Taja tabia yako/mazoea yako fulani hivi ambayo huyapendi na unasumbuka kuiacha/kuyaacha please don't be shy someone might give you a solution here

Mimi ni mwepesi sana kulia yaani sijui nipoje. Hapa yenyewe kuna mtu tumepishana kidogo tu tayari machozi. Sipendi hii hali [emoji57][emoji57]

Kinyongo. Ni mzito kukasirika ila ikitokea nimekasirika kweli inakua ndio kwa kheri kitu msamaha hapo ni kipengele. Nitatembea na masikitiko muda mrefu hii hali inanitesa sana na sijui natokaje huko aargh
 
Namba 2 dawa ninayo😂
 
[emoji23][emoji23][emoji125][emoji125][emoji125] Hii nimechukua kwa mama angu aisee yule mtu akikukasirikia hamna rangi utaacha ona. Huwa namuambia kaniharibu sana mwanae.
Yaani wewe katika hilo umekuwa lekchara wake kwasasa
 
sasa mimi kwa upande wangu sijajua ni tabia au ni weakness,Nina changamoto moja huwa inanitesa sana yaani nina mwandiko mbaya (handwriting) huwa naona aibu kuandika mbele za watu.Wakuu hii ni changamoto inayoweza kurekebishika ukubwani au ndio imetoka hivyo na hairudi!!!??(yaani kurekebisha mwandiko)

Sent from my DRA-LX5 using JamiiForums mobile app
 
sasa mimi kwa upande wangu sijajua ni tabia au ni weakness,Nina changamoto moja huwa inanitesa sana yaani nina mwandiko mbaya (handwriting) huwa naona aibu kuandika mbele za watu.Wakuu hii ni changamoto inayoweza kurekebishika ukubwani au ndio imetoka hivyo na hairudi!!!??(yaani kurekebisha mwandiko)

Sent from my DRA-LX5 using JamiiForums mobile app
 
..kunywa soda ya Pepsi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…