Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Nimefafanua hili kwenye post ya sasa mkuu, ningemalizia ningegundulika kwenye basi niliolopanda maana tulikuwa wawili tu (tuliopandia mazingira yale). Na hiki kipande cha 2 kipo built around hili basi la 2Ila na sisi Wabongo tumezidi uvivu! Sasa itaendelea nini tena!! Imekuwa ni tamthiliya hii ya Bongo muvi?! Si uelezee mkasa wako mwanzo mwisho, ili watu wakaendelee na shughuli zao!!
Ona sasa watu wanasubiri ulete huo mkasa wako wa pili!! Hii siyo poa hata kidogo.
Nilikuwa na wenge la msiba mkuu, hivyo sikufuatilia details zake vizuri kabla ya kukata tiketi. Masaibu yaliponipata ndio nikakumbuka kusoma detailsBuss namba T sijui nini AZZ nawewe ukakata ticket kabisa. Hilo lilipaswa liwe limesha yeyushwa Chuma chakavu
Shukrani mkuu 🙏🏿🙏🏿😂😂😂pole sana aisee
Mkuu nadhani nimepanda hili pia😂😂Nililopanda mimi linaitwa Dream Line kwenye ticket waliandika tunafika dar 21:00 usiku lakini dah picha linaanza nafika stendi picha ya basi kwenye ticket na basi lenyewe nililokutana nalo vitu viwili tofauti yani wanavyopakia huko barabarani hamna tofauti na daladala za mabibo-K/koo
Hizi basi huwa zinaokoa sana.Ila ukipanda lazima uvumilie maana mwendo wake ni sawa na kutembea kwa miguu ila ukiwa umekaa.Mabasi ya aina hii huwa hayana haraka mana yao ni kama fagio kuchukua wale abiria waliochelewa safari na wageni kwenye mabasi ya route za mikoani,mabasi haya huwa yanasimama kila kituo kuchukua abiria yani ni kama daladala.
Huyo boya wakuitwa matete sijui gatete ana ufala mwingi sanaWatoto wa miaka ya 2000's wengi wana akili ndogo. Hivyo kuna wakati unalazimika mtu mzima kulala nao tu mbele kwa mbele.
Hhhhhhhh la majini Tena?Basi la majini hilo
Siku nyingine usithubutu hata kulisogelea
Kisbo saivi wameboresha ni mazuri sana rangi yake ni nyekunduMimi huwa sikubali kupanda gari ambalo silijui au sijapanga kulipanda hasa kwa hizo safari za mbali.
2017 nilipanda Kisbo safari dar-kahama nilijuta aisee. Sijui kama sasa hivi walibadili gari ila lile gari lilikua la ajabu sipata ona.
Kuna gari miaka ya zamani lilikua linapiga mbeya-Tanga aisee ile gari ilikua 3 by 2 ni mbaya sijapata ona.
Kweli aisee japo umeongea Kwahasira ila nakuunga mkonoifike hatua wafalme,ukiona story ya mtu scrow kwanza mpaka mwisho uone,kama kuna neno (itaendelea…..)
umaku umekuwa mwingi sana humj,hii ni sawa unaalika watu waje kula kumbe hata kuku mwenyewe ni wa kuanza kukimbiza.
Do you have a YouTube channel, if no consider it, you are a good content creator.Wakuu, inaendelea.
Kwanza poleni kwa kuiachia njiani. Nilifanya hivyo kwa sababu kuu moja. Mwendelezo wake unahusisha gari niliyopanda hivyo wakati naandika uzi huu nilikuwa ndani nimepanda, na code ilikuwa rahisi kwa dereva na konda waliotupakia pamoja na abiria wengine maana tulipanda wawili tu. Hivyo ningegundulika (hasa kama kungekuwa na mtu anatumia JF muda ule).
Kumradhi sana!
Tuendelee sasa.
Tuliwaacha wale askari 3 na abiria wengine pale porini wakisubiria usafiri, nakumbuka nikiagana na mwanamke mwenye mtoto mdogo niliyekuwa namsaidia kumbeba mara kadhaa akipigwa baridi pale chini.
Gari nililopanda sasa lilikuwa linaitwa Johanvia (Musoma-Dar es Salaam). Silipigii chapuo, lakini moja ya magari mazuri unayoweza kupanda kwa safari za ukanda huo ni hili.
Dada mwenye maji ya kunde (Kondakta) alitukaribisha ndani, akauliza kama tungeweza kulipia Tsh. 10000/= kila mmoja tukamjibu haina neno. Akaruhusu tuingie, gari ikala mafuta.
Safari ilikuwa nzuri sana, tukafika Msamvu, Morogoro. Baadhi ya abiria wakashuka tukaendelea na safari.
Sokomoko la pili linaanza baada ya kuondoka msamvu. Kulikuwa na foleni ambayo kwa miaka ya karibuni kwenye safari zangu zijawahi kuiona. Ilikuwa inafika Chalinze. Magari yalikuwa yamejaa barabarani, hii ikiwa mida ya saa 7.
Tunafikaje sasa Dar es Salaam mapema tukiwa tumechoka sana, kumbuka gari hii inapaswa pia kubeba abiria mapema asubuhi kurudi Musoma.
Alitokea bodaboda mmoja akapiga honi mara kadhaa akimuomba dereva ashuke wazungumze, ndipo akasema atatusaidia kufika Dar es Salaam kwa kutupitisha kwenye mashamba ya katani (Sijui mkonge). Safari ikaanza tena tukipita kwenye mashamba hayo huku bodaboda akiongoza njia kwa pikipiki yake iliyowashwa taa.
Cha kushangaza, foleni ya magari ilikuwa hiishi, hadi sasa sijajua palikuwa na shida gani lakini baadhi ya watu walikuwa wanasema kuna ujenzi wa barabara maeneo hayo.
Tuliendelea kuchanja mbuga tukiwa kwenye shamba la katani (Mkonge) huku foleni ya magari yaliyokwama njia kuu tukiwa tunaiona kwa mbali.
Bila bodaboda huyu ambae baadae alituleta barabarani karibu na sheli moja (sikumbuki jina na sehemu) tungefika Dar es salaam saa 1 asubuhi. Pamoja na kwamba tulitumia njia isiyo sahihi na ilikuwa na risk kubwa ila namshukuru yeye binafsi na Mungu kwa kuwezesha tukaingia tena njia kuu mwendo kidogo karibu na maeneo ya Chalinze.
Baadae aliomba apatiwe Tsh. 10000/= kama sehemu ya wema aliotufanyia, dereva hakuwa na hiana akampatia. Tukaingia njia kuu, safari ikaanza ambapo tulikutana tena na foleni kubwa lakini haikudumu sana, tukaanza kuitafuta Dar es Salaam.
Basi, mambo yasiwe Mengi. Tumefika stand ya Magufuli saa 11 kasorobo alfajiri, nikaenda kwangu kupumzika.
Pamoja na changamoto zote hizi sijalaumu, kwani katika imani yangu ninaamini hii ni sehemu ya changamoto za kawaida za maisha ya binadamu. Nipo imara.
USHAURI NA MAPENDEKEZO
NB: Tulipofika Kibaha kuna wanawake wawili walikuwa wanashuka lakini hawakuwa na tiketi zao. Walianza kudaiana na konda awape kwa sababu wasipofika nazo nyumbani waume zao hawataamini kuwa wametoka safari😂😂
- Nilifanya kosa la kukata tiketi pasipo kuangalia ubora wa gari. Hata hii number plate nimeifahamu baada ya kupatwa na majanga. Ni muhimu kufuatilia kwanza details za gari kabla haujalipia nauli yako. Hapo nilibugi.
- Serikali ifuatilie magari haya, mengi yamechoka hayawezi kuhimili safari ndefu. Itasaidia kuepusha ajali zisizo za lazima
- Utaratibu wa wapiga debe uboreshwe kwenye vituo vya kukatia tiketi. Wengi sio waaminifu wanaongea uongo sana
- Serikali itafute namna ya kuzuia magari yasijaze abiria hadi mlangoni, hii ni hatari. Pia abiria tuwe makini, tukatae kupanda kwenye gari (ya umbali mrefu) ikiwa imejaa kiasi hiki.
- Kama nilivyosema, kuna mchezo wa kufaulisha watu waliozidi kwenye vituo vya polisi na mizani ili kukwepa faini. Serikali fuatilieni, mabasi yanafanya sana hii michezo.
- Matukio ya abiria kutelekezwa na wamiliki wa magari yanapopata changamoto yamekuwa mengi. Kwa nyakati fulani, abiria tuliotelekezwa pale jana usiku wengi walisema wamewahi kupatwa na majanga ya aina hii bila kupewa msaada wowote.
- Safari za basi la Dream Line (la jana) zisimamishwe kabla halijaleta madhara makubwa.
- Kifo kipo kila wakati. Kwa tunaoamini katika Mungu tusisahau kusali. Sali kabla haujasaliwa.
- Ukiwa safarini jitahidi uwe na akiba maana majanga hayatabiriki. Ninao uhakika baadhi ya wanawake wamefanyiwa mambo yasiyo mazuri baada ya kuharibika kwa gari lile polini wakiwa hawana chochote. Viashiria vya matendo haya vilianza kuonekana kabla sijaondoka, wengi walikuwa wanalia kuomba msaada wa kifedha huku baadhi ya vijana pembeni wakijadili namna ya kutumia hiyo fursa kujipatia utelezi.
“Unataka niachike, mume wangu hataamini. Unafikiri nyumbani nitasemaje, ushahidi wa safari uko wapi? Wengine sisi waume zetu ni wakali mno”
Mimi sio Muumini wa ile kampeni maarufu ya kukataa ndoa, ila naona vijana wana hoja. Anyway, walifanyiwa mpango wa kupewa tiketi zao, wakafurahi sana.
Kama upo humu unayedai tiketi, nakufahamisha kuwa una mke mzuri sana na alikuwa katulia kwenye basi peke yake. Punguza wasiwasi, alisafiri kweli.
View attachment 2728066