Tamu na chungu ya safari yangu ya Agosti 24, 2023 Kutoka Kahama kwenda Dar es Salaam

Story yangu inafanana na ya huyu Mleta Mada lakini matokeo tofauti. Ilikuwa mwaka 2006 nimeingia Mwanza toka Dar kwa ndege ili nirudi nayo siku hiyo hiyo. Ndege ya ofisi hiyo, mara paap simu imepigwa ndege ikapewa safari kwenda kwanza Entebe.

Mambo yakavurugika. Nikasema ngoja nichuke basi nigeuze zangu maana wanaenda kuchukuliwa Entebe tayari ndege itakuwa imejaa.

Enzi hizo mabasi yanayowika ni Mohamed Trans na Mombasa Raha. Ila barabara ni vumbi kuanzia Misungwi mpaka Dodoma. Nilipofika stand za Mohamed full kiyoyozi kama stand za Scandnavia, nikakuta tiketi zimejaa. Kuelekea Mombasa Raha nako kumejaa. Nikaona siwezi kuahirisha safari lazima nirudi Dar kesho yake nimeshachelewa.

Sasa hapo ndipo nilipofanya kosa kama la Mleta Mada, maana nikaenda Stand na kuuliza basi lenye nafasi, nikambiwa kata tiketi ya Najma. Basi silijui na hata hapo stendi halikuwepo. Mimi nikaamua kukata hivyohivyo.

Kesho yake asubuhi, nimewahi stendi enzi hizo ipo pale Nata. Kila nikitafuta basi silioni. Kumbe kichwani mwangu taswira ya basi kama Mohamed Trans na Mombasa Raha ilikuwa haijatoka. Hivyo sisomi majina na mabasi ambayo nayaona ni ngarangara.

Baada ya kuzunguka sana, nikmpigia aliyeniuzia tiketi naye akaja kunionesha basi ambalo nilikuwa nalipita nikijua linaenda vijiji vya jirani. Tukabishana sana kuhusu basi lile kama litafika Dar, Kwa kujiamini sana yule jamaa akaniambia hili gari sio kufika tu, bali linafika la kwanza kabla ya Mohamed Trans na Mombasa Raha.

Kwa unyonge nikaingia kwenye ngarangara, huwezi amini ndani halina hata taa, halafu viti vyake vina lile bomba kwa juu bila kushonewa cushion. Sasa kilichonitia moyo ni engine inaunguruma vizuri. Kilichonifurahisha safari ilipoanza, ile lami toka Mwanza mpaka Misungwi ilikuwa ni full tracking force, nikasema hapa basi lipo.

To cut the story short, Dar tuliingia saa mbili asubuhi wakati basi zingine ziliingia saa nne asubuhi. IT WAS A BLESSING IN DISGUISE.
 
Utopolo mtupu
 
Kuna baadhi ya matajiri walikua miamba wa kusuka injini.
Ukilitazama basi limechoka hatari ila mwendo wake sasa usipime. Miaka ya 2012 ilikuepo ngoma inaitwa coast line aisee ile gari ilikua inatembea
 
Halafu utaskia kuna watu hobbies zao ni kusafiri. Mie nasafiri kwa mambo maalum, sina budi ndio nisafiri
 


Huku ndo huwa kunatokea yale mambo ya masihara
 
Shida kupakia au kufika 21:00?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Uktuma sehem ya 2 ,nitaarifu
 
Agosti 23, 2023 nikiwa kahama, niliamua kukata tiketi kwenye basi la Dream Line T 140 AZZ, Kahama-Dar

Hii chuma kama sikosei huwa inapak magomeni Idrisa inaweza kaa hata miezi mi3 ipo ipo tu imepaki, kila kitu ktk bus hilo ni cha kuunga unga. Ni bora ukatoka na bajaj kahama to dar kuliko hiyo Screpa! Kwanza inakopaki tu wanauza chuma chakavu na haya makopo wanayookota mtaani!
 
Unazingua mkuu, kwamba bora bajaji😂😂😂
 
Kuna basi inaitwa osaka na mj safaris zinatoka dar kwenda musoma bwana bwana hz zimechoka hiyo mj tulitoka dar saa 1 tukafika musoma saa 5 ya kesho yake. Gari ilipasuka tairi mara mbili pale simiyu ni usku wa manane na gari inatoa harufu ya dawa za kuulia mende kunguni na viroboto. Inshort haifai kwa safari ndefu kama zile maana haina ubora kabsa
 
Very interesting story..! Nimeburudika kuisoma..btw pole mkuu kwa changamoto ulizokutana nazo.
 
Buss namba T sijui nini AZZ nawewe ukakata ticket kabisa. Hilo lilipaswa liwe limesha yeyushwa Chuma chakavu
Hili gari nimeshapanda mara mbili Kahama-Dom mbona linamwaga moto fresh tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…