Takwimu: idadi ya wanafunzi ni kubwa kuliko walimu. Elimu ya bure haiwaandai watoto kuelewa bali kumaliza shule

Takwimu: idadi ya wanafunzi ni kubwa kuliko walimu. Elimu ya bure haiwaandai watoto kuelewa bali kumaliza shule

Return Of Undertaker

JF-Expert Member
Joined
Jun 12, 2012
Posts
4,572
Reaction score
26,885
IMG_20200906_084801.jpg
 
Botha, aliyekuwa rais wa Afrika Kusini,aliwahi kusema

' The most intelligent black African can not think beyond one year"

Mwafrika anapofikiri jambo anawaza matokeo ya papo kwa papo au anatafuta sifa za muda mfupi na kupigiwa makofi.

Falsafa ya Mwalimu Nyerere kuhusu Elimu ilikua bora sana na ya kiwango cha pekee Duniani.

Mwalimu alikuwa hatumii pesa za Serikali kumwelimisha Mtoto ambaye baadaye anakuwa hana tija kwa Taifa.

Kusomesha Mtoto ni uwekezaji. Uwekezaji wowote ni lazima urudishe pesa iliyowekezwa na ziada.

Tunatumia pesa nyingi kutoa elimu duni kwa watoto na kusababisha tusipate mrejesho wa uwekezaji wetu.

Nyerere alimsomesha Mtoto kwa kulingana na karama za Mtoto kuanzia shule za msingi.

Kila aliyesomeshwa alitumika kikamilifu kulingana na karama zake.

Waliokuwa na karama za utawala, siasa, jeshi, Sayansi n.k waliandaliwa kuanzia shule za msingi.

Wanafunzi wa Kitanzania waliokuwa wanaenda Ng'ambo kusoma masomo ya juu walikuwa na uelewa mkubwa na wazungu walikuwa wanashangaa kuona Watanzania kuwa na akili nyingi.

Sasa hivyo vipaji hivyo havijitokezi kwa sababu ya maandalizi mabovu.
 
Hata idadi ya ngombe siku zote huwa kubwa kuliko mchungaji, idadi ya waumini huwa ni kubwa kuliko mchungaji na hujawahi sikia wakisema huyu kiongoz anatupeleka motoni!!!
 
Nakumbuka mheshimiwa nyerere alipoanzisha elimu bure enzi hizo shule hazikuwa nyingi kutokana na ukomavu wa nchi walimu pia walikuwa wachache na ndo maana akaja na plan ha upe na hata walivyokuwa wanafaulu walikuwa ni mmoja mmoja sana hebu punguza chuki hata kwa siku moja mkuu
 
Elimu bure yawezakuwa Bora Kama watoto wao nao watasoma shule hizo
 
Back
Top Bottom