni ambaye hajakutembelea baada ya muda mrefu hata kama huna chakula mmegee ukoko kutoka kwenye sufuria atafune au hata fundo la maji anywe. Ni mwiko mgeni huyo kuondoka kwako bila kula chochote.
Hii ni baadhi ya miiko ninayoweza kukumbuka kwa haraka haraka. Nitaongezea mingine wasaa mwingine. Je, wewe kwenye kabila lako au mahali ulipokulia, ni miiko gani umewahi kuishuhudia na mpaka inaheshimiwa? Tupia mmoja hapa tujifunze kitu.
Nawasilisha.
Asante kwa nyongeza mkuu. Bila shaka wewe ni mtu kutoka "Kanda Maalumu" Hiyo namba 3 hata kwetu ipo (unaacha kamba hadi mfugo ukipatikana kamba hiyo itatumika kuufunga). Hiyo ya kutooa binti asiyekeketwa au binti huyo kuzaa, ni kutoka kanda maalumu kabisa.yote uliyotaja isipokuwa namba tatu tu ni mwiko kwetu, nyongeza;
1. Mwanamke huruhusiwi kula firigisi, huu ni mwiko kwa jamii yetu
2. Mama mkwe hali kuku ukweni, huu ni mwiko kwa jamii yetu
3. Ukienda kuomba deni ama msaada hasa mfugo ukaenda na kamba, kama hutapata huo mfugo huruhusiwi kurudi na hiyo kamba, unaiacha sehemu husika uliyoenda
4. Mbweha kubweka jirani na nyumbani ni mkosi, tegemea msiba muda wowote
5. Mtoto wa kike kubeba mimba kabla hajakeketwa ni laana, hivyo inatakiwa umtupilie mbali na asirudi nyumbani (zamani)
6. Kuzaa mtoto akatanguliza miguu ni laana kwa ukoo wako
7. Mwanaume kuolewa na mwanaume mwenzake ni laana
8. Kijana kumpiga baba/mama yako ni laana kwa ukoo wako
Na mengine mengi, japo sababu ya mengine sijui maana tumerithi kwa wazee wetu
hata ukimtusi Mama/Baba yako nawe lazima ijirudie kwako..Asante kwa nyongeza mkuu. Bila shaka wewe ni mtu kutoka "Kanda Maalumu" Hiyo namba 3 hata kwetu ipo (unaacha kamba hadi mfugo ukipatikana kamba hiyo itatumika kuufunga). Hiyo ya kutooa binti asiyekeketwa au binti huyo kuzaa, ni kutoka kanda maalumu kabisa.
Halafu hiyo ya mtoto kutompiga baba yake kama ikitokea inakuwa ni laana inayoendelea kizazi hadi kizazi hadi lifanyike tambiko maalumu kuitengua.
Ni hivi ukimpig baba yako, nawe pia utapigwa na watoto wako nao watakaokupiga nao wao pia watapigwa tu....yaani unakuwa ni mwendelezo wa milele.
Hii nimeishuhudia pale kijijini kwetu. Kuna mzee mmoja alikuwa akimpiga baba yake. Naye watoto wake walimpiga na wale watoto wake waliompiga nao pia walipigwa na wao pia wanapigwa. Ni laana isiyofutika hadi tambiko lifanyike kutengua laana hiyo.
π€£π€£π€£π€£ hii tamu sana.Huko nilipotokea ni marufuku mwanamke aliyeolewa kulala na chupi isipokuwa tu kipindi akiwa mwezini
Hiyo ya kumvuka mtu ipo na kwetu pia,Hii ya kutofagia usiku hata kwetu ipo mkuu. Hebu taja nyingine zaidi watu wajifunze.
Kwetu mtu akiwa amelala chini usimvuke. Ukimvuka inasemekana hakuwi (harefuki). Ili undo au ku reverse hilo tatizo la kutokuwa, unatakiwa kumvuka kwa mara ya pili kuelekea upande uliomvukia.
Kurians.yote uliyotaja isipokuwa namba tatu tu ni mwiko kwetu, nyongeza;
1. Mwanamke huruhusiwi kula firigisi, huu ni mwiko kwa jamii yetu
2. Mama mkwe hali kuku ukweni, huu ni mwiko kwa jamii yetu
3. Ukienda kuomba deni ama msaada hasa mfugo ukaenda na kamba, kama hutapata huo mfugo huruhusiwi kurudi na hiyo kamba, unaiacha sehemu husika uliyoenda
4. Mbweha kubweka jirani na nyumbani ni mkosi, tegemea msiba muda wowote
5. Mtoto wa kike kubeba mimba kabla hajakeketwa ni laana, hivyo inatakiwa umtupilie mbali na asirudi nyumbani (zamani)
6. Kuzaa mtoto akatanguliza miguu ni laana kwa ukoo wako
7. Mwanaume kuolewa na mwanaume mwenzake ni laana
8. Kijana kumpiga baba/mama yako ni laana kwa ukoo wako
Na mengine mengi, japo sababu ya mengine sijui maana tumerithi kwa wazee wetu
Mmelelewa vizuri sana, kama una mdogo wa kike niunganishe naye.Desturi ya nyumbani kwetu ukisonga ugali ukimaliza mwiko lazima uuoshe. Marufuku kuacha mwiko mchafu. Hata sijui ina maana gani ila nimekua nayo mpaka leo nikimaliza kusonga ugali lazima nioshe mwiko kabla hata chakula hakijafika mezani.
Mm binafsi cjawahi kusex, nasubir mpaka nikioa ndipo mwanamke wangu huyo awe wa kwanza kunitoa bikra ya rungu languMlivo jeuri na mnafanya tu wakati hamruhusiwi[emoji38][emoji38][emoji38]