Nawashukuru uongozi Wa TANESCO, nimelalamika humu, mmenijibu humu tena jibu la matimaini.

Nasubiria utekelezaji Wa awamu ya pili. Shida yangu ilikuwa kujibiwa sio ukimyaa.
Ahsanteni sana.
 
Kwanini ukinunua umeme mwenyewe Kwa simu ya mkononi unakatwa ada tofauti na ukinunua kwa wakala.
 
Hili mimi naweza kukujibu sidhani kama wanakata ukinunua kwenye simu maana mi ndo huwa natumiaga ila sijawahi kukatwa hata senti
Kwanini ukinunua umeme mwenyewe Kwa simu ya mkononi unakatwa ada tofauti na ukinunua kwa wakala.
 
Niliuliza line yangu haina nguvu umeme mdogo mno na umeshaunguza vitu vingi vya friji nifanyaje je nikitaka kuhama line
Tulikuuliza wilaya gani,eneo,namba ya simu na namba ya mita tafadhali
 
Kwanini ukinunua umeme mwenyewe Kwa simu ya mkononi unakatwa ada tofauti na ukinunua kwa wakala.
Hii ipo muda sasa ukinunua kwa simu utakatwa 1.1% kama tozo ya njia husika lakini ukinunua bank au TANESCO au mawakala wale wakubwa haipo tuzo hiyo.
 
Nijisajili kwa utaratibu wa kuunganishiwa umeme nikafuata taratibu zote za kujaza form na kulipia nikapewa siku 60 ndio watakuja kuniunganishia.Tarehe 20 November hii ndio siku ya 60 ,swali langu wasipo tokea ni utaratibu gani niufuate,
Asante
 
Nijisajili kwa utaratibu wa kuunganishiwa umeme nikafuata taratibu zote za kujaza form na kulipia nikapewa siku 60 ndio watakuja kuniunganishia.Tarehe 20 November hii ndio siku ya 60 ,swali langu wasipo tokea ni utaratibu gani niufuate,
Asante
Jin
Wilaya
Namba ya simu
Tarehe uliyolipa
 
Nashukuru kulishughulikia tatizo hili. Limeshughulikiwa jana.
Hawa jamaa wapo vizuri malalamiko yakiwafikia wanatimiza kwa haraka,mita yangu ilipigwa na radi tangu mwezi wannne mwaka huu wilaya husika ikawa inasuasua tu kuja kunifungia mita mpya ,baada ya kuja hapo jamii forum yaan haikupita hata wiki mzee nikaja fungiwa
 
Naomba kujua Mwaka Jana huku kijijini uliletwa huu umeme wa REA!
Kukawa kuna shida sana hasa ukitaka kuingia labda wale wachache wenye vyeo flani ndio walifanikiwa!

Sasa je, hivi kuna awamu nyingine zinakuja kwaajili ya kusambaza majumbani au ndio tufuate taratibu za kuunganishiwa huo umeme kama maeneo mengine? ( Yaani kulipia gharama kulingana na idadi ya nguzo?)
 
Habari wakuu Tanesco.
Naishi jimbo la Ukonga wilaya ya Ilala jijini Dsm maeneo kata ya Msongola eneo linaloitwa kwa Mbeche.

Tumewekewa nguzo na nyaya za umeme eneo hili inaweza kukaribia miaka miwili sasa nyaya hizi hazina umeme kwa sababu hawajafunga Transfoma.

Tatizo nini hali tunaona maeneo mengine hapa Dsm miradi ikiendelea tu kama kawaida!?

Ilikuwa na maana gani kufunga nyaya zikakaa miaka miwili hali mlikuwa mnajua hamna Tranfoma!?

Mumetutia shauku ya umeme wananchi kisha mkatokomea!!

Shime mje mmalizie mradi wenu.
 
Naomba kuuliza
kuna mita za luku ambazo zilikuwa znatumika zamani kidogo, japo kwa sehemu fulani naona baodo zinatumiwa kwenye umeme wa REA kwa sehemu kubwa kwa sasa zimeingia mita nyingine ambazo zaweza tundikwa juu ya nguzo au zikawekwa sehemu nyingie - kwenye nyumba.
Je kama nataka zile mita za luku za zamani naweza omba nikafungiwa?
 
Ndugu mteja.

Zile zilikuwa toleo la zamani kwa sasa tumekuja na toleo hizo ambazo ndio za kisasa zaidi. Pia kwa utararibu wa Tanesco hatubadilishi mita nzima. Mita inabadilishwa kwa sababu maalum.


Labda tujue ni kwanini mita ya zamani na sio za sasa
 
Jina
Namba ya simu
Eneo/kijiji lako
Wilaya
Mkoa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…