TANESCO isifiche kuhusu mgao wa umeme

Wacha mama aumbuke,lengo si LNG
 
yani iyo treni ya umeme sijui ita operate vipi kwa umeme huu au tutakua tunaenda moro jioni umeme ukiludi yani ndoto zote zimezimwa kuna watu hawana aibu nchi hii sijui kwanini na wananchi tumetulia tunaangalia tu nchi inachezewa na mtu mmoja
 
Wizara ya Nishati bado haijapata waziri sahihi ambaye anaimudu vyema. Bado inaendeshwa kupitia "trial & error" ili kijaribu kutafuta ufanisi wa kuokoteza ambao unakwepa vigezo vya kitafiti katika maamuzi lengwa.

Viongozi wa wizara na shirika bado wanapatikana kirahisi tu kupitia vigezo vya "nepotism & political prejudices" na wala si kwa kupitia "thorough vetting & deserveth competence of office barriers"

Hivi unawezeje kuwaacha watu makini kama Prof. Assad, Rished Bade, John Ulanga, ex GAG Ludovick Otouh na vichwa vingine vyenye uthubutu wa kuongea ukweli ndani ya Bodi ya shirika kubwa linaloshindwa kujiendesha kiufanisi kama vile TANESCO.

Tusiendekeze itikadi bali tujikite kwenye "deriverables" ambazo zitatupa matokeo chanya. Ni "process" rahisi sana kufikia kwayo;

Input > Throughput > Output

Ukikosea tu kwenye "inputs don't expect anything on outputs"
 
Usalama wanafiki sana sana sasa hv km hawapo jahazi linaenda mrama wapo tuu. Enzi za Jpm kupeleka ripoti kila leo.Sasa kwa Bi mdenga hampeleki kuhusu umeme.
 
Halafu haya Matengenezo matengenezo ,Hitilafu hitilafu sijui nini ..... Vitu vya kipuuzi Puuzi ndio vimekuwa vijisababu vya kijingajinga tu, ambavyo serikali ya JPM ilivitokomeza na tukavisahau .... Leo hawa waliovamia fani isiyo wahusu ... Kazi kuangalia matumbo yao ndio wanaturudisha UJIMA . Uchumi wa nchi una drop kwa spidi kubwa. Sekta ya Umeme ndio sekta mama katika ku promote uchumi wa nchi. HAPA WANA HUJUMU SERA YA HAYATI RAIS JPM Isemayo Tanzania Ya Viwanda .
Ndio Maana Jpm alihakikisha upatikanaji wa umeme wa Uhakika. Lakini nashangaa hawa viongozi warithi ... Siku mbili tu ... Wanaipeleka nchi Korongoni .... Kama ndio madereva basi walikula ada ya chuo cha udereva. KWAKWELI tunahitaji WAZALENDO Kwa Taifa Letu hili.

Sent from my TECNO P703 using JamiiForums mobile app
 
Cha kushangaza zaidi ni kwamba, shirika hili sasa lipo chini viongozi wapya tena wengi wao wakitokea katika sekta binafsi, tulitarajia kuwa wangalikuwa "proactive" na kutuandaa kisaikolojia kuhusu adha ambayo wanaiona
Kwa hiyo wafanyakazi wa private sector ndio wako vizuri kuliko public sector, umekitoa wapi hicho kitu ?

Nani kakwambia Mkurugenzi wa DSTV ( Maharage Chande) ana kazi ngumu na ya kitaalam kuliko Mkurugenzi wa TANESCO ?
 
yani iyo treni ya umeme sijui ita operate vipi kwa umeme huu au tutakua tunaenda moro jioni umeme ukiludi yani ndoto zote zimezimwa kuna watu hawana aibu nchi hii sijui kwanini na wananchi tumetulia tunaangalia tu nchi inachezewa na mtu mmoja
WANAHUJUMU Mipango na Mikakati ya JPM kwa makusudi Tuu. Hakuna lolote hapo . Rais MZALENDO alishatutoborea siri kuwa nchi hii sio maskini kabisa na ametudhihirishia hilo kwa vitendo, Kafanya mengi ikiwemo Miaka 5 BILA MGAWO WA UMEME.
Ndio maana alikuwa na uhakika na miradi mikubwa kama huo wa SGR Kuwa utaendeshwa bila Matata.

Sasa hawa viongozi uchwara Usije ukapigwa Butwaa baadae watakwambia hautawezekana kumalizika kwa kuwa nchi ina upungufu mkubwa wa MegaWatts za Umeme.
Huu Mgao wa Umeme waliouanzisha Upo ki mkakati na lengo hapo ni kuhujumu tu miradi mikubwa.

Mungu Tusaidie tupate kambi ya viongozi WAZALENDO

Sent from my TECNO P703 using JamiiForums mobile app
 
mimi ilivyokuja ile pangua pangua tanesco nikajiliza inakuwaje kumbe kuna watu walikua na jambo lao wakahofia kukwamishwa
 
Hapo zamani za kale nakumbuka TANESCO walikuwa karibu sana na vyombo vya habari. Hitilafu yoyote kubwa ikitokea walikuwa wanatoa taarifa kwa umma.

Lakini hivi sasa imekuwa tofauti kabisa. Kupitia kauli mbiu ya "hapa kazi tu" iliwafanya kuchekecha akili na kuhakikisha kuwa nishati hii inapatikana muda wote.

Kubadilika kwa kauli mbiu ya awali na kuja na hii ya "kusalimiana kwa jina la JMT kwa kuitikio cha kazi iendelee" kumbe imeturudisha tena nyuma kwa ile "kasi mpya, ari mpya na nguvu mpya" kwa kiitikio cha mirindimo ya sauti tofauti za majenereta mitaani.

Ukipita utasikia sauti zitokanazo na milio ya jenereta, mara pa pa pa; mara ti ti ti; mara tu tu tu; mara pri pri pri; mara zwi zwi zwi zwi; mara mbwe mbwe mbwe; ili mradi shida na joto hili la sasa huku kitaa sambamba na shida ya maji.
 
Usalama wanafiki sana sana sasa hv km hawapo jahazi linaenda mrama wapo tuu. Enzi za Jpm kupeleka ripoti kila leo.Sasa kwa Bi mdenga hampeleki kuhusu umeme.
Kipindi cha nyuma walivyokuwa wakipeleka mlikuwa mnaenda wote?
 
Mjiandae muda c mrefu wataongeza na bei yenyewe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…