TANESCO isifiche kuhusu mgao wa umeme

TANESCO isifiche kuhusu mgao wa umeme

mbenge

JF-Expert Member
Joined
May 15, 2019
Posts
4,864
Reaction score
10,483
TANESCO wawe wawazi kuwa kuna mgao wa umeme unaoendelea hapa nchini kwa hivi sasa. Pengine itakuwa ni jambo jema zaidi kama ingetoa ratiba ya mgao huu ili watu waweze kujipanga zaidi kutokana na athari zinazojitokeza.

Tumeshuhudia busara kubwa iliyofanyika kupitia taarifa iliyotolewa na viongozi wa DAWASA kuhusu kupungua kwa kina cha maji katika mtambo wa Ruvu Chini. Taarifa hii ilienda sambamba na sababu za kitaalamu kuhusu athari zinazosababisha haja ya mgao wa maji, na hata kutoa ratiba ya mgao jinsi ambayo shirika lilivyojipanga na linavyohakikisha utakavyokuwa.

Hali ni tofauti mno kwa shirika dada la TANESCO. Tunapata hisia ya kuwa uhaba wa maji unaondelea hapa nchini kutokana na kukosekana kwa mvua za kutosha za vuli pengine pia una athari hasi katika uzalishaji wa "hydroelectric power". Hali ambayo inapelekea kuwepo kwa uhaba wa nishati hii muhimu.

Lakini tofauti na uongozi wa DAWASA, wao wamemua kuuchuna tu. Cha kushangaza zaidi ni kwamba, shirika hili sasa lipo chini viongozi wapya tena wengi wao wakitokea katika sekta binafsi, tulitarajia kuwa wangalikuwa "proactive" na kutuandaa kisaikolojia kuhusu adha ambayo wanaiona itakuja katika siku za mbele. Lakini wapi! Walishindwa kufanya hivyo kwa wakati.

Basi kwa sasa hata wawe "reactive" na kutoa maelezo kuhusu nini hasa ambacho kinaendelea kuhusiana na uwepo wa mgao wa umeme. Wananchi wanalalamika kila kona ya nchi, lakini wala wao hawaonyeshi kuguswa na jambo hili.

Serikali ya awamu ya 6 tunawasihi sana ilichukulie suala hili kama jambo la dharura. Tunaona imekuwa ni jambo la lililozoeleka hivi sasa, kila mazuri yote yakifanywa na serikali sifa zote na utukufu hurudi kwake Madam President, lakini mapungufu makubwa kama haya wala nayo hayawi tena "attributed" kwake. Hii si sawa hata kidogo.

Ukubwa ni jalala, kama mazuri tuna ya "attribute" kwake, basi hata mapumgufu pia ni lazima yaende kwake.

Uongozi wa TANESCO tafadhali sana mtuambie kwa uwazi kuhusu jambo hili. Kumbukeni tu ya kwamba mficha .... maradhi humuumbua.
 
aiseee hapa nilipo umeme umekatika kitambo ni joto balaaa
Ukiona tatizo linalalamikiwa bungeni na wabunge mbalimbali, basi hili si tatizo la kimaeneo bali la nchi zima.
 
alafu January anataka tumpe urais wakati kapewa wizara tu ameanza ku abuse.huyu kijana hafai kabisa ana create mgao kama kipindi cha ngereja kwa manufaa yake
January naona kama alikuwa na bifu na JPM. Kwa hiyo anatafuta "approach" mpya iliyokuwa tofauti na yake. Kwa hiyo anataka kujitofautisha naye na kukwepa vipaumbele vyake. Asipokuwa makini suala hili litamgharimu.
 
Duh! Umeme ndio huoo umerudi [emoji2957][emoji2957][emoji2957]
 
Watu ambao maeneo yenu hakuna Umeme ni vizuri kutaja sehem au wilaya
 
Nimeona mada ya Mkuu Cannabis kuhusu matengezo yanayotarajiwa kufanywa na TANESCO. Taarifa kama hizi zikitolewa mapema inakuwa ni jambo jema sana.

Screenshot_20211114-151139.jpg


Sent from my Nokia 2.3 using JamiiForums mobile app
 
January naona kama alikuwa na bifu na JPM. Kwa hiyo anatafuta "approach" mpya iliyokuwa tofauti na yake. Kwa hiyo anataka kujitofautisha naye na kukwepa vipaumbele vyake. Asipokuwa makini suala hili litamgharimu.
litamgalimu sana niemongea na watu kule kwenye bwawa la nyerere wanasema winchi lipo na iyo milango ipo January anahujumu taifa
 
Hapo ndio utaona hata kwa mbali umuhimu wa Magufuli. Alikuwa anawafanya hawa mabwege wawatii wananchi. Angalau walikuwa na hofu. Utendaji kama huu wa mazoea ulipungua kwa kiwango kikubwa. Kipindi chake wasingeweza kukata umeme kiboya hivi,hata bila taarifa kuanzia asubuhi hakuna umeme,imerudi enzi za jk . Naongea niko mbeya. Tangu saa 1 leo asubuhi hakuna umeme. Nasema enzi zake wasingeweza kujiachia hivi. Alikuwa na mazuri yake mengi. Tutamkumbuka kwa hayo
 
litamgalimu sana niemongea na watu kule kwenye bwawa la nyerere wanasema winchi lipo na iyo milango ipo January anahujumu taifa
Makamba ni worst . Sasa tunaelewa kwanini JPM hakutaka hawa watu kwenye serikali yake. Hawajali maslahi ya watu wa chini. Wengine hatuna uwezo wa kununua majenereta na tuna biashara zinazotegemea umeme. Mungu turehemu na viongozi hawa. Tutafutie viongozi wazalendo
 
Back
Top Bottom