Takriban wiki ya pili sasa hatuoni dalili ya yeye kutafuta hata shughuli, yaani yupo tu

Takriban wiki ya pili sasa hatuoni dalili ya yeye kutafuta hata shughuli, yaani yupo tu

We jamaa ungekua ndo mzee wangu mbona ungekufa kama sio kuzirai kabisa,
Nakumbuka mwaka 2009 kipindi tupo shy town mzee alikuwa ni askari na familia yetu kiujumla ilikuwa na watu takribani 7 hvi mara akaja babu yetu na familia yake ya watu 6 kukaa home hapo hapo wazazi wa mke mdogo na mzee nao wakatia timu wakiwa na watoto wao wa2 haya kama haitosh kina binamu watoto wa shangazi nao hawa hapa wa 2 lets calculate 7+6+4+2=19 na mtu anaelisha familia ni mmoja tu broh ungekuwa wewe ungekufaga mazima na iliwachukua takribani miezi zaidi ya miwili mpaka kuja kuondoka.
Dah!!,Hao ni Wanyakyusa Nini??.
 
We jamaa ungekua ndo mzee wangu mbona ungekufa kama sio kuzirai kabisa,
Nakumbuka mwaka 2009 kipindi tupo shy town mzee alikuwa ni askari na familia yetu kiujumla ilikuwa na watu takribani 7 hvi mara akaja babu yetu na familia yake ya watu 6 kukaa home hapo hapo wazazi wa mke mdogo na mzee nao wakatia timu wakiwa na watoto wao wa2 haya kama haitosh kina binamu watoto wa shangazi nao hawa hapa wa 2 lets calculate 7+6+4+2=19 na mtu anaelisha familia ni mmoja tu broh ungekuwa wewe ungekufaga mazima na iliwachukua takribani miezi zaidi ya miwili mpaka kuja kuondoka.
Ufala huu sifanyi, utakuta alikuwa anaumia moyoni kimya kimya tu
 
Extended family inatutesa sana Africa, ndiyo maana hatuendelei maana akitoka huyo atakuja Shangazi then Mjomba
 
ni takribani wiki 2 zilizopitata nilipata ugeni wa kaka yake mke wangu na tulimpokea vizuri tu.

Alifika mida ya saa 2 bila taarifa na niwe muwazi kwamba hata mgao wa chakula ulivurugika,

Usiku ule ule tukiwa chumbani nilikuwa namhoji wife kwanini ndugu yake kaja bila taarifa ila nikapotezea nikijua labda atakaa siku 2 au 3.

kuna vyumba vya wageni vimejitenga na nyumba kuu ndiko tulipompa hifadhi, na choo / bafu ni humo humo.

sasa ni takribani wiki ya pili sasa hatuoni dalili ya yeye akitafuta hata shughuli, yani yupo tu.

Wife akimuuliza hali, yeye anasema kaja kutusalimia na binafsi sina tatizo na hilo bali huyu ni mtu mzima ambae pengine ilibidi awe anafanya shughuli za kumuingizia kipato
Naomba ufanye kitu kimoja mkuu.

Kwanza tambua kwamba maisha ni kupanda na kushuka,unaweza ukafa leo watoto wako wakaja kulelewa na huyo jamaa(mjomba wa wanao) hivyo hakikiaha unahukumu mambo kwa kuepuka vinyongo kwa hao unaowahukumu.

Kiukweli asoli ya aisi wanaume wengi huwa hatupendi ndugu wa kiume wa wake zetu,tunapenda sana ndugu wa kike wa wakw zetu.


Cha kufanya jitahidi siku moja moja utoketoke naye out alafu siku moja ukitoka nae muulize kuhusu maisha zaidi huko alikotoka na wewe muulize viswali vidogo vidogo

Ila kabla ya kutoka nae muulize mkeo kwamba kaka yake alikuwa anafanya shughuli gani akikuambia happ utapata pa kuanzia na kumuuliza maswali yafuatayo..

Dada yako alinambia k2amba unajishughulisha na shughuli fulani kule nybani,vipi inaendeleaje sasa hivi ?

Anakujibu....
Kisha unamuuliza tenaa vipi biashara/shughuli yako jmemuachia nani huko nyumbani...? Hapa ndio utajua mzizi wa jambooo loooteeeeee
 
Week mbili tu unapiga kelele mkuu, sa Mimi kaja baba,mama na mtoto mmoja wa Dada wa kazi wakamaliza mwezi home unafanyaje
 
Una uhakika nibkaka Ake kweli?! Isije ikawa ni mchepuko wake.
 
Binafsi nilishajiongeza kitambo, nikisafiri mikoani sifikii kwa ndugu, nina bajeti yangu ya hotel na isitoshe napenda freedom.

Nitafanya misele yangu iliyonileta nikijisikia nitakuja kuwatembelea nyumbani na kuondoka au ikibidi tukutane maeneo ya town tupige chupa tuachane.

Dunia imeshabadilika binadamu siyo watu.
 
Week mbili tu unapiga kelele mkuu, sa Mimi kaja baba,mama na mtoto mmoja wa Dada wa kazi wakamaliza mwezi home unafanyaje
Mwanaume mlaze chumba cha watoto wa kiume na mke wake mlaze chumba cha watoto wa kike wawe wanakutana sebuleni tu na muda wa kula, wala hawawezi kukaa muda mrefu wataondoka.
 
Binafsi mimi naona uchoyo ndiyo unamsumbua mleta mada,kama umejaaliwa kuwa na sehemu ya kulala mgeni sidhani kama chakula ni shida sana,kwani anakula sado ngapi za mahindi kwa mlo mmoja hadi umchoke kiasi hicho?
 
Back
Top Bottom