TANESCO hali mbaya, Serikali yasuasua kununua mita na nyaya za kuunganishia umeme

HUU UTAKUWA NI UZEMBE KWA TANESCO HAKUNA KUREMBA HAPA,KWA SASA UMEME UNASAIDIA TRA KUKUSANYA KODI YAKE P/T,HUDUMA LAZIMA IWE YA HARAKA KWA WATEJE WAKE WITHIN 72 HOURS MTU AWE AMESHAFUNGIWA UMEME
KWELI KABISA MKUU HUU UPUUZI NASHINDWA KUELEWA ,WAHUSIKA WAWAJIBISHWE SERIKALI INAJITAMBA KUANZA KUKUSANYA KODI KUPITIA LUKU, HARAFU KUNA WATU WENGI WANADAI UMEME, SASA HAYO MAPATO NA UNAFUU KWA MWANANCHI UKO WAPI
 

Tanesco wafanyakazi wenu hasa "saveya" wanataka rushwa sana kwenye kufanya survey na pia Control number ya kulipia nayo kupata inabidi utoe rushwa yaani ni rushwa rushwa rushwa ,hili swala ni general kwa tanesco nchi nzima ,litatueni kiujumla maana si la mtu mmoja mmoja,maombi mengi ya watu kutaka kuunganishwa umeme ila sababu ya rushwa mnayatupa kwenye dustbin ndio maana watu wanaohitaji umeme ni wengi lakini hamuwaunganisha kwasababu mnataka rushwa.
 

Elimu Elimu Elimu ,kwani wewe Ukitaka huduma ya mawasiliano unachangia Kujenga Mnara wa Simu? Sehemu zilizoendelea kote interconnection fees hakuna ,wewe unaletewa free unalipia gharama za kutumia huduma tu! Mimi nataka umeme ukiniletea kwa bluetooth/wireless au kwa cable ni jukumu lako halinihusu.
 
Juzi Jumamosi Mitaa yetu kuna Jamaa wawili walibebwa na pikipiki wamebaba nyaya na Mita ,pikipiki inakimbia speed wanaenda kumfunga nyumba ya jirani walivotoka nikaenda kumuuliza jirani kapateje umeme, kaniambia katoa 120,000 : 50000 ya store kuchukua mita store,30000 ofisini na 40000 ya wafungaji
 
Kubali tu ndugu yangu kuwa Jiwe alishadondoka na ishi hivyo. Acha kujipa matumaini hewa
 
Bei ya shs 27.000 ni ndogo haitoshi kununua hata nusu waya wa kummunganishia mteja waitafakari upya ....
 
Hamna haja ya kubishana.... Hata ubaya una kiwango, hali ni mbaya sana sasa hivi
 
Una akili sana wewe
 
Unafikri walioweka hiyo bei ni wajinga?

Kwanza jiulize kwanini si 28, 000 au 30,000 bali ni 27,000?
 
Unafikri walioweka hiyo bei ni wajinga?

Kwanza jiulize kwanini si 28, 000 au 30,000 bali ni 27,000?
Sasa kama sio wajinga mbona wanashindwa kutoa huduma?

Narudia tena, tuache siasa. Hakuna vitu vya bure, usipolipa wewe ujue kuna mtu anakulipia. Sasa jiulize kama nguzo moja ni 600,000 na wewe unawekewa kwa meter + wire + nguzo kwa 27,000; nani analipia hiyo hela nyingine?

REA ilikuwa kazi yake ni vijijini huko kwenye kaya maskini, leo wanaleta siasa hata watu wa mjini, nani analipa hiyo extra?
 
Kwa hiyo kwa akili yako unadhani wanashindwa kuwafungia watu umeme sababu hela ndogo??

Unaishi wapi wewe?

Kwa bajeti hiyo hiyo ya 321,000 unayoitetea watu wameusotea kufunguwa umeme mwaka mzima, napo hapo utasema hela ni ndogo?
 
Kwa hiyo kwa akili yako unadhani wanashindwa kuwafungia watu umeme sababu hela ndogo??

Unaishi wapi wewe?

Kwa bajeti hiyo hiyo ya 321,000 unayoitetea watu wameusotea kufunguwa umeme mwaka mzima, napo hapo utasema hela ni ndogo?
Wewe unaleta siasa.... nimekuuliza hapa kama nguzo ni 600,000 wanawezaje kufunga kwa 27,000. Nijibu, sio unaleta siasa.

Tafuta insiders wakuambie ukweli. Kwamba hata wakati wanalipa 320K ilikuwa ina matatizo haina uhusiano na shida iliyopo sasa hivi. Matatizo ya kwanza yalikuwa ni operational issues, sasa hivi ni operational + financial. Uwezo wa kufungia kila anayetaka umeme kwa 27,000 haupo.
 
Hao insiders wako si ndio wanasababisha shida sasa unataka wakuambiaje?

Nimekwambia kabisa hata bei ya 321,000 watu wanaisotea mwaka mzima alafu wewe unaongelea habari za gharama ndogo?

Hiyo nguzo ya laki 6 unaweza kutupa mchanganuo wake mpaka inafika laki 6?
 
Nenda Iringa kaulize bei ya nguzo, au kama ni mbali nenda hata Mwenge kaulize. Narudia tena, tusifanye siasa. Kwamba 321,000 bado watu walikuwa wanasota is irrelevant, issue ni kwamba kuunganisha umeme kwa 27,000 ni siasa. Hakuna kitu cha bure, kama vipi kila mtu apewe specifications akanunue kwa 27,000 yake tuone.
 
Hafu ukimsikia maza anavyojimwambafy kuwa result oriented .I personally miss JPM's actions si hizi drama
 
Hafu ukimsikia maza anavyojimwambafy kuwa result oriented .I personally miss JPM's actions si hizi drama
Rais angejitaidi kutembelea sehemu zenye Matatizo na kutatua , watu wake hawa aliowewaka, hakuna wanachokifanya ndio maana inafika sehemu wananchi wanaona Utawala dhaifu no action haiwezekani kituo kimoja cha kutoa huduma watu wafike 3000 na wameshalipia tuache unafiki, ukifanya tathimini nchi nzima utakuta watu zaid million wanahitaji kuunganishiwa , Huduma muhimu wananchi wanavyokasa yaani nchi hiyo ijue ni Maskini ya kutupwa poor Tanzania ,The strongest Man died in battle
 
We ulisikia wapi gharama ya kuunganisha umeme ni tzs 27,000 kiukweli tanesco wamezidiwa hawana uwezo wa kununua materials kumeet mahitaji ya wateja siasa zenu za kutafuta sifa ndo zimeleta haya
 
3000 kaungenisheni umeme kisesa,kishiri,Buswelu,Nyamongolo ,igoma acheni Maneno na uzembe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…