Tamaduni 10 za kidini ambazo hazimo kwenye Biblia au Quran

Tamaduni 10 za kidini ambazo hazimo kwenye Biblia au Quran

Katika uislamu kasome Qur an na sunnah kwanza then tujadili maana tutabishana kumbe hujui kitu.

Unasema swala hawachanganyikani lakini Hijja wanachanganya...Mbona huulizi ibada ya funga wakifunga wanachanganyikana? Na funga ni ibda na hiyo hijjah sio lazima kama hujui.!

Kila ibada na sheria uislamu haswa mwanamke anatakiwa kujua dini na kuswali anaweza kuswali nyumbani kwake kupunguza fitna ..

Kuongoza ibada mwanamke umeona ile ya wamarekani basi kweny uislamu haipo kama umeona mara kadhaa leta ushahidi.
Huyu sio muisilamu ni mwanasiasa
 
Weka Aya ya Quran yaishe. Haya sio mashindano ya Elimu. Aya tunaelewana.
Karibu kwa maoni zaidi.
Pinga hapo tuone
1684580936213.jpg
 
Hizi hazimo kwenye Biblia.
1: Sikukuu za Krismass na Easter.

2: Kunena kwa Lugha ambazo mnenaji na wasikilizaji wote hawaelewani.

3: Maombezi kwa maiti ili isamehewe dhambi alizofanya akiwa hai.

4: Sabato ya Jumapili.

5: Mchungaji au askofu wa kike. Katika biblia mchungaji ni Mume wa mke mmoja sio mke wa Mume mmoja.

HAYAMO KWENYE QURAN

1: Ishmail kuwa Bora kuliko Isaka.

2: Waislam Kufanya miujiza wakati mtume hakuwahi kufanya muujiza wowote ndani ya quran.

3:Kuvaa suruali ambazo hazifiki chini.
Zile Suruali fupifupi.

4: Wanawake na wanaume kuchangamana wakati wa ibada ya hijja kwenye kaaba (ibada ya heshima kabisa) wakati huku misikitini hawachangamani.

5: Wanawake kuwa maimam na kuongoza ibada zanye mchanganyiko wa jinsia zote.

Nini maoni yako.
No 1,2.....ukitoa Christmas,vipo.
Kasome Tena biblia Yako vzr ,hasa kabla Yesu Hajafa.....utakutana pasaka .
Kasome nyaraka za Paulo vzr ,wakorinto zote, na matendo ya mitume....
Bila kusahau,kasome Mwanzo alipochafua lugha kwenye mnara wa babeli ,na akaamua kurudisha lugha Tena kwenye agano jipya ...
 
Yesu hakuzaliwa tarehe 25 mwezi wa 12. Tarehe hiyo ilikua sikukuu ya warumi. Jmapili ni siku ya bwana, nayo ni kusanyiko takatifu. Hivyo hoja yako wewe msabato haina mashiko.
Ni kweli. Na ipo wazi...
Ni siku iliyochaguliwa ili kusherehekea kuzaliwa kwa Yesu haimaanishi kwamba alizaliwa tarehe hiyo.
 
Wasabato hata wakiwa wamesoma sana ila dini ikiwakaa kichwani hata ile akili ya reasoning inawatoka...nani kakwambia/alisema au analazimisha kuwa Yesu alizaliwa trh 25??
Nyie yale makambi yenu yapo kwenye biblia?
 
nani anauhakika kuwa huyo mtume alitamka maneno hayo?
Nahofia sidhani kama utaelewa.

Ila kwa ufupi mno na kwa uchache wangu wa elimu, ngoja nikuandikie kidogo mno;

Mafundisho ya Mtume katika maneno aliyoyazungumza, vitendo alivyovifanya, yaliyofanyika mbele yake akayanyamazia au kuyasifia, yote hayo yamehifadhiwa. Kuna kitu kinaitwa Sanad, ambayo ni chain ya wapokezi inayokwenda mpaka kwenye chanzo. Sasa katika kutaja hadith kutoka kwa Mtume, aliyeiweka hadith hiyo anataja Sanad inayorudi mpaka kwa Mtume. Ukiileta habari bila sanad, haikubaliki.

Sasa kuhusu yaliyopokelewa kutoka kwa Mtume, hakujaishia tu katika Sanad, bali wapokezi na wasimulizi wote wanachunguzwa na kuna masharti na misingi imewekwa kuhakiki nani ni nani, nini ni nini, masharti ya kupokea hiyo hadith na ni masharti magumu. Wapokezi wanachunguzwa mpaka maisha yao, walizaliwa wapi, walisoma kwa nani, je maneno waliyosimulia ni kweli wameyapokea kutoka kwa wanaowataja, dini yao iko vipi, tabia zao, walikuwa wakweli? au hawakuwa waongo? vipi kuhusu kumbukumbu, walikuwa nazo? Hivyo, uadilifu, tabia njema, memory na kadhalika (mengine sikumbuki) vinazingatiwa na mwisho wapokezi wanawekwa kwa madaraja wao na waliyoyapokea.

Literally, kila mmoja ambaye aliwahi kupokea maneno akasema "amesema Mtume", basi jina Lake limedhibitiwa, hali yake, amechunguzwa na kuwekwa wazi hali yake na akasemwa kuwa ni reliable au unreliable baada ya kuwekwa kwenye mizani kuzingatia masharti.

Mfano hapo uliyemnukuu, hiyo hadith kaipokea Imam Bukhari, ambaye hali yake inajulikana na ni reliable mno. Imam Bukhari katika Kitabu chake alichokusanya Hadith Sahih tu kwa masharti magumu mno, kitabu maarufu kama Sahih Bukhari, ameiweka Hadith hiyo. Hapo, for the sake of brevity, imetajwa tu text ya Hadith na kuwa ameipokea Bukhari. Lakini ukirejea kwenyewe utaona ameitaja Sanad inayorudi mpaka kwa Mtume kutokea kwake Imam Bukhari aliyefariki mwaka 256 H;

حَدَّثَنَا آدَمُ، حَدَّثَنَا شُعْبَةُ، حَدَّثَنَا سَعِيدُ بْنُ أَبِي سَعِيدٍ الْمَقْبُرِيُّ، عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ ـ رضى الله عنه ـ عَنِ النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم قَالَ ‏ "‏ مَا أَسْفَلَ مِنَ الْكَعْبَيْنِ مِنَ الإِزَارِ فَفِي النَّارِ

Na wote waliotajwa hapo wanajulikana na mambo yao yamehakikiwa.

Na hata hiko kitabu cha Sahih Bukhari nacho kimepokelewa na kurithishwa mpaka kwetu na kinaweza kuthibitishwa kielimu kuwa kweli Imam Bukhari ndie alikiandika.

Kiufupi, kuna fani kabisa zinaitwa Ilm Al Hadith, ambazo zinaelezea yote hayo. Na watu wanamaliza umri kuzisoma.

Na misingi hiyo ya uhakiki, uchunguzi na utafiti wa Hadith iko madhubuti mno. Na Waislam tunajivunia mno hili, kwa sababu tunajua hakuna watu waliopewa ilmu hizi ila Waislam Ahlu Sunnah wal Jama'ah.

Lau misingi ya Ilm al Hadith, ikitumika kuhakiki habari na masimulizi haya ya kidunia tu, habari nyingi kama sio zote zitakosa vigezo. Picha linaanza nyingi zitakataliwa kwa kukosa sanad tu. Au hata vitabu, vingi vitakataliwa kwa kukosa sanad tu. Sikuambii masharti mengine.

Ngoja niwaite ndugu zangu wakufafanulie Kisai Kazakh destroyer


Allah ni Mjuzi zaidi
 
Kuhubiri kwa kufokafoka, shetani toka, zizani kama Yesu na wanafunzi wake walikuwa wanapiga makelele hivi?
 
Acts 2:4
[4]And they were all filled with the Holy Ghost, and began to speak with other tongues, as the Spirit gave them utterance.
Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia kutamka.
Matendo ya Mitume 2:7
Wakashangaa wote, wakastaajabu wakiambiana, Tazama, hawa wote wasemao si Wagalilaya?

Matendo ya Mitume 2:8
Imekuwaje basi sisi kusikia kila mtu lugha yetu tuliyozaliwa nayo?

Matendo ya Mitume 2:11
Wakrete na Waarabu; tunawasikia hawa wakisema kwa lugha zetu matendo makuu ya Mungu.
 
Mavazi ya wanaume kwenye uisilamu hayatakiwu kuvuka kongo 2 buruza chini hiwe kanzu suruali kikoa swali hili neno suruali unajua hasili yake linatokana na kabila lugha gani?View attachment 2632157
Weka Aya bro.
Mada haihusu hadith inahusu Qura na Biblia. Tusubiri mada ya hadith mkuu🤔
 
Najua hutaelewa.

Ila kwa ufupi mno na kwa uchache wangu wa elimu, ngoja nikuandikie kidogo mno;

Mafundisho ya Mtume katika maneno aliyoyazungumza, vitendo alivyovifanya, yaliyofanyika mbele yake akayanyamazia au kuyasifia, yote hayo yamehifadhiwa. Kuna kitu kinaitwa Sanad, ambayo ni chain ya wapokezi inayokwenda mpaka kwenye chanzo. Sasa katika kutaja hadith kutoka kwa Mtume, aliyeiweka hadith hiyo anataja Sanad inayorudi mpaka kwa Mtume. Ukiileta habari bila sanad, haikubaliki.

Sasa kuhusu yaliyopokelewa kutoka kwa Mtume, hakujaishia tu katika Sanad, bali wapokezi na wasimulizi wote wanachunguzwa na kuna masharti na misingi imewekwa kuhakiki nani ni nani, nini ni nini, masharti ya kupokea hiyo hadith na ni masharti magumu. Wapokezi wanachunguzwa mpaka maisha yao, walizaliwa wapi, walisoma kwa nani, je maneno waliyosimulia ni kweli wameyapokea kutoka kwa wanaowataja, dini yao iko vipi, tabia zao, walikuwa wakweli? au hawakuwa waongo? vipi kuhusu kumbukumbu, walikuwa nazo? Hivyo, uadilifu, tabia njema, memory na kadhalika (mengine sikumbuki) vinazingatiwa na mwisho wapokezi wanawekwa kwa madaraja wao na waliyoyapokea.

Literally, kila mmoja ambaye aliwahi kupokea maneno akasema "amesema Mtume", basi jina Lake limedhibitiwa, hali yake, amechunguzwa na kuwekwa wazi hali yake na akasemwa kuwa ni reliable au unreliable baada ya kuwekwa kwenye mizani kuzingatia masharti.

Mfano hapo uliyemnukuu, hiyo hadith kaipokea Imam Bukhari, ambaye hali yake inajulikana na ni reliable mno. Imam Bukhari katika Kitabu chake alichokusanya Hadith Sahih tu kwa masharti magumu mno, kitabu maarufu kama Sahih Bukhari, ameiweka Hadith hiyo. Hapo, for the sake of brevity, imetajwa tu text ya Hadith na kuwa ameipokea Bukhari. Lakini ukirejea kwenyewe utaona ameitaja Sanad inayorudi mpaka kwa Mtume kutokea kwake Imam Bukhari aliyefariki mwaka 256 H. Na wote waliotajwa hapo wanajulikana na mambo yao yamehakikiwa.

Na hata hiko kitabu cha "Sahih Bukhari" nacho kimepokelewa na kurithishwa mpaka kwetu na kinaweza kuthibitishwa kielimu kuwa kweli Imam Bukhari ndie alikiandika.

Kiufupi, kuna fani kabisa zinaitwa Ilm Al Hadith, ambazo zinaelezea yote hayo. Na watu wanamaliza umri kuzisoma.

Na misingi hiyo ya uhakiki, uchunguzi na utafiti wa Hadith iko madhubuti mno. Na Waislam tunajivunia mno hili, kwa sababu tunajua hakuna watu waliopewa ilmu hizi ila Waislam Ahlu Sunnah wal Jama'ah.

Lau misingi ya Ilm al Hadith, ikitumika kuhakiki habari na masimulizi haya ya kidunia tu, habari nyingi kama sio zote zitakosa vigezo. Picha linaanza nyingi zitakataliwa kwa kukosa sanad tu. Au hata vitabu, vingi vitakataliwa kwa kukosa sanad tu. Sikuambii masharti mengine.

Ngoja niwaite ndugu zangu wakufafanulie Kisai Kazakh destroyer


Allah ni Mjuzi zaidi
Nitajia hadith sahih ambazo zinakubalika na UMMA wa madhehebu yote ya kiislam kama hadith jazilizi ya vile ambavyo vilisahaulika au havikufafanuliwa katika Quran.

Tuanzie hapo.
 
Back
Top Bottom